Yeriko Nyerere: CIA waliamini Mtu aliyepaswa kukabidhiwa Nchi ya Tanganyika baada ya Wakoloni Waingereza kuondoka ni Mangi Thomas Mariale!

Yeriko Nyerere: CIA waliamini Mtu aliyepaswa kukabidhiwa Nchi ya Tanganyika baada ya Wakoloni Waingereza kuondoka ni Mangi Thomas Mariale!

Hupaswi kumuamini muongo/lijongo hata akisema ukweli-Fareed Kubanda.
 
Mjumbe wa mikutano mkuu wa CHADEMA Yeriko Nyerere amesema Taarifa za Siri za Shirika la Ujasusi la Marekani CIA za mwaka 1953 zinaonyesha CIA waliamini mtu aliyepaswa kukabidhiwa Nchi ya Tanganyika basda ya wakoloni wa Kiingereza kuondoka ni Kiongozi wa Wachagga Mangi Thomas Mariale

Yeriko Nyerere ameweka Taarifa Ukurasani kwake X

Mlale unono

Kwako Madaraka Nyerere 😄
HILO NI LIJINGA
 
Thomas Marealle alitaka Uhuru ucheleweshwe angalau miaka 10 baada ya 1961. Ni kweli kuwa Nyerere njia yake haikuwa nyepesi hasa kipindi cha utawala wa Gavana Edward Twinning.

Pia Machifu wa Tanganyika kipindi hicho walikuwa washirika wa Utawala wa Kikoloni kwa njia ya Indirect Rule na walikuwa na baraza lao(Chiefs Council)

Uwezekano wa Mangi Marealle kuwa chaguo la kuachia nchi ulikuwa mkubwa kwa sababu alikuwa kwenye mfumo na pia alikiwa msomi.

..Mangi Marealle ni mmoja kati ya Watanganyika waliokwenda UN kudai Uhuru wa Tanganyika.

..Ushahidi wa maelezo ya Mangi Marealle akiwa UN upo hapa Jamii Forum, hakuna mahali alisema uhuru ucheleweshwe.

..Tanu ilisaidiwa na vyama vya kikabila pamoja na Machifu wakati wa kudai Uhuru ndio maana hakukuwa na masuala ya ukabila hata baada ya kupatikana uhuru wa Tanganyika.
 
Mjumbe wa mikutano mkuu wa CHADEMA Yeriko Nyerere amesema Taarifa za Siri za Shirika la Ujasusi la Marekani CIA za mwaka 1953 zinaonyesha CIA waliamini mtu aliyepaswa kukabidhiwa Nchi ya Tanganyika basda ya wakoloni wa Kiingereza kuondoka ni Kiongozi wa Wachagga Mangi Thomas Mariale

Yeriko Nyerere ameweka Taarifa Ukurasani kwake X

Mlale unono

Kwako Madaraka Nyerere 😄
Halona Ubishi hili.
 
..Mangi Marealle ni mmoja kati ya Watanganyika waliokwenda UN kudai Uhuru wa Tanganyika.

..Ushahidi wa maelezo ya Mangi Marealle akiwa UN upo hapa Jamii Forum, hakuna mahali alisema uhuru ucheleweshwe.

..Tanu ilisaidiwa na vyama vya kikabila pamoja na Machifu wakati wa kudai Uhuru ndio maana hakukuwa na masuala ya ukabila hata baada ya kupatikana
Wakati wa harakati za Uhuru kuanzia 1954 Nyerere alikuwa ameanzisha TANU na katika harakati zake za mwanzo alikumbana na kizingiti cha mkono wa dola ambapo katika baadhi ya sehemu hakuwa anapewa ushirikiano na Machifu ambao walikuwa upande wa Serikali ya Kikoloni. Mwaka 1956 aliteuliwa kuingia katika LEGCO lakini alijiuzuru mwaka mmoja baadae kutokana na kutotambuliwa kwa mchango wake wowote.

Baada ya Mkutano wa Tabora na Uchaguzi wa 1958 wa kura tatu na TANU kuibuka na ushindi mkubwa dhidi ya UTP na TANC basi ilionekana kuwa Machifu wasingeweza kuikwepa TANU. Hata hivyo walikuwa wamechelewa. Na katika kikao chao cha Februali 1959 Saidi Maswenya wa TANU kutoka Maswa na kwa niaba ya Chama Aliwaambia Machifu kuwa ni vyema wakadandia gari wakati muda ukiwa upande wao, vinginevyo wangeachwa. Katika kikao chao kingine mwaka huo Machifu waliamua kutumia ushawishi wao kubagain na TANU iwapo wanaiunga mkono ni maslahi gani wangelipata.

