Tetesi: Yanga Sc kuachana na Kocha Mkuu Nabi

Tetesi: Yanga Sc kuachana na Kocha Mkuu Nabi

uchawi sio lazima tunguli kwahio mechi iliisha ngapingapi???na fifa wanaandika atokeo ni 1 kwa 1 au wanaandikaje??kwamba 1 kwa 1 ila huyu alitembezewa pila????ndo yale unamfunga al ahly makundi alafu unajisifu wakati mwenzako anaenda kuchukua ubingwa
Mashabiki ya Simba yalishaitwa na Ismail Aden Rage kwamba ni mambumbumbu! Eti jitu linasimama Yanga walitembezewa mpira! Pambaff!
 
Alimfunga ngapi? Budog'ombehi!
Acha boli itembee.
JamiiForums-1742009958.gif
 
Kwa lile pira alilotembezewa na simba juzi wana haki ya kuachana nae, maana walisema wanajipima na simba kimataifa. Watamchukua mgunda sasa
Defense za Yanga zote ni mbovu , Safu ya ushambuliaji ipo vizur but poor organized ( mostly hawachezi ki timu )
 
Kama hii tetesi ina ukweli basi Yanga haina uongozi.

Hersi ni mbabaishaji, huwezi kumtimua kocha aliyekupa ubingwa kwa mechi zaidi ya 40 bila kufungwa

Kama kumtimua kocha kumesababishwa na perfomance ya kimataifa basi nalo mnatakiwa mjitafakari sana.

Kwasababu wote mechi tuliangalia na kitu kilichoonekana ilikuwa ni uzembe wa wachezaji na sio Kocha.

Mayele alikuwa anacheza kwa faida yake na sio timu, kila mtu anataka aibuke worrior. Sasa hapo kosa la Nabi liko wapi?
 
Hizi habari za kuuzia magazeti. Nabi bado yupo sana Yanga
 
View attachment 2397066
YANGA YAACHANA NA KOCHA NASREDDINE NABI.
Taarifa rasmi zitakuijia hivi punde. Usiondoke
Professionally ulipaswa utoe Credit kwa Source ya hii Taarifa ambako ni katika Gazeti la Michezo la Mwanaspoti na siyo Kujifanya kama ni yako Mwenyewe umeitafuta ( umeichimba ) wakati hata Uwezo huo huna.

Povu rukhsa baada ya hii Sindano.
 
Kama hii tetesi ina ukweli basi Yanga haina uongozi.

Hersi ni mbabaishaji, huwezi kumtimua kocha aliyekupa ubingwa kwa mechi zaidi ya 40 bila kufungwa

Kama kumtimua kocha kumesababishwa na perfomance ya kimataifa basi nalo mnatakiwa mjitafakari sana.

Kwasababu wote mechi tuliangalia na kitu kilichoonekana ilikuwa ni uzembe wa wachezaji na sio Kocha.

Mayele alikuwa anacheza kwa faida yake na sio timu, kila mtu anataka aibuke worrior. Sasa hapo kosa la Nabi liko wapi?
Ndo maana huwa sitaki ujiite shabiki bali MWANASOKA. Haya ni maoni ya Mtu anayejua soka. Hata Mechi ya juzi naona watu wanamsema Okrah Kwa uchoyo na kumsahau Mayele.

Tukio la Mayele aliyekuwa pembeni kulazimisha kufunga badala ya kutoa pasi kwa Farid Mussa aliyesahaulika na mabeki wa Simba ni Sawa na kutafuta faida binafsi.

Mechi ya Al Hilal alitakiwa kutoa pasi kwa Morrison mara 2 lakini akaopt kupiga na mabeki wakablock. Aziz Ki amesajiliwa kama playmaker, lakini Kila wakati anawaza kufunga.
 
Watu wa Simba mnapata tabu, tukiwambia mechi ya juzi mlikamia mnabisha haya msikilizeni msemaji wenu kinywa chake kwamba Simba ni teja kwa Yanga.


Halafu huyu nae kuongea hivi ndo kutaka Mgunda aonekane mbaya wamfukuze au? Maana Mgunda hajafungwa mpk sasa iwe utopolo au timu nyingine.
 
Back
Top Bottom