Yaliyoko Simu2000 yanaumiza na kuhuzunisha sana

Yaliyoko Simu2000 yanaumiza na kuhuzunisha sana

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Haya mambo yakiendelea hivi na kwingine ni wazi Tanganyika inarudishwa utumwani

Mwanzoni mwa wiki hii kituo kizuri cha daladala cha Mawasiliano Simu 2000 kilifungwa rasmi na fremu zote zinazohudumia kutoka ndani ya kituo kuvunjwa ili kumpisha mwekezaji mpya anayetaka kuweka karakana ya mabasi ya mwendokasi

Kwa siku tatu mfululizo pale Simu 2000 ilikuwa ni zogo hasa nyakati za jioni kwakuwa magari ya abiria toka kona zote za jiji yalikuwa yanasimama barabarani kupakia na kushusha abiria

Sasa zimechukuliwa hatua sijui ni za dharura ama la, 'kutengeneza kituo kipya' ndani ya soko la vyakula na matunda lililoko pembeni ya kituo

Imagine sehemu ya soko hilo ilivyo ndogo na isiyo na miundombinu ya magari hasa ya abiria sasa ni sehemu ya kupakia na kushusha abiria 🤔😭
Mahali palipokuwa panafanyika mnada wa mahindi, miwa nk sasa ni maegesho ya daladala kupakia na kushusha abiria

Hapana zege, hapana lami, hapajasindiliwa ni mavumbi kwenda mbele na zile vurugu za daladala
Usalama na usafi wa vyakula vinavyouzwa hapo sasa uko shakani kutokana na miundombinu hafifu, vurugu za daladala na wingi wa watu

Wafanyabiashara waliokuwa ndani ya kituo nao sasa wanabanana na wengine hapo sokoni
Sasa hivi hali ni hiyo ya vumbi je ikinyesha mvuta patakuwaje?

Dhana ya maendeleo na maamuzi kengeufu

Sijui huyo mwekezaji ana nguvu kiasi gani na sina hakika walioruhusu kituo kigeuzwe karakana kama waliwaza kwa weledi, hekima na uzalendo.. Kuondoa watu wote wale na uwekezaji wote ule na kusababisha adha ya usafiri na ongezeko la gharama kwa abiria na usumbufu mwingine mwingi ni maamuzi yenye kutatiza mno na shaka kubwa juu ya hekima ya waliobariki hilo zoezi!

Hata hivyo kama ilibidi kupisha maendeleo mengine basi haya yaliyokuwepo tayari yangetafutiwa mbadala mapema na kabla ya haya mapya. Nina hakika mwekezaji mpya kalipa pesa kulipata lile Eneo, sasa kwanini pesa hizo zisitumike kutengeneza mbadala wa kilichokuwepo ili kuepusha usumbufu, hasara na adha kwenye maisha?

Kwanini mwananchi mwenye nchi yake anayepaswa kupewa heshima, thamani na kipaumbele namba moja anageuzwa kama raia wa daraja la pili? Mtumwa anayepaswa kutii kila agizo bila kuhoji hata kama haki zake za msingi zinapokwa? Aende wapi sasa🥺

Pale Simu 2000 kuna kila aina ya harufu ya uvundo mkali wa maadili na uzalendo.. Waliofanya hiyo dili wakakubali sijui walipewa nini huko na walisainishwa mikataba ya aina gani huko! Maana ni wazi mwenye eneo kacharuka anataka eneo lake na wao walikuwa bado hawajajiandaa kulikabidhi kwake!

Soma Pia:
Wanaoumia na kuteseka sasa ni wananchi wenye nchi yao! Lakini la kushangaza zaidi vyombo vya habari karibia vyote hakuna hata kimoja kilichoripoti hali ilivyo simu 2000 .

Je wametishwa? Na nani?
Kama mwekezaji kafaulu kufanya hivyo pale Mawasiliano Simu 2000 tujiandae kwa machungu mengi zaidi.

