SIDANGANYIKI2015
JF-Expert Member
- Apr 19, 2015
- 1,054
- 114
Wewe nawe....mmetumana au ndio umeingia shifti ya mchana....
Wewe nawe....mmetumana au ndio umeingia shifti ya mchana....
Kumbe wahenga hawakukosea kusema Kuimba nyimbo za kitoto ndio utoto wenyewe......OverBe specific! Usitaje taje maneno yenye mkanganyo hapa. "Shifti" kawaulize mafundi wa nguo za kike
Kumbe wahenga hawakukosea kusema Kuimba nyimbo za kitoto ndio utoto wenyewe......Over
Kama kawaida na ngonjera zako za kujidharau na kujidharirisha,huna cha kushauri hapa kwanza hujielewi kama unaishi kwenye taifa huru linaloongozwa kwa kufuata misingi ya katiba,unawaza mambo ya utawala wa giningi ambao haupo hapa!ustaraabu kitu cha kawaida kama huna constructive ideas bora usichangie hapa kupotosha!
jamii inao watu wa aina mbalimbali, wapo wanaonuifaika na mifumo mibovu kwa maana wao riziki zao zinatoka huko na hawana sifa hivyo watafanya kila njia mifumo mibovu isiondoke.
lakini wapo wenye mawazo ya kuwasaidia wanajamii kuuondokana na mifumo ya ubabaishaji inayowaletea umasikini.
kati yangu mimi na wewe nani yuko kundi gani ni swala la wanajamii kusoma tunayoyachangia na kutubaini hivyo fikra zetu ndizo zitatupambanua na sio mtizamo wangu juu yako au wako juu yangu.
wananchi kufuta ujinga ndio hatua ya kwanza katika kujiletea maendeleo.
Pumba tupu ulizoweka hapo, kwani nani kakwambia katiba yetu hasa hii inayopendekezwa sio nzuri mpaka uanze kuifananisha na mambo ya Burundi.lipo tatizo la nchi nyingi kuwa na nadhalia ya mihimili mitatu ya utawala lakini mihimili hiyo kuuliwa kutokana na jinsi mihimili hiyo inavyoundwa katika katiba na mwisho ni kuwa na mhimili mmoja katika uhalisia wenye nadhalia ya mihimili mitatu.
unapokuwa na mhimili mmmoja uliounganisha mihimili mingine pale inapotokea mhimili mmoja kutenda kinyume badala ya mihimili mingine kurekebisha basi inasapoti.
tuwe makini na uandishi wetu wa katiba kwa kuangalia iwapo siku moja atatokea kiongozi mmoja aliyechaguliwa na wananchi akamaliza mda wake wa kuongoza kwa mujibu wa katiba yetu je akitamani kuongeza mihimili mingine inaweza kulinda katiba yetu au itamsapoti?
na hapo tutambue huyu anayetaka kubadili katiba hamtumjui kwa sasa hivyo yawezekana akawa mbaya au mzuri lakini kama tukiunda mifumo ambayo kundi fulani wenyewe au kwa kutumiwa na watu wanaweza kufanya lolote kwa maana vyombo vyote wamevishikilia tutakuwa tunalipeleka wapi taifa letu huko mbeleni.
katiba hizi tusidhani ni siri na mapungufu haya tunayoyafanya ipo siku watayatumia wageni kututesa achilia mbali kutumiwa na wenyeji wenye uchu wa madaraka.
tufikiri nje ya viganja vyetu kwa kutokuangalia fursa zetu bali tuangalie na "risk tunazozichukua kwa gharama ya karanga tu za kutafuna"
Pumba tupu ulizoweka hapo, kwani nani kakwambia katiba yetu hasa hii inayopendekezwa sio nzuri mpaka uanze kuifananisha na mambo ya Burundi.