Mwalimu Nyerere aliamua kukata mizizi wa fitna kwa kuitisha kamati yao ya watu 12 ambapo kulikuwa na Chifu Amri Dodo wa Babati, John Maruma wa Rondo, Petro Marealle wa Vunjo, Abdiel Shangali wa Hai, Abdala Fundikira wa Unyanyembe, Haruna Lugusha wa Itetemia, Patrick Kunambi wa Morogoro, Michael Lukumbuzya wa Ukerewe, Kimweri Magogo wa Usambara, Mwami Theresa Ntare wa Kasulu, Adam Sapi wa Kalenga na Humbi Ziota wa Nzega...na akawaambia kuwa katika Utawala mpya hawakuwa na nafasi labda waiunge mkono TANU na pia wagombee ili kuendelea kuwepo katika Halmashauri. Na kuwa hadi kufikia Julai 1962 ingelibidi wawe wamekabidhi ofisi.

Na kweli ilipofika Julai 1962 hawakupata tena mishahara na kazi zao zikafungwa rasmi. Baadhi yao waliendelea kupewa heshima na jamii zao lakini wengi wao walibaki maskini.

Hata hivyo kuna baadhi ya Machifu waliopatana na Mwalimu kama Adam Sapi ambaye aliteuliwa kuwa Mbunge na Spika, Chifu Haruna Lugusha aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tanganyika Agricultural Society na Michael Lukumbuzya aliteuliwa kuwa Balozi wa Tanganyika huko India. (Soma. Aspects of Colonial Tanzania cha Prof. Lawrence Mbogoni)
 
Wengi mnabisha bisha kipumbavu bila kuwa na hoja. Hizo smartphone zenu mnatumia kufanyia nini badala ya kujisomea mambo mbalimbali? Maandiko mengi ya Yericko ni copy & paste kutoka kwa waandishi wengine. Kabla ya social media nilikuwa nikisoma sana gazeti la Rai na baadae Raia mwema. Kule kulikuwa na waandishi nguli tupu. Na makala nyingi za Rai na Raia mwema zipo kwenye kitabu cha Yericko.
Tatizo ni credibility ya mwandishi.
 
Wakati wa harakati za Uhuru kuanzia 1954 Nyerere alikuwa ameanzisha TANU na katika harakati zake za mwanzo alikumbana na kizingiti cha mkono wa dola ambapo katika baadhi ya sehemu hakuwa anapewa ushirikiano na Machifu ambao walikuwa upande wa Serikali ya Kikoloni. Mwaka 1956 aliteuliwa kuingia katika LEGCO lakini alijiuzuru mwaka mmoja baadae kutokana na kutotambuliwa kwa mchango wake wowote.

Baada ya Mkutano wa Tabora na Uchaguzi wa 1958 wa kura tatu na TANU kuibuka na ushindi mkubwa dhidi ya UTP na TANC basi ilionekana kuwa Machifu wasingeweza kuikwepa TANU. Hata hivyo walikuwa wamechelewa. Na katika kikao chao cha Februali 1959 Saidi Maswenya wa TANU kutoka Maswa na kwa niaba ya Chama Aliwaambia Machifu kuwa ni vyema wakadandia gari wakati muda ukiwa upande wao, vinginevyo wangeachwa. Katika kikao chao kingine mwaka huo Machifu waliamua kutumia ushawishi wao kubagain na TANU iwapo wanaiunga mkono ni maslahi gani wangelipata.

Mwalimu Nyerere aliamua kukata mizizi wa fitna kwa kuitisha kamati yao ya watu 12 ambapo kulikuwa na Chifu Amri Dodo wa Babati, John Maruma wa Rondo, Petro Marealle wa Vunjo, Abdiel Shangali wa Hai, Abdala Fundikira wa Unyanyembe, Haruna Lugusha wa Itetemia, Patrick Kunambi wa Morogoro, Michael Lukumbuzya wa Ukerewe, Kimweri Magogo wa Usambara, Mwami Theresa Ntare wa Kasulu, Adam Sapi wa Kalenga na Humbi Ziota wa Nzega...na akawaambia kuwa katika Utawala mpya hawakuwa na nafasi labda waiunge mkono TANU na pia wagombee ili kuendelea kuwepo katika Halmashauri. Na kuwa hadi kufikia Julai 1962 ingelibidi wawe wamekabidhi ofisi.

Na kweli ilipofika Julai 1962 hawakupata tena mishahara na kazi zao zikafungwa rasmi. Baadhi yao waliendelea kupewa heshima na jamii zao lakini wengi wao walibaki maskini.

