LIVE Yanayojiri vita ya Israel dhidi ya Palestina na HAMAS

Live coverage on JamiiForums
wengi hawaelewi kwamba pamoja na kwamba wayahudi wengi waliondoka kwenda uhamishoni, sio wote, wapo wengi walibaki na vizazi vyao vipo hadi leo. though kuna kipindi eneo lile liliwahi kutawaliwa na waislam, ila ni mali ya wayahudi.
 
Marekani anapenda kuonea banana, Hamas ndo wakuwasumbua hivi?. Hizo meli walizopeleka zinaweza kuwa target nzuri kabisa, hata hao HAMAS sio walikurupuka wamejipanga vizuri kabisa.

Tuombe Amani tu, vita ikitokea Middle east pale hakuna atakayepona na kuna nchi zingine lazima zitaingia tu,
 
[emoji845][emoji1134][emoji3538][emoji1193] BREAKING! Currently unconfirmed reports that an Israeli Air Force F-16 has been shot down over #Gaza. Eyewitnesses say the pilot ejected. #Palestine

Some reports are saying that a second F-16 was also shot down, but both of these claims have not been confirmed.
 
Kipindi vita ya Ukrein na Urusi inapamba moto, Mitandao mbalimbali kama Facebook, YouTube, Instagram na mingineyo ilipiga marufuku kabisa habari zozote za kuunga mkono Urusi au kupost habari yoyote ya kuonesha Urusi inashinda. Walitaka muda wote habari za Ukrein ndio zioneshwe hili kila mtu haiunge mikono Ukrein kwa sababu Urusi ndio alikuwa mvamizi wa ardhi na muonezi dhidi ya mwenzake.

Lakini katika vita hii ya Israel na Palestina, Israel hana tofauti yoyote na Urusi kwa sababu wote ni wamelazimisha kushambulia ardhi za nchi nyingine, na Palestina ni kama Ukrein kwa sababu yeye ndio anakula kichapo mpaka ndani ya ardhi yake, na maeneo yao kuzidi kutekwa.

Mbona hapa Mitandao hii haikutaka kusimama na Palestina kama ilivyosimama na Ukrein. Mitandao hii haijaamua kuchagua upande wowote na imeruhusu habari za pande zote mbili kuwekwa mitandaoni humo. Mitandao hii inajua fika palestina anapelekewa moto, ila imeamua kukaa kimya na kutokumsapoti.

Inaonekana kabisa hii mitandao hipo kwa ajili ya kulinda masilahi ya Marekani, Ulaya na washirika wao wanaowaunga mkono kama Israel. Lakini kama wewe unatoka Asia au Afrika ukaleta ushubwada kutaka kuzingua washirika wa ulaya na Marekani, jua kabisa utapigwa vita mpaka mitandaoni.

Palestina haijapigwa vita mitandaoni kama Russia kwa sababu walioanzisha mashambulizi sio Nchi bali kikundi tu, hivyo inakuwa ngumu kwa mitandao hii kufungia habari za palestina. Japo mpaka sasa habari nyingi tunazopewa ni za kumpamba Israel ili aonekane anaonewa na hivyo anavifyeka vikundi vya kigaidi.
 
Sasa chakushangaza ni nini mbona wayahudi wamepeleka vifaru mpkani MWA Gaza ujashangaa
 
Arab League wamesema kitendo cha kuwataka Wapalestina wahame kwa lazima kutoka Gaza ni Uhalifu.

Waarabu katika Umoja wao wamesema wanafuatilia kwa karibu kila kinachoendelea Gaza.

Source BBC news.
 
Vilio vya kutaka kuonewa huruma vimeanza. natanyau alishasema anataka apabadilishe middle east na ndicho anachokifanya. gaza itakuwa deserted island. hatakaa mwanadamu pale tena, na pakikaa kitambo wao watajenga makazi ya wayahudi. mwana kulitafuta mwanakulipata.
 
makamanda hadi toka nchi jorani wametinga maeneo😄gaza itabaki historiaa🔥🔥
 
Hao mlisahau kama walishindwa na Hizbullah miaka michache iliyopita ,hii vita sio ya kitoto ,wapalestina wamepiga ambush na kuondoka na wakuu kibao wa kiyahudi,ambao ni mateka.
Hivyo hio kuhamisha ni vizuri kwa wapalestina ili kuweka uwanja mzuri wa mapambano.
 
Nonsense wamguse Iran waone Yule anampaka hypersonic missiles huku anabackup ya Mrusi.
Sina uhakika kama anaweza pata backup ya urusi maana hata urusi waliancha kusupply S300 surface to air missile.
Na urusi kwa sasa anafocus na ukraine ndo jicho analoangalia kwa sasa.
 
Na kama hamna habari jamaa kibao wanajiandaa wapo kwenye maandalizi kuelekea front line,kutokea kwa talaban,Chechya pakistani irani ,swaiba hajui asaidie ukurane au izraeli .
nafikiri wanatafuta ruti ya kusogea au kuingilia.
 
mrusi hana uwezo kumsaidia yeyote yeye mwenyewe anapumulia mashine ukrain tu amemshinda. kama iran iana hypersonic, israel anayo hadi nuclear.
Mkuu mimi ninagyojua wenye huyoersonic missile ni Urusi na china, North Korea alipewa na China.
USA wanatest sana zinafeli.

Ila najua miezi 4 iliyopita Iran walisema wamefanikiwa.
Ni taarifa ambayo not confirmed kivile. Sijui labda.
 
Tumieni akili Israel anasavive kwa misaada ya Marekani hana lolote hawezi kushinda vita na Iran wanaojitegemea Kwa kila kitu
Hata Iran yeye mwenye anawasiwasi na Israel ndo maana anashirikisha nchi za waarabu na za kiislamu.

Juzi waliitisha kikao na nchi za kislamu.
Iran yeye mwenyewe ajiamini.
 
Arab League wamesema kitendo cha kuwataka Wapalestina wahame kwa lazima kutoka Gaza ni Uhalifu.

Waarabu katika Umoja wao wamesema wanafuatilia kwa karibu kila kinachoendelea Gaza.

Source BBC news.
Sasa watafanya nini?
Wale wanaenda kutafuta hamas ndo maana wanawaamisha watu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…