Kurunzi
JF-Expert Member
- Jul 31, 2009
- 9,753
- 10,747
Kwa upande mwingine laana ya kumkataa Yesu inawagharimu Israeli
YESU alipokuwa duniani, watu walivutiwa sana na mambo aliyofundisha na kushangazwa na miujiza aliyofanya. Kwa sababu hiyo, wengi “walimwamini” na kumkubali kuwa ndiye Masihi aliyetabiriwa, au Kristo. Waliuliza: “Kristo atakapofika, je, atafanya ishara zaidi ya zile ambazo mtu huyu amefanya?”—Yohana 7:31.
Ingawa kulikuwa na uthibitisho mwingi ulioonyesha kwamba Yesu ndiye Masihi, wengi wa wale waliomwona na kumsikia hawakumwamini. Kwa kusikitisha, hata wale ambao mwanzoni walimwamini walimwacha baadaye.
Kufikia wakati Yesu alipokuja duniani, kufikiri na kutenda kwa wafuasi wa dini ya Kiyahudi kulikuwa tofauti sana na yale ambayo Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu yanafundisha.
Viongozi wa kidini wa wakati huo—Masadukayo, Mafarisayo, na waandishi—walikuwa wakishikilia mapokeo ya wanadamu, wakiyatanguliza badala ya kutanguliza Neno la Mungu. Mara kwa mara, walimshutumu Yesu kwa kuvunja Sheria kwa sababu alifanya miujiza na kuponya siku ya Sabato.
Kwa kuonyesha waziwazi kwamba mafundisho yao hayakuwa ya kimaandiko, Yesu alipinga mamlaka na madai yao kwamba walikuwa na msimamo mzuri mbele za Mungu. Tofauti nao, Yesu alizaliwa katika familia maskini na hakuwa na elimu ya kidini kama wao.
Si ajabu kwamba ilikuwa vigumu sana kwa viongozi hao wenye kiburi kumtambua Yesu kuwa ndiye Masihi! Makabiliano hayo yaliwakasirisha sana hivi kwamba ‘walifanya shauri juu ya Yesu ili wapate kumwangamiza.’—Mathayo 12:1-8, 14; 15:1-9.
Hawakupinga kwamba miujiza hiyo ilifanyika. Badala yake, kwa kukufuru walijaribu kuwafanya watu wasimwamini Yesu wakidai kwamba anapata nguvu kutoka kwa Shetani na kusema hivi: “Mtu huyu hatoi roho waovu ila kwa nguvu za Beelzebuli, mtawala wa roho waovu.”—Mathayo 12:24.
Baada ya Yesu kumfufua Lazaro, viongozi wa madhehebu mbalimbali walishauriana na kusema: “Tufanye nini, kwa sababu mtu huyu anafanya ishara nyingi? Tukimwacha hivyo, hao wote watamwamini, na Waroma watakuja na kuondolea mbali mahali petu na taifa letu pia.” Kwa kuwa waliogopa kupoteza mamlaka na vyeo vyao, viongozi hao walipanga njama ya kumuua Yesu na Lazaro!—Yohana 11:45-53; 12:9-11.
Mtazamo wa viongozi wa dini ya Kiyahudi ulifanya watu wamchukie mtu yeyote aliyekubali kuwa Yesu ni Masihi. Kwa kujivunia vyeo vyao, walimdharau mtu yeyote aliyemwamini Yesu, wakisema: “Je, kuna hata mmoja wa watawala au wa Mafarisayo ambaye amemwamini?” (Yohana 7:13, 48)
Baadhi ya viongozi wa Kiyahudi, kama vile Nikodemo na Yosefu wa Arimathea, walikuwa wanafunzi wa Yesu, lakini kwa sababu ya hofu walificha jambo hilo. (Yohana 3:1, 2; 12:42; 19:38, 39)
Viongozi wa kidini walikuwa wameazimia kwamba “ikiwa yeyote angemkiri [Yesu] kuwa ndiye Kristo, angefukuzwa katika sinagogi.” (Yohana 9:22) Mtu kama huyo, angeepukwa na kudhihakiwa na jamii.
Upinzani kuelekea mitume na wanafunzi wa Yesu mwishowe ulichochea mateso makali. Kwa sababu ya kuhubiri kwao kwa ujasiri, mitume waliteswa na Sanhedrini, mahakama kuu ya Wayahudi. (Matendo 5:40) Wapinzani walitunga mashtaka ya uwongo dhidi ya mwanafunzi Stefano.
Alihukumiwa na Sanhedrini na kupigwa mawe hadi kufa. Kisha, “mateso makubwa yakatokea juu ya kutaniko lililokuwa katika Yerusalemu; wote isipokuwa mitume walitawanywa kotekote katika maeneo ya Yudea na Samaria.” (Matendo 6:8-14; 7:54–8:1)
Sauli ambaye baadaye alikuja kuwa mtume Paulo, alishiriki katika kampeni hiyo ya kulitesa kutaniko ambayo iliungwa mkono na kuhani mkuu na “kusanyiko lote la wanaume wazee.”—Matendo 9:1, 2; 22:4, 5.
