Kikubwa nembo ya timu ya Wananchi Mkuu.
Ila usiwaze Mkuu mechi zijazo watatinga uzi wa chapa GSM.
Mume halali wa mikia amesema sisi ni akina nani hata tumpinge!?MORRISON AHAIDI RAHA YANGA SC:-
Bernard Morrison ni moja ya wachezaji ambao walisajiliwa katika dirisha dogo kwenye kikosi cha Yanga akiwa mchezaji huru tangu alipoachana na DC Motema Pembe ya DR Congo.
Mshambuliaji wa Yanga, Bernard Morrison amewataka mashabiki wa timu hiyo kukaa mkao wa kula kwani anajipanga kuwa na kiwango bora zaidi ya kile alichokionyesha katika mechi chache alizoichezea ambacho hajaridhika nacho. Akizungumza na Mwanaspoti Morrison alisema kuwa mechi aliyofunga bao pekee la ushindi dhidi ya Simba ndio alikuwa anaanza kuwa katika makali yake.
"unajua hata wakati nacheza mechi na Simba nilikuwa na maumivu ya mguu ndio maana baada ya kuifanya kazi ambayo niliagizwa na kocha wangu nilitolewa.
Kwa muda mchache niliokuwa hapa Tanzania nadhani bado sijacheza kwa kiwango ambacho natamani kukiona kwanza nilikuwa sijazoea mambo mengi lakini kwa sasa naona vitu vingi vipo sawa," alisema.
"Nikirudi katika ligi nitakuwa nimeimarika zaidi kwa maana hiyo nadhani kuna vitu vingi ambavyo nitavifanya uwanjani katika kila mechi ili kuona timu yangu inaweza kupata ushindi.
Nadhani nikifanya mambo mengi mazuri kwa timu yangu nitaweza kuisaidia kupata matokeo ambayo inahitaji lakini kufikia malengo yake wakati huo huo nitakuwa najitangaza mwenyewe," alisema Morrison.
Haiezekani kabisa aisee.
Shadeeya unajua Mkwasa yeye plani zake kuifunga Simba tu basi anakua ameridhika, hana mipango ya kuiendeleza Yanga baada ya hapo!!!MABOSI:- MKWASA KUKABIDHIWA TIMU
Mabosi wa Klabu ya Yanga wamechungulia mbali na kuona ligi inaweza kurejea hivi karibuni lakini bila ya kuwa na makocha wao wawili, Kocha Mkuu Luc Eymael na yule wa viungo, Riedoh Berdien raia wa Afrika Kusini. Sasa kwa ajili ya kuweka mipango sawa bila ya kutetereka, mabosi hao wa Yanga wameamua kumuachia mikoba kocha msaidizi, Charles Mkwasa kuwa ndiye awe msimamizi mkuu wa timu hiyo wakati ambao Eymael atachelewa kurejea nchini endapo tangazo la ligi kuendelea litakapotangazwa. 
Mabosi hao wamefikia muafaka huo baada ya kuona Eymael ni ngumu kurejea Bongo kwa sasa kutokana na kwao, Ubelgiji kufunga uwanja wa ndege kutokana na janga la Corona ambapo pia akirejea atatakiwa kubakia karantini kwa siku 14.
Habari ambazo Championi limezipata ni kwamba timu hiyo itakuwa chini ya Mkwasa ambaye wamejiridhisha kuwa kutokana na uzoefu wake, ataweza kuibeba timu hiyo kwenye mechi zilizobaki.
Kabla ya kuja Eymael, Mkwasa aliachiwa timu hiyo baada ya kocha mkuu Mwinyi Zahera kuvunjiwa mkataba wake. “Inaonekana labda kocha Eymael anaweza kuchelewa kurejea Bongo kama ligi itaanza hivi karibuni, lakini hilo tayari limeshafanyiwa utaratibu wa kuweza kulikamilisha na kuwa vizuri.
“Kitakachofanyika ni kuwa Mkwasa ndiye atapewa timu aiendeshe kwa wakati huo kwa sababu wengi wamemuamini kutokana na kile alichokifanya wakati alipopewa timu baada ya Zahera kuvunjiwa mkataba,” kilisema chanzo hicho.
Kwa upande wake, Ofisa Mhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz, amesema mipango hiyo wanaendelea nayo kuhakikisha hawapati tatizo lolote hata kama kocha huyo atachelewa kurudi na ligi ikianza.
Ndio maana tukasema anashikia kwa muda na Luc basi anarudi kwenye nafasi yake.Shadeeya unajua Mkwasa yeye plani zake kuifunga Simba tu basi anakua ameridhika, hana mipango ya kuiendeleza Yanga baada ya hapo!!!
Hahahaa. Hamutamsahau eee?Shadeeya unajua Mkwasa yeye plani zake kuifunga Simba tu basi anakua ameridhika, hana mipango ya kuiendeleza Yanga baada ya hapo!!!
Bora iwe hivyo kwakweliNdio maana tukasema anashikia kwa muda na Luc basi anarudi kwenye nafasi yake.
Nguvu ya soda tu ile, mzee wa kubahatisha😀Hahahaa. Hamutamsahau eee?
Mana aliwaduwaza mechi ya round ya kwanza.
Bora iwe hivyo kwakweli
Huruma hii kwa Timu ya Wananchi imeanza lini eti? 😅😅😅Bora iwe hivyo kwakweli
Kagoli kamoja ka faulo basi mnajiona mabingwa wa Afrika eeh!!!? Yanga bana😀😀😀
Tynawqtakia mema, msimkubali Mkwasa kama kocha🤣🤣🤣Huruma hii kwa Timu ya Wananchi imeanza lini eti? 😅😅😅