Yanga ni timu iliyoimarika sana kimbinu na kiufundi, michuano mikubwa na uzoefu vimewasaidia sana

Yanga ni timu iliyoimarika sana kimbinu na kiufundi, michuano mikubwa na uzoefu vimewasaidia sana

Majok majok

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2023
Posts
783
Reaction score
2,057
Kuna baadhi ya mashabiki na wachambuzi wanasema Jana yanga kacheza kawaida sana lakini awajui gamond alikuwa na mbinu Gani kwenye Ile mchezo, zifuatazo ni mbinu za gamond na sababu ya kucheza kwa akili kubwa;

1) Gamond aliitaji kumsoma mpinzani wake kwakuwa alikuwa ajawaona Simba na wachezaji wao popote, pia mbinu za kocha wao!

2) Gamond alijua ulikuwa ni mchezo wa matokeo na sio kufurahisha watu ivyo alikwenda kucheza objective football ili afuzu kwenda hatua inayofata aijalishi kachezaje, izo ni mbinu alizoziaply kutoka kwenye michuano mikubwa ya caf champions league namna ya kufuzu hatua za robo fainali na nusu fainali!

3) Gamond alijua kabisa kwamba Kuna mechi nyingine ingechezwa baada ya siku 3 ambayo ni fainali ivyo Kama angetumia nguvu kubwa dhidi ya Simba na akafuzu wachezaji wangepata fatique kubwa kuelekea mechi ya fainali ambayo wanakwenda kukutana na Azam, ivyo alikuwa anapoozesha mchezo makusudi ili kutunza nishati ya mechi inayofata ambayo itapigwa ndani ya siku 3!

Izo ni sababu 3 muhimu za kiufundi zilizopelekea yanga ionekana aijacheza kwenye kiwango Chao kile tulichokizoea, mambo ya kimbinu na kiufundi ndiyo yanayozidi kuiimarisha yanga Kila siku pamoja na UZOEFU wao kwa sasa kutokana na kucheza na timu ngumu nyingi wamejifunza mambo mengi sana!
 
Back
Top Bottom