Ndugu taifa la Burundi limepitia katika vipindi mbalimbali vizito,sio hili la Nkurunziza na mgogoro wa kugombea urais, yapo kibao ambayo yamewafikisha hapa!kwa nature yao wanajifanya wazoefu wa migogoro wakati sio kweli!Tanzania ni moja ya nchi za EA ambayo nature yake iko tofauti kabisa na Burundi tangia uhuru wake,uongozi wa kupokezana madaraka,uchaguzi mkuu huru na mission mbalimbali ambazo Tanzania imezifanya abroad!haya yote yanatufanya tuwe mfano halisi wa ukomavu wa Demokrasia,utulivu na uzoefu katika kusuluhisha migogoro katika nchi nyingi barani Afrika, ninaposema hatuna cha kujifunza Burundi ninamaanisha,Burundi wako kwenye vurugu Je tujifunze vurugu zao wakati sisi hatuko huko?
kojoa ukalalwe wewe acha mbwembwe zako hapa ndani, ulichoandika ni sifuri tupu hapo, acha ubishi ubali matokeo.it depends on how far your vision can go.
mchumia tumbo wewe njaa itakuua mwaka huu.siku moja mzee mmoja nisiyemfahamu aliniuliza swali kuwa wewe unafanya kazi gani? nikamtajia akaoniuliza tena "were you made to be ...... or were you born to be ....."
sikumuelewa nikabaki nimepigwa bumbuwazi
akaniambia yapo mambo ni hulka mtu anazaliwa nayo lakini yapo mambo mtu anafanywa kuwa.
machafuko au migogoro si hulka za kuzaliwa nazo bali ni mambo yanayotengenezwa katika jamii.
yapo mambo ambayo mkiyalea yatawapeleka katika vurugu.
wapo wanaopenda kuwaonea wanadamu wengine hawa wanaleta vurugu na wapo wanaopenda kuanzisha vurugu pasipo sababu nao hawa ni hatari kwa jamii.
ili jamii iwe salama inahitaji kudhibiti wote ili kila mmoja aenende katika mstari.
wapo vipofu wanaoonea watu lakini hawaoni uonevu wao na wanaangalia kila anayepaza sauti kuwa analeta vurugu.
wapo vopofu wanaofanya vurugu wakikemea matatizo madogo huku wao wakifanya upumbavu zaidi.
wote hawa ni vipofu ambao jamii isipowadhibiti kwa sheria itatumbukia kwenye machafuko.
sijui kwa nini unasema tuna uzoefu wa kusuluhisha migogoro kwani mimi nadhani kama tungekuwa na uzoefu huo basi tusingeanza kuchipua mambo ambayo yanaleta vurugu kwa wenzetu hapa kwetu kwani machipukizi hayo yakikomaa lazima tutavuna matunda yake.
tusipende kujifunza kwa kufanya makosa sisi wenyewe na yatugharimu bali ni wakati wa kujifunza kwa makosa ya wenzetu.
mchumia tumbo wewe njaa itakuua mwaka huu.
identity inakuhusu nini wewe? Wewe utabaki kuwa mchumia tumbo tuuuuna bahati kwa kuficha identity yako kwa maana upumbavu wako hauwezi kuanikwa hadharani, lakini jipime upeo wako wa kufikiri mwenyewe.
afrika tumebaki kuwa masikini na kuonekana wajinga kwa kuwakumbatia watu kama wewe kwenye maamuzi.
ni wakati wananchi kutambua kuwa tunahitaji kuchambua makapi kwenye vyombo vyao na kuyaondoa na huo ndio mwanzo wa kupiga tambo ndefu za maendeleo.
identity inakuhusu nini wewe? Wewe utabaki kuwa mchumia tumbo tuuu
And who are you by the way? Au we ndo wale wale wachumia matumbo toka Ukawa eeenh? Usione kichaka unataka kukojoa, katiba yetu imetulia hasa hii inayopendekezwa, usiifananishe na nyingine hapa. Na uache kupotosha watu humu ndani kisa unapiga dili za Ukawa kwa jero jero, njaa itakuua wewe kijanawho are you to make such a statement
Naona humu wengi tu ni kama mimi.
(Nakiri sipo vizuri kwenye masuala ya kisiasa)
Wengi hawajui nini hasa wanajadili kuhusu Burundi,
Hawajui muda wake wa urais unaisha lini, au kama uliisha ni tangu lini kwa mujibu wa kalenda yao ya uchaguzi.
Hawaelewi kuhusu katiba na madai ya PN kuhusu kugombea kwa kipindi kingine.
Yani naona ni ushabiki tuuuuuu!
Sipo upande wowote, ila kiukweli humu kuna watu wanapotosha sana kuhusu yanayoendelea.
