Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ukifika mbezi mwisho kwenyewe ndio hatari zaidiHawataki kuwaudhi wapigakura...
Waafrika hasa watanzania hakuna wanacho tii barabarani.Nasema kila siku humu,madereva wapumbavu wengi sana. Wanaendesha kama mbuzi tu hawafuati utaratibu hata wa kusubiri taa.
====
Saa 10 Usiku: Zoezi la kuondoa lori lililoparamia watu linaendelea
Bado vyombo vya uokoaji vinapambana kulinyanyua lori lililoacha barabara na kuparamia abiria na baadhi ya madereva bodaboda katika eneo la Kimara Stop Over jijini Dar Es Salaam.
=====
Saa Tisa Usiku: Kamanda Polisi Kinondoni, RPC Mtatiro Kitinkwi athibitisha Bodaboda 6 kutolewa
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni RPC Mtatiro Kitinkwi amethibitisha kuwa bodaboda sita zimetolewa chini ya lori ambalo liliacha njia na kuparamia abiria na madereva wa bodaboda katika eneo la Kimara Stop Over jijini Dar es Salaam.
Taarifa ya awali iliyothibitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Albert Chalamila ilieleza kuwa miili ya watu watatu ilitolewa chini ya lori hilo wakati hadi kufikia saa 9:00 Usiku wakati zoezi la uokoaji likiendelea.
=====
Saa Tisa Usiku: Chalamila athibitisha ajali kutoke, Mili 3 yatolewa
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila amethibitisha kuwa miili mitatu imetolewa chini ya lori lililoacha barabara na kuanguka katika eneo la Stop Over Usiku wa kuamkia leo
Zoezi la kuliondoa lori hilo lenye namba za usajili T 908 BYM limeendelea ambapo kwa mujibu wa Chalamila hadi kufika saa 9 Usiku lilinyanyuliwa kwa zaidi ya asilimia 95%.
Pamoja miili hiyo mitatu jumla ya pikipiki Sita zimetolewa baada ya lori hilo kunyanyuliwa kwa asilimia hizo.
=====
Saa saba usiku
Watu kadhaa wanahofiwa kufariki dunia, baada ya lori kuacha njia na kuparamia waendesha bodaboda eneo la Stop Over, Kimara jijini Dar es Salaam.
Mashuhuda walioshuhudia ajali hiyo iliyotokea usiku wa leo Ijumaa, Februari 14, 2025 wamesema huenda lori hilo limefeli breki.
Hadi muda huu ndo police wamefika wanafanya jitihada za kuokoa baadhi ya boda boda waliofunikwa na gari.
Aidha Polisi wametoka hapa kwenda kwa mchina kuomba gari lije lisaidie kuitoa hii gari maana kuna watu chini
Poleni Sana wana kimara-stopOver,
Hapo jirani Kimara Suka ndo home nilikokulia mpk Nmefika kutoka home kwenda kujitegemea😢
Sio mwezi ni wiki tu.Kimara suka napo majanga sana, mi naishi golani mwezi haupiti mtu anapasuka
Upo sana pugu hadi mlandizi huko juu kwa juuHivi hakuna uwezekano wa kuchonga barabata ipite huko pugu pembezon mwa reli ikatokee morogoro huko...ili malori yawe yanapita huko jamano...
Baadhi ya madereva vichwa ngumu.hatari tupu. naishi pale, huwa nasema kila siku kuwa mbio hizi za magari , pikipiki , mabasi etc kuna siku zitaleta maafa! spidi huwa ni kubwa mno mpaka unashangaa kuwa huyu si amefika spidi za hivi za nini?
Mwenyekiti wao aliwaambia wasogee Ila baadhi yao waligomaIla pia boda kila siku wanaambiwa msipaki njiani
Sasa mkuu yangepita njia gani? Sema mkombozi atakuwa sgr kile kituo cha Kwala kikikamilika! Kwa sasa hivi hakuna mbadala!Ukiniuliza malori yanatoka bandarini yanakuja mjini huku kutafuta nn. Ni Ujinga wa CCM huu. Yan lory litoke kurasini lije ubungo then liende chalinze 😂😂 akili za CCM wanazijua wenyewe
Una uhakika kwamba halijafanyiwa kazi? Huwa unasikia habari ya Kwala kule kwenye sgr?Hivi kwanini lile wazo la dry port kuwa ruvu halikufanyiwa kazi
Ova
Hii kama ni mwakajana naikumbuka hiiKuna siku nilikuwa hapo ubungo Riverside.
Lori lika angusha kontena, Bahati nzuri kontena hilo lilianguka chini kwenye ule uwazi unaotenganisha barabara mbili.
La sivyo lingeanguka upande wa pili, lingeponda magari na kuua watu.
Yeah ni mwaka jana.Hii kama ni mwakajana naikumbuka hii
Mosi Engine brake sio practical at high speed,Lori lina breki tatu
Engine Brake
Air Brake
Spring Break
Zinafelije zote ?
Iliwahi kutokea pia kimara baruti miaka ya 90 kama sijakoseaHii kama ni mwakajana naikumbuka hii
Kwala nishafika sana kule,chaka lile lina mpaka mafisiUna uhakika kwamba halijafanyiwa kazi? Huwa unasikia habari ya Kwala kule kwenye sgr?