Yanayojiri Bunge Maalum la Katiba leo Tarehe 7.3.2014.

Yanayojiri Bunge Maalum la Katiba leo Tarehe 7.3.2014.

Chabruma

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2013
Posts
5,660
Reaction score
1,780
Wadau, leo tutaendelea kuwaletea kila kinachojiri kwenye semina ya Bunge Maalum hapa Dodoma. Kazi kubwa itakayofanyika leo ni kupitisha vile vifungu vilivyoachwa kiporo kwa siku ya juzi. Vifungu hivyo ni kuanzia kifungu cha 32 hadi 43 ambavyo vilifanyiwa ukarabati mkubwa. Wabunge wamepewa muda wa kupitia vifungu hivyo na kuwasilisha majedwali ya marekebisho yao kwa Kamati Teule. Kwa siku ya jana, zoezi la kupitisha kanuni lilienda vizuri hasa wakati wa jioni kwani wabunge walipitiaha vifungu kuanzia cha 58 hadi kifungu cha mwisho cha 87. Hakukuwa na mivutano mikali kama ilivyojitokeza kwenye kikao cha jana asubuhi.

Mara baada ya vifungu vyote kupitishwa, zoezi litakalofuata ni uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bunge Maalum ambapo hapa pia inatarajiwa kuwa zoezi litakuwa jepesi hasa kutokana na kudhihiri kuwa SAMUEL SITTA ni kama amepita kutokana na kukubalika miongoni wa makundi yote matatu yanayounda Bunge hilo. Uchaguzi wa Mwenyekiti unatarajiwa kufanyika kesho Jumamosi tarehe 8.3.2014

Kwa vile nitakuwa mjengoni, nitawajuza kila kitu kitakachoendelea. Mimi na Simiyu Yetu tunawaakilisha vema na hakika mnapata taarifa sahihi na kwa wakati.

View attachment 143283
View attachment 143284
View attachment 143285
 
Tujuze bana
Mkuu usijofu kila kitu kitawekwa wazi hatuakwa hatua jambo kwa jamno mjumbe kwa mjumbe.

kwa sasa bunge linaelekea kuzuri sana suala la kanuni ndiyo ilikuwa jamno la gumu na msingi wa katiba yote kwa vile leo litatamatika basi kila kitu kitaenda vema.
 
Msingi wetu ni kuwapa ukweli wa mambo bila ushabiki hii ni kwa manufaa ya watanzania waliowengi ambao ndiyo wenye katiba yao.
 
Sawa sawa....natumai utoto utoto.....ujivuni ujivuni......hautatamalaki leo hii......
 
kwa busara za Mwenyekiti Kificho ukichanganya na hotuba ya Kikwete nina imani kila kitu kitakwenda vizuri
 
kuna kitengo chochote inaweka uwazi ulio zaidi kwenye youTube ?? Wengine huwa tupo mihangaikoni na hatunanafasi za kuangalia TBCmichujo ,,,kazi ni kwenu kutushushia vitu kwenye utandawazi huo ,napenda kuungwa mkono !
 
]
Leo bunge linaanza saa ngapi?
Mkuu, leo bunge linaanza saa 4 asubuhi ila tutarajie pia kuchelewa kama inavyojitokeza siku zote. Wanaweza kuchelewa kwa zaidi ya dakika 20. Si unajua tena, wajumbe wengi wana umri mkubwa hivyo kujivutavuta hakukosekani
 
Ngoja tuone itakuwaje leo!maana wajumbe wenyewe hawatabiriki hawa!
 
Msingi wetu ni kuwapa ukweli wa mambo bila ushabiki hii ni kwa manufaa ya watanzania waliowengi ambao ndiyo wenye katiba yao.

Mhhh wewe utaweza kweli bila ushabiki?

aione mzee tupatupa wa lumumba(sasa Dodoma)
 
Msingi wetu ni kuwapa ukweli wa mambo bila ushabiki hii ni kwa manufaa ya watanzania waliowengi ambao ndiyo wenye katiba yao.

Tunaombeni heshima yetu watanzania yale myafanyayo bungeni mnatia aibu.Hilo bunge halina UTUKUFU wowote kwa sasa,kwa upande wangu ninaona siutendei haki UTANZANIA wangu kwa kuliita hilo BUNGE TUKUFU.Tupeni watanzania tunaowalipa hizo POSHO heshima yetu kwanza.
 
Ngoja tuone itakuwaje leo!maana wajumbe wenyewe hawatabiriki hawa! mkuu wanabishana balaa tumwombe mungu awape hekima ya kimumgu tu!!! hawa wanasiasa hawaeleweki kabisa
 
Back
Top Bottom