... mwamba katu-let down kinoma; hasa kwenye cross-exam ndipo macho na masikio yetu huelekezwa badala yake ka-mute mazima.
Baada ya kuahirishwa kwa muda kwaajili ya mapumziko sasa muda si mrefu kesi hiyo itaendelea tena
Jaji ameshaingia mahakamani kwa ajili ya kuendelea na kesi na kwasasa ni upande wa utetezi kumhoji shahadi kuhusiana na ushahidi aliotua
Shahidi aanaza kuhojiwa na wakili wa utetezi Jeremiah Mtobesya
Wakili: Shahidi Nilisikia unasema mnafabya audit ya mifumo Ni sahihi?
Shahidi: Ni sahihi.
Wakili: Ni mifumo ya Nini?
Wakili: Mifumo inayotumika kuhifadhi taarifa.
Wakili: Nitakuwa sahihi nikisema audit unafanya na IT Department na kampuni za audit?
Shahidi: Inategemea
Wakili: Kwenye Ushahidi wako ulielezea kuwa ulifanya kazi kwenye IT Department?
Shahidi: Hapana.
Wakili: Mheshimiwa Jaji naomba nipatiwe kielelezo namba 15 na 16 vilivyolewa na upande wa mashtaka.
Wakili Mtobesya anapewa vielelezo hivyo na kumpatia shahidi.
Wakili: Mheshiwa Jaji narejea katika kielelezo namba 15 ambayo ni barua ya uchunguzi wa kisayansi kutoka Jeshi la Polisi iliyotumwa Airtel kuomba taarifa za wateja, ieleze mahakama imeandaliwa chini ya kifungu namba ngapi?
Shahidi: Imeandaliwa chini ya kifungu namba 34 chini ya sheria ya makosa ya mtandano.
Wakili: Katika shughuli zako za kila siku ulishawahi kukutana na Sheria hiyo?
Shahidi: Ndio.
Wakili: Huwa mnalindaje taarifa za wateja wenu?
Shahidi: Mteja kwetu ni mtu muhimu hivyo tunayemheshimu na kumlinda na hatuwezi kutoa taarifa ya mteja bila muongozo wowote au court order na ndio maana tunatoa taarifa kwa taasisi husika.
Wakili: Kama kweli mnalinda taarifa za wateja wenu kwanini mmetoa taarifa kwa hawa wateja watatu?
Wakili: Kwa mujibu wa sheria ya makosa ya mtandao, kifungu cha 34 (1) Mheshimiwa Jaji mimi nilitenda majukumu yangu kwa mujibu wa sheria na miongozo mwingine.
Wakili: Sawa mwanasheria, sasa kwanini mlitoa taarifa za wateja wenu?
Shahidi: Mimi nilitekekeza majukumu yangu kwa mujibu wa sheria na miongozo iliyopo na sio kwamba natumia sharia… zipo sheria nyingi ambazo zimetumika hapa kutekeleza majukumu yangu.
Wakili: Kwa maelezo yako, hizi taarifa za wateja zinazosajikiwa na kuingizwa na msajili, je Msajili anaweza kuonekana kwenye hizo taarifa? Yaani kwamba Mtobesya amesajiliwa na mtu flani? Msajili anaweza kuonekana hapo?
Shahidi: Hapana.
Wakili: Sasa mtu anajuaje?
Shahidi: Kimya
Wakili: Ulileta taarifa hapa, zote hazionyeshi jina la msajili sindio?
Shahidi: Ndio.
Wakili: Niliona unaongea kwa umaridadi sana, ulimueleza Jaji kuwa wewe ulishakuwa msajili wa line?
Shahidi: Hapana.
Wakili: Unafahamu watu wanaoitwa hackers?
Shahidi: Nina ufahamu nao.
Mtobesya: Unawaelewaje?
Shahidi: Nawaelewa ni wale watu wanaoingilia mifumo ya taarifa.
Mtobesya: Ikiwemo data?
Shahidi: Ndio
Wakili Mtobesya: Ulisema baada ya kukamilisha taarifa hizo, ulienda kuhojiwa Central Polisi Dsm na Inspekta Swilla je ilikuwa ni tarehe gani? Kama unakumbuka.
