Yanayojiri Bunge Maalum la Katiba leo Tarehe 7.3.2014.

Yanayojiri Bunge Maalum la Katiba leo Tarehe 7.3.2014.

Taswira ya ukumbi wa bunge kama ilivyochukuliwa saa 4.16 asubuhi hii
image.jpg
image.jpg
 
Hivi hawa wajumbe nao tuwaeleweje? Ya nini kupoteza muda kwa kuchelewa kufika ukumbini? Wanateketeza kodi zetu bila huruma
Mkuu, hata Mwenyekiti Kificho huwa analilalamikia sana jambo hilo.
 
SITTA ndo habari ya mjini nasikia mlitaka wengine lakini mkasikia atachukua fomu kivyake! Baada ya hapo mkaona anakubalika wahafidhina wakaamua kumfuata baada kuona atawashinda kwa vile anakubalika sana Chezea mzee VIWANGO
 
Kwa mujibu wa picha hii nahisi kuna kamgomo baridi bungeni

..."Enyi Wajumbe wa Baraza la Katiba, mmekuwa wajinga Kweli! 'mnakuwa kama watoto wachekechea! Kwanini mna poteza muda kwa mambo yasiyokuwa na tija kwa Watanzania? Kodi za watanzania zipotea kwa upuuzi wenu wa kitoto' kwa mabishano yasiyokuwa na maana! Ni nani aliyewaroga?"
...watanzania tunakatwa fedha nyingi kwenye ujira wetu kwa ajiri ya kuwalisheni ninyi, alafu bado mnaanza kuleta na kuchangia upuuzi. Watanzania tumewachokama mapema kwa upambav* wenu, kwanini hamna uchungu na kodi za walala hoi?
 
WAJUMBE WA BUNGE MAALUMU LA KATIBA FANYENI LILILO WAPELEKA

Inasikitisha sana kuona wajumbe wa bunge maalum wakisahau jambo moja tu lililowapeleka, ambalo ni kuandaa katiba mpya. Haiwezekani kabisa watu kwenda huku hawajui nini umuhimu wa jambo wanalolifanya kwa TAIFA lao. Yapo mengi yameendelea yanayokatisha tamaa, na kusababisha tuliowengi kukosa imani na bunge hili katika uandaaji na upatikanaji wa KATIBA ILIYO HAKI NA KWELI. Naamini kabisa utakubaliana na mimi kuwa TANZANIA ya sasa imetawaliwa na siasa ambayo ni ya vyama vingi, ambapo tunapata vyama vikuu viwili yani CCM na CHADEMA, na nje ya vyama hivi vipo CUF,NCCR,UDP,TLP, N.K ambavyo ni dhahiri kuwa wanachama wake wamegawanyika wengine wakiwa wafuasi wa CCM na wengine CHADEMA. Jambo hili lio wazi na ni dhahiri kabisa ingawaje wapo watakaokataa kwa sababu moja tu ya kuwagusa.
Wajumbe halikadhalika nao wamegawanyika katika makundi makuu mawili yaani wafuasi wa itikadi za kivyama ambao ni wafuasi wa itikadi za CHADEMA na wafuasi wa itikadi za CCM.Awe ni mwenyekiti, awe ni mlemavu, awe ni kutoka NGO’S, awe ni padre, awe ni sheikh, awe ni mpagani wootee itikadi zao zimelala katika vyama hivyo vikuu viwili. Hii ni sababu kuu iliyonipelekea mimi kuandika huu ujumbe kwa wajumbe wa bunge maalum. Hakuna haja ya kudanganyana ni dhahiri watu wametawaliwa na uvyama ndani ya bunge hili. Na hi indo sababu kuu itakayo pelekea watanzania tushindwe kupata KATIBA ILIYO HAKI kama hali itaendelea hivi. Kila mmoja anataka kuvutia kwake na kusahau kuwa hawapo pale kwa ajili ya maslahi ya vyama vyao. Hivi si vikao vya vyama, na kama umetumwa kuja kuwakilisha chama chako na misimamo yake fanya hivo kwa kuzingatia na kuongezea akili zako ili ujue ni yepi yaliyo misimamo ya chama chako yana maslahi kwa Watanzania wote na yepi yana maslahi kwa wafuasi wa chama chako tu, kisha ufanye maamuzi.
Haupo bunge maalum kwa ajili ya maslahi ya CCM au CHADEMA, upo kwa maslahi ya wote haijalishi mtu katokea kijijini au laa, ila katiba mnayoiandaa lazima iguse watu wote kwa haki na kweli. Najua waliowengi wana imani kubwa sana na vyama vyao, na wengine ni wanafiki na waoga, na ingawaje wanaona kabisa misimamo ya vyama vyao haina tija kwa taifa bado hawadhubutu kuipinga. Ewe mjumbe lazima utambue kuwa si kila kinasemwacho na kuungwa mkono na CCM ni sahihi, kwani wakati mwingine kinaweza kuwa hakina maana, na pia si kila kisemwacho na CHADEMA ni sahihi wakati mwngine kinaweza kuwa hakina maana. Nikiwa na maana kuwa eti kwa kuwa jambo limesemwa na mtu wa CHADEMA basi wewe wa CCM yakupasa kulipinga kivyovyote vile hata kama wajua lina umuhimu, that’s nonsense and stupidity. Na wewe wa CHADEMA kwa kuwa jambo limesemwa na mtu toka CCM basi wewe wapaswa kulipinga tu hata kama wajua lina umuhimu that’s is a shame. Na kwa misingi hiyo hatutopata kamwe katiba ya haki na kweli kama wajumbe hawatakuwa tayari kuwa wazalendo wa TANZANIA rather than been CCM or CHADEMA. FANYENI LILILO WAPELEKA acheni kufanya mambo ya AIBU, kupitisha mambo kwa kuwa tu, yameletwa na kuungwa mkono na chama chako bali yana manufaa gani kwa watanzaniaa.
Zilindwe haki za watanzania wote, walemavu,wakina mama, watoto,waandishi wa habari na pia bila kusahau watu muhimu sana katika jamii yaani WASANIi. Naamini muda bado upo, mwakilishi anaweza kupatikana au kwa njia yeyote ile haki zao zihakikishwe zinawekwa kwenye katiba na pia kwa yale yaliopitishwa kimabavu, wanaharakati mpo, nafasi ya kuyatetea ipo, kwani ‘’haitoshi tu kujiita mtetezi au mwanaharakati bali lazima utetezi wako uonekane na upatikane kwa haki’’ na kwa kufanya ivo tutakua mmewatendea haki watanzania kwa kuwaletea rasimu ambayo itakua imebeba mambo yanayo wanufaisha na sii kuaandaa rasimu ambayo mnajua kabisa kwenye referendum haitapita kwa vyovyote vile. Na nimalizie kwa kusema kuwa
‘’Ni bora kulinda heshima yako kama kiongozi katika kusimamia haki na kweli KULIKO kulinda madaraka yako kama kiongozi kwa kusimamia unafiki na udhalimu katika jamii’’
 
