Kabla mjumbe hujatuletea habari, naomba msaada wa kujua mambo yafuatayo.
1. Ni mamlaka gani huwa inaamua kutegeneza michongo, mamlaka ambayo hakuna chombo kingine kinaweza kuhoji? Hii mamlaka husimamiwa na chombo gani kisichoweza kutambua kwamba mamlaka hazifanya sawa?
2. Kesi za michongo kama hizi hutumia gharama kubwa sana. Juzi Mama amewaambia polisi waache kubambikia watu kesi, na PCCB wakafuta kesi kama sikosei 300 za michongo. Ninategemea kwa dhamira hiyo hiyo, Mamlaka zinatakiwa ziwawajibishe watu wote wanaohusika kwenye hiyo michongo kwa matumizi mabaya ya madaraka, uzembe kazini, uvunjaji wa katiba, kula njama na uhujumu uchumi.
3. Baada ya PCCB, kufuta kesi 300 za michongo, hatua gani zimechukuliwa kwa wachongaji?