Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake. Shahidi wa 12 Luteni Urio kuendelea kutoa ushahidi Januari 31, 2022

Kesi ya makomandoo iliisha jana baada ushahidi wa Urio, kesi ya Mbowe imebaki sehemu ndogo sana, Mbowe kusema tu hakumwambia shahidi Urio, then kesi yote itakua imeisha mana Urio keshasema Hana uthibitisho wowote na hawakuwai kujadili tena kuhusu ugaidi.
 
Mjue shahidi ni komandoo na wala si mtu mjinga mjinga
angalia Comedian Mh. Matata anavyojiingiza mdomoni mwa komandoo Urio

Matata: kwenye huo Umuhimu hukuona Kuna Umuhimu Wa Vinasa Sauti na Meseji ambao Vitasema Exactly Kuwa anataka Kulipua
Masoko

Shahidi: Mheshimiwa Jaji Mbowe alikuwa alishaniambia Kwa Meneno, asingerudia

Matata: Narudia Swali langu, kwenye huo Umuhimu hukuona Kuna Umuhimu Wa Vinasa Sauti na Meseji ambao Vita, sema Exactly Kuwa anataka Kulipua Masoko

Shahidi: Sikuwa na Vifaa Vya kunasa Sauti
 
na mukae kwa kutulia sindano zinakuja ,mutu wenu shayidi ana kesi ya kujibu.tena amepasuwa simu isiwake ili siri zisijulikane.NURU ITALISHINDA GIZA
shahidi ana kesi ya kujibu? wakati hata kushitakiwa hajashitakiwa? na wanaoweza kuamua ashitakiwe au la ni wale waliomwita kama shahidi, na hapohapo unaamini una akili? mnafikiri kwa kutumia kamasi aisee.
 
Anasema uthibitisho wa Ugaidi wa Mbowe Ni msg iliyoandikwa 'Muda umeisha' [emoji1][emoji1][emoji1]
 
Mh. Jaji kwa mamlaka uliyonayo maliza hii kesi - hamna kesi humu ni kupotezeana muda na kulighalimu taifa.

Matata: Freeman Mbowe akikataa leo hakusema, ni ushahidi gani unao mbele ya Mahakama Kwamba Mbowe alisema hayo maneno uliyosema?

Shahidi: Ni ushahidi wa meseji ya kusema "muda umeisha"

Matata: hiyo meseji inayosema muda umeisha ina sehemu inasema kulipua masoko

Shahidi: Hakuna mahali inasema

Matata: hiyo Meseji ina sehemu inasema kushambulia viongozi ambao hawapendi upinzani?

Shahidi: Hakuna mahali inasema hivyo

Matata: Hiyo meseji kuna sehemu inasema kulipua vituo vya mafuta

Shahidi: hakuna mahali inasema hivyo
 
Matata: Freeman Mbowe akikataa leo hakusema, ni ushahidi gani unao mbele ya Mahakama Kwamba Mbowe alisema hayo maneno uliyosema?

Shahidi: Ni ushahidi wa meseji ya kusema "muda umeisha"

Matata: hiyo meseji inayosema muda umeisha ina sehemu inasema kulipua masoko

Shahidi: Hakuna mahali inasema

Matata: hiyo Meseji ina sehemu inasema kushambulia viongozi ambao hawapendi upinzani?

Shahidi: Hakuna mahali inasema hivyo

Matata: Hiyo meseji kuna sehemu inasema kulipua vituo vya mafuta

Shahidi: hakuna mahali inasema hivyo

Kwahio kusema "muda umeisha" ndio ushahidi wa ugaidi[emoji28]dah!
Nchi inachezewa hii
 
Huwa tunaaminishwa tuna jeshi na askari bora kwa ukanda wetu wa east Africa,dah!! nimemsikiliza Luteni wetu anavyojichanganya kujibu maswali..namashaka sana na vikosi vyetu.
 
Yaani hadi kufikia leo hakuna sehemu hata moja inayojaribu kuonesha palikuwa na njama za kupanga vitendo vya kigaidi.

Halafu kamanda zero aliuhakikishia umma kwamba wanao ushahidi mzito na wa kutosha juu ya vitendo vya njama za ugaidi.

Halafu eti kamanda zero naye ni mwanasheria ambaye baada ya kusoma meseji hizo akajiridhisha kwamba wana ushahidi wa kutosha.

Hii kada yetu pendwa ya sheria inaharibiwa na vilaz.a wachache. Inakera sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…