Hata hivyo kuna baadhi ya Machifu waliopatana na Mwalimu kama Adam Sapi ambaye aliteuliwa kuwa Mbunge na Spika, Chifu Haruna Lugusha aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tanganyika Agricultural Society na Michael Lukumbuzya aliteuliwa kuwa Balozi wa Tanganyika huko India. (Soma. Aspects of Colonial Tanzania cha Prof. Lawrence Mbogoni)

..Muandishi Mohamed Said anasema Machief walianza kushawishiwa kuhusu Uhuru wakati mipango ya kuanzisha Tanu inafanyika.

..Pia safari ya Mwalimu Nyerere, na Mangi Marealle kwenda UN nadhani ilikuwa mwaka 1955, kwa hiyo inaelekea baadhi ya Machifu hawakuchelewa kuunga mkono harakati za uhuru.
 
Taarifa za siri za CIA za miaka ya 1953 zinaonyesha kwamba shirika hilo liliamini kwamba baada ya Wakoloni Waingereza kuondoka Tanganyika, mtu aliyepaswa kukabidhiwa nchi alikuwa ni kiongozi wa Wachaga Thomas Mariale.

(Soma kielelezo cha nyaraka hiyo chini ya CIA)Lakini katika nyaraka za shirika la Ujasusi la Uingereza la MI6 za mwaka 1944, zinaonyesha kwamba shirika hilo liliamini Chifu Kidaha alikuwa mtu sahihi wakukabidhiwa nchi baada ya Waingereza kuondoka.

Nyaraka za shirika la Ujasusi la Kanisa Katoliki la Jesuiti za mwaka 1942 ambazo baadae zilikuja kufanyiwa kazi kupitia kwa makasisi Arth Wills na Wash zinaonyesha kwamba wao waliamini Kambarage Burito Nyerere ndie alikuwa mtu sahihi wa kukabidhiwa nchi baada ya Uingereza kuondoka...Wazo lililoshinda ndio shirika lenye nguvu dunia.... Roma ikisema mashauri yote yamekwisha....

Yeriko Nyerere ameweka Taarifa Ukurasani kwake X

Mlale unono

Kwako Madaraka Nyerere 😄

View attachment 3215798

Kuna watu bafo wanamwamini Yericko?

Huyu jamaa hata hivyo vitabu kumbe kawaibia watu na kujifanya kaviandika yeye. Kuna Wakili moja wa Kihaya aliyoa hiyo siri kwa vile na yeye ni muathitika.Alitaka kumfungulia kesi Yerick aksomba msamaha. Mazungumzo ya huyo Wakili yaliyatoa kwenye sauti ts Watanzania early this month.
 
Yeriko anawadanganya wajinga. Kipindi hicho cha ukoloni Uingereza alikuwa na nguvu za kijasusi kuliko hata hao marekani. Waingereza waliijua nguvu ya Nyerere ndo maana wakampa nchi bila kumwaga damu kama kwingine. Julius K Nyerere alikuwa ni akili-kubwa aliwazidi akili machifu wote akiwemo huyo mareale.
🤣 🤣 🤣
 
Yericko mweupe na hivyo vijalida vyake kama vya shigongo. Yeye anaviita vitabu
 
Taarifa za siri za CIA za miaka ya 1953 zinaonyesha kwamba shirika hilo liliamini kwamba baada ya Wakoloni Waingereza kuondoka Tanganyika, mtu aliyepaswa kukabidhiwa nchi alikuwa ni kiongozi wa Wachaga Thomas Mariale.

(Soma kielelezo cha nyaraka hiyo chini ya CIA)Lakini katika nyaraka za shirika la Ujasusi la Uingereza la MI6 za mwaka 1944, zinaonyesha kwamba shirika hilo liliamini Chifu Kidaha alikuwa mtu sahihi wakukabidhiwa nchi baada ya Waingereza kuondoka.

Nyaraka za shirika la Ujasusi la Kanisa Katoliki la Jesuiti za mwaka 1942 ambazo baadae zilikuja kufanyiwa kazi kupitia kwa makasisi Arth Wills na Wash zinaonyesha kwamba wao waliamini Kambarage Burito Nyerere ndie alikuwa mtu sahihi wa kukabidhiwa nchi baada ya Uingereza kuondoka...Wazo lililoshinda ndio shirika lenye nguvu dunia.... Roma ikisema mashauri yote yamekwisha....

Yeriko Nyerere ameweka Taarifa Ukurasani kwake X

Mlale unono

Kwako Madaraka Nyerere 😄

View attachment 3215798
Mkoloni mwingereza na beberu mkuu marekani walitaka kukabidhi nchi yetu kwa machifu. Ujue machifu ni kama wafalme maana uongozi ni kurithishana kiokoo. Nchi isingekua na demokrasia ya kweli ila vibaraka wanaotumikia maslahi ya mabeberu kwa moyo wao wote.
 
Back
Top Bottom