changaule
JF-Expert Member
- Jan 10, 2020
- 6,039
- 10,151
Huu mpira wa Media ndio iliifanya SSC kuporomoka sana na kufikia hapo ilipofikia.
Goli ambalo hatuwezi kujivunia nalo deep down lisitutoe kwenye reli kuwa kuna TAFSIRI 2
1. Inawezekana Yanga SC Imeanza kuwa na kiwango cha kawaida au wachezaji wetu wameanza kuchoka, Sijaona Shambulia la hatari lililofanywa na Yanga jana dhidi ya SSC , Gamondi asijekuwa ameanza kuwa mzee wa Objective football , na sasa za mpira kwa ushindi wa butua butua , maneno maneno huku tunaona timu inavyo struggle kupata ushindi hata kwa timu ndogo
2. Inawezekana SIMBA imeimarika ndio maana tunaona yanga anashindwa tena kumfunga SIMBA, tukumbuke Yanga bora ndio iliyofichua Simba mbovu, tuangalie kinyume chake isijekuwa kweli.
Kitendo cha kunywa Supu kwa OWN goal , ni sehemu ya kujitafakari timu kiwango kinashuka au ni nini kinaendelea au wachezaji wameanza kulewa Sifa, SSC jana ilikuwa bora walikosa umakini wao wenyewe otherwise tungelala hata Goli 3.
Hata ile Penalt it was clear penalty but Refa had to balance the game , na kama kungekuwa na VAR , hata goli walilojifunga SSC, halikupaswa kuwa Goli maana mpira ulikuwa nje clear , ni kukosa umakini kwa marefa wetu lakini pia kukosekana kwa technology kama VAR uwanjani otherwise halikupaswa kuwekwa kati.
So sijaelewa furaha ya supu inatoka wapi, ni sawa na ile furaha ya mamelodi kuitoa Yanga, ni ukichaa
Let’s focus na timu yetu kuwa tumeshindwa kutengeneza chances mbele ya SSC iliyoimarika na hii ni red light ahead pamoja kwamba tunaamini tunawachezaji wakubwa.
Hata kutoboa makundi mwaka huu inaweza kuwa ni kipengele. Timu inaanza kushukq kiwango tubaki humo
Umechambua kishabiki sana hii mechi ya jana
1) Unazungumzia wachezaji kuchoka, hivi uliona wachezaji kama Diarra, Azizi Ki, Chama, Dube, Musonda, Abuya hawa walikuwa kwenye mechi za ratiba ya CAF tarehe 15 hapo kuna siku ya kusafiri na siku ya kujiandaa na mechi jumlisha uchovu na mwisho wa siku imetokea hadi mchezaji kufika Tanzania siku ya mechi hivi hili nalo umeshindwa kutumia maarifa kulijua lina athari kiasi gani kwenye mchezo wa jana?
Kuna hawa waliokuwa Tanzania lakii pia wakatumika kwa mechi ngumu dhidi ya D.R.Congo tarehe 15 ni uchovu wa kiasi gani walikuwa nao kuelekea kwenye hiyo mechi?
2) Unasema Simba ina imarika ndio maana Yanga kashindwa kumfunga Simba tena, inamaana matokeo ya jana mwenzetu uliona ni 0-0 na Simba na Yanga wakagawana point? Au kuna mmoja kapata point maanake kuna timu imeshinda mechi.
3) umezungumzia penati ok ni clear penati vipi kuhusu kadi nyekundu ya Hamza ambaye ndiye mtu wa mwisho?
Jana Saliba kala kadi nyekundu kwenye mechi ya Arsenal vs Bournemouth katika tukio linalofanana kabisa na la Hamza vs Dube. Vipi kuhusu Camara kucheza miguu ya mchezaji badala ya mpira katika eneo la 18 baada ya mchezaji wake kutoa boko?
Vipi kuhusu mpira wa Ateba kwenda kufunga ilihali alikuwa katika eneo la kuotea na waamuzi waliacha tu, bila Diarra goli lingehesabika.
4) La mwisho unasema kuwa ule mpira haukustahili kuwa goli kwavile mpira ulikuwa umeshatoka nje, naomba niambie ni teknolojia ipi mwenzetu uliyotumia ukatambua kuwa mpira ulikuwa umevuka mstari kwa asilimia 100? Maana kama Azam hawakuchora mstari wa kivuli kuonesha position ya mpira dhidi ya mstari wewe umewezaji kupata mstari mnyoofu wa kujiridhisha kuwa mpira upo nje kwa asilimia 100?
Mwisho unasema Yanga hawakufanya mashambulizi ya maana, lakini nilijua utaonesha takwimu kuonesha short on target kwa pande zote mbili zipoje ila umeishia kuimba nyimbo za faraja.
Yanga ilikuwa mbovu zamani na kujitafuta haswa na kutengeneza timu ila haikuwahi kufikia kufungwa mara tatu mfululizo na Simba ila nashangaa timu inafungwa mara nne halafu unasema Simba inaimarika huku Yanga inashuka. Kufungwa derby mfululizo sio ishara nzuri ila inakoelekea itakuwa ni mazoea ya Simba kufungwa hata goli moja na kujisifia tumejitahidi.