Marya alimzaa Yesu ana miaka13,na kabla ya alikuwa na mchumba Yusufu,fikiria alikuwa na miaka mingapi alipoanza mambo hayo ya ukubwani.
Ndio wanaoana wanaume kwa wanaume?
Hivi ulishikwa mkono na mtu.....??
tatizo ni elimu ya madrasa
hawabakani hao, wanaoana kwa ridhaa yao, mtoto wa miaka 9 ana ridhaa ya kuolewa na babu wa miaka 54?
Dini ya Allah imeweka sheria za kuhukumiana. Unapopitishiwa hukmu duniani maana yake siku ya Akhera ile dhambi imefutwa huendi kusomewa huko. Sasa wewe dini yako si imekufundisha dhambi zako kazibeba yesu? Sasa confession ya nini kama dhambi zimesamehewa?
lakini haijaripotiwa popote muumini kapigwa hadi damu kumchuruzika kwa sababu kavaa kimini kanisani mkuuMbona uulizi kwanini makanisa mengi sana huko Tanzania Bara yanazuia kwa nguvu zote waumini kuingia na vimini wakti wa ibada? Je hujui kwa nini?
hapa tuangalie zaidi ya kufikiria "Wakristo" wanapigwa maana katikati ya wanaokula kunawasioamini chochote na wapo Waislam pia ambao kwa hali zao, maamuzi yao au vinginevyo wanakula.
tuzungumzie kupigwa kwa "watu" wanaokula.
leo asubuhi nilikutana na mama mmoja muislam (nilimgundua baada ya kuona amejitanda ushungi mweupe) anauza vitafunwa baada ya kununua nikamuuliza kwanini auze vyakula ndani ya mwezi mtukufu wakati wenzie hadi Hoteli wanafunga? akajibu "mwanangu kufunga ni imani yangu na Allah anatutaka tukifunga tufanye kazi, hii ndio sehemu ya kupata rizki ya wanangu sasa nisipouza itakuwaje" nikajiongezea jibu kichwani ...hata futari hutapata...
Tunapowaadhibu wanaokula kwakuamini tunafanya lililosahihi (sijui kama ndivyo ama sivyo) tunawaadhibu hata watoto wadogo na wategemezi wa wale wanaouza vile vyakula huko majumbani.
niliwahi kusikia toka kwa marafiki zangu na siku moja kwenye redio (sikumbuki stesheni gani) kwamba watoto wadogo hawafungi. kama ndivyo kwa kumnyima mama ama baba yake njia ya kujipatia kipato hatuoni tunakosea?
nakaribisha kusahihishwa
Na nyie na watoto zenu wanaolawitiana na mapadri na maaskofu kanisani mpaka Umoja wa Mataifa unapiga kelele si mnafanya kwa ridhaa yenu? vipi Umoja wa Mataifa uwaingilie?
Nimestushwa na kuogopa tena nikalazimika kuisoma Katiba ya Zanzibar mara mbili.
Leo Waislamu wa Zanzibar wanawavamia na kuwapiga vibaya Wazanzibar wenzao ambao sio Waislamu kwakuwa tu wanakula kwa mama lishe mchana mda ambao wale waislamu wanakuwa wamefunga,
Vipigo vimeenea kila kona ya mji wa Zanzibar na uhasama unakua kila kukicha, serikali ipo kwenye mfungo mtukufu, Wakristo hawa Wazanzibar hawana msaada, nani awaokoe vijana wa kikikristu ambao hawajao wanaotegemea kwa mama lishe na migahawani kupata mlo wao? Nao wafunge???
Nini tutarajie majibu ya wahanga hawa kama sio gharika? Serikali inasubiri kuunda tume baada ya mauaji??
Nimeisoma na kuipekua katiba ya Zanzibar kuona kama kuna kifungu kinachowapa haki waislamu kudhibiti uhuru wa watu wengine,
Zaidi nilitaja kujua kama Zanzibar ni nchi ya kidini au ni nchi inayotawaliwa kwakufuata sharia.
