Unachosimulia kinaendana na kisa kilichomkumba 'mtu wangu mmoja'. Yeye tulikua naye mjink, mimi nikawa nimekaa grocery, nakunywa huko mwanza, mtaa wa ghana. Yeye akaniambia kuna nguo anahitaji kununua. Akaenda duka la nguo lipo jirani na hiyo grocery, kuingia akamkuta dada amevaa dizaini kama huyo na macho kama hayo unayoyasema na yanang'aa sana. Akaogopa akaondoka dukani kwa woga, alipotoka tu akakutana na muuzaji mwingine wa hilo hilo duka, lakini huyu ni wanaume. Akamsihi arudi anunue wala asiogope. Basi kiuoga akanunua hiyo nguo. Huku huyo mwanamke mwenye macho paka ndio muuzaji. Aliporudi nilipo, kunisimulia nikamwambia hiyo nguo itupe.
Nadhani ni 'utaalamu' wa kibiashara.