John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya Yanga dhidi ya Mbeya City, mchezo umeshaanza kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.
YANGA 0-0 MBEYA CITY - FULL TIME
Dk 1: Timu zimeanza kwa kusomana, matokeo ni 0-0.
Dk 5: Mchezo una kasi na timu zote zinashambuliana kwa zamu.
Dk 10: Mashambulizi ya zamu kwa timu zote, Mbeya City wanaonekana kufunguka.
Dk11: Winga wa Yanga, Moloko yupo chini, anapewa matibabu baada ya kuumia.
Dk 17: Zawadi Mauya wa Yanga anapiga shuti kali kutoka nje ya 18, kipa wa Mbeya City, Deo Munisha anapangua na kisha kuudaka.
Dk 18: Mchezo una kasi, Mbeya City hawaonyeshi dalili ya kukaa nyuma kuzuia, Yanga nao wanatengeneza mashambulizi mdogomdogo.
Dk 20: Kasi ya mchezo inatulia kidogo.
Dk 23: Yanga wanawapa presha Mbeya City.
Dk 25: Yanga wanapata kona lakini hawaitumii vizuri.
Dk 28: Yanga wanafika langoni mwa Mbeya City mara mbili lakini mipira inaishia kwa kipa Deo Munishi.
DK 30: Dickson Job wa Yanga anafanya kazi nzuri ya kuzuia mashambulizi ya Mbeya City.
Dk 31: Yanga wametulia na kumiliki mpira muda mwingi.
Dk 35: Saido anachezewa faulo nje ya eneo la 18, inakuwa faulo.
Dk 36: Saido anapiga inagonga ukuta na kuokolewa.
Dk 40: Mchezo bado ni wa kushambuliana kwa zamu.
Dk 45: Kipa wa Yanga yupo chini ameumia na anapatiwa matibabu.
Dk 45+5: Licha ya kuongezwa dakika 3 lakini bado mchezo unaendelea
Dk 45: MAPUMZIKO
Dk 46: Kipindi cha pili kimeanza.
Dk 49: Yanga wanaumikili mpira muda mwingi lakini safu ya ulinzi ya Mbeya City inakuwa ngumu.
Dk 50: Saido anapambana kutafuta nafasi lakini anakutana na upinzani mgumu.
Dk 55: Mbeya City wanarudi nyuma kidogo na kuwapa nafasi Yanga kuuchezea mpira.
Dk 63: Yanga wanaendelea kuonyesha kuwa imara hasa sehemu ya kati.
Dk 67: Yanga wanafanya shambulizi kali, Mayele anashindwa kutumia nafasi nzuri aliyopata kutoka kwa Aucho.
Dk 70: Yanga wanapata faulo karibu na lango la Mbeya City.
Dk 71: Saido anapiga lakini inaokolewa.
Dk 75: Kasi ya mchezo imepungua kiasi, timu zote zikipambana kutafuta nafasi ya kufunga.
Dk 76: Zawadi Mauya anacheza vizuri na Farid Musa lakini mpira unapotea.
Dk 77: Mayele anabaki na kipa lakini mwamuzi anapuliza filimbi kumaanisha ni faulo kwa Mbeya City.
Dk 86: Presha ni kubwa kwa timu zote, lakini Yanga ndiyo wanaonekana kuwa na presha ya kuafuta ushindi.
Dk 90: Mbeya City wanachelewesha kuanza mpira.
Dk 90: Yanga wanapata kona lakini wanashindwa kuitumia vizuri.
Dk 90: Mwamuzi anamaliza mchezo matokeo ni 0-0.
FULL TIME
YANGA 0-0 MBEYA CITY - FULL TIME
Dk 1: Timu zimeanza kwa kusomana, matokeo ni 0-0.
Dk 5: Mchezo una kasi na timu zote zinashambuliana kwa zamu.
Dk 10: Mashambulizi ya zamu kwa timu zote, Mbeya City wanaonekana kufunguka.
Dk11: Winga wa Yanga, Moloko yupo chini, anapewa matibabu baada ya kuumia.
Dk 17: Zawadi Mauya wa Yanga anapiga shuti kali kutoka nje ya 18, kipa wa Mbeya City, Deo Munisha anapangua na kisha kuudaka.
Dk 18: Mchezo una kasi, Mbeya City hawaonyeshi dalili ya kukaa nyuma kuzuia, Yanga nao wanatengeneza mashambulizi mdogomdogo.
Dk 20: Kasi ya mchezo inatulia kidogo.
Dk 23: Yanga wanawapa presha Mbeya City.
Dk 25: Yanga wanapata kona lakini hawaitumii vizuri.
Dk 28: Yanga wanafika langoni mwa Mbeya City mara mbili lakini mipira inaishia kwa kipa Deo Munishi.
DK 30: Dickson Job wa Yanga anafanya kazi nzuri ya kuzuia mashambulizi ya Mbeya City.
Dk 31: Yanga wametulia na kumiliki mpira muda mwingi.
Dk 35: Saido anachezewa faulo nje ya eneo la 18, inakuwa faulo.
Dk 36: Saido anapiga inagonga ukuta na kuokolewa.
Dk 40: Mchezo bado ni wa kushambuliana kwa zamu.
Dk 45: Kipa wa Yanga yupo chini ameumia na anapatiwa matibabu.
Dk 45+5: Licha ya kuongezwa dakika 3 lakini bado mchezo unaendelea
Dk 45: MAPUMZIKO
Dk 46: Kipindi cha pili kimeanza.
Dk 49: Yanga wanaumikili mpira muda mwingi lakini safu ya ulinzi ya Mbeya City inakuwa ngumu.
Dk 50: Saido anapambana kutafuta nafasi lakini anakutana na upinzani mgumu.
Dk 55: Mbeya City wanarudi nyuma kidogo na kuwapa nafasi Yanga kuuchezea mpira.
Dk 63: Yanga wanaendelea kuonyesha kuwa imara hasa sehemu ya kati.
Dk 67: Yanga wanafanya shambulizi kali, Mayele anashindwa kutumia nafasi nzuri aliyopata kutoka kwa Aucho.
Dk 70: Yanga wanapata faulo karibu na lango la Mbeya City.
Dk 71: Saido anapiga lakini inaokolewa.
Dk 75: Kasi ya mchezo imepungua kiasi, timu zote zikipambana kutafuta nafasi ya kufunga.
Dk 76: Zawadi Mauya anacheza vizuri na Farid Musa lakini mpira unapotea.
Dk 77: Mayele anabaki na kipa lakini mwamuzi anapuliza filimbi kumaanisha ni faulo kwa Mbeya City.
Dk 86: Presha ni kubwa kwa timu zote, lakini Yanga ndiyo wanaonekana kuwa na presha ya kuafuta ushindi.
Dk 90: Mbeya City wanachelewesha kuanza mpira.
Dk 90: Yanga wanapata kona lakini wanashindwa kuitumia vizuri.
Dk 90: Mwamuzi anamaliza mchezo matokeo ni 0-0.
FULL TIME