Yanayofanyika viwandani Tanzania ni utumwa. Kazi ngumu, maslahi duni. Serikali haina mpango na wananchi wake, inachoangalia ni kodi tu

Yanayofanyika viwandani Tanzania ni utumwa. Kazi ngumu, maslahi duni. Serikali haina mpango na wananchi wake, inachoangalia ni kodi tu

Kuna kiwanda kiko Pale Keko karibu na ukumbi wa DDC nadhani ni cha cello. Malipo kwa siku ni sh. 3500 kwa siku ilikuwa kwa muda mrefu. Sasa ni sh. 4000, kazi masaa 12 yaani lisaa limoja sh. Mia tatu na centi.

Viwanda vingi malipo ni sh. Elfu 5000 kwa siku, hii maana yake lisaa limoja la kazi ni sh. 400. Viwanda vyenye majina makubwa malipo kwa siku ni sh. 7000 hii maana yake lisaa limoja sh mia 6.

Hata kama ni non skilled labor ni haki Mtanzania alipwe sh. Mia 4 kwa lisaa limoja? Ni utumwa wa wazi uliopata baraka za serikali.

Hawa mabilionea wetu akina Bakhressa na Mo huwabebesha Watanzania viroba vya unga wa ngano kwa sh. 50 au pungufu kwa kiroba kimoja. Ni utumwa.

Nimewahi kufanya kazi siku moja tu kwa wahindi Kariakoo ni zaidi ya utumwa , kula juu yangu, nauli juu yangu malipo 7500 kwa siku na kazi very risk. Kazi ya kupeleka mizigo ghorofa ya 12 kutoka chini. Sikurudi tena.
Alafu utasikia ohhh sijui Mo na Bakresa ni vichwa vya biashara,wakati ni wanyonyaji wakubwa.Utajiri wao unatokana na dhuluma na jasho jingi sana la walalahoi.
 
Baada ya kumaliza chuo 2018, nlikua na jamaa angu tumemaliza wote, tukashauriana tutafute vibarua vya kusogeza maisha ,tukaingia keko pale lilipo Go-down la Monalisa,

Adse sio mchezo pale kibarua kwa siku unapewa 4000, hizo kazi zao km una roho ndogo unaweza ukazima

Wana kawaida yao asubuhi kabla hamjaanza kazi mnaenda kupanga mstari
Kiongozi anasema

"Good one Good" wafanyakazi mnaitikia "Good"

Baada ya hapo ni kupigika mpaka jioni
 
Uko sahihi mkuu. Kuna wapakistan na wahindi pale Deira, Dubai wanaishi maisha ya hovyo sana na kupigishwa kazi balaa. Kuna mmoja ni fundi cherehani aliniambia nikiweza kumlipa mshahara kama laki 9 na kumtafutia work permit yupo tayari kuja na kupiga kazi kwenye ufundi cherehani kama nitafungua hiyo biashara. Kazi yake ni balaa na nusu. Ni kipaji.

mkuu wale wabangladesh pale deira ni hatari sana kwa kushona, yani zaidi ya hatari. Jamaa wanapiga kazi si mchezo.
 
Kuna kiwanda kiko Pale Keko karibu na ukumbi wa DDC nadhani ni cha cello. Malipo kwa siku ni sh. 3500 kwa siku ilikuwa kwa muda mrefu. Sasa ni sh. 4000, kazi masaa 12 yaani lisaa limoja sh. Mia tatu na centi.

Viwanda vingi malipo ni sh. Elfu 5000 kwa siku, hii maana yake lisaa limoja la kazi ni sh. 400. Viwanda vyenye majina makubwa malipo kwa siku ni sh. 7000 hii maana yake lisaa limoja sh mia 6.

Hata kama ni non skilled labor ni haki Mtanzania alipwe sh. Mia 4 kwa lisaa limoja? Ni utumwa wa wazi uliopata baraka za serikali.

Hawa mabilionea wetu akina Bakhressa na Mo huwabebesha Watanzania viroba vya unga wa ngano kwa sh. 50 au pungufu kwa kiroba kimoja. Ni utumwa.

Nimewahi kufanya kazi siku moja tu kwa wahindi Kariakoo ni zaidi ya utumwa , kula juu yangu, nauli juu yangu malipo 7500 kwa siku na kazi very risk. Kazi ya kupeleka mizigo ghorofa ya 12 kutoka chini. Sikurudi tena.
Muhimu tujiulize matajiri wakubwa tanzania wanawalipaje wafanyakazi wao. Kuanzia Dewji, Bakhresa, Rostam, Manji na Marehemu Mzee Mengi. Unataka kuniambia Twiga cement inaingiza hela kuliko Bakhresa ? Cocacola Tanzania inaingiza hela kuliko Dewji ? Hii ni mifano ya makampuni machache ambayo yanalinda haki za mfanyakazi japokuwa hazina mapato makubwa kuliko kampuni za Matajiri wa Tanzania. Wafanyakazi hawathaminiwi kwa sababu matajiri wanawahonga watu wachache ili waishi bila kufuata sheria.
 
Aisee umenikumbusha SBL iliopo nyakato mwanza waliingiza magari mawili yamejaza sukari tukapewa kibarua cha kushusha sukari kwa malipo ya 6000 tu, aisee mimi nilitoka niliwambia siwezi[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] kazi za viwandani.ni.ngumu baraa afu.malipo ni.kiducho yaani toka asbh hadi jioni unashusha makereti ya soda kwa malipo ya 6000 [emoji16]
 
Aisee umenikumbusha SBL iliopo nyakato mwanza waliingiza magari mawili yamejaza sukari tukapewa kibarua cha kushusha sukari kwa malipo ya 6000 tu, aisee mimi nilitoka niliwambia siwezi[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] kazi za viwandani.ni.ngumu baraa afu.malipo ni.kiducho yaani toka asbh hadi jioni unashusha makereti ya soda kwa malipo ya 6000 [emoji16]
Duh ni noma sana..
 
Back
Top Bottom