LIVE Yanayojiri vita ya Israel dhidi ya Palestina na HAMAS

LIVE Yanayojiri vita ya Israel dhidi ya Palestina na HAMAS

Live coverage on JamiiForums
Kwahiyo nini kilitokea 1947 ghafla wakawa taifa?
Mwaka 1947 Umoja wa Mataifa ulipiga kura kuigawa ardhi ya Palestina kuwa nchi mbili. Wayahudi ambao idadi yao ilikuwa 650,000 walikubaliana na uamuzi huo na kutangaza rasmi kuunda Taifa la Israel mnamo 14 May 1948 chini ya David Ben Gurion ambaye alikuwa Mkurugenzi mkuu wa Shirika la kizayuni Duniani (World Zionist Organization)


Wapalestina (Waarabu) ambao idadi yao ilikaribia 1,200,000 waliuchukulia uamuzi huo kama muendelezo wa mkakati wa muda mrefu wa Wayahudi kuwaondoa katika ardhi zao waliukataa mpango huo. Huo ndio ukawa mwanzo wa Mgogoro wa ardhi unaoendelea sasa baina ya Wapalestina na Waisrael. Wanamgambo wa Wapalestina wakisadiwa na mataifa ya kiarabu ya Misri, Jordan, Iraq na Syria walitangaza vita dhidi ya Israel mnamo tarehe 15 May, 1948.Vita vilimalizika tarehe 10 March 1949 kwa Israel kushinda na kunyakua ardhi zaidi kutoka mikononi mwa Wapalestina ambao wengi wao waliuawa na zaidi ya laki saba (700,000) kulazimishwa kuondoka katika ardhi zao hali iliyopelekea waishi katika makambi ya wakimbizi tatizo ambalo hadi sasa bado halijapata ufumbuzi.
 
Nimesha kwambia kuhamisha watu milion moja ndani ya siku moja tena kipindi cha vita ni hatari.

Alafu hao watu wanao takiwa kuhamishwa hawana mabawa kusema watapaa watoke hapo walipo bali wana hitaji usafiri wa kuwatoa hapo yaani kiufupi sio rahisi kama unavyo fikiri.
Sasa mbona kama unatuambia sisi wkt wameambiwa wapalestina?ebu tuone kama hawataweza...wanaweza kutia tia huruma wakaongezewa masaa mengine 12
 
Hamas ndiyo walioanzisha mashambulizi dhidi ya Israel na sasa Israel inajibu mapigo kwa nguvu zilizopitiliza!
 
Hellow guys.
kupitia michango ya wadau mbalimbali kupitia vita hivi basi kuna hatua muhimu ambazo serikali inapaswa kuzichukua.

1-Ifatilie kwa karibu saana mafundisho yanayotolewa kwenye dini zetu zote.
2-Serikali iwe na mkono wake kwenye vikao,mikutano na mikusanyiko ya dini zote na ikibidi kabla ya kutoa vibali vya vikao na mikutano basI hata ajenda za wanachoenda kujadili zijulikane.
3-Missionary personally wote kutoka nje wanaokuja kuhubiri katika dini zetu inabidi wafanyiwe vetting ya maana kabla ya kupewa vibali vya kazi.
4-Elimu ya uraia hasa uhusiano wa nchi(ardhi) na taifa(watu) ipewe kipaumbele mno kama somo la msingi.
5-Wakati wa ajali/maafa jamii ikumbushwe umuhimu wa kutoa msaada kwa wahanga badala ya kurekodi matukio au majanga kwa lengo la kupata engagement.
6-Viongozi wenye misimamo mikali sana ya kiimani WASIPEWE MADARAKA NA NAFASI NYETI KWENYE VYOMBO VYA MAAMUZI NA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA
7-Watu wakumbushwe hakuna aliyewahi kumuona mungu ila waishi kwa AKILI katika matabaka yao.
8-Watu wakumbushwe kuivunja amani ni tukio la sekunde,dakika,saa au ikizidi siku.ILA mchakato wa kujenga na kuleta amani unagharimu VIZAZI VINGI.
 
Kwahiyo Israel ilipora zaidi ya ilichopewa na azimio, sio?
Kitu kama hicho.

Mara tu baada ya UN (1947) kupitisha mpango wa ugawaji wa Palestina baina ya Wayahudi na Waarabu, vikazuka vita -- na havijawaji kukoma.

Vita hivyo kwa sehemu kubwa sana vimekuwa na matokeo mabaya kwa upande mmojawapo -- ardhi kumegwa, ongezeko la Wayahudi wahamiaji, wakimbizi kwa upande mwingine, uendelezaji wa makazi mapya, sheria kandamizi dhidi ya upande hasimu, na fursa ya kujitanua kijeshi, kisiasa, diplomasia na uchumi.

