FRIENDLY MATCH: YANGA SC VS KMC FC
Wakati Ligi Kuu Tanzania Bara inatarajiwa kuanza Juni 13, kikosi cha Timu ya Wananchi, kitashuka dimbani Jumapili, Juni 7, kujipima nguvu dhidi ya KMC ya Dar es Salaam. "Tumeona tuwe na mechi moja ya kirafiki kabla ya kurejea rasmi kwenye Ligi, mashabiki wetu wangependa kuiona timu yao baada kipindi kirefu, sasa tunaenda kuwapa burudani kwenye Uwanja wa Uhuru," amesema Thabit Kandorro, Mkurugenzi wa Mashindano.
Amesema mechi hiyo ni sehemu ya programu ya benchi la Ufundi ambalo lilihitaji mechi mbili, lakini kutokana na muda tumeona walau ipatikane moja ili kuweka mambo sawa. "Tutakuwa na wiki nzima ya mazoezi na mechi moja, hapo kikosi kitakuwa tayari kwa ajili ya michezo ya Ligi," ameongeza Kandorro.
Katika mchezo huo, mashabiki wataruhusiwa kuingia kuanzia saa 10:00 jioni. Utaratibu wa ushiriki wa mashabiki utaenda kwa mujibu wa muongozo wa Wizara ya Afya na Wizara ya Michezo.