Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Mtani huwa upo hapa Mjini? Unaendaga Uwanjani hasa mechi za Simba na Yanga? Yana ugeni gani hayo?

Mi ni mmoja wao Mtani na nikwambie tu hiyo haifanyiki Yanga pekee hata huko Simba ipo pia tena inafanyika sana tu, mfano itokee mtu wa Yanga halafu ni mgeni kazunguka Uwanja wee kisha kaja kuibukia upande wa 5imba yaani hapo lazima achezee kichapo na pona pona yake basi watamvua ile tishirt waichane chane hapo ndio anaeza pata salama ya kufika huko anakotaka au akishindwa basi atimue mbio kurudi alikotoka. [emoji23][emoji23]

Niseme tu tunahitaji kubadilika wote na sio Yanga pekee kwani kuna watu wanachukuliaga ukiwa shabiki wa Yanga basi mshabiki wa Simba tayari ni adui yako ambaye hamuezi kaa mkaongea lugha moja jambo ambalo si kweli.
Mimi imewahi kunikuta hii, first time naingia taifa mechi ya simba na yanga,, japo nilikua nimewahi kuingia mara 2 nyuma kwenye mechi za kawaida, sijui ilikuaje nikajichanganya nikaingilia kule kwa simba tena nikiwa na jezi na skafu, na kipindi hicho yanga ya babu ni ya moto sana (tulishinda ile mechi 2-0) simba wenyewe walijua kabisa kua wanafungwa.

Ile nimetokea tu upande wao aiseh wakanifukuza nashukuru Mungu mbio ziliniokoa, nilikimbia huku navua jezi na skafu nikabaki na singrendi tu ya ndani hivo hata niliokua nakutana nao mbele hawakutilia maanani kama wale walionitoa baruti huko nyuma.

Isingekua Mungu na mbio I'm sure ningeyachezea makofi ya kutosha siku ile.
 
Caf online
20200903_000655.jpg
 
yanga ilianzishwa mnamo mwaka 1935 na inasemekana ndo klabu kongwe na yenye mafanikio zaidi hapa nchini. klabu hii ilianzishwa na wazalendo halisi wa nchi hii waliokuwa wakiji shughulisha na uchuuzi wa nazi na samaki na muda wao wa jioni ulipofika walikuwa wakijumuika pamoja kusakata kabumbu na hapo ndipo ilizaliwa yanga.

kama hiyo haitoshi wazalendo hawa waliendelea kujikusanya kwa pamoja na kuanza mishemishe za kusaka uhuru wa nchi hii, na ndipo tarehe 9 disemba mwaka 1961 tanganyika ikapata uhuru, hivyo kama tutazungumzia uhuru wa taifa hili basi hatusiti kwa namna moja au nyingine kuitaja yanga, na kwa heshima yake inatakiwa unapoitaja yanga kama umekaa basi unatakiwa usimame.
MAFANIKIO.

yanga ndio timu iliyochukua ubingwa wa ligi ya bara mara nyingi zaidi, na ndio klabu inayofahamika zaidi kitaifa na kimataifa kwa sababu ndiyo klabu iliyopeperusha vizuri bendela ya taifa hili la tanzania nje ya mipaka.
na kama hiyo haitoshi yanga ndiyo klabu yenye washabiki wengi zaidi ndani na nje ya nchi, ndani ya africa na dunia kwa ujumla.

na pia yanga ndiyo klabu ya mwanzo hapa nchini au hata afrika mashariki kwa ujumla kwa kuwa na makao makuu sambamba na uwanja wa mazoezi ambao unajulikana kwa jina la Kaunda, jina la muasisi na mpigania uhuru mwengine wa taifa la zambia muheshimiwa keneth kaunda.
mfumo huu wa kuwa na makao makuu pamoja na uwanja wa mazoezi ni wa timu kubwa barani ulaya na dunia kwa ujumla.

yanga pia ndio timu ya kwanza kuwa na gazeti hapa nchini. gazeti hili linajulikana kama "Yanga imara". lilipotoka katika wiki ya kwanza liliuzwa takriban nakala 50,000 nchi nzima na baadhi ya nchi za jirani.
mfumo wa kuwa na gazeti la klabu pia umeigwa na baadhi ya klabu hapa nchini lakini unaonekana kusua sua katika mauzo na hata ukisoma nakala ya gazeti lao utakuta limejaa matangazo ya waganga tu.

yanga ndo timu pekee iliyowahi kuuza mchezaji nje ya nchi na kung'aa katika vilabu mbali mbali barani ulaya, mchezaji huyu alijulikana kama Nonda Shaaban al maarufu kama "papii".
nonda ambaye aliwahi kutamba na mashujaa hawa wa jangwani amepata kuchezea vilabu kama val profesional ya south africa, FC zuurich ya uswis, stade rennes na AS monaco zote za ufaransa, AS roma ya italia akicheza pamoja na francesco totti, blackburn ya uingereza na sasa anakipiga katika klabu ya galatasaray yenye maskani yake katika uwanja wa ali sami yen nchini uturuki.