Mkuu, hata Mwenyekiti Kificho huwa analilalamikia sana jambo hilo.

Kwa utovu wa nidhamu kwa kodi za wananchi, wajumbe wataanza kulalamika eti muda hautoshi huku wengine wakidai wana njaa mkutano uahirishwe wakale, yani naihurumia kodi yangu.
 
Bravo Kiongozi! Tunashukuru JF kuwa ya kwanza kutujuza yanayojiri ndani ya Bunge lao Maalum.
 
MkuuChabruma
si walitangaza kuwa wageni hawaruhusiwi kupiga picture?
Mkuu, walitangaza lini? By the way, mie si mgeni kwenye ukumbi huu wa bunge. Nitawndelea kuwajuza kila knachoendelea ukumbini kila siku kwa kadri Mungu atakavyoniwezesha
 
Taswira ya Ukumbi wa Bunge kama ilivyochukuliwa saa4.30 asubuhi hii. kikao bado hakijaanza na wajumbe wanaendelea kuingia ukumbini
image.jpg
 
hili bungee au.wanapeana michapo ya chako ni chako na whatsap wakiwa mjengoni.utadhan bar ya pombe mchanganyiko.----
 
kwa nini mkuu hali ya mahudhurio sio nzuri
Mkuu, ni kwa vile hakuna kanuni zinazowaongoza. Kwani hakuna kitu kinachomsukuma mtu kuwahi ukumbini. Wabunge vijana ndo wanaongoza kwa kuchelewa hasa wa bunge la Jamhuri ya Muungqno na baraza la wawakilishi. Wazee wengi nimewaona wamefika kwa wakati kama akina mzee Kingunge, Cheyo, Mrema, Lowasa, Mwandosya na wale wabunge 201.
 
Wadau, hali ya mahudhurio inaaza kuridhisha. Wajumbe wengi wameingia ingawa nawaona wengine wanaranda kule nje hasa maeneo ya canteen nanwengine wamekaa karibu na lango la kuingilia wabunge ukumbini
 
Nakusudia kuna wajumbe wabunge mabomu ,hawana uchangiaji wowote ,wapo hapo kama furniture za ukumbi ,wakingojea kuburuzwa tu na waccm ,wanafurahia posho ile mbaya utawasikia wakigonga meza na wengine kupiga vigelegele kama wameelewa kwa kina kumbe hamna kitu,wengi wa wabunge hawa wamepitishwa au tuseme wamepelekwa kubackup hoja za CCM na huku ni kwa waTanzania kutungiwa katiba ileile yenye utashi wa chama kimoja.
 
Back
Top Bottom