Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Angalau katika hili la kupinga mchezo wa kibabe na kuumizana kwa makusudi uwanjani tunaweza kuungana Shadeeya. Kuna wachezaji wanadhani mpira ni vita au ni boxing. Bila kuumiza wenzao hawajisikii vizuri.

Ni vyema vilabu vyote viwe vinatoa elimu kwa wachezaji wao waache kukusudia kuumiza wachezaji wa timu pinzani kwani wajue hata wenzao ajira zao zipo kwenye miguu yao na sio kitendo cha kiungwa kumchezea mchezaji mwenzio rafu mbaya itakayomuumiza na pengine hata kuhatarisha afya yake ya kiwiliwili au kutishia carrier yake ya uanamichezo

Tuungane sote bila kujali itikadi zetu za Usimba na Uyanga kupinga tabia za wachezaji kuumizana, na tutoe wito kwa vilabu vyetu vianze kutoa adhabu kwa wachezaji wao wenyewe watakao cheza rafu mbaya dhidi ya wachezaji wa timu pinzani wakati wakisubiri Shirikisho la mpira nalo litoe adhabu yake. TFF nayo wawe wakali sana kwenye hili
 
Sema wanaenda kutia chachu ya kuja kumkata mtu mkia. ๐Ÿ˜€
Shadeeya, unajua tumewatafuta longtime ili tuwaonyeshe kua kunguru kumnyea binadamu sio kwamba anashabaha saaana bali kabahatisha tu. Na sasa mmeingia kwenye 18 zetu.

Njooni na woooote akiwemo mshambuliaji hatari sana bwana Ykpe, mfungaji wenu bora wa muda wote Molinga na hata Morison acheze tu ili kusiwe na sababu ya kuitoa pale tutakapokua tunakatisha ndoto na matumaini yenu ya kushiriki michuano yoyote ya kimataifa msimu huu
 
Sina pupa mie sababu najua sehemu ambayo tukiwashikka hutakuwa na pa kufurukuta.

Na najua mwisho wa siku lawama zote mtazipeleka kwenye imani za kishirikina. ๐Ÿ˜€
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