na hapa ndipo tunapoitofautisha yanga na vilabu vingine vya soka hapa nchini ambavyo wachezaji wake huuzwa burundi, rwanda na uarabuni ambako hakuna soka la ushindani.

pia yanga ndo timu ya kwanza hapa nchini kuongozwa na rais.
pia yanga ndo timu ya kwanza kuwa na mfumo wa wanachama kuwa wana hisa wa klabu kama timu nyingi za ulaya, hivyo kumfanya kila mwanachama kuhusika kikamilifu katika mipango na malengo ya klabu, tofauti na majirani zetu ambao mfumo wao wa uongozi haueleweki na hata mishahara ya wachezaji wanalipwa kimkanda mkanda na inafika kipindi mchezaji anakaa miezi minne hajalipwa mshahara mwisho wanatimkia kucheza ligi za mchangani.

MAFANIKIO NJE YA MIPAKA.
Yanga kama yanga ndo timu pekee iliyowahi kuchukua kombe linalotambuliwa na shirikisho la soka barani afrika CAF na shirikisho la soka duniani FIFA. itakumbukwa tu yanga waliwafunga express ya uganda kwa goli 3-1 katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la klabu bingwa afrika mashariki na kati na mechi ya fainali walitakiwa wakipige na SC villa.

yanga waliwacharaza bila huruma SC Villa goli 2-1 katika uwanja wa nakivubo kwenye mechi ya fainali ya kombe lililokuwa na msisimko kipindi hicho la klabu bingwa afrika mashariki na kati na kupelekea serikali ya tanzania kutuma ndege mpaka katika uwanja wa ndege wa entebe kwenda kuwachukua waheshimiwa waliolitoa taifa kimasomaso yaani yanga.
hivyo kuweka adabu kwa waganda ambao hawawezi kuisahau yanga maishani mwao.

yanga katika mechi hiyo iliwakilishwa na:
1) steven nemes
2) mwanamtwa kihwelu
3) keneth mkapa
4) willy mtendamema
5) issa athuman
6) method mogella
7) steven mussa
8) hamis thobias gagarino
9) said mwamba kizota
10) mohamed husein chinga one
11) edibily jonas lunyamila


pia yanga walikuwa na bunduki nje kwenye benchi kama willy martin, rifat said, aboubakar salum "sure boy" david mwakalebela "MP" na wengine wengi ambao walikuwa ni miiba kwa waganda.

katika mechi hiyo mnamo dakika ya 81 beki mahili wa villa na timu ya taifa ya uganda marehemu Paul Hasule alivua jezi na kutoka nje kwa kile ambacho mwenyewe alikiri kuwa ameshindwa kumkaba winga wa yanga edibily lunyamila, lakini alilazimishwa na kocha wake kumaliza mechi kutokana na aibu iliyokuwa inawakabili.

kutokea hapo waganda walitekwa akili kutokana na kabumbu safi lililoonyeshwa na yanga na kupelekea daladala nyingi nchini humo kuandikwa majina kama "lunyamila trans" "kizota trans" au hata wengine walifuta majina ya salon zao na kuandika "gagarino hair salon" na mpaka leo hii waganda wakisikia timu kutoka tanzania inakwenda huko wanauliza "je ni yanga?".

na baada ya ushindi huo mwanamuziki nguli wa afrika marehemu kabasele yampanya al maarufu kama peppe kalle alitunga wimbo wa kuisifia timu hiyo baada ya kuonyesha dhahili kiwango cha juu na kuvutia washabiki wengi wa soka kitu ambacho hakijawahi kufanywa na klabu yoyote nyingine hapa nchini.

HISTORIA ISIYO SAHAULIKA.
mwaka 1972 katika pambano la watani wa jadi lililokuwa lifanyike katika uwanja wa taifa, watanzania walishuhudia kituko cha mwaka pale kilabu ya simba ya dar es salaam ilipoishia chang'ombe na kugeuza basi na kurudi katika mtaa wa msimbazi na kufanya timu ya yanga ya tanzania kupewa ushindi baada ya mpinzani kufyata mkia na kutokomea vichakani.

mnamo pia tarehe 13 mwezi novemba mwaka 1991 katika uwanja huo huo wa taifa timu ya yanga ya tanzania waliingia uwanjani na basi la sharuksi lililokuwa likimilikiwa na mfadhili wa yanga wa kipindi hicho marehemu abbas gulamali, timu ya soka ya simba ya dar es salaam iliweka mpira kwapani wakati wa mapumziko na kutokomea kusiko julikana.

na kauli hii ya kuweka mpira kwapani iltolewa na mtangazaji aliyekuwa anatangaza soka redio tanzania siku hiyo ndugu Charles Hillary, na magazeti kama motomoto, mfanyakazi, uhuru na mzalendo ya kipindi hicho yalipambwa na kichwa kikubwa cha habari "mgonjwa atema dawa".

na kuweka mpira huko kwapani kulifuatia vipigo mfululizo vya august 31, october 9 lakini hii iltanguliwa na kipigo cha Said Sued "Scud" cha mei 18.

