Yesu si Mungu, Paulo ana kesi ya kujibu

Yesu si Mungu, Paulo ana kesi ya kujibu

Status
Not open for further replies.
Mkuu ,Unaizungumzia biblia ipi ???



Biblia ipi inahitaji huo utulivu ???

Gonga hapo chini

Translation Comparison Charts
Gavana nisaidie tafsiri ya hizi Aya!!!..
1475735057138.jpg
1475735063076.jpg
HUYO MTU ALIYE MWENZAKE NA BWANA WA MAJESHI NI NAN IKIWA MTU HAWEZ KUVAA UMBO LA BINADAMU?
 
Unanikoromea Mimi na kulia lia Mimi hayanihusu!; ilaha nimenukuu ilimu isilam! nimekuwekea sababu za muisilamu kuoga na aya za kuluani suratul nisaa 14 na 15 + suratul baqara 223 hata nimeuliza humu Allah katoa adhabu gani kwa wale wawili wanao shikishana ukuta? badala ya kujibu unaleta khutba?! hiyo khutba peleka masgidi ukaambulie takbir! Humu watu ni ma-GT tunaona hats huku uswazi unaitwa in mchezo wa kisilamu...hebu nikuulize! Juhudi yoote hii unayo ifanya humu unapigania nini?
Suuratu nnisaa aya ya 14 na 15 haizungumzii mambo ya kushikishana ukuta "ushoga" ila inazungumzia "uchafu" unaofanywa na wanawake wa jinsia moja "us*g*ji".

Na imeelezwa katika aya hiyo kuwa inatakiwa kitendo hicho kiwe kimeshuhudiwa na mashahidi 8 ili kuwatia hatiani, na kama watatiwa hatiani basi adhabu yao ni kuwafungia wanawake hao katika jumba mpaka pale atakapopatikana mwanaume wa kumnusuru "kuoa" ndipo adhabu yao itaisha. Kinyume na hapo watafungiwa humo mpaka mauti yawakute.
Wallahu a'lam
 
Unanikoromea Mimi na kulia lia Mimi hayanihusu!; ilaha nimenukuu ilimu isilam! nimekuwekea sababu za muisilamu kuoga na aya za kuluani suratul nisaa 14 na 15 + suratul baqara 223 hata nimeuliza humu Allah katoa adhabu gani kwa wale wawili wanao shikishana ukuta? badala ya kujibu unaleta khutba?! hiyo khutba peleka masgidi ukaambulie takbir! Humu watu ni ma-GT tunaona hats huku uswazi unaitwa in mchezo wa kisilamu...hebu nikuulize! Juhudi yoote hii unayo ifanya humu unapigania nini?
"Mwenye kumuingilia mwenye hedhi au mwanamke kwa nyuma au kumuendea mchawi na kumuamini kwa anayosema basi amekufuru kwa aliyoteremshiwa Muhammad" (Abu Daawuud, at-Tirmidhiy na Ibn Maajah, na Isnadi yake ni Sahihi).
 
Kwa nini mnapenda ku-edit kauli ya allah? Ref hapo ulipochomekea eti allah kapuliza tumbo la mariam...!? allah mwenyewe kasema kapuliza kum#@ ya (farjaha)ibnata al imran ref q.66:12 wewe unasema kapuliza tumbo...karudia tena ktk q.21:91 anasema waallatee ahsanat 'f a r j a h a.....feeha min roohina...... wewe badala ya kusema kapuliz k%&@ma unasema tumbo...hiyo aya 4:171 inaeleza wazi kwamba Hakika Masihi ni Neno na Roho ya M'Mungu na sema labda sio ya allah hapo tutakubaliana...nasema hivi waAllah huna ubavu wa kumtetea allah wala muhammad kwa uzwazwa waliofanyia dunia...tukiwaelimisha na kunukuu kauli za allah na muhammad mnasema ni matusi na kashfa why? mf; fundisho hili unafundishaje family > sababu za kuoga no ukimuingilia maiti, mnyama, kuntha, mtoto tundu yeyote iwayo ya nyuma au mbele au ukiingiliwa wewe...View attachment 412620View attachment 412620 Utafundishaje wanao na mameko au utaona ni matusi na kashfu..huu ni msiba dogo...