Naona humu wengi tu ni kama mimi.
(Nakiri sipo vizuri kwenye masuala ya kisiasa)
Wengi hawajui nini hasa wanajadili kuhusu Burundi,
Hawajui muda wake wa urais unaisha lini, au kama uliisha ni tangu lini kwa mujibu wa kalenda yao ya uchaguzi.
Hawaelewi kuhusu katiba na madai ya PN kuhusu kugombea kwa kipindi kingine.
Yani naona ni ushabiki tuuuuuu!
Sipo upande wowote, ila kiukweli humu kuna watu wanapotosha sana kuhusu yanayoendelea.
kusema haupo upande wowote haihalishi kuwa kweli haupo upande wowote bali unachokisema kinaegemea wapi au kipo katikati ndio jambo la kuangalia.
hapa hakuna mwenye historia iliyo huru ya burundi ambayo imekubalika kwani kila mmoja akitaka kutoa historia anaangalia yale yanayoegemea upande anaousapoti ambayo ni mabaya hayasemi bali lakini mtiririko ni ule ule. hivyo historia haifai.
jambo la msingi hapa ni warundi wamechoka na vita, watanzania wamechoka na wakimbizi, jumuiya ya afrika mashariki inaathiriwa na migogoro ya burundi, afrika mpaka umoja wa mataifa hakuna anayenufaika na migogoro ya burundi labda wauza silaha.
ni jambo gani linaweza kuepusha vita burundi ndio suluhisho.
haijalishi nkulunzinza ana haki ya kuendelea na muhula wa tatu lakini kama kuendelea kwake kunaweza kuleta vurugu kwa burundi basi akae pembeni maana haki isiyotimiza wajibu haipo.
hapa tunajadili swala la burundi kwa mustakabali wa tanzania.
tunatakiwa kujua kuwa kinachozidi kuivuruga burundi ni madaraka ya raisi ya kuteua viongozi mbalimbali.
madaraka haya yanamfanya raisi kuwa na washirika wa kumuunga mkono na wakiwa tayari kuingia kwenye mapambano kwa maana wanajua kuondoka kwa nkurunziza ndio mwisho wa utumishi wao.
lakini kwa upande wa hatua iliyochukuliwa na jeshi ya kutangaza nkurunzinza asirudi ilikuwa ni hatua ya kupongeza kama hatua hiyo ingekomesha machafuko na katika mda mfupi kurudisha utawala wa kidekrasia kwa kuitisha uchaguzi.
na hivyo ndivyo vyombo vya wananchi vinatakiwa kufanya kazi kwa kuwatumikia wananchi na pale viongozi wanapotaka kuipeleka jamii kubaya kunatokea chombo chenye uwezo kuirudisha jamii katika mstari.
lakini jukumu hili la vyombo vya wananchi kutumikia wananchi linakwazwa na madaraka ya raisi kuteua kwani nani ashikilie madaraka kama hayo ya kufanya mfumo mzima uwe wake akaiacha?
lakini ukisha muondoa aliyekiuka na kurudisha kwa wananchi nani ataingia na kukuamini wewe uliyemtimua mtangulizi na kukuacha kwenye madaraka?
nani anaweza kucheza upatu kama "waziri mkuu msaidizi pekee tanzania" kukamata mpaka wakubwa lakini malipo yake tunayaona leo?
hapo ndipo mimi binafsi naamini tukitengeneza katiba ikawa nzuri kwa kuondoa mianya ya watu kujiimarisha kwa kutengeneza mitandao ya kuwasapoti bila kujali wanachokifanya kila mtu anaweza kuitumikia jamii yetu kwa uaminifu naweledi mkubwa.
Bonge la ngonjera!afu unaruka unakanyaga,kuna hoja kibao umejichanganya mwenyewe na kutoka nje ya topic!Narudia tena hatujafikia hatua ya kujifunza kutoka Burundi,fanya viceversa wao ndo wajifunze kutoka kwetu na tutaendelea kuwa hivyo hayo mawazo yako ya kutaka kuigeuza Tz kichwa cha mwendawazimu yaishie huko huko!Tunaheshimu utawala wa sheria na Oktoba tunamwingiza rais wa awamu ya tano kikatiba kupitia uchaguzi mkuu achana na ndoto za alinacha wewe!