YESU alipokuwa duniani, watu walivutiwa sana na mambo aliyofundisha na kushangazwa na miujiza aliyofanya. Kwa sababu hiyo, wengi “walimwamini” na kumkubali kuwa ndiye Masihi aliyetabiriwa, au Kristo. Waliuliza: “Kristo atakapofika, je, atafanya ishara zaidi ya zile ambazo mtu huyu amefanya?”—Yohana 7:31.
Ingawa kulikuwa na uthibitisho mwingi ulioonyesha kwamba Yesu ndiye Masihi, wengi wa wale waliomwona na kumsikia hawakumwamini. Kwa kusikitisha, hata wale ambao mwanzoni walimwamini walimwacha baadaye.
Kufikia wakati Yesu alipokuja duniani, kufikiri na kutenda kwa wafuasi wa dini ya Kiyahudi kulikuwa tofauti sana na yale ambayo Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu yanafundisha.
Viongozi wa kidini wa wakati huo—Masadukayo, Mafarisayo, na waandishi—walikuwa wakishikilia mapokeo ya wanadamu, wakiyatanguliza badala ya kutanguliza Neno la Mungu. Mara kwa mara, walimshutumu Yesu kwa kuvunja Sheria kwa sababu alifanya miujiza na kuponya siku ya Sabato.
Kwa kuonyesha waziwazi kwamba mafundisho yao hayakuwa ya kimaandiko, Yesu alipinga mamlaka na madai yao kwamba walikuwa na msimamo mzuri mbele za Mungu. Tofauti nao, Yesu alizaliwa katika familia maskini na hakuwa na elimu ya kidini kama wao.
Si ajabu kwamba ilikuwa vigumu sana kwa viongozi hao wenye kiburi kumtambua Yesu kuwa ndiye Masihi! Makabiliano hayo yaliwakasirisha sana hivi kwamba ‘walifanya shauri juu ya Yesu ili wapate kumwangamiza.’—Mathayo 12:1-8, 14; 15:1-9.
Hawakupinga kwamba miujiza hiyo ilifanyika. Badala yake, kwa kukufuru walijaribu kuwafanya watu wasimwamini Yesu wakidai kwamba anapata nguvu kutoka kwa Shetani na kusema hivi: “Mtu huyu hatoi roho waovu ila kwa nguvu za Beelzebuli, mtawala wa roho waovu.”—Mathayo 12:24.
Baada ya Yesu kumfufua Lazaro, viongozi wa madhehebu mbalimbali walishauriana na kusema: “Tufanye nini, kwa sababu mtu huyu anafanya ishara nyingi? Tukimwacha hivyo, hao wote watamwamini, na Waroma watakuja na kuondolea mbali mahali petu na taifa letu pia.” Kwa kuwa waliogopa kupoteza mamlaka na vyeo vyao, viongozi hao walipanga njama ya kumuua Yesu na Lazaro!—Yohana 11:45-53; 12:9-11.
Mtazamo wa viongozi wa dini ya Kiyahudi ulifanya watu wamchukie mtu yeyote aliyekubali kuwa Yesu ni Masihi. Kwa kujivunia vyeo vyao, walimdharau mtu yeyote aliyemwamini Yesu, wakisema: “Je, kuna hata mmoja wa watawala au wa Mafarisayo ambaye amemwamini?” (Yohana 7:13, 48)
Baadhi ya viongozi wa Kiyahudi, kama vile Nikodemo na Yosefu wa Arimathea, walikuwa wanafunzi wa Yesu, lakini kwa sababu ya hofu walificha jambo hilo. (Yohana 3:1, 2; 12:42; 19:38, 39)
Viongozi wa kidini walikuwa wameazimia kwamba “ikiwa yeyote angemkiri [Yesu] kuwa ndiye Kristo, angefukuzwa katika sinagogi.” (Yohana 9:22) Mtu kama huyo, angeepukwa na kudhihakiwa na jamii.
Upinzani kuelekea mitume na wanafunzi wa Yesu mwishowe ulichochea mateso makali. Kwa sababu ya kuhubiri kwao kwa ujasiri, mitume waliteswa na Sanhedrini, mahakama kuu ya Wayahudi. (Matendo 5:40) Wapinzani walitunga mashtaka ya uwongo dhidi ya mwanafunzi Stefano.
Alihukumiwa na Sanhedrini na kupigwa mawe hadi kufa. Kisha, “mateso makubwa yakatokea juu ya kutaniko lililokuwa katika Yerusalemu; wote isipokuwa mitume walitawanywa kotekote katika maeneo ya Yudea na Samaria.” (Matendo 6:8-14; 7:54–8:1)
Sauli ambaye baadaye alikuja kuwa mtume Paulo, alishiriki katika kampeni hiyo ya kulitesa kutaniko ambayo iliungwa mkono na kuhani mkuu na “kusanyiko lote la wanaume wazee.”—Matendo 9:1, 2; 22:4, 5.