Shahidi: Sikumbuki kama nitapewa maelezo hayo itakuwa vizuri.
Mtobesya: Unakumbuka ilikuwa tarehe ngapi?
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji tunaomba Question statement ya shahidi.
Mtobesya: Haya soma hiyo statement kuanzia kwenye maelezo yako.
Shahidi: Nakumbuka 2/7/2020 nilipokea barua kutoka Idara ya uchunguzi wa Sayansi ya Polisi iliomba niwapatie taarifa ya miamala ya fedha na usajili wa namba.
Mtobesya: Sasa nita refer kwenye hayo maelezo yako, sasa mueleze Jaji kama ulisema katika ushahidi wako asubuhi kuwa wewe access ya kuingia katika mifumo.
Shahidi: Hapana Sikusema.
Mtobesya: Nilisikia ulisema kwenye ushahidi wako kuhusu ubora ya mifumo wakati wa kuprint, je kwenye maelezo yako uliyotoa polisi hayo maneno yapo hapo kwenye hiyo karatasi?
Shahidi: Hapana.
Mtobesya: Ungependa hayo maelezo yako uliyoyasoma sasa hivi yaingie kwenye rekodi za Mahakama?
Shahidi: Ningepewa muda niweze kushauriana na upande wa mashtaka.
Mtobesya: Hutaki?
Shahidi: Nimeshatoa vielelezo, hivyo siwezi kusema chochote.
Mtobesya: Kwa hiyo nyaraka hii nyiingie au ikatae?
Shahidi: Nimeshasema tayari.
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba guidance (Muongozo) wa mahakama.
Jaji: Kwani wewe umesikiaje?
Mtobesya: Mimi naomba ajibu swali langu shahidi.
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji sisi tunaomba kui' move Mahakama kuwa tunaomba maelezo yake aliyoyatia Polisi yaingie katika taarifa za mahakama kwa kutumia Kifungu cha 154 na Pamoja na 164 (1)C ya Sheria ya Ushahidi.
Mtobesya: Hizi ni taarifa muhimu kwetu, hivyo hazikutakiwa kuwa hold.
Mtobesya: Tena shahidi anafanya hivyo akiwa katika witness box.
Mtobesya: Ukisoma Kifungu Cha 246 cha CPA, Kina sema Mshitakiwa apewe The Whole Substance, there is a reason to that
Mtobesya: Kwa kusema hayo Mheshimiwa Jaji naomba statement iweze kuingizwa ili niweze kuitumia kum contradict.
Mtobesya: Hivyo tunaomba taarifa hizi ziingie kwenye record ya mahakama.
Akijibu hoja ya Mtobesya, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Robert Kidando: Hiyo sio contradiction.
Kidando: Mheshimiwa Jaji, shahidi aliyopo mahakamani ameulizwa mambo manne na katika majibu yake ametanguliwa na neno kuwa sikusema, sasa suala la kujiuliza hapa suala la kuwa hakusema linakinzana vipi na nini?
Kidando: Sisi tunaona wakili Mtobesya ombi alilowasilisha halina mashiko kisheria na ameshindwa kufikia kikwazo hicho cha kuonyesha consistent na ndio maana anaomba statement hiyo aiote kama kielelezo na sisi tunasema hana nafasi ya kuitoa questions statement hiyo ya shahidi kwa Mahakama.
Kidando: Tunasisitiza huu ni upande wa cross examination, hivyo Wakili msomi Mtobesya angejielekeza katika kuuliza maswali.
Kidando: Hivyo tunaomba ombi hilo likataliwe na tuendelee na cross examination kwa mujibu wa sheria.
Wakili wa Serikali Mwandamizi, Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji nina nyongeza kidogo, vifungu alivyotumia wakili msoni Mtobesya sio sahihi.
Hilla: Mheshimiwa Jaji mwenzangu Wakili Chavula nae anataka kuongezwa kujibu hoja hiyo.
Hata hivyo kabla ya Chavula haijaanza kujibu hoja ...amesimama Mtobesya na kusema Mheshimiwa Jaji naomba kuondoa pingamizi hili.
