kwahiyo unataka kusema kwamba hezbullah waliishinda israel? au israel aliondoka mwenyewe kwasababu dunia ilikuwa inalalamika mno jambo ambalo kwa uchinjaji uliotokea majuzi hata dunia haiongei chochote?
Mzee! Labda hili suala uwe unaliongelea kiushabiki. Lebanon kuna jeshi la nchi halafu kuna jeshi la Hizbullah.
Israel alilipiga jeshi la nchi na kuingia Lebanon. Hizbullah akaingia vitani kuinusuru nchi yao. Jeshi la nchi la Lebanon lilishindwa. Lakini jeshi la Hizbullah waliikomboa nchi.
Hizbullah walikuwa wanapigana vita ya namna mbili; ya ardhini na angani. Kitu ambacho kwa mara ya kwanza mashambulizi yakawa yanafika mpaka Israel na matokeo mshindi hakupatikana.
pia, kwenye vita, jua kuwa ni kitu kigumu sana kupigana na gaidi anayejificha kwenye raia na kukurushia bomu wakati wew ehautaki kuua raia unataka kumpiga yeye peke yake. hapo ndipo wanatofautiana. ila kwa hilo, nafikiri unajua kinachoendelea gaza, kama raia wanajaliwa tena basi waambie waendelee kubaki gaza. anapiga bila kuangalia sasaivi.
Labda kama hufahamu sheria za kimataifa za vita. Hata vunge la EU mbunge kutoka Irish kawaumbua wenzake kuwa Israel anavunja sheria za vita za kimataifa: Kuzuia huduma muhimu kama maji, umeme, msaada wowote kuwafikia, chakula n.k uhalifu wa kivita
Ninachomaanisha ni kwamba; Israel si kikundi cha mgambo kama Hamas! Au ni kikundi cha kigaidi. Wao ni nchi kamili na wanajeshi ambao wapo ndani ya sheria za kimataifa za kivita.. Kinachotakiwa kufanywa ni kitumia weledi wa medani za kivita kwa upande wao na si kulipua makazi ya raia. Waingie Gaza na wapambane kuwatokomeza Hamas.
Kwa sasa unashindwa kumtofautisha Israel na Gaidi kwa sababu mbinu wanazotumia zote ni sawa!
pia, jambo ninalokuhakikishia ni kwamba, Hezbullah wangekuwa na uwezo kuishinda israel, basi israel ingeshafutika kwenye uso wa dunia zamani sana. kama huamini endelea kubaki na imani yako. hezbullah na hamas siku zote huwa wanapona kwa njia ya kulialia ili waonewe huruma na dunia lakini sio uwezo wa kupigana
Sasa utavamiaje pasipo kuvamiwa?
Yaani Hizbullah ashambulie tu Israel? Hata wewe ukilipima hili linakuingia akilini?
Unachoshindwa kuelewa ni kwamba: Hamas ni kikundi tu cha wanamgambo! Wanatengeneza roketi kwa kutumia pipe za kupitishia maji, hawana zana zozote za kufanya liwe na sifa ya kuitwa jeshi.
Hizbullah wana jeshi la anga, la ardhini na majini. Hawana tofauti na Israel kwa sifa wote wanaitwa jeshi. Wana vifaru n.k
Kwa misingi hiyo Israel hawezi kupambana na Hizbullah hata mnadhimu wao wa jeshi kwa sasa kinachoendelea ameshakizungumzia.