Sehemu mhimu ya katiba ya Zanzibar ni hii hapa, jioneeni kama ni haramu kula chakula hadharani nchini Zanzibar.
SURA YA KWANZA- ZANZIBAR
Sehemu ya Kwanza
1.Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.
2. Zanzibar ni miongoni mwa Nchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 2A. Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali, Rais aweza kuigawa Zanzibar katika Mikoa, Wilaya na maeneo mengineyo kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
3.(1) Kutakuwa na Muhuri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambao alama yake itakuwa kama itavyokubaliwa na sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
(2) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itakuwa na uwezo wa kuweka kitu chochote kitachokuwa kielelezo cha Serikali kama itavyokubaliwa na sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
4. Katiba hii ni Katiba ya Zanzibar na itakuwa na nguvu za kisheria nchini kote na isipokuwa kutokana na kifungu 80 ikiwa sheria yoyote inatofautiana na Katiba hii, basi Katiba hii ndiyo itayokuwa na nguvu na sheria hiyo itakuwa batili kwa kiwango kile ambacho kinahitilafiana.
5. Zanzibar itafuata mfumo wa Kidemokrasia wa Vyama Vingi vya Siasa wenye kuheshimu utawala wa sheria, haki za binaadamu, usawa, amani, haki na uadilifu.
5A.(1) Zanzibar itafuata mfumo wa mgawanyo wa madaraka kati ya mamlaka tatu, Mamlaka ya Utendaji, Mamlaka ya Kutunga Sheria na Kusimamia Utekelezaji wa Shughuli za Umma na Mamlaka ya Kutekeleza Utoaji Haki.
(2) Mamlaka ya Utendaji ni Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mamlaka ya kutunga Sheria na Kusimamia Utekelezaji wa Shughuli za Umma ni Baraza la Wawakilishi na Mamlaka ya Kutekeleza Utoaji Haki ni Mahkama.
(3) Hakuna mamlaka itakayoingilia Mamlaka nyengine isipokuwa kama na kwa kadri ilivyoelezwa katika Katiba hii.
Mambo mengine yanataka utumie Hekima siyo kwasababu sheria ni yako utaacha gari ikugonge. Inajulikana wazi asilimia kubwa saana ya wananchi wa Zanzibar ni waislamu, sasa kwanini tusikae kwa kuheshimiane na muda wenyewe ni Mwezi mmoja tu kama unataka kula, usile hadharani wakati unajua wenzako wanafunga na ni mwezi wao mtukufu.
Kwa hiyo kuvaa kimni ndo unalinganisha na kula?? Umeona kwenye kimini muislamu analazimishwa..??Mbona uulizi kwanini makanisa mengi sana huko Tanzania Bara yanazuia kwa nguvu zote waumini kuingia na vimini wakti wa ibada? Je hujui kwa nini?
Umenena vyema mkuu. Hawa watu nashindwa kuelewa na siamini kama wanaofanya haya ni waislamu kamiliki, mimi nahisi ni mamluki. Na huyo mama anajua nini maana ya uislamu na kufunga. Nini maana ya kufunga kama unaathiri uhuru wa watu hasa katika mambo ya kula mgahawani? Je kuwaadhibu watu kwa kula ndio mfungo? Mbona mnakwaza watu? Ndio maana ya mfungo? Kama wewe umeamua kufunga toka moyoni kwa nia ya kuijenga imani yako, kula kwangu kunaathiri nini msimamo wako? Au wenzetu mnakuwa mmeamua kubadilisha ratiba ya chakula? Mchana kuwa usiku mnaona wivu anayekula mchana anafaidi. Msitake kila mtu awe bundi bwana. MBONA WAISLAMU WENZENU WANAPIKA VYAKULA MAHOTELINI HAMUWAPIGI VIBOKO KWA KUKIUKA UTARATIBU?? Nyie mnafikiri hizo hela za ftari waumini wenzenu watapata wapi? Hainingii kichwani kama wanaopiga viboko wakristo ni waislamu. Hawa na wale wanaotetea wanaopiga viboko wenzao kwa kula mchana ni vibaka waliojivika kanzu la uislamu. What a fake world!