Kidando: Mheshimiwa Jaji sisi tumesha- concede kwa kiasi kikubwa, hivyo tunaomba wao waendelee tu ...Wala wasi- withdraw nyaraka hiyo.
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji mimi naomba ku- withdraw sina nia ya kuendelea na pingamizi hilo.
Kicheko mahakamani hahahhahaha.
Kibatala anasimama na kwenda kujadiliana na mawakili wa upande wa mashtaka.
Kibalata: Mheshimiwa Jaji naomba sekunde 30 kujadiliana na wenzangu.
Baada ya majadiliano hayo, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Abdallah Chavula anasimama na kuridhia kuwa upande wa mashtaka wamekubaliana kuondoa pingamizi hilo.
Wakili Chavula: Mheshimiwa hatuna pingamizi juu ya wenzetu kuondoa ku-withdraw nyaraka hiyo.
Jaji: Kama walichoomba upande wa utetezi na kuridhia upande wa mashtaka naondoa nyaraka hii.
Mawakili wa pande zote wanasimama na kuinamisha kichwa kwa Jaji kuashiria kuwa wamekubali.
Baada ya Jaji kuondoa pingamizi hilo, ameelekeza wakili Mtobesya kuendelea kumhoji shahidi wa upande wa mashtaka.
Mtobesya: Sasa mliwezaje kulinda taarifa za watu wengine ambao wamefanya miamala kwenye namba za simu hizo?
Shahidi: Taarifa hizi zimeombwa na Mamlaka husika ambayo iko authorized (Jeshi la Polisi) na hakuna namna ambavyo tungefanya kwa kuwa mfumo wetu ulitoa taarifa kuanzia Juni 1, 2020 hadi Julai 31, 2020.
Mtobesya: Kwa taarifa hiyo mnatambua hiyo ni taraarifa ya mtu fulani au hakiwezi?
Mtobesya: Kupitia mfumo huo wa taarifa hiyo inaweza kueleza mtu flani alituma hela kwa sababu gani?
Shahidi: Hapana haiwezi
Mtobesya: Mheshimiwa kwa upande wangu ni hayo tu.
Kwa Sasa i zamu ya Wakili Mallya kumuuliza shahidi.
Mallya: Shahidi unafahamu Mbowe anashtakiwa kwa kesi gani?
Shahidi: Sifahamu.
Mallya: Sasa Mimi nakufahamisha Mbowe anatuhumiwa kutumia fedha hao wenzake kwa ajili kufanya matukio ya ugaidi na upo hapa kwa ajili ya hilo.
Shahidi: Kimya
Mallya: Barua ya Julai 2, 2021 kutoka Jeshi la Polisi, iliomba idadi ya miamala ya fedha ya watu wangapi?
Shahidi: Haijafafanua.
Mallya: Muamala wa mwisho inaonyesha ilitumiwa Julai 31, 2020 kiasi cha Sh80, 000 kwenda kwa Bwire, sasa mbona namba nyingine hukuitaja hapa mahakamani?
Shahidi: Oversight
Mallya: Sasa nikwambie tu hiyo namba ya Bwire alikuwa ametuma hela ACP Kingai Sh80, 000 mbona hukutuelezea hapa mahakama wakati unatoa ushahidi? kuhusiana na muamala huo wa Bwire kumtumia Kingai pesa hiyo?
Shahidi: Nilipitiwa
Mallya: Unafahamu kuna miamala ya waziri wa zamani ulinzi alikuwa anamtumia fedha Bwire? kwa sababu wamefanya kazi wote?
Jaji: Mhh
Jaji: Hizo information umezipata wapi?
Mallya: Kutoka kwa watuhumiwa mwenyewe (Bwire)
Jaji: Chini ya kiapo?
Mallya: Kimya
Jaji: Unafikiri mwenyewe atakuja kutoa ushahidi hapa mahakama.
Mallya: Hatuzuiwi Mheshimiwa Jaji kumuita aje kuwa shahidi wetu.
Jaji: Mimi nafikiri ujikite kuuliza maswali kwenye ushahidi uliotolewa hapa mahakakani, kuliko kuongoza vitu ambavyo havipo hapa.
