Yanayojiri Bunge la Katiba Dodoma leo 06/03/2014

Yanayojiri Bunge la Katiba Dodoma leo 06/03/2014

... Mwenyekiti wa muda ameshindwa kusimamia shuguli za Bunge, maana nadhani anaposhindwa kufuata kanuni lazima haya yatokee. ..
Kanuni hazipo, ndio hizo zinazotengenezwa sasa na kusababisha tafrani
 
Hata agenda ya Katiba hakuiuzam2010 akiomba ridhaa tena lakini hapa akiongea na Baraza la Demokrasia la Tanzania aliweka wazi na kuikana nafsi yake kwa manufaa ya Nchi.

Kwanini ninyi wabunge wa Bunge la Katiba mbona hamumuelewi Rais wetu.

Leo mmeniudhi sana ninyi wabunge wa Bunge hili.
 
Ndugu zangu wadau wa JF! Ni kweli tumekuwa tukilalamika juu ya mambo mbalimbali yanayotokea hapa nchini, miongoni mwa matukio hayo ni pamoja na hili lililojitokeza Bungeni dk chache zilizopita, hii ni kutokana na namna wale ambao tunadhani kuwa ndio wanaoweza kutuwakilisha wanavyofanya mambo ya kipuuzi. Hawajui kuwa muda wanaoutumia pale unatumia fedha za walipa kodi wa Taifa hili maskini.

Ushauri wangu ni huu, ifike mahali tuseme sasa basi, kwani ni wiki tatu sasa wapo Bungeni hakuna kitu kinachoendelea zaidi ya kujadili kanuni ambazo, nazo zinakiuka kanuni, na hapo bado Bunge halijaanza ili tuanze rasmi kuona filamu, kwani hii ya sasa ni trela tu. Tuungane kwa pamoja na sote tuwaambie hawa WABUNGE hawatufai na wala hawastahili kutuwakilisha kwenye Bunge hili ambalo lina wajibu wa kuunda Tanzania mpya yenye mwelekeo wa kesho kwa ajili yetu na ya Vizazi vyetu vijavyo.

Tuzingatie kauli za wazee wetu kuwa, "Mchelea mwana kulia, hulia yeye"; na pia "Kila mchuma janga, hula na wa kwao"!

Tuinusuru Tanzania kwa kufanya maamuzi magumu badala ya kulalamika pembeni!!
 
Baada ya Bunge kuqhirishwa kwa vurugu za hawa wahuni TBC wanarusha speech yake.....jamaa alikuwa wazi sana
 
Kwa mara nyingine Mwenyekiti Kificho imebidi aahirishe bunge maalumu la katiba baada ya kutokea maneno kati ya Ole Sendeka na Mabruk hadi kupelekea kukashifiana. Wabunge wengine wakawa wanataka Ole Sendeka aombe radhi huku wengine wakipinga kwa misingi ya chama. Imeonekana Aden Rage akizuiwa na wajumbe wengine asipigane na mjumbe mwingine ingawa alionekana kama kutania. Hata hivo nyuma kabisa ya ukumbi, wajumbe walionekana kutaka kuzipiga hali iliyopelekea Mwenyekiti kuahirisha semina.
Sijui tunaenda wapi nchi yetu!
Halafu mbona Ole Sendeka na Aden Rage kama vile wanafanana hivi! Naona tofauti ni nywele tu, mmoja anazo za kimasai mwingine za kisomali!
 
Kwa mara nyingine Mwenyekiti Kificho imebidi aahirishe bunge maalumu la katiba baada ya kutokea maneno kati ya Ole Sendeka na Mabruk hadi kupelekea kukashifiana. Wabunge wengine wakawa wanataka Ole Sendeka aombe radhi huku wengine wakipinga kwa misingi ya chama. Imeonekana Aden Rage akizuiwa na wajumbe wengine asipigane na mjumbe mwingine ingawa alionekana kama kutania. Hata hivo nyuma kabisa ya ukumbi, wajumbe walionekana kutaka kuzipiga hali iliyopelekea Mwenyekiti kuahirisha semina.
Sijui tunaenda wapi nchi yetu!


Hii inanikumbusha kenya siku walipokuwa wanamchagua speaker katika uchaguzi wao uliohusisha vurugu kubwa miaka ya 2007/2008. Uchaguzi ule ulikuwa na vurugu kama ninazoziona leo hii bungeni. watu hawakukubaliana kabisa na vurugu kubwa zilizuka. uchaguzi ulitakiwa umalizike katika muda wa kawaida kabisa lakini majadiliano yalisababisha masuala yasogee hadi usiku wa manane. Sijui jioni ya leo itakuwaje. Ninachokiona sasa kadri vurugu zinavyokuwa kubwa ndivyo watu wa kundi fulani wanakwenda kujipanga zaidi. Observation yangu nyingine ni kama vile naona kuna watu wana kila dalili ya kutaka kukwamisha huu mchakato. Kazi yenyewe haijaanza mambo ni hivi; shughuli yenyewe ikianza si itakuwa balaa.

