Nimekuwa kipofu kwa bao la Mwaisa David Kaseke, nikitazama macho yananiambia mpira ulivuka mstari, nikifumba na kufumbua tena macho yananiambia yule beki alinyanyua mguu ukiwa sambamba na mstari wa goli. Kwa maana hiyo mpira haukuvuka wote mstari. Pale unahitaji bahati ya kipenga cha mwamuzi ikuokoe.
Penalti ya Pastory Atanas ilikuwa sahihi. Hakukuwa na utata sana dhidi ya Yassin Mustapha. Mpira ulipiga mkono kwasababu mkono haukuwa katika eneo lake halisi. Sijui kwanini 'reaction' ya wachezaji wa Yanga ilikuwa vile. Hapa si Macho yangu tena bali hakika yangu inaniambia ni penalty.
Tunaweza kumminia refa kila aina ya lawama. Tunaweza kuwatukana wasaidizi wake kila aina ya tusi, lakini tukumbuke kuwa uwanjani tukio linaonekana kwa mara moja. Sisi tunapata nafasi ya kurudia-rudia, ndiyo maana tunaweza kutoa tafsiri sahihi. Nazidi kuelewa kwanini wazungu wamekubali kuzidisha teknolojia viwanjani. Muda mwingine, marefa wetu wanafanya kazi katika mazingira magumu sana.
Wananchi niwaambie kitu?? Nilijua mmeamua kuleta magoli kwa kumsajili mshambuliaji wa kati, Fiston Abdulrazaq. Lakini nadhani Cedric Kaze anataka kutuaminisha tena kuwa, mlisajili winga na siyo mshambuliaji wa mwisho. Mbona anatumia muda mwingi kukimbia mbali na lango kiasi kile??
Wananchi mnaweza kumchukia Michael Saprong, wapinzani mnaweza kumtanania Michael Saprong. Lakini mkituliza kichwa kuna kitu cha ziada mnaweza kukikubali kwake, anajua kutunza mali, anajua vita ya nguvu, anachokosa ni kile kinachotafutwa kwa washambuliaji wote duniani, MABAO. Wananchi kama mtaamua kumfanya mpishi zaidi ya mlaji, mnaweza mkafaidi zaidi.
Pastory Atanas, NDIYO mzee. Mabeki wagumu kama 'rastaman' Mustapha Yassin, wanahitaji mawinga wasumbufu kama Pastory mwana Atanas. Alimkosa mtu mmoja tu, Kibu Denis. Labda Kibu angekuwepo Lamine na Bakari wasingekula bata kama vile.
Japo mnaweza mkanichukia lakini acheni Niwaambie ukweli mwingine wananchi, leo mmedondosha pointi mbili za muhimu sana kwasababu ya UBUTU mlionao kwenye safu yenu ya ushambuliaji. KUNRADHI, Pale mwisho hampo makini kabisa WANANCHI.