Tetesi: Yanga Sc kuachana na Kocha Mkuu Nabi

Tetesi: Yanga Sc kuachana na Kocha Mkuu Nabi

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
d888af0d1aad44669bac07436371b610_312506272_851013876036703_1430470041145433183_n.jpg

YANGA YAACHANA NA KOCHA NASREDDINE NABI.
Taarifa rasmi zitakuijia hivi punde. Usiondoke

Anaandika Jemedari Saidi

Habari za uhakika zinasema Kocha NASRIDEEN MOHAMED NABI maisha yake na Yanga SC yamefikia tamati na ataondoka muda wowote.

Pamoja na mambo mengine lakini usajiri wa baadhi wa mastaa unahusishwa, huku ikisemekana kwamba aligomea kwa kutoa sababu za kiufundi. Nabi pia anahusishwa na magomvi na wasaidizi wake kwa muda sasa na misimamo mikali.

Kwenye soka sajili zingine ni "Political Signings" ambazo wakubwa ndiyo wanajua zaidi kwanini wanamtaka Kisinda, Morrison au Makambo kwa mfano, kuliko vile Kocha anavyotaka.

Kwahiyo kocha kuleta mambo yake ya kiufundi ni kutaka kuchelewesha maisha kuwa mepesi na kuyatia ugumu.

Kocha wa Vipers ya Uganda Mbrazil Roberto Oliveira anahusishwa na kuchukua nafasi ya Nabi ambaye ameiongoza Yanga SC kwenye michezo 43 ya Ligi Kuu bila kupoteza.

Mechi ya Derby ilikuwa ndiyo njia rahisi kumuondolea kama Yanga wangepoteza lakini mechi ikaisha kwa sare. Kama atafika salama mechi dhidi ya Club Africain itakua mtihani mkubwa sana kwake, asipotoboa hana chake. Waswahili wanasema 'Kamba hukatikia pabovu

Credit: Bin Kazumari
 
Simba yamfukuzisha kazi Nabi ndicho kilipaswa kuwa kichwa cha habari, ule moto waliopelekewa jpili ilikuwa lazima hiki kitokee

Ingawa sasa timing ya kumfukuza imekuwa mbaya maana atarudi kwao na yanga mna mechi na timu ya kwao mtapigwa nyingi sana mkienda

Na jumatano na kmc ni kipigo cha kwanza wananchi watakipokea
 
Kwa lile pira alilotembezewa na simba juzi wana haki ya kuachana nae, maana walisema wanajipima na simba kimataifa. Watamchukua mgunda sasa
Uchawi sio lazima tunguli kwahio mechi iliisha ngapingapi???na fifa wanaandika atokeo ni 1 kwa 1 au wanaandikaje??kwamba 1 kwa 1 ila huyu alitembezewa pila????ndo yale unamfunga al ahly makundi alafu unajisifu wakati mwenzako anaenda kuchukua ubingwa
 
Back
Top Bottom