chizcom,
Nimekusoma mwanzo hadi mwisho na nimejiridhisha wala huna uelewa wa kutosha kwenye hii mada. Ngoja nikupe mawili matatu. Kwanza ni kweli watu aina ya Ontario walikuwa wanamwaga darasa kwa sababu kuu 2. Sababu ya kwanza wapate watu watakaojiunga na classes zao, na sababu ya pili hao watu wawaunganishe kwa brokers ili hatimae wapate kamisheni!! Na mara nyingi kama sio zote, hawa brokers wanakuwa brokers uchwara ambao hawajaji-establish.
Tukija kwenye crypto, kwanza ni mjinga tu ndie atalipa kusoma crypto class! Forex ina mambo mengi ya kujifunza kulinganisha na crypto. Kikubwa unachotakiwa kufahamu kwenye crypto ni legit exchange markets na jinsi ya ku-point hizi crypto. Na kama ni mgeni kwenye game, kikubwa unaweza tu uka-focus kwenye well established crypto ambazo hazipo kwenye risk ya kutoweka ingawaje kwa wenye mitaji midogo crypto kama hizi zitaishia kukupa hela ya kula tu, lakini kama unahitaji kutusua basi unatakiwa kulenga new crypto ambazo ni very risk kwa sababu, kimsingi crypto haina tofauti na biashara zingine tunazofanya kila leo!! Kama ambavyo watu 100 wanaweza kuanzisha biashara mpya na kwa mara ya kwanza leo, lakini baada ya mwaka 1, huku ni 10 tu kati yao ndio wali-survive, na 90 wote walikata mtaji. Hivyo ndivyo huwa kwa new cryptos. Nyingi huwa zinaingia sokoni lakini ni chache ndizo zina-survive! Sasa kama huku-point sawasawa, unaweza kujikuta vidola vyako 200 uli-invest kwenye new crypto ambayo inakuja kupotea baada ya muda!
It's business. Lakini $200 hiyo hiyo kama uli-invest muda muafaka, na crypto husika ika-survive, amini usiamini pesa ambayo unaweza kuingiza unaweza hata kuona aibu kuichukua. Ngoja nikupe mfanmo wa Shiba Inu
View attachment 2095289
Unaona hapo juu, August 13, 2020 coin moja ilikuwa inauzwa $0.000000000157. Sasa jiulize kwabei ndogo kama hiyo, na kama ungewekeza $200 ungepata coins ngapi? Kwa hesabu za haraka haraka, ungepata at least coins 1 Trillion. Baada ya Shib kwenda kwa slow motion kwa miezi kadhaa baadae baadae bei ya Shib ikapanda kwa kasi ya roket, ndo hapo nilipoweka box. Siku hizi bei ya Shib imeporomoka (hii ndo tabia kuu ya crypto) lakini pamoja na kuporomoka huko, bei yake kwa sasa ni $0.0000212. Sasa piga hesabu mwenyewe. Assume ndo uliwekeza zile $200, ukapata coins Trilioni 1, na leo ndo unaamua kuuza kwa $0.0000212 kwa coin. Hivi ulishajiuliza ungechukua dola ngapi hapo?! Hivi usingeona aibu kuchukua pesa yote hiyo wakati uliwekeza $200?
NInachokueleza hapo ni kwamba, Crypto sio utapeli. Utatapeliwa endapo umeingia kichwa kichwa bila kupata right information kutoka kwa right people. Tatizo lingine ndo hilo la ku-point, na upoint wakati gani. Kwa mfano, hivi sasa Shib bei yake ndo hiyo $0.0000212. Ukiona hayo mazero zero unaweza kujipa matumaini kwamba ni very cheap! In a long run, unaweza kuita ni cheap, lakini in a short run, tayari hapo bei yake imeshangamka!
Kwahiyo utake usitake, dunia ndo inaenda huko hivi sasa. Badala ya kujitisha na kuwatisha wenzako, chukua muda ujifunze! Huna haja ya kumlipa mtu kujifunza crypto. Lakini kama unaona kuwekeza pesa hapana, basi pitia hii post hii
hapa. Hapo nimeelezea crypto inayoitwa Pi ( π) Coin. Hii haijaingia sokoni, kwahiyo hulipii hata senti 5 isipokuwa through mining. Of course, ingawaje Developer wa hii coin hawajaweka wazi lakini technique wanayotumia ndo kama hiyo uliyoita pyramid scheme. Hata hivyo, huyo haiwezi kuwa pyramid scheme kama unavyoweza kudhani. Kwanza, Founders wa hiyo project ni United States Citizens ,a ni graduates wa Stanford na ni PhD Holders. There's no way wanaweza kuanzisha pyramid scheme wakati pyramid scheme ni illegal ndani ya US. Na taarifa za hao founders zipo public, na kwahiyo kama wangelenga kuanzisha pyramid schemes, basi wasingeweka taarifa zao public. Hata hivyo, wanatumia hiyo model ambayo kwa haraka haraka unaweza kuamini ni pyramid scheme kwa sababu nguvu ya kwanza ya crypto coin yoyote ni kuwa na users wengi. Ikishakuwa na users wengi, itasajiliwa kirahisi tu kwenye legit exchange markets. Na pili, users wengi ni tafsiri ya kuwa na holders wengi waliosambaa sehemu mbalimbali duniani. Kuna biashara nyingi tu siku hizi zinapokea crypto kama medium of exchange. Sasa crypto inapokuwa na users wengi, inakuwa pia rahisi kutumuka na baadhi ya merchants kama medium of exchange. Kadri coin husika inavyozidi kukubalika, ndivyo bei yake inavyozidi kupanda kwa sababu demand inaongezeka!
Kutokana na hilo, unakosea sana unaposema "wanataka wafuasi wa ku-boost coin yao" huku ukiamini ni coin ya developers. Ingia twitter na utakuta coins nyingi zina akaunti kama hizi hapa chini
View attachment 2095322
Unaona hizo ni Army Accounts ambazo members/coin holders wanazianzisha wenyewe bila kutumwa na yeyote ili kui-promote coin. Wakati wewe unaamini ni "coin yao" kwa maana ya coins za developers, hawa armies wanaamini ni "coin yetu" kwa sababu bei ikitusua, na wenyewe wanatusua.
Chifu, usikubali kujifungia kwenye box la mbao, jifunze!! Hayo uliyoandika hapo juu ni kituko ambacho kinaonesha moja kwa moja hii industry bado kabisa huifahamu! Na pia ushauri wangu ni ule ule, kama hutaki kutumia pesa,
bofya hapa kwa ajili ya uzi utakaokuwezesha kupata coins bila kulipa hata senti 5!
Naogopa post itakuwa ndefu lakini ningeonesha jinsi ambavyo nilipata zaidi ya Dogelon zaidi ya 100M bila kulipa hata senti 5. Of course, kama ilivyokwa crypto zingine, hivi sasa bei yake imeshuka sana lakini nikisema niziuze leo, sikosi $100 lakini nikivumilia na kuziacha zikae tu, usishangae baada ya muda zikafikia hata $10K