Yanga: Haji Manara hajatendewa haki, tunamuunga mkono kudai haki vyombo vya juu zaidi

Yanga: Haji Manara hajatendewa haki, tunamuunga mkono kudai haki vyombo vya juu zaidi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
FB_IMG_1658428064969.jpg


Yanga: Tunamuunga mkono manara kudai haki vyombo vya juu zaidi

Klabu ya Yanga imesema kuwa adhabu ya Ofisa Habari wao, Haji Manara kufungiwa miaka miwili kujihusisha na soka na faini ya Tsh. Milioni 20 siyo ya haki na adhabu ni kubwa.

Yanga wametoa tamko na kueleza kuwa inamuunga mkono Manara katika kudai haki yake kwenye vyombo vya juu zaidi vya kimamlaka. Adhabu ya Afisa huyo imetangazwa leo Julai 21, 2022 na Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania.
 
Club ya Yanga imetoa tamko lake kuhusu hukumu aliyopewa Msemaji wake Haji Manara na kusema hajatendewa haki hivyo inamuunga mkono katika kudai haki yake kwenye vyombo vya juu zaidi vya kimamlaka.

“Uongozi wa Club umepokea kwa masikitiko makubwa uamuzi wa Kamati ya maadili ya TFF, adhabu hii inakwenda kuathiri moja kwa moja mchango wa Ndugu Haji Manara katika maendeleo ya mpira wa miguu kwenye Club yake, Ligi Kuu Znz, Ligi Kuu Tanzania bara na Nchi jirani (Burundi) ambazo amezihudumu” imeeleza taarifa ya Yanga.

My take: Karia wewe ni mtu mdogo sana, nazidi kumsihi ndugu Majaliwa aliye kuweka hapo kuwa akupigie simu kukujulisha kuwa wewe ni mdogo sana. Namkumbusha ndugu Majaliwa kuwa alikupigia simu wewe baada ya yeye kupokea simu toka sehemu nyingine. Atafakari.
 
Hivi kuwa na pakti ya embassy na kiberiti ni kosa katika nchi hii ya wayebusi.
 
Utopolo bwana.wanasahau kuwa malipo NI hapa hapa duniani.
alitukanwa Barbara gonzalez mtoto wa watu akakaa kimya.
Sasa huyu aliyemvaa ni level nyingine.kwa hyo wao walikuwa wanafurahi rais wa mpira alitukanwa na manara?.
TFF Hawa utopolo ni wajeuri.
 
Unahalakia wapi?
Muulize moderator aliye edit , na mara nyingi tumeomba sana hawa moderator wanaoedit heading za nyuzi zetu wawe ni wale wenye weledi basi , makosa ya kuedit kwake natupiwa mimi !
 
Back
Top Bottom