Yanga imekata moto, Ijiandae kwa vipigo

Yanga imekata moto, Ijiandae kwa vipigo

Kinachomtokea Gamond saizi ndio kilichomtokea Rhulan Mokwena.
Baada ya kucheza na Yanga kila mtu akajua kumbe hawa ukipaki Semi hawaendi ikawa ngumu tena kwao kushinda ndo mana jamaa wamemtoa!
Gamond ligi kuu wameshamsoma ukichanganya na wachezaji nao wanaugua homa ya kikosi kipana hawana jitihada zaidi...
Yani kimataifa wakitusoma kama walivyotusoma ligi kuu tumekwisha
Mkuu 🫡
 
Huu ndo ukweli ulio wazi. Ile circle ya mafanikio kwa Wananchi inaenda kutamatika msimu huu.

Timu haina mbinu mbadala, ukizuia zile pass mpenyezo basi hawawezi kupata bao.

Msimu huu tujiandae tu kwa vilio maana hata huko Klabu bingwa sidhani kama tutatoboa huko kwenye makundi...

Nipo tayari kuitwa mbumbumbu/kolo
Wewe ni mbumbumbu
 
Mkuu,tatizo siyo kushinda goli moja moja kama usemavyo!

Hata wakati wa Nabi tulikuwa tunashinda hivyo hivyo Kwa taabu na tukawa mabingwa!

Tatizo mbinu za Gamondi Huwezi fananisha na Nabi,Gamondi mbinu zake ni open mno na makocha wengi hapa ndani wameshazisoma,ni tofauti na Nabi,Nabi alikuwa akifanya mabadiliko ya Mchezaji mmoja tu kikosi kizima kinabadilika kiuchezaji na inakuwa hatari sana!

Gamondi yeye akifanya mabadiliko unakuta mambo ni yale Yale tu!

Kimataifa Gamondi atafanya vizuri kwasababu ni timu ambazo tunakutana nazo mara moja,lakini humu ndani Gamondi atapata taabu sana kwasababu makocha wengi wameshamsoma!

Kwasababu timu pinzani Kucheza Kwa kupaki bus wameshaelewa kabisa kwamba wakipaki bus Kwa mbinu za Gamondi hawezi kupangua kwasababu Hana wachezaji wa kulazimisha!

Wachezaji kama AZIZ KI,NZENGELI,MUDATHIR,CHAMA na DUBE,yaani ilitakiwa wakifika ndani ya eneo la 18 la mpinzani wawe wakatili kupita maelezo hata kama wasipofunga lakini kila mtu atakuwa ameona hatari walizosababisha!

Lakini ukiwangalia hao wachezaji ndiyo kwanza wanaongoza Kwa kutoa na Kucheza maboko!,that's why timu zinapaki bus kwakuwa wanajua Kwa wachezaji hao wa Yanga hakuna wa kuwasumbua!
Nenda kafundishe wewe unaandika gazeti refu hata danadana hujawahi kupiga jinga sana wewe yanga sio ya baba Yako acha shobo nayo
 
Huu ndo ukweli ulio wazi. Ile circle ya mafanikio kwa Wananchi inaenda kutamatika msimu huu.

Timu haina mbinu mbadala, ukizuia zile pass mpenyezo basi hawawezi kupata bao.

Msimu huu tujiandae tu kwa vilio maana hata huko Klabu bingwa sidhani kama tutatoboa huko kwenye makundi...

Nipo tayari kuitwa mbumbumbu/kolo
Yanga haijakata moto shida Yao ipo nje ya uwanja,kama injinia hata jirudi haraka ubingwa haupo hata gemu za kimataifa mtashuhudia vituko chakufa wale WOTE waliomsaidia kuchukua ubingwa mara tatu awakusanye haraka na kupatana nao.Yeye ni rais wa yanga KAZI yake ya kwanza ni kuwaunganisha wananchi na siyo kuwagawa Hilo ndilo lililo wasumbua Simba kwa kumbeza manara harafu ikawagharimu kwa kuamini pesa za moo ndiyo kila kitu wenzao hawana mchango WOTE.Gemu na kmc wamekosa magoli MENGI kweli ila afanye niliyosema ataona matokeo yake akizubaa mtani atashinda kwenye dabi
 
Mkuu acha Ubishi,sote mpira tunaangalia,Ukweli ni kwamba,Yanga kwasasa hawachezi vizuri!