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE NA KWA SASA HAWA WANAOTUWAKILISHA KIMAKUNDI HUMU NDANI YA BUNGE. UWAONDOE NYONGO WALIZONAZO NDANI YA MIOYO YAO KWA MAONO YA MAKUNDI YAO NA KUTULETA PAMOJA NA HSA KATIKA YALE TULIYOYAPENDEKEZA KATIKA RASIMU. WAPE SUBIRA NA KUVUMILIANA KATIKA MICHANGO YAO. AMINA
 
Kwa hili kwa kweli tumechemsha lakini Mwenyekiti wa muda ameshindwa kusimamia shuguli za Bunge, maana nadhani anaposhindwa kufuata kanuni lazima haya yatokee. Kukiwa na haki amani lazima itatawala.
Afuate kanuni zipi wakati ndio zinajadiliwa?......binafsi simlaumu mwenyekiti kwa kuwa anaendesha bunge kwa kutumia mbinu za medani tu...mibunge/mijumbe yenyewe ndio haina busara.......nimeudhika sana.
 
ni aibu kubwa sana kwa nchi yetu wakati jambo kubwa la kihistoria likifanyika baadhi ya wajumbe wanakosa nidhamu na kushindwa kutambua umuhimu wao kuwepo pale ndani ya lile bunge.ukweli inakera sana..sisi tuna wasiwasi mkubwa kama kwa style wanayoenda nayo hiyo katiba tutaipata kwel??
 
Mtikila aliposema 'bunge hili ni la kihuni kuliko mabunge yote yaliyo wahi kuepo duniani' watu walimdhihaki, haya sasa
 
Kwa hili kwa kweli tumechemsha lakini Mwenyekiti wa muda ameshindwa kusimamia shuguli za Bunge, maana nadhani anaposhindwa kufuata kanuni lazima haya yatokee. Kukiwa na haki amani lazima itatawala.

Jamani tusimulaumu mwenyekiti tatizo ni kutokuwa na kanuni ambazo ndiyo zinatungwa na bado hazijaidhinishwa kuanza kutunika.Kwa uzoefu niliouona ktk kipindi hiki bila kanuni inaleta sura kama ni wajuni fulani walio mjengoni wasio na malengo yoyote.

Kanuni zikikamilika utaona jinsi kamanda Sitta atakavyozisimamia na kuanza kuwatoa wahuni wote nje.Hebu ngoja tuendelee kuwavumilia hawa wawakilishi wetu hadi JK atakapolifungua rasmi hili bunge la katiba.
 
Wanasiasa wanapaswa kutuliza munkali wao sisi tunataka katiba.
 
Mimi,Petro Eusebius Mselewa,Msomi wa Sheria,mtanzania mtu mzima mkazi wa Kibaha,Pwani NATAHADHARISHA Wajumbe wote (pamoja na viongozi wao) wa Bunge Maalum la Katiba kwa kusema ifuatavyo:

1. Kwamba, nikiwa ni mfanyakazi wa Serikali ninayekatwa kodi kila mwezi kuchangia maendeleo ya nchi yangu yakiwemo ya kupata Katiba mpya.

2. Kwamba, malipo ya posho na marupurupu mengine wanayopewa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba nayachangia kupitia makato hayo na mengine kupitia kununua bidhaa zenye kodi ya ongezeko la thamani.

3. Kwamba, Wajumbe wa Bunge Maalum wako Dodoma kama wawakilishi wa watanzania wote na si vyama vyao vya kisiasa au taasisi watokazo.

4. Kwamba, Bunge Maalum la Katiba limekuwa na mweneno usiovutia hasa kubishania vitu visivyo vya msingi,kupiga kelele Bungeni, kukejeliana na kutusiana.

5. Kwamba, siku zilizopangwa kwa suala la kujadili na kuipisha Rasimu ya Katiba mpya,kwa mwenendo ulivyo sasa Bungeni, hazionekani kuwa zitatosha.

6. Kwamba, mifarakano inayoendelea na kushamiri kila uchao ni dalili mbaya za kupata Katiba mpya inayokidhi matakwa na matarajio ya watanzania.

HIVYOBASI, Wajumbe wote wa Bunge Maalum nawatahadharisha na kuwaambia kwamba:

1. Mfanye mambo yaliyowapeleka hapo Dodoma kadiri ya majukumu yenu na maslahi mapana ya Taifa.

2. Watanzania hawashindwi kuwaondoa hapo Dodoma kwa kusitisha au kuondoa kabisa mchakato huu

3. Watanzania bado wana imani nanyi ingawa uvumilivu wao unakaribia mwisho

4. Mchukue hatua stahiki kuepusha mifarakano ya kitaifa inayoweza kuzaliwa na matendo na maneno yenu hapo Bungeni Dodoma.
 
Hao ndio lugha wanazo zijuwa kelele utafikiri wapo majumba ya hall ya muziki hawana ishu kazi waliofata sio kutunga sheria bali ni. Mayowe tu
 
Kulee mbali kabisa naona giza nene, hivi kweli kwa staili hii kuna Katiba kweli ?? naona giza tuu totorooo. Something must be done, hivi JK hawa jamaa aliwachagua yeye au alipewa majina tu !
 
Mpaka wazichape mule ndani ndio heshima itakuwepo mana kila mmoja anajiona kijogoo kwa mwenzake.
 
Tbc kazi yao kurudia kila siku... Hata wakati wa kuonyesha bunge sametime wanaonyesha upuuzi... Sijui hii tbc imekuwaje siku hizi..
 
Kweli hili bunge linmfaa sita,angekua bi kiroboto angejiudhuru...mzee wa watu kificho namuonea huruma sana..kinachoendelea bungeni ni upuuzi mtupu
 
Back
Top Bottom