Hio picha kama ni kuran naomba unukuu aya ya ngap?
Lkn kuhusu kusema ALLAH kapuliza tumbo kwani ww hujui kama tupu ni sehem ya tumbo? au mpaka utukane kwa kusema ku**** au utupu? Tumia tafsida kk...
Kuhus yesu kuwa masihi nahisi cwez tena kubadlisha kile unacho kiamni kwa kuwa sio kazi yangu kukkuaminisha jambo lolote kwenye kuran,wajibu wetu ni KUKUMBUSHA TU.,Na mimi nmeshakukumbusha sasa kama unamtazamo mwengine baada ya ukumbusho huu ,Allahu aalamu...
 
Mambo ya imani ni magumu sana, ni sawa mungu kujigeuza mtu hashindwi ila kweli alikosa namna ya kumfanya kiumbe dhaifu kama mwanadamu amuamini mpaka ajifanye mtu, mpaka asulubiwe ili viumbe wake wamuamini? Imani ni ngumu sana. Acha baniani waamini ng'ombe acha babu zetu waabudu waabudu miti na mapango tu.
MUNGU anaweza kila jambo rafiki,kuna mtu aliwahi kutumwa na MUNGU na mtu huyo akambishia MUNGU mpaka apate uhakika kama anaesema nae ndiye MUNGU kweli,na walibishana mpaka huyo mtu akamshinda na kumpa MUNGU masharti ya nini afanye ili ajidhihirishe kama ni MUNGU kweli anaesema nae ndo aende anakomtuma.na ndivyo ilikua,sasa huyo alikua ni mtu na kwa uwezo wa MUNGU unaomaanisha ulivyo mkubwa si angemuamulu kwa uwezo wake tu huyo ndugu na akafuata maelekezo?lakini MUNGU alikua mpole ili watu waelewe,anazo njia nyingi za kujidhihirisha na kuwafundisha watu
 
Suuratu nnisaa aya ya 14 na 15 haizungumzii mambo ya kushikishana ukuta "ushoga" ila inazungumzia "uchafu" unaofanywa na wanawake wa jinsia moja "us*g*ji".

Na imeelezwa katika aya hiyo kuwa inatakiwa kitendo hicho kiwe kimeshuhudiwa na mashahidi 8 ili kuwatia hatiani, na kama watatiwa hatiani basi adhabu yao ni kuwafungia wanawake hao katika jumba mpaka pale atakapopatikana mwanaume wa kumnusuru "kuoa" ndipo adhabu yao itaisha. Kinyume na hapo watafungiwa humo mpaka mauti yawakute.
Wallahu a'lam
sawa kabisa allah hapo katoa hukumu kwa hao wanawake wanao sagana hiyo ni nisaa.14! aya ya kumi na tano inahusu wanaume...allah katoa hukumu gani?
 
"Mwenye kumuingilia mwenye hedhi au mwanamke kwa nyuma au kumuendea mchawi na kumuamini kwa anayosema basi amekufuru kwa aliyoteremshiwa Muhammad" (Abu Daawuud, at-Tirmidhiy na Ibn Maajah, na Isnadi yake ni Sahihi).

soma hii ufunguke!; omary ibn khatab alimuuliza mtume sababu ya kushuka baqara 223!; akasema imeshuka kwa ajili ya kuwaingilia wanawake tupu zao za nyuma..
Addrul manthur j.uk 473
Fat'hul baary j.8 uk.38-39
Kasome ufunguke!; Allah amewafaridhia ndogo kwa nini mnatakaabar? kula tu..hhhhhhhhhh...
 
Born in a Stable?


manger.jpg




Was Jesus born in a stable? Or a barn? Or a cave?


Luke* says only a manger. There was no room for him in the kataluma ("inn" or guest room).

