Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

KISINDA ANAANZA KUWA WA KAWAIDA SASA

Anaandika @exaud_msaka_habari

Pamoja na Kufunga goli la Kwanza leo lakini Tuisila niliyemuona Siku ya Mwananchi sio huyu ninayemuona sasa, hasa huyu wa leo alikuwa wa kawaida sana, mipira aliyopoteza ni Mingi mno

Inawezekana mwalimu anataka kumfanya abadilishe mchezo kutoka kwenye Staili yake ya Kuchukua kijiji na kuamsha nacho sasa aanze kuchukua na kutoa mpira, ila leo hilo hajalifanya kabisa.

Kadiri siku zinavyoenda tunaweza kuanza kupata majibu ya yale maswali yetu tunayojiuliza huku kwenye vibanda umiza kuwa Imekuaje AS VITA wakamuuza? Tutaendelea kupata majibu kadiri siku zinavyoendelea ila kwangu leo hajafanya kile tulichomtambua nacho mechi yake ya kwanza.

Niweke sawa Hajacheza vibaya ila hajafanya yale yaliyotufanya tumuite TK MASTER. na alistahili kutoka mapema sana maana ni kama alichoka

ALL IN ALL KWA MNAOAMINI MORRISON KAPIGWA MISUMARI BASI KISINDA KAPIGWA NONDO
 
NYAMAZENI HAMNA CHA KUWAELEZA WANANCHI

Anaandika @exaud_msaka_habari

Kuizungumzia Yanga inahitaji uwe na akili sana maana unaweza kusema kitu hata usieleweke. Unatamani uisifie kiwango chake kuna roho inakuambia nyamaza, unatamani uwakosoe kuna roho inakuambia nyamaza wewe

Huna cha kuwaambia wananchi, huna cha kuwaeleza wakuelewe wakati wameshinda Goli Mbili Kirumba, Kama unasubiri Biriani endelea kuisubiri ila Wananchi wameshinda.

Unataka kuwaambia wananchi bado hawaeleweni? Watakulaani, wanakupiga mawe Yanga imeshinda Mbili Kirumba.

Unataka kuwaambia bado umiliki wa Mpira kwao sio wa kiwango mnachotarajia? Watakuelewa? Yanga ameshinda Mbili Kirumba.

Unataka kuwaambia Yanga Sarpong Bado sio mfungaji wa kutegemewa, watakuambia asipofunga yeye atafunga Waziri Jr. Asipofunga Sarpong atafunga hata Mukoko. Wananchi wanayo majibu sahihi ya kukujibu.

Kiwango cha Kisinda usiwaeleze kabisa wananchi watakuambia kafunga leo, Wananchi wameshinda.

Wananchi wapo juu ya Simba na wanamsogelea Azam huna cha kuwaambia wananchi, ukiwaambia kitu utakuwa unajisumbua tu.

ALL IN ALL USIWAAMBIE WANANCHI KUHUSU ILE PENAT YAO
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Naangalia magoli yenu hapa, ile penalty mlipewa zawadi ,


Hata Mechi na Simba sikuangalia ndio naangalia Highlights hapa, aisee, huyo mnamwita Lawi [emoji119][emoji119][emoji119], mtu analambwa kiatu tena miguu miwil ndani ya box mara mbili alafu kapeta tu

Human error kwenye ligi yetu zinafikirisha sii kidogo, hawa jamaa hawalipwagi nn au wanasheria zao tofuati
 
Wazazi muwe mnaangalia jezi za kuwavalisha watoto..
Badae mnaanza kulalamika watoto wenu wakilala wanaweweseka ndotoni.
Kumbe jezi inamjia ndotoni inamtisha.
 
Nilikua nahesabu dakika najua ungekuja tuπŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
Muhindi alibana leo nikawa busy kutwa hapa ndo napata chance ya kushika simu.

Hivi utaamini wala sikuwa najua kama mnacheza? Kuna mtu tu hapa kaniambia weka Azam Hd ndio nikajua kumbe mpo Uwanjani mna jambo lenu πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ mie nilikuwa busy na mechi ya Azam.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…