Yanga msishangae sana, hizi hasira mmetupa nyie wenyewe

Yanga msishangae sana, hizi hasira mmetupa nyie wenyewe

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Tunajua upande wa pili bado wamepigwa na butwaa wa hizi sajili zinazoendelea pale Msimbazi. Msimu huu ulioisha kuna mambo yaliyotokea katika ligi na hasa mashindano ya kimataifa ambayo kwa kweli yalituumiza sana wanaSimba. Sitaongelea sana ligi ya NBC maana huku tulikuwa tunawamudu ni basi tu kuna steps chache tuliteleza ila nitagusia mashindano ya kimataifa.

Ni kweli Yanga walifika fainali ya shirikisho kwa ubovu wa timu walizokutana nazo ila haipingiki kuwa Yanga msimu uliopita walikuwa na focus na nidhamu ya hali ya juu uwanjani na nje ya uwanja. Tulipowakumbusha hata sisi fainali tulifika, hawakutaka kusikia hili wala lile na nguvu yao ilikuwa kubwa sana kupinga kumbukumbu hiyo. Hawa washenzi wako vizuri kwenye idara ya propaganda. Huko CAF mambo yao yalikuwa yanakwenda yamenyooka kama rula. Dua zetu zilikuwa wakwame ila kila hatua kenge wale walikuwa wanatembea tu, kwa kweli tulipata ahueni sana walipokosa lile kombe maana daah!! Kamba tu zile walizopata wamekuja kutupulizia mimoshi pale Msimbazi, ingekuwa ndoo je?

Safari hii hatutaki hali ile ijirudie, huu ni wivu wa maendeleo tu. Hatutazuia wala kuwafanyia fitna wanachofanya wao ila tutahakikisha mafanikio yetu kimataifa yanazidi yao. Hii ndiyo siri ya usajili huu wa kutisha na wa hasira. Na hivi CAF wamehakikisha janja janja ya kudondokea shirikisho haiwezi kuwepo, basi tupo tayari kupimana makali.

Kila la kheri.
 
358132229_18226265845226150_1278681305450744382_n.jpg
 
Akili za Mokolo, Rage hakukosea.
Mnajipa ma confo kua mtatoboa Yanga hata Group stage hakanyagi, atatolewa mapema tu.
Haya subiri ije iwe vice versa muanze kudai bilioni ISHIRINI zenu.
 
N vema ungeandika haya baada ya mashindano kuanza na kikosi kupata muunganiko mzuri

Mkuu unakumbuka ya SAWADOGO MOHD WATARA OKRA mliandika mashair Kama haya ya mapambio lakn kilochotokea n wewe mwenyewe umeona

MUDA NI MWALIMU MZURI

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbe rolemodel wenu ni YANGA SC.

Mimi nilijuaga ni Al Ahly, Mamelodi na Wyday huko.

Kweli maisha yanaenda kwa kasi aisee.[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji599]
 
Usinene ukamara,muda utasema kama nyie ni mbumbumbu au mikia
 
Akili za Mokolo, Rage hakukosea.
Mnajipa ma confo kua mtatoboa Yanga hata Group stage hakanyagi, atatolewa mapema tu.
Haya subiri ije iwe vice versa muanze kudai bilioni ISHIRINI zenu.
Hakuna ndondokela hapa. Ukitolewa champions league tukutane ubaruku.
 
Tunajua upande wa pili bado wamepigwa na butwaa wa hizi sajili zinazoendelea pale Msimbazi. Msimu huu ulioisha kuna mambo yaliyotokea katika ligi na hasa mashindano ya kimataifa ambayo kwa kweli yalituumiza sana wanaSimba. Sitaongelea sana ligi ya NBC maana huku tulikuwa tunawamudu ni basi tu kuna steps chache tuliteleza ila nitagusia mashindano ya kimataifa.

Ni kweli Yanga walifika fainali ya shirikisho kwa ubovu wa timu walizokutana nazo ila haipingiki kuwa Yanga msimu uliopita walikuwa na focus na nidhamu ya hali ya juu uwanjani na nje ya uwanja. Tulipowakumbusha hata sisi fainali tulifika, hawakutaka kusikia hili wala lile na nguvu yao ilikuwa kubwa sana kupinga kumbukumbu hiyo. Hawa washenzi wako vizuri kwenye idara ya propaganda. Huko CAF mambo yao yalikuwa yanakwenda yamenyooka kama rula. Dua zetu zilikuwa wakwame ila kila hatua kenge wale walikuwa wanatembea tu, kwa kweli tulipata ahueni sana walipokosa lile kombe maana daah!! Kamba tu zile walizopata wamekuja kutupulizia mimoshi pale Msimbazi, ingekuwa ndoo je?

Safari hii hatutaki hali ile ijirudie, huu ni wivu wa maendeleo tu. Hatutazuia wala kuwafanyia fitna wanachofanya wao ila tutahakikisha mafanikio yetu kimataifa yanazidi yao. Hii ndiyo siri ya usajili huu wa kutisha na wa hasira. Na hivi CAF wamehakikisha janja janja ya kudondokea shirikisho haiwezi kuwepo, basi tupo tayari kupimana makali.

Kila la kheri.
Dua la kuku alimpati mwewe mkuu, kwa akili zenu ndogo bado mmejenga mentality ya kwamba yanga anaferi tena klabu bingwa na nyie mtafanya vizuri? Mnachosahau ni kwamba yanga safari hii anaingia klabu bingwa akiwa anajiamini vya kutosha na sababu za kujiamni anazo, Sababu ya kwanza ni uzoefu mkubwa alioupata kwenye michuano ya shirikisho, kacheza fainali ya shirikisho akiwa kapitia changamoto za kila aina nyumbani na ugenini,
Kakutana na kila aina ya timu, kutoka afrika magharibi mpaka za waarabu anajua namna ya kudili nazo, Sababu ya pili ni ubora wa squad yao, yanga wametengeneza kikosi bora ambacho bado kipo mpaka sasa, uti wa mgongo wa timu ambao ni wachezaji muhimu awajaguswa mpaka sasa, kwa maana iyo kitakachoongezeka ni kuziba mapungufu machache yaliyojitokeza msimu ulioisha, Simba mtakuwa na maingizo mapya mengi kwenye kikosi chenu na mpira sio kama ugali wa kusonga hapo hapo na kula, muunganiko wa kikosi aupatikani kwa haraka kama unavyodhani wewe, kwa mantiki iyo unaodhani wataaga mashindano mapema kwa kukariri maisha ndio watakaowaziba midomo kwa mara nyingine tena kwa kuwa wana kila sababu ya kufanya ivyo!
 
Back
Top Bottom