But Joseph supposedly had returned to his ancestral home, "the lineage of David". So the place should have been chock-full with his own relatives. And not one of them would accommodate a heavily pregnant woman? Tut-tut.

The reality is that the story of Jesus is enhanced by the "humble birth".

Early Christians were taken by the idea that he was, in fact, born in a cave. Can you get any more humble than that?

* Matthew, a tad more realistic, says, "And when they had come into the house ..." (2.11).

Yesu Alizaliwa na yuko Hai...bishia na hiyo mzee wa kadi za kliniki...hhhhhhhh...
 
Kasauti kadogo kidole juu Ulimzaa we we!!¡¡? kaza kiuno ubishie!; hatuna maskhara na mtoto wa MTU humu..

Ukimaliza ngonjera zako ,poa kama maji ya mtungini ujibu suali, ulimzaa wewe???
 
Matayo 28:19 ```Basi,enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu""""""

Mstari huu unakuonyesha mambo kadhaa Dotto,,,,
1.Yesu sio mtume(ktk Qur'an Yesu sio issa ila Yahsua ibn masihi) issa anaweza kuwa mtume ila YESU Hana hadhi ya chini kiasi hicho..YESU Anaongelea utatu mtakatifu hapo na hadhi yake ni MUNGU.

2.Yesu ni mwana wa MUNGU na kama ilivyo mwana wa binadamu ni binadamu basi pia kama ilivyo YESU ni mwana wa MUNGU basi yeye ni MUNGU.Yeye alizaliwa kabla ya kuumbwa kiumbe chochote ""Wakolosai 1:15-17"""pitia hapa kuna maneno ya kweli na kila unachotaka kuelewa kuhusu YESU.

3.Usiwe unamuongelea Paulo kulingana na viongozi wako wa dini wanaomdharau na kumchukia(nimesikia wengine wakijitoa ufahamu na kumwita Shoga)) Jiulize kwamba Yeye alie katika Ukristo amezuia nini katika dini Yenu ya Uislam,,,amehatarisha maslahi ya nani???
Kwa nini mnashindwa kuongea mambo mnayoyaona sahihi kwa kumhofia???

Je!! Wewe muislamu utaweza kumbainishia mkristo ubaya wa Paulo kulingana na uelewa wako mdogo na mtazamo wako finyu wa biblia??

Je!? Huwezi kumwongelea Yesu pekee pasi na kumchanganya na Paulo mtume wa mataifa??
 
Ama kwa hakika kabisa nina ujasiri wa kusema maneno haya ""YESU yupo na kila mmoja wa binadamu atampigia goti na kumsujudia katika maisha haya au baada ya kufa kwenye maisha yajayo.NASISITIZA KILA MTU.Kwa hakika pasi na shaka yoyote.
 
Hivi hawa wanaodai yesu ni Mungu hivi wako sawa lakini?yaani Mungu huyu ale afu aenda chooni afu bado unasema huyu ni mungu hivi mko sawa kweli?hapa nakumbuka maneno kutoka ktk kitabu cha isaya...hata nyota sio safi machoni sembuse binaadamu aliyezaliwa na mwanamke tena buu.
 
Ama kwa hakika kabisa nina ujasiri wa kusema maneno haya ""YESU yupo na kila mmoja wa binadamu atampigia goti na kumsujudia katika maisha haya au baada ya kufa kwenye maisha yajayo.NASISITIZA KILA MTU.Kwa hakika pasi na shaka yoyote.
Tutampigia goti kama nani sasa? Kama Mungu au kama mwanaye Mungu?
 
View attachment 406746

"Lakini sasa mnatafuta kuniua mimi, MTU ambaye nimewaambia iliyo kweli, niliyoisikia kwa Mungu. Ibrahimu hakufanya hivyo."

Yohana 8:40

Katika andiko hilo YESU kwa kinywa chake yeye mwenyewe amejiita kuwa ni "MTU". Kama kuna mtu ana ushahidi wowote katika biblia YESU akijiita MUNGU, basi nami hapo nitaamini kuwa YESU Mungu.