Hatuitaji timu ishinde Magoli mengi but mpira uonekane!

Yanga kwasasa inakosa kuwapa pressure wapinzani,mipira mingi wanarudisha nyuma badala ya kupeleka pressure Kwa mpinzani!,Ile timu ya miezi michache nyuma ambayo ilikuwa ikiwapa presha wapinzani Sasa hivi ni kama imefifia!

Pia Gamondi abadilike,aanze kuwaamini wachezaji,sijaona sababu ya Aucho Leo Kucheza,nje una Sure boy na Mkude!


Akiendelea kukaza fuvu na style yake hii ya Uchezaji,Ubingwa utakuwa historia!

Nasredin Nabi alikuwa hatabiriki,japo alikuwa na wachezaji wa kawaida lakini kila Mchezaji alipata nafasi ya Kucheza na akaonyesha Ubora wake!,Tatizo la Gamondi anatabirika na ndiyo maana makocha wengi wameshamsoma!

Nabi alikuwa akikubadilishia wachezaji wawili tu kila kitu kinabadilika,huyu Gamondi yeye akibadili Mchezaji hakuna kinachobadilika!
Hukuangalia mechi wewe, unaongelea presha ipi kwa wapinzani? Hao KMC wameokoa Mpira kwenye mstari wa goli zaidi ya mara tatu. Hebu tuwaheshimu wapinzani pia.
 
Yanga haijakata moto shida Yao ipo nje ya uwanja,kama injinia hata jirudi haraka ubingwa haupo hata gemu za kimataifa mtashuhudia vituko chakufa wale WOTE waliomsaidia kuchukua ubingwa mara tatu awakusanye haraka na kupatana nao.Yeye ni rais wa yanga KAZI yake ya kwanza ni kuwaunganisha wananchi na siyo kuwagawa Hilo ndilo lililo wasumbua Simba kwa kumbeza manara harafu ikawagharimu kwa kuamini pesa za moo ndiyo kila kitu wenzao hawana mchango WOTE.Gemu na kmc wamekosa magoli MENGI kweli ila afanye niliyosema ataona matokeo yake akizubaa mtani atashinda kwenye dabi
Imani za kishirikina.. Sikujua kwamba Manara anaweza kuwa suluhisho la madhila ya Manchester United..
 
Selection ya Gamond siku za karibuni imekuwa mbovu, Clement mzize ni complete package ila utashangaa anaanza Dube.

Timu inatakiwa ijengwe kumzunguka Pacome ila unashangaa hata benchi hayupo..
Huu ndo ukweli ulio wazi. Ile circle ya mafanikio kwa Wananchi inaenda kutamatika msimu huu.

Timu haina mbinu mbadala, ukizuia zile pass mpenyezo basi hawawezi kupata bao.

Msimu huu tujiandae tu kwa vilio maana hata huko Klabu bingwa sidhani kama tutatoboa huko kwenye makundi...