baadhi ya mashujaa waliowahi kukipiga yanga miongoni mwao ni rifat said, joseph katuba, peter manyika, anwar awadh, salum kabunda "ninja", godwin aswile "baba subi" au scania, said zimbwe, thomas kipese, joseph lazaro, omar husein, costantino kimanda, sanifu lazaro "tingisha" na wengine wengi.

hili nililokupa hapo ni tone tu la maji, ila bahari ntakupa siku nyingine.
na hii ndo yanga, klabu bora kabisa hapa nchini, isiyotishwa na kelele, adhabu wala faini yoyote.
Gang Chomba huwezi fanya editing kwenye majina yakawa na capitals? Au wasimamizi wa JF saidieni thead hii ikae vizuri please.....
 
Wananchi ishu ya kiingilio uwanjani J2 utaratibu upoje?

Ingekuwa hiyari yangu Game zote za Yanga zichezwe kuanzia saa 12 jioni au saa 1.
 
Jamani hivi jezi zetu zinatoka lini? Maana viongozi na wasemaji kila tukiuliza wanatupiga chenga.
 
Jamani hivi jezi zetu zinatoka lini? Maana viongozi na wasemaji kila tukiuliza wanatupiga chenga.
𝙽𝚒𝚖𝚜𝚒𝚔𝚒𝚊 𝚓𝚊𝚗𝚊 𝚋𝚞𝚖𝚋𝚞𝚕𝚒 𝚊𝚕𝚒𝚜𝚎𝚖𝚊 𝚕𝚎𝚘 𝚠𝚊𝚝𝚊𝚕𝚒𝚝𝚘𝚕𝚎𝚊 𝚞𝚏𝚊𝚏𝚊𝚗𝚞𝚣𝚒 𝚗𝚊𝚘𝚗𝚊 𝚖𝚙𝚔 𝚜𝚊𝚜𝚊 𝚔𝚒𝚖𝚢𝚊, 𝚗𝚐𝚘𝚓𝚊 𝚝𝚞𝚜𝚞𝚋𝚒𝚛𝚒 𝚖𝚙𝚔 𝚓2 𝚝𝚞𝚘𝚗𝚎 𝚔𝚖 𝚣𝚒𝚝𝚊𝚝𝚞𝚖𝚒𝚔𝚊 𝚖𝚙𝚢𝚊 𝚊𝚞 𝚣𝚊 𝚣𝚊𝚖𝚊𝚗𝚒.
 
𝙽𝚒𝚖𝚜𝚒𝚔𝚒𝚊 𝚓𝚊𝚗𝚊 𝚋𝚞𝚖𝚋𝚞𝚕𝚒 𝚊𝚕𝚒𝚜𝚎𝚖𝚊 𝚕𝚎𝚘 𝚠𝚊𝚝𝚊𝚕𝚒𝚝𝚘𝚕𝚎𝚊 𝚞𝚏𝚊𝚏𝚊𝚗𝚞𝚣𝚒 𝚗𝚊𝚘𝚗𝚊 𝚖𝚙𝚔 𝚜𝚊𝚜𝚊 𝚔𝚒𝚖𝚢𝚊, 𝚗𝚐𝚘𝚓𝚊 𝚝𝚞𝚜𝚞𝚋𝚒𝚛𝚒 𝚖𝚙𝚔 𝚓2 𝚝𝚞𝚘𝚗𝚎 𝚔𝚖 𝚣𝚒𝚝𝚊𝚝𝚞𝚖𝚒𝚔𝚊 𝚖𝚙𝚢𝚊 𝚊𝚞 𝚣𝚊 𝚣𝚊𝚖𝚊𝚗𝚒.
Ktk hili GSM wanafeli wapi tena?
 
Ktk hili GSM wanafeli wapi tena?
𝚂𝚒𝚓𝚞𝚒 𝚔𝚠𝚊𝚔𝚠𝚎𝚕𝚒, 𝚕𝚊𝚋𝚍𝚊 𝚗𝚒 𝚖𝚊𝚛𝚔𝚎𝚝 𝚜𝚝𝚛𝚊𝚝𝚎𝚐𝚢 𝚊𝚞 𝚠𝚊𝚝𝚊 𝚕𝚊𝚞𝚌𝚑 𝚙𝚊𝚖𝚘𝚓𝚊 𝚗𝚊 𝚔𝚞𝚋𝚠𝚊 𝚔𝚞𝚕𝚒𝚔𝚘?
 
Kwani Mungalu nae alienda kuoa!? Mnajaribu kuikwepa aibu. Terminator keshawasha mitambo sahizi msipotoa shikamoo kwa wakati anawazabua tu vibao. Bado Mzee Onyango hajaanza kuwagonga makofi
𝚜𝚑𝚒𝚔𝚊𝚖𝚘𝚘 𝙼𝚉𝙴𝙴 𝙺𝙸𝙳𝚄𝙽𝚄𝙻𝙰1
 
Back
Top Bottom