Hata hivyo, mnaweza kusema pia, kuwa YESU alikuwa Mungu na Pia alikuwa mtu. Hata hivyo tukitazama sifa mbalimbali za mungu kama zilivyo tajwa au ainishwa na biblia, utaona hata kiduchu YESU hana sifa hizo.

Mathalani.

"Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifikiliza.."

Hesabu 23:19

Tumeona katika Yohana 8:40 Yesu akijiita Mtu, na hapa katika hesabu tunaambiwa Mungu si mtu, sasa wewe unayemuita Yesu Mungu umepata wapi?

NANI KAFUNDISHA YESU NI MUNGU?

"tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; "

Tito 2:13

Hayo maneno katika kitabu cha Tito, kimsingi ni barua ya kimisionari aliyo andika Paulo kwa watu wa Tito, kama tuonavyo katika barua hiyo, pamoja na mambo mengine Paulo anawaambia watu wa Tito kuwa Yesu ni Mungu Mkuu, maneno haya ya Paulo yanakwenda kinyume kabisa na maneno ga Yesu mwenyewe aliyo yasema katika Yohana 8:40 lakini kinyume kabisa na mafundisho ya kinabii kutoka katika kitabu cha Hesabu 23:19.

YESU ANASEMAJE KUHUSU PAULO?

Awali ya yote Paulo hakuwahi kuwa mwanafunzi wa Yesu na hakuwahi kumuona Yesu Kristo. Yesu kabla hajapaa kwenda mbinguni aliwahi kusema maneno haya.

"Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa. Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada. Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi"

Yohana 16:1-3

Hapa Yesu anatabiri kuwa wanafunzi wake watakuja kuuliwa, anatabiri wakristo na wafuasi wa kanisa lake watakuja kuuliwa, na akasisitiza huyo atajaye wauwa wanafunzi wake hamjui yeye wala Baba(Mungu)

Nani huyo aliyeua wanafunzi wa Yesu? Jawabu ni Sauli ambaye ni Paulo.

"Lakini Sauli, akizidi kutisha na kuwaza kuwaua wanafunzi wa Bwana, akamwendea Kuhani Mkuu, akataka ampe barua za kuenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili akiona watu wa Njia hii, waume kwa wake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu."

Matendo 9:1-3

Kwa hivyo Mtu aliyetajwa na Yesu katika injili ya Yohana 16:1-3 kuwa atawaua wanafunzi wa Yesu si mwingine Paulo, na katika kitabu cha matendo tunaoneshwa ukatili wa Paulo kwa wanafunzi wa Yesu. Hata hivyo, Bwana Yesu anaendelea na utabiri wake juu ya Paulo katika aya hii.

"Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo"

Yohana 8:44

Katika aya hiyo Bwana Yesu anasema huyo Paulo si kwamba ni muuaji tu, lakini pia mtu muongo sana. Na uongo mkubwa alio ufanya Paulo ni pale aliposema kakutana na Yesu na kisha akajifanya kipofu.

"Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni. Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe. Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda"

Matendo 9:3-7

Baaada ya Paulo kuwaua sana wanafunzi wa Yesu na kuwatesa sana ili waache mafunzo ya Yesu, lakini wanafunzi wa Yesu waligoma na walikataa katakata kuachana na mafunzo Yasu. Pia naomba mjue, mafunzo ya Yesu yalikuwa mwiba kwa serikali(Dola ya Rumi) na Paulo alikuwa anatumiwa na serikali katika kuhakikisha wanafunzi wa Yesu wanaachana na ukristo/uyaudi.

Pamoja na juhudi hizo za Paulo lakini alishindwa, hivyo njia aliyo amua kuitumia si nyingine bali ni kujiunga na wanafunzi wa kristo. Na ili aaminike ndipo hapo alipotengeneza stori ya kumuona Yesu na maagizo ya upofu, lakini kubwa zaidi alimnunua Anania ili msaidie kufanikisha lengo lake. Kwa kumtumia Anania na kwa kudanganya kwake kuwa kamuona Yesu, wanafunzi wa Yesu walimkubali.