Wakati wa majibishano hayo, wakili Kidando amesimama na kabla ya kuongea.
Jaji anamuelekeza Mallya ajielekeze kwenye ushahidi.
Kidando: Mheshimiwa Jaji tunapinga maswali hayo ya wakili Mallya kumuuliza shahidi hata kama anajua.
Mallya: Sawa mheshimiwa Jaji nashukuru nitajielekeza.
Mallya: Sasa Shahidi Oversite yako (Yaani kupitiwa) unafikiri nani atakuja ku-cover?
Shahidi: Sifahamu.
Mallya: Je taarifa zenu za usajili (Format) zina fanana
Shahidi: Ndiyo muundo au format unafanana
Mallya: Sasa hapa umesajili watu mmoja anaitwa Mbowe, Katika Kielelezo namba 18 Je unaweza kuona sehemu ya juu imeandikwa Kanda, Je Kanda gani
Shahidi: Morogoro
Mallya ukitizama pia taarifa za Denis Urio, sehemu ya Kanda kwa Denis Urio, ipo au haipo
Shahidi: Ipo kwa Denis Urio
Mallya: Sasa angalia kielelezo namba 17 cha Freeman Mbowe kama Kuna sehemu ya kanda au mnapendelea Wanajeshi.. Ukiona Mwambie Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Haionekani
Mallya: Haionekani au haijaandikwa
Shahidi: Haijaandikwa
Mallya: Ni sahihi sasa kwa kuwa mtu anaitwa Freeman Mbowe, haina Sehemu imeandikwa Kanda ni sahihi hizo taarifa zipo tofauti
Shahidi: Ndiyo neno kanda halija onekana
Mallya: Ulitoa hiyo Clarification wakati wa Chief Examination
Shahidi: Sikuulizwa
Mallya: Nakushauri jibu ulitoa au hukutoa?
Shahidi: Nimeshajibu
Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba ajibu swali langu sasa
Jaji: Umeelewa swali?
Shahidi: Sikutoa Mheshimiwa Jaji
Mallya: Kwenye kielelezo namba 20 muamala wa tarehe 20 Julai 2020, Ulisema P to P maana yake ni nini
Shahidi: Airtel kwemda Airtel
Mallya: Na hiyo cash in..?
Shahidi: Namba ya muhusika ambayo imepokea?
Mallya: Ilipokea kutoka kwa wakala itaandikaje..?
Shahidi: zote zinaonekana kama Cash In. Mteja Kwa Mteja ni P to P
Mallya: Sasa mimi Interest yangu ni tarehe 20 Julai 2020, cash in ni Wakala
Shahidi: Kuna ufafanuzi
Mallya: Ufafanuzi utampatia dada yangu Kitale, mie nataka majibu
Mallya: Katika hawa washitakiwa wanne kuna hata mmoja kasajiliwa kama Wakala?
Shahidi: Mimi sifahamu
Mallya: Mheshimiwa Jaji nina maswali bado kwa shahidi wetu, na muda umetutupa mkono, ningeleta ombi kwako tuhairishe hadi Kesho tuendelee na Mahakama
Kibatala: Mheshimiwa Jaji kabla ya kufunga naomba kutoa tarifa kuwa kutokana na nature ya ushahidi wake tunaweza kesho tukamaliza mapema kuhoji, hivyo tunawaomba wenzetu upande wa mashtaka kama wana shahidi ambaye anaushahidi mfupi wamlete ili tuweze kuendelea naye.
Kidindo: Tunaendelea na mawasiliano na shahidi wetu kwa sababu hadi mchana alikuwa ametupa taarifa kuwa anauguliwa na baba yake mzazi, hivyo tutaendelea kuwasiliana naye ili kujua kama hali yake inaendelea vizuri ili aje.
Jaji: Naahirisha kesi hii hadi kesho, Januari 14, 2022 saa 3:00 asubuhi.
Jaji: Naelekeza shahidi kesho ufikie mahakmani hapa na washtakiwa wataendelea kuwa chini ya usimamizi wa magereza.
Niwatakie jioni njema.