Tanganyika...!🤔🙇🏿‍♂
downloadfile-1.jpg
 

Kwani pale ilipokuwa stendi ya mabasi ya mikoani zamani (Ubungo) jirani na jengo la TBS si wana eneo kubwa tu ni la nini hasa?
Pale manapageuza maegesho.. Simu 2000 wanataka kuweka karakana
Hii stand mpya ya mwenge lin itaanza rasmi? Naona sahv inatumika partially - Naskia pia stand ya makumbusho haina mda mrefu itaondolewa
Ile ilikuwa stand ya muda tuu. Japo huo muda umekuwa mrefu kuliko ilivyo tarajiwa
 
Haya mambo yakiendelea hivi na kwingine ni wazi Tanganyika inarudishwa utumwani

Mwanzoni mwa wiki hii kituo kizuri cha daladala cha Mawasiliano Simu 2000 kilifungwa rasmi na fremu zote zinazohudumia kutoka ndani ya kituo kuvunjwa ili kumpisha mwekezaji mpya anayetaka kuweka karakana ya mabasi ya mwendokasi

Kwa siku tatu mfululizo pale Simu 2000 ilikuwa ni zogo hasa nyakati za jioni kwakuwa magari ya abiria toka kona zote za jiji yalikuwa yanasimama barabarani kupakia na kushusha abiria

Sasa zimechukuliwa hatua sijui ni za dharura ama la, 'kutengeneza kituo kipya' ndani ya soko la vyakula na matunda lililoko pembeni ya kituo

Imagine sehemu ya soko hilo ilivyo ndogo na isiyo na miundombinu ya magari hasa ya abiria sasa ni sehemu ya kupakia na kushusha abiria 🤔😭
Mahali palipokuwa panafanyika mnada wa mahindi, miwa nk sasa ni maegesho ya daladala kupakia na kushusha abiria

Hapana zege, hapana lami, hapajasindiliwa ni mavumbi kwenda mbele na zile vurugu za daladala
Usalama na usafi wa vyakula vinavyouzwa hapo sasa uko shakani kutokana na miundombinu hafifu, vurugu za daladala na wingi wa watu

Wafanyabiashara waliokuwa ndani ya kituo nao sasa wanabanana na wengine hapo sokoni
Sasa hivi hali ni hiyo ya vumbi je ikinyesha mvuta patakuwaje?

Dhana ya maendeleo na maamuzi kengeufu

Sijui huyo mwekezaji ana nguvu kiasi gani na sina hakika walioruhusu kituo kigeuzwe karakana kama waliwaza kwa weledi, hekima na uzalendo.. Kuondoa watu wote wale na uwekezaji wote ule na kusababisha adha ya usafiri na ongezeko la gharama kwa abiria na usumbufu mwingine mwingi ni maamuzi yenye kutatiza mno na shaka kubwa juu ya hekima ya waliobariki hilo zoezi!

Hata hivyo kama ilibidi kupisha maendeleo mengine basi haya yaliyokuwepo tayari yangetafutiwa mbadala mapema na kabla ya haya mapya. Nina hakika mwekezaji mpya kalipa pesa kulipata lile Eneo, sasa kwanini pesa hizo zisitumike kutengeneza mbadala wa kilichokuwepo ili kuepusha usumbufu, hasara na adha kwenye maisha?

Kwanini mwananchi mwenye nchi yake anayepaswa kupewa heshima, thamani na kipaumbele namba moja anageuzwa kama raia wa daraja la pili? Mtumwa anayepaswa kutii kila agizo bila kuhoji hata kama haki zake za msingi zinapokwa? Aende wapi sasa🥺

Pale Simu 2000 kuna kila aina ya harufu ya uvundo mkali wa maadili na uzalendo.. Waliofanya hiyo dili wakakubali sijui walipewa nini huko na walisainishwa mikataba ya aina gani huko! Maana ni wazi mwenye eneo kacharuka anataka eneo lake na wao walikuwa bado hawajajiandaa kulikabidhi kwake!

Soma Pia:
Wanaoumia na kuteseka sasa ni wananchi wenye nchi yao! Lakini la kushangaza zaidi vyombo vya habari karibia vyote hakuna hata kimoja kilichoripoti hali ilivyo simu 2000 .

Je wametishwa? Na nani?
Kama mwekezaji kafaulu kufanya hivyo pale Mawasiliano Simu 2000 tujiandae kwa machungu mengi zaidi.

Tanganyika...!🤔🙇🏿‍♂View attachment 3100763
Walidhan uongozi wa hovyo utawaathiri Chadema tu.

Na bado
 
Back
Top Bottom