Yuko wapi aliyeimba wimbo wa Watoto Wasafi moyoni show?

Yuko wapi aliyeimba wimbo wa Watoto Wasafi moyoni show?

Half London

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2014
Posts
261
Reaction score
112
Habari wana Jamiiforums?

Leo nimeisikia ile nyimbo ya kipindi cha Watoto Show Radio One, nikamkumbuka yule mtoto aliyeiimba.

Wanaojua yuko wapi na anafanya nini kwa sasa atujuze. Ni hayo tu!

"Watotoo wasafi moyoni ni nyota za macho za wazazi, sisi ni maua tulioopendwa na Mungu mwenyezi"

======

Semboko said;

Utashangaa kwamba aliyeimba rekodi "Watoto (1986)" ni binti wa kihindi anaitwa Nipa alikuwa na miaka 6 wakati huo.Varda Arts ni wasanii wa kihindi ambao waliishi mkoani na kuhamia Dar baadaye.Kazi yao kubwa ilikuwa ni kupiga picha na baadaye wakageuzia muziki.Walitoa rekodi kama "Tazama Tanzania (1986"),"Maridadi Sana (1984)" na "Mwl Nyerere (1984)".Walikuwa wasanii wa kwanza kwanza kutoa swahili movie iitwayo "Maridadi".Waliwahi kushirikishwa kwenye All Stars Orchestra iliyotengenezwa na BASATA wakati huo kuimba katika charity balls mbali mbali Tanzania aidha za CCM au Serikali wakisindikizwa na wanamuziki wengine wazalendo.Kwa hesabu za haraka haraka Nipa atakuwa mtu mzima sana sasa!

Aliyeimba "Tanzania eeh" song anaitwa Martina Chambiri na hii ilikuwa katika tamasha la kimataifa la watoto huko Italy maarufu kama Zecchino d'Oro.Watanzania wengi hawakufahamu nyimbo ile mpaka presenters maarufu wa Radio One (Master T na Mike Mhagama) wakati ule walipomleta studio na kuzungumza naye na toka hapo wimbo ukawa maarufu sana.Binti sasa yuko chuo kikuu na anafanya vizuri sana,ila bahati mbaya baba yake mzazi alifariki dunia akiwa bado sekondari.

 
ni mtoto wa kihindi, mara ya mwisho marehemu julius nyaisanga akiwa radio one, alisema aliwasiliana na wazazi wa mtoto huyo na walimwambia yuko uingereza kwa elimu ya juu.

Radio One hawawezi pata nyimbo nzuri ya kipindi cha watoto kama ile. Haina count down ile,bali ni ya siku zote na everlast kama DJ JD.
 
"watoto wasafi moyonii!" aisee yule mdosi anajua.. nafkiri atakua kaolewa sasa.Kama bado anaimba anitafute nimpe shavu la kurecord album
 
"watoto wasafi moyonii!" aisee yule mdosi anajua.. nafkiri atakua kaolewa sasa.Kama bado anaimba anitafute nimpe shavu la kurecord album

Nadhani ndiye aliyeimba nyimbo ya mbuga za wanyama. Ni nyimbo ya mda mrefu sana,ikitoka kupigwa hiyo nyimbo inapigwa ya Emmanuel Nkulila.
 
Kuna mtu mmoja anaitwa yunus varda wa varda arts kama yupo hai maana sijamsikia siku nyingi anaweza kukupa taarifa ya huyu mtoto,....unakumbuka na wimbo wa varda arts tazama tanzania(funga safari ya tanzania)?
 
jaman naomba mtu mwenye mashairi ya hiyo nyimbo ya watoto show aniandikie maana kuna mdogo wangi a
naipenda sana ila kuimba inamshinda sababu kuna maneno hayasikii vizuri...
 
Kuna mtu mmoja anaitwa yunus varda wa varda arts kama yupo hai maana sijamsikia siku nyingi anaweza kukupa taarifa ya huyu mtoto,....unakumbuka na wimbo wa varda arts tazama tanzania(funga safari ya tanzania)?

Yule mdosi naona keshazeeka sasa. Kuna kipindi alijaribu kurejea lkn hakupokewa vzr.
 
Nadhani ndiye aliyeimba nyimbo ya mbuga za wanyama. Ni nyimbo ya mda mrefu sana,ikitoka kupigwa hiyo nyimbo inapigwa ya Emmanuel Nkulila.

aliyeimba mbuga za wanyama nadhani anaitwa martina chambili, ni giza sio muhindi
nenda u tube andika hilo jina na jina la wimbo ni tanzania-e
 
ynaikumbuka hiyo nyimbo nzuri sana nilikuwa naipenda inakumbusha mbali sana.

watoto wasafi moyoni....
 
Back
Top Bottom