Yanayojiri bungeni Dodoma: Jumatatu 17 machi 2014-Viapo kwa wajumbe, Jaji Warioba Kuwasilisha Rasimu


Katika hao wataalam wa katiba na HISTORIA ya Tanzania , ingekuwa busara kama angealikwa mzee Mohammed Said, Mzee Moyo na Mzee Abdu Jumbe.
 
Viapo vimemalizika. Matangazo yanatolewa kuwa wabunge watumie geti kubwa kwa ajili ya usalama zaidi badala ya lile geti dogo mkabala na barabara ya Dodoma- Dar es Salaam
 
Katika hao wataalam wa katiba na HISTORIA ya Tanzania , ingekuwa busara kama angealikwa mzee Mohammed Said, Mzee Moyo na Mzee Abdu Jumbe.
Mkuu, hayo ni mapendekezo yako. Huenda katika hao walioalikwa, wamo pia hao uliowapendekeza.
 
Tangazo linatolewa kuwa wanachama wa UKAWA (Umoja wa Kambi ya Wapinzani) wakutane kwenye ukumbi wa Pius Msekwa mara baada ya kikao hiki
 
Viapo vimemalizika. Matangazo yanatolewa kuwa wabunge watumie geti kubwa kwa ajili ya usalama zaidi badala ya lile geti dogo mkabala na barabara ya Dodoma- Dar es Salaam

Pamoja sana mkuu
 
Bunge limesitishwa hadi saa 11 jioni. Nami pia niwage wadau na niwqombe tukutane hapo saa 11 jioni
 
Naomba kuweka hisia zangu wazi kuwa mchakato wa kupata katiba mpya inayotokana na maoni ya wananchi umevurugika hasa baada ya mambo ya uvyama kutawala mchakato mzima mpaka sasa.
 
Hivi hili jina Tanzania bara ni kitu gani? ni nchi au ni muunganiko wa Tanganyika bara na Zanzibar bara?
 
Hivi hili jina Tanzania bara ni kitu gani? ni nchi au ni muunganiko wa Tanganyika bara na Zanzibar bara?

Mkuu, utaumwa kichwa bure, inavyoonekana wanasiasa wameamua kutetea uanasiasa wao badala ya masilahi ya wananchi
 
nashukuru kwa taarifa nzur sana hii kwani nimeibiwa TV
na sijaona taarifa kwa wiki sasa nashukuru sana hapa jf
 
mimi naomba kujua ni wabunge wangapi bado kuapishwa hadi sasa (kama inawezekana)
 
Hapa Sitta kakosea kabisa. Hadi sasa wajumbe wa bunge la katiba wako kwenye maandalizi yaani uandaji wa kanuni, uchaguzi wa viongozi wa bunge hilo pamoja na viapo. Baada ya haya kufanyika ndipo bunge linaanza kazi ramsi ya kujadili katiba mpya na kazi hii inazinduliwa na rais.

Busara ndogo tu ilimtushota Sitta kitambua kuwa mwenyekiti wa tume ya kukisanya maoni/kuandaa rasimu ya katiba hawezi kuwasilisha rasmi rasimu kwa bunge ambalo bado halijazinduliwa rasmi na rais. Hii ni sawa na kukabidhiana rasimu vichochoroni. Kosa.
 

Mkuu, ulichokinena umeniwakilisha vyema kwa asilimia zaidi ya mia
 
Ngoma ikivuma sana mwisho upasuka sita kalewa sifa


Sent from my iPhone 5 using JamiiForums
 
mimi naomba kujua ni wabunge wangapi bado kuapishwa hadi sasa (kama inawezekana)

List ipo kwa uongozi wa bunge, ni vigumu kwa mtu wa kawaida kufahamu unless uombe upewe majina ya walio bado kuapishwa...........lakini sio wengi sana; sana sana wale walioenda jana uchaguzini kalenga wale ambao hawajaapishwa tu!

Usiumize kichwa ndg yangu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…