Yapo mengi ya kujifunza kutoka burundi juu ya katiba yetu



Unapoteza muda tu hata hiyo elimu yako ya kushindwa siitaki!ni bora taifa likawa na watu kibao dizaini yangu kuliko wewe unayekalia kulazimiasha mambo,unakalia kutaja michakato ipi hiyo kwa mawazo yako unakaa na kufikiri habari za Burundi Tanzania?fikiri sawasawa!tunajifunza nini?tungekua tunajifunza kwao tungezuia hata hivyo vikao vikqfanyikia nchini kwao badala ya Dar es salaam wao si ndo role mode,nasema tena hatuna cha kujifunza hapa,kaa ukijua nafasi ya Tanzania ni very special hatutakaa tufikiri uliyonayo kichwani mwako.
 
wahenga walisema ukiona mwenzako kaanguka wewe tembea na fimbo.

kwako wewe unadhani ambaye hajaanguka hastahili kujifunza kwa aliyeanguka ili ujilinda bali siku akianguka ndio atajifunza!

 
Ni mambo mawili tofauti,na kwa Tanzania siyo rahisi kiasi hicho ndugu tupo makini hasa kipengele hicho cha kubadilishana madaraka.
 
Ni mambo mawili tofauti,na kwa Tanzania siyo rahisi kiasi hicho ndugu tupo makini hasa kipengele hicho cha kubadilishana madaraka.

Umakini huo pia umejengwa siyo umeibuka tu! Misingi imara ya Katiba na Watanzania kupenda kuheshimu madaraka ya Katiba ya nchi yao.
 
wahenga walisema ukiona mwenzako kaanguka wewe tembea na fimbo.

kwako wewe unadhani ambaye hajaanguka hastahili kujifunza kwa aliyeanguka ili ujilinda bali siku akianguka ndio atajifunza!

Hivi kwa nini na wewe Ego unawaza kushindwashindwa tu, nimefuatilia michango yako nakuona huna uhakika na Tanzania yako kiasi cha kutaka kuilinganisha na Burundi yenye makabila 2 na eneo lenye ukubwa sawa na mkoa wa Kigoma!usilinganishe Papa na kibua!
 
wahenga walisema ukiona mwenzako kaanguka wewe tembea na fimbo.

kwako wewe unadhani ambaye hajaanguka hastahili kujifunza kwa aliyeanguka ili ujilinda bali siku akianguka ndio atajifunza!
umeishiwa hoja naona ckuhizi umekuwa mwalimu wa Kiswahili, nenda kafundishe shule za msingi hiyo misemo yako
 
Tanzania hatutegemei kuwa na tatizo kama la Burundi,kwani hakuna utata wowote wa kubadilishana madaraka,na wala si suala ambalo mtu waweza lala ukawaza kuwa ati kwa Tanzania hii mtu atagomea madarakani never ever!!!kwa hiyo mnapolinganisha matatizo angalau yawe yanaendana kidogo jamani mbona ni vitu viwili tofauti,am proud being a Tanzanian.
 
kwa mada inayozungumziwa hakuna logic yoyote katika ukubwa wa nchi.

migogoro haina cha kusema nchi ikiwa ni ndogo au kubwa basi kuna mahusiano na migogoro.

mimi binafsi sipendi nchi kuweka mifumo ya mtu mmoja kufanya maamuzi ya taifa na hili limekuwa ni tatizo kubwa katika nchi nyingi leo mnakuwa na kiongozi mzuri anafanya mnavyotaka lakini kesho mkipata kiongozi mbaya basi kwa maamuzi yake anaipeleka nchi kusikotakiwa.

suluhisho ni kutawanya maamuzi ya nchi katika vyombo na muondoe nafasi ya watu kuunda mtandao wa kuvishikilia vyombo vyote hivi vinavyofanya maamuzi.

tengeneza mifumo ya wananchi wanatii kwa nchi yao na sio kiongozi kwa maana kiongozi akiasi wengine wanabaki kwenye mstari.

 
tunatofautiana katika aproach tunayoitumia. mimi natumia "preventive" kwa maana kuzuia jambo lisitokee kabla ya kutokea lakini wewe unatumia "corrective" yaani hujisumbui na yajayo bali unataka tushughulikie tatizo linapotokea.

usitake tufike hatua ya burundi ndio muone kuwa yanayowakuta hata sisi yanaweza kutukuta bali jifunze kutoka kwao kuwa hivi kilichowafikisha hapo ni kitu gani na sisi tuangalie kama kwetu tunacho.

kama kwetu kiini cha tatizo lao ki mfumo kipo basi tujue hilo ni bomu ambalo hata kama halijalipuka tujue linaweza kulipuka siku moja hivyo njia ni kulidhibiti mapema.

lakini ninyi mnasema kwa nini tulidhibiti haliwezi kulipuka na hapo ndipo tunapotofautiana.

 
Tanzania hatuna cha kujifunza kutoka kwa vibaka wa Demokrasia popote walipo duniani.
 
Acha kuwanga kijana, nchi yetu ni ya amani sana hatutarajii hayo yatokee kamwe na Mungu mweza wa yote hakika hayatatokea.
 
Ego unaonekana kwanza upo kwa maslahi yako binafsi na sio ya taifa hili, maana hata mimi nimekuwa nkifatilia hoja zako daima zinaonekana mtu wa kukata tamaa na mpinga maendeleo ya nchi yako, sasa wewe tukuite mzalendo ama mzamiaji? Husomeki
 
hakika wewe ni kipofu maana mtu anaweza akawa hajaona kitu fulani lakini akionyeshwa sasa hapo ndio unaweza kutambua kipofu na anayeona. kipofu atabaki kuuliza kiko wapi sasa na wewe nimegundua ni kipofu katika haya tunayoyazungumza.

lakini kipofu wewe hujiuliza bado kuwa huyo mungu mweza wa yote ni wako peke yako tanzania au hata hao walio kwenye vurugu anawahusu. ukigundua hilo utajua kuwa kila mtu anavuna anachopanda lakini unaweza kugutuka mapema ukangoa hata mazao ambayo yangekuletea matunda mabaya kabla hayajatokea.

Acha kuwanga kijana, nchi yetu ni ya amani sana hatutarajii hayo yatokee kamwe na Mungu mweza wa yote hakika hayatatokea.
 
mimi nadhani fanya research uwaulize watu kama kumi wenye busara kwa kuwaeleza mimi ninayoyasema na wewe unayoyasema bila kuwaonyesha wewe una msimamo gani alafu uangalie majority watasemaje.

mimi na wewe kila mmoja akimchambua mwenzake tutashutumiana lakini ukweli ni kuwa unaweza kuwa mjinga na ukatumia ujinga bado kufanya tathmini ambayo inaweza kuwa na matokeo ya kijinga.

labda kautafiti kadogo kanaweza kusaidia.

Ego unaonekana kwanza upo kwa maslahi yako binafsi na sio ya taifa hili, maana hata mimi nimekuwa nkifatilia hoja zako daima zinaonekana mtu wa kukata tamaa na mpinga maendeleo ya nchi yako, sasa wewe tukuite mzalendo ama mzamiaji? Husomeki
 

Hilo ndo tatizo la kuvimbiwa!hakika uwezo wako wa kufikiri umeishia hapa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…