Kwa Hali nayoiona hapa huu uwanja haujai
Promo ndogo viingilio vikubwa Sana
Naona maget yakiwa waz kuanzia saa 10 alasiri watu wataingia bure kujaza uwanja
Siyo sifa kuonekana umejaza uwanja bila kuingiza kipato. Nimeingia wakati Yanga inatambulisha wachezaji. Ilikuwa 17:30hrs. Nilipata tiketi mzunguko na niliingia.
Uwanja attendance yake ilikuwa 90%, Siyo mbaya kwa kuzingatia:-
1. Muda tangu kutangazwa tamasha hadi tamasha. Ulikuwa mfupi sana na timing yake ilikuwa ngumu. Watumishi wa serikali hawakuwa na purchasing power nzuri.
2. Ni ukweli kuwa mashabiki wa Yanga wamekuwa na shughuli nyingi za Yanga zinazohitaji fedha. Mashindano ya CAF kuanzia makundi, robo, nusu na fainali, wamekuwa wanaingia.
Zaidi tumezundua jersey juzi tu, Hivyo ni wazi fedha nyingi zimetumika kufanikisha hayo sambamba na kulipia kifurushi cha Azam
3. Sintofaham ya Mayele na Nabi nayo imechangia. Ni wazi mashabiki wangekuwa na uhakika wa kutetema wangekuja.
4. Matokeo ya mechi za nyuma za kilele siku ya wananchi. Wenye moyo laini hawapendi kuona timu yao inafungwa. Hivyo kwa kuzingatia ubora wa Kaizer Chief, baadhi walijua matokeo ni kufungwa tu hivyo wakaamua kuitafuta amani ya moyo wao.
All in all, kupata 90% ya wahudhuriaji, siyo jambo dogo sana, ni kubwa mno.