Yanayojiri ajali ya Lori Stop Over-Kimara: Miili 3 na bodaboda 6 zatolewa, zoezi la kuondoa lori linaendelea

Yanayojiri ajali ya Lori Stop Over-Kimara: Miili 3 na bodaboda 6 zatolewa, zoezi la kuondoa lori linaendelea

Nasema kila siku humu,madereva wapumbavu wengi sana. Wanaendesha kama mbuzi tu hawafuati utaratibu hata wa kusubiri taa.
Waafrika hasa watanzania hakuna wanacho tii barabarani.

Mijitu inajiendea tu pakachu pakachu kama mapanya.
 
====

Saa 10 Usiku: Zoezi la kuondoa lori lililoparamia watu linaendelea


Bado vyombo vya uokoaji vinapambana kulinyanyua lori lililoacha barabara na kuparamia abiria na baadhi ya madereva bodaboda katika eneo la Kimara Stop Over jijini Dar Es Salaam.
=====

Saa Tisa Usiku: Kamanda Polisi Kinondoni, RPC Mtatiro Kitinkwi athibitisha Bodaboda 6 kutolewa


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni RPC Mtatiro Kitinkwi amethibitisha kuwa bodaboda sita zimetolewa chini ya lori ambalo liliacha njia na kuparamia abiria na madereva wa bodaboda katika eneo la Kimara Stop Over jijini Dar es Salaam.

Taarifa ya awali iliyothibitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Albert Chalamila ilieleza kuwa miili ya watu watatu ilitolewa chini ya lori hilo wakati hadi kufikia saa 9:00 Usiku wakati zoezi la uokoaji likiendelea.

=====

Saa Tisa Usiku: Chalamila athibitisha ajali kutoke, Mili 3 yatolewa


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila amethibitisha kuwa miili mitatu imetolewa chini ya lori lililoacha barabara na kuanguka katika eneo la Stop Over Usiku wa kuamkia leo

Zoezi la kuliondoa lori hilo lenye namba za usajili T 908 BYM limeendelea ambapo kwa mujibu wa Chalamila hadi kufika saa 9 Usiku lilinyanyuliwa kwa zaidi ya asilimia 95%.

Pamoja miili hiyo mitatu jumla ya pikipiki Sita zimetolewa baada ya lori hilo kunyanyuliwa kwa asilimia hizo.

=====

Saa saba usiku

Watu kadhaa wanahofiwa kufariki dunia, baada ya lori kuacha njia na kuparamia waendesha bodaboda eneo la Stop Over, Kimara jijini Dar es Salaam.

Mashuhuda walioshuhudia ajali hiyo iliyotokea usiku wa leo Ijumaa, Februari 14, 2025 wamesema huenda lori hilo limefeli breki.

Hadi muda huu ndo police wamefika wanafanya jitihada za kuokoa baadhi ya boda boda waliofunikwa na gari.

Aidha Polisi wametoka hapa kwenda kwa mchina kuomba gari lije lisaidie kuitoa hii gari maana kuna watu chini

Poleni Sana wana kimara-stopOver,
Hapo jirani Kimara Suka ndo home nilikokulia mpk Nmefika kutoka home kwenda kujitegemea😢

maisha ya mwanadamu huwa ni kitu kidogo sana, sometimes!

Ee Mwenyezi Mungu tunaomba utujalie mwisho mwema!
 
hatari tupu. naishi pale, huwa nasema kila siku kuwa mbio hizi za magari , pikipiki , mabasi etc kuna siku zitaleta maafa! spidi huwa ni kubwa mno mpaka unashangaa kuwa huyu si amefika spidi za hivi za nini?
Baadhi ya madereva vichwa ngumu.
 
Ukiniuliza malori yanatoka bandarini yanakuja mjini huku kutafuta nn. Ni Ujinga wa CCM huu. Yan lory litoke kurasini lije ubungo then liende chalinze 😂😂 akili za CCM wanazijua wenyewe
Sasa mkuu yangepita njia gani? Sema mkombozi atakuwa sgr kile kituo cha Kwala kikikamilika! Kwa sasa hivi hakuna mbadala!
 
Hii ajali inasemekana wamekufa watu 17 lakini habari zinaripoti watatu something doesn't add up.
 
Kuna siku nilikuwa hapo ubungo Riverside.

Lori lika angusha kontena, Bahati nzuri kontena hilo lilianguka chini kwenye ule uwazi unaotenganisha barabara mbili.

La sivyo lingeanguka upande wa pili, lingeponda magari na kuua watu.
Hii kama ni mwakajana naikumbuka hii
 
Lori lina breki tatu

Engine Brake
Air Brake
Spring Break

Zinafelije zote ?
Mosi Engine brake sio practical at high speed,
Spring brake ni redundancy system kwenye air brake na inatumia same component za air brake, kwa hiyo kama ni kifaa chenyewe kimefeli (brake chamber drum, disc etc) spring brake na air brake haiwezi kufanya kazi n zitafeli kwa pamoja
Engine brake na air brake zote zinategemea air pressure, kama gari lililkuwa na shida ya ait pressure basi engine brake na air brake zote zinafeli kwa pamoja.
 
Back
Top Bottom