Yuko wapi aliyeimba wimbo wa Watoto Wasafi moyoni show?

Yuko wapi aliyeimba wimbo wa Watoto Wasafi moyoni show?

..'Huukasirishwa na wenzao, mara hutembea na hao hao, wakigoombana na wenzao muda si muda huzungumza nao, la la laa..'

Kipindi hicho nasoma mafundisho ya kipaimara. Nimeikumbuka nyimbo ya "Machozi" ya Lady Jay Dee.
 
Habari wana Jamiiforums? Leo nimeisikia ile nyimbo ya kipindi cha Watoto Show Radio One, nikamkumbuka yule mtoto aliyeiimba. Wanaojua yuko wapi na anafanya nini kwa sasa atujuze. Ni hayo tu!

Wanaitwa VARDA Arts walikuwa wana band yao walikuwa wanakaa mitaa ya msasani ukishapita shule ya msasani kama unakwenda slipway, ni wahindi wa mwanzo mwanzo kuishi msasani, pia ndio watu wa kwanza kwanza Kuuza UROJO aka Mix
 
Utashangaa kwamba aliyeimba rekodi "Watoto (1986)" ni binti wa kihindi anaitwa Nipa alikuwa na miaka 6 wakati huo.Varda Arts ni wasanii wa kihindi ambao waliishi mkoani na kuhamia Dar baadaye.Kazi yao kubwa ilikuwa ni kupiga picha na baadaye wakageuzia muziki.Walitoa rekodi kama "Tazama Tanzania (1986"),"Maridadi Sana (1984)" na "Mwl Nyerere (1984)".Walikuwa wasanii wa kwanza kwanza kutoa swahili movie iitwayo "Maridadi".Waliwahi kushirikishwa kwenye All Stars Orchestra iliyotengenezwa na BASATA wakati huo kuimba katika charity balls mbali mbali Tanzania aidha za CCM au Serikali wakisindikizwa na wanamuziki wengine wazalendo.Kwa hesabu za haraka haraka Nipa atakuwa mtu mzima sana sasa!

Aliyeimba "Tanzania eeh" song anaitwa Martina Chambiri na hii ilikuwa katika tamasha la kimataifa la watoto huko Italy maarufu kama Zecchino d'Oro.Watanzania wengi hawakufahamu nyimbo ile mpaka presenters maarufu wa Radio One (Master T na Mike Mhagama) wakati ule walipomleta studio na kuzungumza naye na toka hapo wimbo ukawa maarufu sana.Binti sasa yuko chuo kikuu na anafanya vizuri sana,ila bahati mbaya baba yake mzazi alifariki dunia akiwa bado sekondari.

Umechambua vizuri sana! Siku hizi vijana maridadi sana maridadi sana,kuna m-bongo aliyekuwa kwenye hiyo movie ya maridadi alikuwa anahojiwa na Star TV msanii wetu.
 
Last edited by a moderator:
Habari wana Jamiiforums? Leo nimeisikia ile nyimbo ya kipindi cha Watoto Show Radio One, nikamkumbuka yule mtoto aliyeiimba. Wanaojua yuko wapi na anafanya nini kwa sasa atujuze. Ni hayo tu!
Mkuu yupo ni mkubwa sasa anaitwa Melody Mbasa anawimbo mzuri sana unaitwa Nikoleze, anaimba huyo Bella anakaa pembeni.
 
Nadhani ndiye aliyeimba nyimbo ya mbuga za wanyama. Ni nyimbo ya mda mrefu sana,ikitoka kupigwa hiyo nyimbo inapigwa ya Emmanuel Nkulila.

Hahaha ikitoka ya Emmanuel Nkulila inaingia ya Sama Mapangala dunia tunapita kila kitu kitabakia, halafu kisa cha mpemba Twangapepeta kina luiza mbutu wanakata mauno wameshika nyungo
 
Kuna ile pia ya kabinti kanaimba "Tanzania eeh,jela mia,jela mia,sijui na nini,karibu mumuone"

Kuna kabinti keusi kanaimba huku nyuma kuna kwaya ikimsapoti,na mbele kuna kwaya masta akiongoza.

Ilikuwa inapigwa pia wakati wa kipindi cha watoto cha itv.
 
Kichuna,Amina Chifupa alianza hivyo hivyo,mwisho "akafundishwa" utangazaji na akina Mike Mhagama na Deo Mshigeni,baadaye akaupata ubunge.Mungu amrehemu alikuwa mbunge matata sana na shukrani ziwaendee waliomfanya awe maarufu.Kutembea kwako kwa miguu basi wewe ulikuwa unakaa Mlimani,Mwenge,Kijitoonyama au Sinza maana ni sehemu hizo tu ni karibu na Mikocheni,lol.
Semboko,Hivi Mike Mhagama sio ndio Marehemu Deo Filikunjombe?
 
Mwny ule wimbo auweke humu tujikumbushe kipindi kile mambo ya kwenda studio radio one
 
Back
Top Bottom