Na hapo ndipo Paulo alipoanza kuyachakua mafunzo ya Yesu, na ndio maana ukristo wa sasa si ule alio ufundisha Yesu.

YESU NA MFARISAYO.

"Ewe FARISAYO KIPOFU, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi. Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote."

Mathayo 26:23

Paulo msomi mkubwa alikuwa Farisayo, lakini Yesu alisema nini juu mafarisayo? Kama tulivyo ona, Yesu anawaona mafarisayo kama vipofu, lakini kubwa katika andiko hili Yesu anamtabiri pia Paulo na maigizo yake ya upofu.

"Paulo alipotambua ya kuwa sehemu moja ni Masadukayo, na sehemu ya pili ni Mafarisayo, akapaza sauti yake katika ile baraza, Ndugu zangu, mimi ni Farisayo mwana wa Farisayo; mimi ninahukumiwa kwa ajili ya tumaini la ufufuo wa wafu"

Matendo 23:6

Kwanza Paulo amekiri kwa kinywa chake kuwa yeye ni farisayo. Lakini hiyo haitoshi Paulo alijitia upofu aso kuwa nao.

"Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski. Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi."

Matendo 9:8-9

Katika aya hizi tunaona kuwa Paulo amekiri kuwa Farisayo lakini pia tunaona Paul yuko katika maigizo ya upofu. Yote haya mawili yanakamilisha unabii wa Yesu pale aliposema

"Ewe farisayo kipofu.."

Mathayo 26:23

Katika aya hizo inatajwa sifa kuu au tabia kubwa ya Mafarisayo, na ambayo imethibiti(ilitimia) kwa Paulo. Sifa hiyo si nyingine bali UNAFIKI.

Paulo alikuwa mnafiki, yaani alijifanya muumini wa mafundisho Yesu ili mradi apate kuwapotosha wanafunzi wa Yesu, na hili kwakweli kafanikiwa sababu hakuna hata kanisa moja ambalo linafuata mafunzo ya asili ya Yesu. Kila kanisa lina kituko chake.

MWISHO.

Kwa kifupi huku nikizingatia maelezo yangu yote ya huko juu, kuwa YESU SI MUNGU, lakini hakumaanishi kuwa hakuna wanao muita au wanao amini Yesu Mungu. La kuzingatia kama tukiambiwa kauli ipi ya kushika kati ya YESU mwenyewe na ya Paulo kwa vyovyote vile tunatakiwa kushika kauli ya Yesu.

Kauli zote za Paulo ambazo hazipingani na za Yesu, kauli hizo tutazifuata, lakini kauli yoyote ya Paulo inayo pingana na Yesu, kauli ya Paulo itapuuzwa na kuanguka, alafu watu wote wanatakiwa wafuate kauli ya Yesu.

Hakuna kauli ya Yesu anayo alijiita Mungu, lakini zipo nyingi akijiita Mtu au mwana wa adamu. Na siku zote alijitafautisha na Mungu. Yesu anakata mzizi wa fitina katika andiko hili.

"Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma"
Yohana 17:3

Nasema YESU SI MUNGU, na Paulo ana kesi ya kujibu kwa kudanganya ulimwengu, na kwa kuharibu mafundisho ya Yesu na kubwa zaidi kwa kuwatesa na kuwaua wanafunzi wa Yesu na wafuasi wake.

Katika kuendeleza urongo wa Paulo, watu wameambukizwa urongo, sasa wanatusambazia picha na sanamu za wacheza sinema na kisha wanataka tuziheshimu kama Yesu, kweli watu wanaangamia kwa kukosa maarifa.

TUJADILI!

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
Call/whatspp 0622845394 Morogoro.
Akili yako imeishia hapo. Hazikutoshi, ipo siku utaju kuwa Yesu Kristu ni kweli na uzima. Mohamed mwenyewe kapinga sana ukirsto mwisho kafa yeye ukirsto upo utakuwa wewe?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom