Yanayojiri Bungeni Dodoma: Jumatano, Tarehe 12 Machi 2014 - Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bunge Maalum

Yanayojiri Bungeni Dodoma: Jumatano, Tarehe 12 Machi 2014 - Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bunge Maalum

Namuona Mwenyekiti wa Muda ameshindwa kutamka neno "FALSAFA" na kusema "SALFASA"

Kazi kwelikweli.!!!!
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mwenyekiti wa muda wa Bunge la Katiba ameshindwa kutamka neno hilo ila yeye akadai SALFASA na kuibua vicheko kwa wajumbe amejaribu zaidi ya mara tano bila ya mafanikio Ha ha haaaa. Amenikumbusha enzi za Masanja Mkandamizaji.
 
Watu wawili wameingia kwenye kinyang'anyilo cha kugombea uenyekiti wa kudumu wa wa bunge maalumu la katiba. Watu hao ni Hashim Rungwe na Samuel Sitta.

Kabla ya kuanza upigaji kura wagombea walipewa dakika tatu kila mmoja wao za kutoa maelezo ili mwishoe aombe kura. Wakati hoja ya kuuza magari ikionyesha kuwagusa wajumbe wengi kwa upande wa maelezo ya bwana Rungwe, Sitta alitoa mpya pale aliposema "Nitapambana na wale wachache wanaopinga kuwepo kwa muungano"

Kwa maoni yangu naona Mh. Sitta hakupaswa kusema maneno hayo. Anaonyesha wazi mapema kupambana na wale wenye mtazamo tofauti na wake.

Niliwaambia huyu CCM hafai! Rasimu ni matakwa ya wananchi, sasa yeye atapambana na matakwa ya wananchi? CCM inaona serikali 3 zitavunja muungano, naye ni CCM, atapambana na all who are against serikali 2.
 
Zoezi la upigaji kura limemalizika tusubiri matokeo.Wagombea wanachagua mawakala.Sita amemchagua mwana mama mh Bahati Ally Abeid na Rungwe amemchagua Rashid Ray kuwa wasimamizi wao. Mwenyekiti wa muda amesema zoezi la kuhesabu kura litachukua muda mfupi hivyo wajumbe wasitoke ukumbini wasubiri matokeo

Mimi kura yangu nimempa SITTA , ni muwazi tu, siri ya nini?
 
Wabunge ndiyo watakaoamua kama kauli ya SITTA ni mbaya au la, wewe huozi kuona umuhimu wa Kauli ya SITTA na hapo ndipo tunakosea kuwahukumu watu. Kuna kosa gani SITTA kuonesha msimamo wake? Kura zimepigwa nitashangaa kuona wewe unapingana na kauli ya SITTA wakati anazoa kura zote zikiwemo za wapinzani.

Kauli zako si njema kwa minajili ya uzi huu, tafadhali jirekebishe.
 
Sitta amemchagua Mhe Bahati kuwa wakala wake wa kuhesabu kura. Makonda kaonekana kukunja uso sijui alidhani atateuliwa yeye? Yaani huyo kijana ni poyoyo kweli kweli.


Sent from my iPad using JamiiForums

Ha ha ha ha
 
Pia Lucy Owenya naye yupo ila kamera za waandishi zimemnasa akipiga miayo (ya kawaida)
 
Wale wenye nia mbaya ya kuvunja muungano watashughulikiwa, nijuavyo mimi Samuel Sita ni muumini wa Julius K Nyerere..

Angekuwa Rais wengi wa wanaopinga muungano wangekuwa ndani...

Mawazo yako kamaya kwangu mkuu, na hata mimi nakubaliana na msiamo huu.
 
Huyu siyo watu walikuwa wanamlilia.sitta ni utumbo mtupu
 
Mjumbe Amoni anashukuru uendeshaji wa shughuli hizi pia kwa ujumla anashukuru miundombinu yote kwa kuzingatia na kujali mahitaji maalum
 
Wabunge ndiyo watakaoamua kama kauli ya SITTA ni mbaya au la, wewe huozi kuona umuhimu wa Kauli ya SITTA na hapo ndipo tunakosea kuwahukumu watu. Kuna kosa gani SITTA kuonesha msimamo wake? Kura zimepigwa nitashangaa kuona wewe unapingana na kauli ya SITTA wakati anazoa kura zote zikiwemo za wapinzani.

Kama wewe mpaka hapo huoni kosa, samahani...nilidhani utaeleza huo msimamo wake una manufaa gani kwa wajumbe wa Bunge la Katiba, kumbe! Endeleaaa...
 
Back
Top Bottom