Half London
JF-Expert Member
- Jul 12, 2014
- 261
- 112
- Thread starter
-
- #41
..'Huukasirishwa na wenzao, mara hutembea na hao hao, wakigoombana na wenzao muda si muda huzungumza nao, la la laa..'
Habari wana Jamiiforums? Leo nimeisikia ile nyimbo ya kipindi cha Watoto Show Radio One, nikamkumbuka yule mtoto aliyeiimba. Wanaojua yuko wapi na anafanya nini kwa sasa atujuze. Ni hayo tu!
"Watotoo wasafi moyoni ni nyota za macho za wazazi, sisi ni maua tulioopendwa na Mungu mwenyezi"
(niekee beat kwanza)
Utashangaa kwamba aliyeimba rekodi "Watoto (1986)" ni binti wa kihindi anaitwa Nipa alikuwa na miaka 6 wakati huo.Varda Arts ni wasanii wa kihindi ambao waliishi mkoani na kuhamia Dar baadaye.Kazi yao kubwa ilikuwa ni kupiga picha na baadaye wakageuzia muziki.Walitoa rekodi kama "Tazama Tanzania (1986"),"Maridadi Sana (1984)" na "Mwl Nyerere (1984)".Walikuwa wasanii wa kwanza kwanza kutoa swahili movie iitwayo "Maridadi".Waliwahi kushirikishwa kwenye All Stars Orchestra iliyotengenezwa na BASATA wakati huo kuimba katika charity balls mbali mbali Tanzania aidha za CCM au Serikali wakisindikizwa na wanamuziki wengine wazalendo.Kwa hesabu za haraka haraka Nipa atakuwa mtu mzima sana sasa!
Aliyeimba "Tanzania eeh" song anaitwa Martina Chambiri na hii ilikuwa katika tamasha la kimataifa la watoto huko Italy maarufu kama Zecchino d'Oro.Watanzania wengi hawakufahamu nyimbo ile mpaka presenters maarufu wa Radio One (Master T na Mike Mhagama) wakati ule walipomleta studio na kuzungumza naye na toka hapo wimbo ukawa maarufu sana.Binti sasa yuko chuo kikuu na anafanya vizuri sana,ila bahati mbaya baba yake mzazi alifariki dunia akiwa bado sekondari.
Habari wana Jamiiforums? Leo nimeisikia ile nyimbo ya kipindi cha Watoto Show Radio One, nikamkumbuka yule mtoto aliyeiimba. Wanaojua yuko wapi na anafanya nini kwa sasa atujuze. Ni hayo tu!
Habari wana Jamiiforums? Leo nimeisikia ile nyimbo ya kipindi cha Watoto Show Radio One, nikamkumbuka yule mtoto aliyeiimba. Wanaojua yuko wapi na anafanya nini kwa sasa atujuze. Ni hayo tu!
kumbeee!!! hivi ule wimbo upo mitandaoni kweli nimeuMiss....sijui naupataje!Yule alikuwa mtoto wa Kihindi, sijui hata alipotelea wapi.
Varda Arts GroupYule alikuwa mtoto wa Kihindi, sijui hata alipotelea wapi.
hahaha"Watotoo wasafi moyoni ni nyota za macho za wazazi, sisi ni maua tulioopendwa na Mungu mwenyezi"
(niekee beat kwanza)
Mkuu yupo ni mkubwa sasa anaitwa Melody Mbasa anawimbo mzuri sana unaitwa Nikoleze, anaimba huyo Bella anakaa pembeni.Habari wana Jamiiforums? Leo nimeisikia ile nyimbo ya kipindi cha Watoto Show Radio One, nikamkumbuka yule mtoto aliyeiimba. Wanaojua yuko wapi na anafanya nini kwa sasa atujuze. Ni hayo tu!
Nadhani ndiye aliyeimba nyimbo ya mbuga za wanyama. Ni nyimbo ya mda mrefu sana,ikitoka kupigwa hiyo nyimbo inapigwa ya Emmanuel Nkulila.
Nashukuru KWA hilo songi
ni profesa huko kwao anafundisha music
Semboko,Hivi Mike Mhagama sio ndio Marehemu Deo Filikunjombe?Kichuna,Amina Chifupa alianza hivyo hivyo,mwisho "akafundishwa" utangazaji na akina Mike Mhagama na Deo Mshigeni,baadaye akaupata ubunge.Mungu amrehemu alikuwa mbunge matata sana na shukrani ziwaendee waliomfanya awe maarufu.Kutembea kwako kwa miguu basi wewe ulikuwa unakaa Mlimani,Mwenge,Kijitoonyama au Sinza maana ni sehemu hizo tu ni karibu na Mikocheni,lol.