Yanga yaingia mkataba wa Tsh Bilioni 34.8 na Azam Media

Yanga yaingia mkataba wa Tsh Bilioni 34.8 na Azam Media

Kobello

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2011
Posts
8,967
Reaction score
8,547
Klabu kongwe ya Young Africans Sports Club leo inaingia mkataba na Azam Media utakaogharimu jumla ya shilingi Bilioni 34.8 (Bilioni 41 with VAT). Mkataba huu utadumu kwa miaka kumi(10) na utafanyiwa marudio/maboresho baada ya miaka mitano.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Kaimu Katibu mkuu wa klabu ya Yanga Haji Mfikirwa alisema kuwa mkataba huu, utakua ni kichocheo kwa wadau wote wanaotaka kushirikiana na klabu hii ya Yanga. Kwa mfano, wawekezaji, makampuni ya matangazo n.k.

Kabla ya hapo, Katibu Mwenezi wa klabu ya Yanga Hassan Bumbuli alibainisha kuwa Yanga ndiyo klabu ambayo habari zake zinafuatiliwa sana hewani, magazetini (print) na kidijitali kwa ujumla. Akishukuru, CEO wa AZAM MEDIA ndugu Tido Mhando aliahidi kuboresha huduma ya matangazo inayotolewa na Azam Media. kalabu ya Yanga itakuwa inapokea jumla ya Shilingi 200 kwa mwezi, ambazo zitaongezeka kwa jumla ya milioni 20 kila mwaka hadi kufikia milioni 380 kwa mwezi.

Klabu ya Yanga itaweza kupokea hadi shilingi Bilioni 5.9 kwa mwaka kama Media rights ambapo kwa miaka kumi (10), watapokea kiasi cha Shilingi Bilioni 52.4 (jumlisha VAT).

Klabu nyingine pia zinakaribishwa kuingia mkataba na Azam Media.

My Take:
Simba (Vunjabei Sports Club) tunasubiri mkataba wenu.
 
Yanga mabadiliko yake ni ya kisomi sana..

Ndio raha ya kuwa na bosi msomi mwenye PHD na nafasi ameipata kwa mchakato wa wazi wa kugombania fursa.. sio mambo ya nyumba ndogo ya bosi inapewa uongozi wa timu kubwa bila uzoefu wa kuongoza hata timu ya rede
 
Ko mechi pia tutakuwa tukiziangalia kupitia hio channel yao ya youtube au naomba ufafanuzi kidogo ?
Nafikiri ukiacha za ligi michezo ya kirafiki, maziezi, mahojianl na makala zitakuwa zinaonyeshwa kwenye channel ya Yanga kwenye kingamuzi cha Azam
 
i.e Azam watakuwa wanatengeneza maudhui/contents kuhusu Yanga na kuzirusha kwenye Channels zao?..kama Yanga TV vile au?
Yes EXCLUSIVELY.
Live events zote ni Azam tu.
Hakuna live kurushwa na Global au sijui Dar 24 ... No!
Kama ulisikia Haji AKIIPONDA app ya YANGA. Yale yalikuwa ni maumivu.
Yanga app. imechochea sana mkataba huu, hata zile friendly matches katikati ya Ligi kule Chamazi, Yanga ilikuwa inachukua milioni 25 na Azam waliona jinsi gani Yanga inavyofuatiliwa.
 
Back
Top Bottom