Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Hakika Mkuu.

Pia mashabiki tulijitahidi kuwa wavumilivu mana Luc alikuja na gundu tukapoteza mechi mbili ile ya Azam na Kagera ambapo upande wa pili walianza kumbeza kumbe lilikuwa swala la muda tu.

Nina imani tutazidi kufanya vizuri zaidi huko mbeleni na pia yabidi nguvu zaidi tuzihamishie kwenye FA ili kuzidi kujihakikishua kucheza kimataifa mwakani.

Alibezwa hadi na washabiki wenyewe wa Yanga hasa baada ya kupoteza mechi ya pili dhidi ya Azam. Mashabiki wengi walianza kuulalamikia uongozi kwa kumleta huyu mzungu badala ya kumuacha Mkwasa. Kwenye mitandao ya kijamii watu waliandika kwa jazba kabisa kuwa mzungu arudishwe kwao hatumtaki.

Upande wangu niliiona yanga ikianza kucheza mpira unaoeleweka tokea mechi ya kagera ukiachana na swala la matokeo, maana matokeo yalisababishwa na makosa binafsi ya wachezaji.

Nina mashaka na huyu kocha kwenye upande mmoja tu, upande wa kukaa na timu kwa muda mrefu ndio shida ilipo. Huyu kocha angefaa sana kwenye kuijenga Yanga na kuwa moja ya timu iliyo ya ushindani na tishio kwa ukanda Africa, na kama inavyojulikana timu imara haiwezi jengwa kwa kipindi kifupi bali ni project ya zaidi ya msimu mmoja.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
BADO TUNAJIWINDA NA LIPULI. MAZOEZI YALIYOFANYWA JANA NA TIMU YA WANANCHI.
20200205_055112.jpg
 
YANGA SC KUENDELEZA BURUDANI UWANJA WA TAIFA LEO.

Kikosi cha Yanga leo saa moja usiku kitashuka kwenye uwanja wa Taifa kuikabili Lipuli Fc katika mchezo wa ligi kuu.

Baada ya kushinda michezo mitatu mfululizo, mabingwa hao wa kihistoria watakuwa wakisaka ushindi mwingine ili kuendelea kuweka hai matumaini ya kuwania ubingwa msimu huu.

Afisa Mhamasishaji Antonio Nugaz amesema vijana wana ari na wamepania kuwapa furaha mashabiki, hivyo amewataka kujitokeza kwa wingi.

Viingilio vya mchezo huo VIP A ni Tsh 15,000/-, VIP B na C ni Tsh 10,000/- wakati upande wa mzunguuko ni Tsh 5,000/- "Sisi tuna timu bora, tunashinda michezo yetu kwa nguvu zetu hatutegemei kubebwa kama wanavyofanyiwa wengine. Mashabiki njooni kwa wingi mpate burudani kutoka kwa timu yenu," alisema Nugaz.

"DAIMA MBELE NYUMA MWIKO"
 
yanga hamna uhakika wa timu yenu kushinda ndo maana hamuwezi anzisha uzi hapa
 
Back
Top Bottom