^To the victor goes the spoils^
 
Sasa mbona kama unatuambia sisi wkt wameambiwa wapalestina?ebu tuone kama hawataweza...wanaweza kutia tia huruma wakaongezewa masaa mengine 12
Hata wangeweka wiki nzima bado haitoshi watu milioni 1 na laki 2ni wengi usichukulie kirahisi.
 
Israel ndo mchokozi na mvamizi. Imagine anapigana vita na watu ambao anawakalia kimabavu, ambao hawawezi kutoka mpaka kwa amri yake, halafu kawakatia umeme, maji na kazuia madawa, nyie israehell ni washenzi na waoga

Soma historia vzr acha ushabiki maandazi,wote niwavamizi,cha msingi atakayeshinda achukue ardhi.
 
Waisrael wanapozungumzia Historia ya utaifa wao, huanzia kwenye ufalme wa Daudi (David) ambaye ndiye muasisi wa Ufalme wa Israel uliojulikana kama United Monarch mnamo mwaka 1004- 960BC. Baada ya kifo cha Daudi, mwanaye Suleiman (Solomon) alishika hatamu ya uongozi kuanzia mwaka 961-922BC. Baada ya kifo cha mfalme Suleiman mwaka 922BC Makabila kumi ya upande wa Kaskazini yalikataa kuwa chini ya Utawala wa mfalme Rehoboam ambaye alikuwa ni mtoto wa Mfalme Suleiman, hivyo makabila haya yalifanya uasi na kuanzisha ufalme wao walioupa jina la Ufalme wa Israel-Samaria, mji mkuu wa Ufalme huu uliitwa Samaria, baadae walihamishia makao makuu kwenda mji wa Wacaanan wa Sichem ambao kwa sasa unajulikana kama Nablus. Ufalme huu ulisambaratika baada ya kuangukia mikononi mwa dola ya Assyria ( Assyrian Empire) mnamo mwaka 720BC.


Hali hii ilipelekea kuwepo kwa falme mbili za Kiebrania za upande wa Kaskazini na upande wa kusini ambayo hii ya upande wa kusini ilibaki kuwa chini ya Mfalme Rehoboam ilijulikana kama nchi ya Yuda (Judah), makao yake Makuu yalibaki katika mji wa Jerusalem na baadae yalihamishiwa katika mji wa Hebron. Ufalme huu ulisambaratika baada ya kushindwa vita na kuangukia mikononi mwa mfalme Nebuchadnezzar wa Babeli mnamo mwaka 587BC.


Mwaka 63BC nchi ya Yuda iliwekwa chini ya uangalizi wa dola ya Kirumi na mwaka wa 6CE iliunganishwa na kuwa jimbo la Warumi. Mnamo kwaka 135CE Wayahudi waliasi na kupelekea vita baina yao na Warumi ambapo walishindwa vibaya, walipoteza uhuru wao na mji wa Jerusalem uligeuzwa kuwa mji wa kipagani.Wayahudi walipigwa marufuku kuishi Jerusalem na Warumi waliibadili jina nchi ya Yuda na kuiita Syria Palestina.


Kusambaratika kwa falme hizi mbili za kiyahudi na kutawaliwa na madola makubwa kuanza Assyria empire, Babylonian empire, Persian Empire (Iran), Greek empire, Roman Empire, Rashidun Caliphate, Ummayad Caliphate, Ayyubid Dynasty, Mamluk Sultanate, Ottoman Empire na British Empire (United Kingdom) kulipelekea Wayahudi kutawanyika katika maeneo mbali mbali Duniani. Kutawanyika huku kuliwagawa Wayahudi kwa majina kutegemea na maeneo waliyotawanyikia. Makundi haya ya Wayahudi ni Ashkenazi (Ashkenazi Jews) kundi hili ni lile lililohamia katikati na Mashariki ya bara la Ulaya. Sephard (Sephardic Jews ) ni kundi lililohamia maeneo ya kusini ya bara la Ulaya na Kaskazini ya Afrika na Mizrahi (Mizrahi Jews) ambao walibaki mashariki ya kati, Asia ya Kusini na Asia ya kati.
And this is it
Hata kwenye biblia ndivyo ilivyo...
Watu wabishi wanakuja hapa na ngonjera za 1947
Wakati ilianzia kabla ya Yesu......

Anyway,haya mambo hayapo kimwili zaidi km wanavyoona , ndo maana tunacheka sbb tunajua it's a spiritual thing....
 
ukitaka kujua chanzo cha tatizo jitahidi kutafuta chimbuko, hii ndiyo himaya ya Israel wakati wa utawala wa Mfalme Daudi - ambapo tawala ziligawanyika pande mbili baada ya vita - Yuda kwenye light green na kaskazini.

Kwa maana hiyo wafilisi (waparestina) hawakuwa na eneo kubwa kama wanavyodai leo kwamba eneo karibia lote la Islael lilikuwa la kwao.
Unajua ni marangapi wapalistina walitawala Israel mkuu au kwakua Una iko kijiramani unadhani ndio basi
 
Back
Top Bottom