Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Hivi wewe unaamini Feisal amastahili kuendelea kucheza hapa TZ?
Ikiw hajapata timu ya Tanzania na dili nzuri imekuja unataka agome?
IMG-20221224-WA0018.jpg
 
Naona kama propaganda vile.
Itakuwa afadhali shem sababu ni kama kitu ambacho hatujakitarajia vile.

Sababu Kitanzania Tanzania tumeshazowea kwanza zinaanza tetesi kisha ndo inakuwa kweli lakini hii imekuwa taarifa ya siri kuwahi kutokea.
 
Itakuwa afadhali shem sababu ni kama kitu ambacho hatujakitarajia vile.

Sababu Kitanzania Tanzania tumeshazowea kwanza zinaanza tetesi kisha ndo inakuwa kweli lakini hii imekuwa taarifa ya siri kuwahi kutokea.
Hufuatilii mambo ndio maana....
Hii sio ghafla ika ni mchakato na Alikamwe ndio kampeleka Fei azam
 
Mmh!! We unaefuatilia hayo mambo yaani uache kabisa kuleta huu umbea huku jf. [emoji1787][emoji1787]

Au umeshawahi hata kugusia hii kitu humu.
Mwaka 2010, Azam FC ilimtaka Mrisho Ngassa, kipenzi cha Yanga na mashabiki wao.

Zikatumwa barua mfululizo za kuulizia bei na kuomba vikao vya majadiliano na viongozi wa Yanga.

Mwenyekiti alikuwa mwanasheria nguli, Imani Madega. Akasema kama mnataka kuongea na sisi, basi kikao kifanyike Serena Hotel. Akaambiwa panga siku na muda.

Siku ikafika na Madega hakutaka majadiliano marefu, akasema kama mnamtaka Ngassa toeni dola 40,000. Wakati huo uhamisho wa wachezaji ulikuwa hauzidi dola 5000!

Hapo hapo akatumwa mtu aende kuchukua hizo hela. Kumbe watu walijindaa kweli kweli...walikuja na dola laki 5 kwenye gari, zikabaki nje zinapumua tu...dola 40,000 kitu gani?

Madega kusikia hivyo akasema hapana jamani, msizilete...Yanga wataniua, ngojeni kwanza nikaongee na wenzangu.

Kumbe wao walipanga kutaja hela nyingi ili kukatisha tamaa, na walijiandaa kukataa kuombana heri.

Siku mbili baadaye, Ngassa akatua Chamazi.

KWANINI HAIENDELEI?

Moja ya sababu ya Azam kuacha ubabe wa usajili kwa Simba na Yanga ni kauli ya Zakaria Hans Pope (RIP) aliyoitoa pale Millennium Tower Basement baada ya Azam kupita na Ramadhan Singano mwaka 2015.

'Tunanunua bidhaa za Azam, wanapata pesa halafu wanatuchukulia wachezaji wetu. Kuanzia sasa nawaagiza mashabiki wa Simba wasinunue bidhaa yoyote ya Azam'.

Hii haikuwa kauli ya kiushindani wa mpira bali ya makasiriko na hasira zikizotokana na kukata tamaa.

Mwaka 2014, ubabe mwingine ulifanyika kwa usajili wa Frank Domayo, tena akiwa kambi ya timu ya taifa, Tukuyu Mbeya.

Hili suala liliwatingisha Yanga hadi mamlaka za soka nchini na Rais Malinzi akaunda tume ya kuchunguza usajili huo.

Ilikuwa kawaida kwa Simba na Yanga kusajili wachezaji wakiwa kwenye kambi ya timu ya taifa, na hata Yanga walifanya hivyo kwa Domayo...lakini kwa Azam ikawa tabu, hadi mamlaka zinaingilia.

Ikaonekana kuendelea kushindana na watu wa aina hii kwenye usajili, siyo uungwana. Bora kuhangaika na usajili kutoka sehemu nyingine kabisa.

Kama ni kutoka Simba au Yanga basi kwa wachezaji ambao wenyewe hawana mipango nao.

Lakini kwa hizi kauli zako bwana mdogo @alikamwe, watu watajifikiria upya.

Azam maana yake ni KUBWA KULIKO ZOTE...tusije kulaumiana!

Naitwa Zaka!
 
Mmh!! We unaefuatilia hayo mambo yaani uache kabisa kuleta huu umbea huku jf. [emoji1787][emoji1787]

Au umeshawahi hata kugusia hii kitu humu.
Mimi siangalii tetesi naangalia habari??????[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kinachofanyika kwa Feitoto Wala si kigeni, yamefanyika mengi ya Aina hiyo na yamepita. Always Azam Ni kuwad wa Simba SC, tunza hii post yangu, Feitoto pale Azam fc Ni njia ya kuelekea Kolowizard na hapo ndiyo itskuwa mwisho wa care yake kwenye mchezo wa soka. Ninachoshauri uongozi wetu chini ya kijana Mhandisi Hersi watulie watafute vipaji vingine, akiba Feitoto wako wengi Sana tu dunia hii, Ni suala la kutulia na kusaka mbadala wake na maisha yakaendelea Kama walivyotoka kina Msuva, Ngassa, Domayo, Chirwa, Ngoma, Ebibily Lunyamila, na Mohamed Hussein Mmachinga, bado tuliweza kupata mbadala wao na maisha yaliendelea. Wacha wao waangaike na Feitoto sisi tuwajibu kwa vitendo kwa kurecruit machine nyingine Kali zaidi ya Feitoto. Hatuitaji kupanic, Ni mbele kwa mbele tu.
 
Kinachofanyika kwa Feitoto Wala si kigeni, yamefanyika mengi ya Aina hiyo na yamepita. Always Azam Ni kuwad wa Simba SC, tunza hii post yangu, Feitoto pale Azam fc Ni njia ya kuelekea Kolowizard na hapo ndiyo itskuwa mwisho wa care yake kwenye mchezo wa soka. Ninachoshauri uongozi wetu chini ya kijana Mhandisi Hersi watulie watafute vipaji vingine, akiba Feitoto wako wengi Sana tu dunia hii, Ni suala la kutulia na kusaka mbadala wake na maisha yakaendelea Kama walivyotoka kina Msuva, Ngassa, Domayo, Chirwa, Ngoma, Ebibily Lunyamila, na Mohamed Hussein Mmachinga, bado tuliweza kupata mbadala wao na maisha yaliendelea. Wacha wao waangaike na Feitoto sisi tuwajibu kwa vitendo kwa kurecruit machine nyingine Kali zaidi ya Feitoto. Hatuitaji kupanic, Ni mbele kwa mbele tu.
YANGA ni WANANCHI....katu hatutaweza kushindwa na mashangazi wa kina AISHA...


MBUMBUMBU NI WANGESE SANA.
 
Back
Top Bottom