Nipo tayari kuitwa mbumbumbu/kolo
Yanga wanahitaji kufanya mazoezi ya kutosha jinsi ya kupangua ngome ya watu 10, how to penetrate low blocking team
Wabongo mna tatizo sana.. Hivi huwa mnaziangalia kweli match? Hivi huwa mnadhani wachezaji wa timu pinzani wenyewe hawajifunzi kitu? Mlitarajia nini kwa kucheza na timu ambayo imeshusha wachezaji wake wote na kuwa park golini?
Kabla ya kufikiri Yanga imeshu viwanga ulipaswa pia uuangalie mchezo badala ya kusubiri magoli pekee
 
Defence ya Yanga inapitika kirahisi sana, ni umakini mdogo wa washambuliaj wa KMC ndio umepelekea clean sheet kwa Diara leo. Ukija kweny build up hapo ndo tunazidi kupotea.. Mpinzani akipaki bus kwisha habari yetu.. tuna bakia kupiga back pass tu muda uende
Mashambulizi ya jana ya KMC ni mashuti mawili ya Long Range, sasa hapa unamlaumu beki anapitika kirahisi,mtu kapiga mita zaidi ya thelathini, halafu unasema wanapitika how.Nyie wengine mpira sijui mnaangaliaje,long range unamlaumu beki....... duu.

Huu uzi wako nitakukumbusha baada mechi chache tu zijazo.
 
Wanongo mna tatizo sana.. Hivi huwa mnaziangalia kweli match? Hivi huwa mnadhani wachezaji wa timu pinzani wenyewe hawajifunzi kitu? Mlitarajia nini kwa kucheza na timu ambayo imeshusha wachezaji wake wote na kuwa park golini?
Kabla ya kufikiri Yanga imeshu viwanga ulipaswa pia uuangalie mchezo badala ya kusubiri magoli pekee
Umesoma na kukielewa nilicho kiandika kuna sehemu nimeongelea magoli?
 
Huu ndo ukweli ulio wazi. Ile circle ya mafanikio kwa Wananchi inaenda kutamatika msimu huu.

Timu haina mbinu mbadala, ukizuia zile pass mpenyezo basi hawawezi kupata bao.

Msimu huu tujiandae tu kwa vilio maana hata huko Klabu bingwa sidhani kama tutatoboa huko kwenye makundi...

Nipo tayari kuitwa mbumbumbu/kolo
samahani mkuu hapa umeandika kiufundi au mihemko ya kimpira?
 
Selection ya Gamond siku za karibuni imekuwa mbovu, Clement mzize ni complete package ila utashangaa anaanza Dube.

Timu inatakiwa ijengwe kumzunguka Pacome ila unashangaa hata benchi hayupo..
Mpira Ni biashara wewe huwezi kuelewa. Yanga Ni timu Bora kwasasa kuliko timi yoyote Tanzania. Ubora alio nao yanga, sisi Simba Tunasubiri. Hata mchezo ujao NBC yanga atashinda 1-0
 
Selection ya Gamond siku za karibuni imekuwa mbovu, Clement mzize ni complete package ila utashangaa anaanza Dube.

Timu inatakiwa ijengwe kumzunguka Pacome ila unashangaa hata benchi hayupo..
Yaani kaka unamfananisha dube na mzize? Kuwa serious
 
Wapenetrate ngome ya watu 10 ili iweje? Pia mliojibiwa pale ni zaidi ya wewe
The main objective of a team is to win a match, have made my suggestion for future reference . I will never ever express my mind, to please your mind set, similarly to think the way you want me to
 
Gamondi anapanga wachezaji kulingana na upinzani .
Msimu huu timu dhaifu zinafungwa goli chache Timu ngumu zinafungwa goli nyingi .
Na muhimu kupumzisha wachezaji Muhimu Kwenye mechi ndogo .
Msimu uliopita hakufanya hayo, si team ndogo au kubwa zote zilipata kipigo cha magoli mengi. Hoja yako haina mashiko
 
The main objective of a team is to win a match, have made my suggestion for future reference . I will never ever express my mind, to please your mind set, similarly to think the way you want me to
Has the team not won? This isn’t about me, and it's not personal. Did the team underperform? If not, why comment as though the team is at its worst? Are you considering the opponents? Do you see that they recognized how strong Yanga is, which is why they focused so heavily on defending their goal? When you’re analyzing a match, you have to consider both sides, not just your own. We’ve got to give credit where it’s due.
 
Back
Top Bottom