Yanga usajili wote huo mnakwenda kuweka kambi Bigwa, Morogoro, kweli nyie ni wa kimataifa au wa hapa hapa?

Nyie Makolo Nendeni Mkaweke Kambi Hata Marekani...ila Mkirudi Hapa Kichapo Kipo Pale Pale Na Hatuna Mjadala Na Nyie [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Huu uzi watani zetu wa utopolo wanaudiss kinoma noma🤣🤣🤣
 
Nawaza hapa kwa mfano ingekuwa simba ndyo kabak kamb hapa nchn na yanga kaenda nje ya nchn hakuna rangi wanasimba wangeacha kuona kwa yule zungu pori na wanaharakat wa mchongo...
ila all in all aziz k kasepa na mpunga wa pre season alaf wanakuja kutuongopea et kocha ndyo kapendekeza wabak hapa sas kwann asngependekeza kabla hawajaweka bukng
 
Unaenda kuweka kambi misri kwenye baridi na viwanja vya kisasa halafu unakuja kucheza ligi kwenye uwanja wa nankumbu ni akili au matope?
 
Kule instagram wale wachambuzi wangemkalia Mo kooni aisee. Barba na Mo.wange kosa furaha kwa kusemwa.
 
Japokuwa mimi ni Simba Sc. damu lakini nitakuwa wa mwisho kubeza Yanga kwa hili baada ya Ngao ya jamii na mechi za awali za CAF
 
Hayakuhusu
 
Matokeo ya hizo kambi tutayaona uwanjani ayo mengine ni maneno ya kwenye khanga na vijiwe vya kahawa
Msimu uliopita tuliyaona kimataifa kwa kipigo cha dar 2 lagos
 
Tulia wewe kila mtu na mipango yake tutakutana Lupaso hapo "kupiga gozi"
 
Zamani kabla ya Mechi ya Simba Vs Yanga timu hizo zilikuwa ninaweka kambi nje ya Dar. Moja ikienda Zanzibar nyingine inakwenda Morogoro. Lakini matokeo ya hizo kambi yalikuwa hayaonekani. Kwa uchumi wa kiafrika na Kiwango cha mpira wa kiafrika timu Kuweka kambi ya mazoezi nchini, au nchi yoyote ya Kiafrika yenye Hali ya hewa kama ya Tanzania ni maamuzi sahihi.
 
We unaona sawa kweli, usajili wachezaji wa gharama halafu ukaweke kambi Matombo, au ndio ushabiki maandazi

Kwaiyo ukiweka kambi kaskazini ndio utahifunza mbinu zao.

Nani amekwambia wamebandika mabango ya mbinu zao kwenye viwanja?

[emoji23][emoji23]
 
Kuna msemo unasema kambi popote.

Tusiwaseme saana watani zetu, tusubiri msimu uanze.
Kambi inajumuisha vitu viingi saana, ingekuwa ubora tu, basi timu za uingereza ziingekuwa zinatoka au kwenda vinchi vidogo mfano wa kama Austria huko.

Manchester United wameenda Thailand kufanya pre season.

Naona kuna mbinu za kimpira ambazo kocha Erik Ten Hag anaenda kuchukua kutoka kwenye Vilabu vya mpira vya Tailand.
 

Ongeza sauti hatujakusikia.

 
Ni ushamba tu unatusumbua,haina haja ya kwenda mbali kama facilities zipo hapa hapa, kuna jamaa kawekeza sana Arusha...... niliwahi fanya tour pale.... natamani Yanga wakatulie kule

Kwa mujibu wa mleta mada.

Anataka Yanga SC waendw huko kaskazini wakajifunze mbinu za wenzetu waarabu.

Ko yeye ndio kaona hilo ndio lengo kuu la kuweka kambi nje.

Barcelona na Madrid wako marekani kuweka kambi. Nadhani kuna mbinu hivi vilabu vinaenda kujifunza kutoka kwenye vilabu ya marekani.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…