Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

FRIENDLY MATCH: YANGA SC VS KMC FC

Wakati Ligi Kuu Tanzania Bara inatarajiwa kuanza Juni 13, kikosi cha Timu ya Wananchi, kitashuka dimbani Jumapili, Juni 7, kujipima nguvu dhidi ya KMC ya Dar es Salaam. "Tumeona tuwe na mechi moja ya kirafiki kabla ya kurejea rasmi kwenye Ligi, mashabiki wetu wangependa kuiona timu yao baada kipindi kirefu, sasa tunaenda kuwapa burudani kwenye Uwanja wa Uhuru," amesema Thabit Kandorro, Mkurugenzi wa Mashindano.

Amesema mechi hiyo ni sehemu ya programu ya benchi la Ufundi ambalo lilihitaji mechi mbili, lakini kutokana na muda tumeona walau ipatikane moja ili kuweka mambo sawa. "Tutakuwa na wiki nzima ya mazoezi na mechi moja, hapo kikosi kitakuwa tayari kwa ajili ya michezo ya Ligi," ameongeza Kandorro.

Katika mchezo huo, mashabiki wataruhusiwa kuingia kuanzia saa 10:00 jioni. Utaratibu wa ushiriki wa mashabiki utaenda kwa mujibu wa muongozo wa Wizara ya Afya na Wizara ya Michezo.
 
Nawatakia maandalizi mema Shadeeya

Simba nguvu moja
 
Sawa Shadeeya nimeipokea kwa mikono miwili salamu kutoka kwa mutu ya Congo, straika bora wa muda wote kuwahi kusajiliwa Yanga.😜
Namkubali sana papaa Mo linger namtabiria kuwa top scorer msimu huu😝.
Au unasemaje Shadeeya?
Hahahahaaaa!!!! Umemuona anavyojifua akirudi mtamsahau.
 
#BlackLivesMatter
#NguvuMoja
 

Attachments

  • 101274467_1614144295411246_3099089212125741056_o.jpg
    8.9 KB · Views: 2
  • 101274467_1614144295411246_3099089212125741056_o.jpg
    8.9 KB · Views: 2
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…