InvisibleTarget
JF-Expert Member
- Dec 20, 2014
- 1,138
- 2,176
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Bado muendelezoMbona ya pili siion jamni
Nashangaa shangazi ananisema tu bila sababuShangazi
Huyu kikojozi
Vipi tena[emoji848]
😂😂😂DahUtakuwa mchawi wewe. Unasonga ugali usiku huu wa manane? Mna kikao na wanga wenzako?
Nimefika tayari, asante mrembo
Ukisikia Mwanakulifaindi mwanakuligeti ndo hii😂Daah! Clepatina kuna jambo unalitafuta, umejibu comments zote umeshindwa kuweka ep 2,
Ngoja wananzengo wakushukie kama Eagle [emoji23]
Episode ya kwanza tu tuanze kulia... hapa ni kuweka alama na kurudi akiweka nukta..... hadi page ya 12 hakuna muendelezo?tembo atatia maji muda si mrefu, fanya kitu Clepatina tumesubiri vya kutosha.
Ngoja na sisi wengine tuianze...Niko nimejilaza zangu kitandani nikiwaza na kuwazua huku nikifurahia mvua na radi zinazoendelea huko nje.
Katika kuwaza na kuwazua nikamkumbuka Clepatina wa umri wa miaka saba au nane hivi aliyekua akiishi na baba na mama yake wa kambo huko kijijini.
Mvua hizi zimenikumbusha mbali utotoni ambako kumbukumbu zangu 91% ni za majonzi lkn mapito yaliyotengeneza kumbukuku hizo ndio yamefanya niwe huyu Clepatina niliye leo.Leo hii nikoje?
Leo hii nina miaka 26,nina nyumba 8 Dar za kupangisha na moja Mwanza.Yenye kuleta kodi ndogo ni ile ya 450,000 kwa mwezi.Ni mhitimu wa darasa la 4..Ninaongea kiingeraza kizuri kuliko degree holders wengi(sijatukana ni uhalisia)..Ninapenda tough cars mojawapo ni Jeep..Nina vitabu 6 vya passport vilivyojaa mihuri ya nchi mbalimbali duniani..Ninamiliki shepu halisi la kiafrika na sura nzuri ya upole..Ninamiliki roho mbaya(kwa wanaume na kundi fulan la wanawake)Nina mashamba,viwanja na majengo ya biashara,ninaishi kwenye appartment ya kupangisha..Nina mchumba ninayempenda sana ila ninampenda Yesu zaidi yake.(Ashukuru hili).
Clepatina ni moja ya wanawake wachache duniani wanaojua kwa hakika namna ubongo wa mwanaume unavyofanya kazi.Ukimuona kaka yako au jamaa yako yeyote wa kiume anamrushia manati Clepatina mwambie aache au aendelee at his own risk mana kabla ya kumpokea Yesu moja ya fantansy ya Clepatina ilikua ni kuhakikisha siku moja kabla siku ya kurudi kwa muumba wake haijafika awe amekunywa supu nzuuri isiyokosa ndimu na pilipili na chumvi ya kutosha ya nyama ya DUSHE la mwanaume atakaejipendekeza kwake at the wrong but right time.Moyo wa Clepatina ni mweusi sana juu ya wanaume.
Baba wa Clepatina ni memba mkongwe hapa JF.Ana ID maarufu inayojulika a na wengi.Ni miongoni mwa members wanaochangia madini ya maana humu na kamwe humkuti kwenye nyuzi za upupu. Very cool guy na hakwaruzani na mtu na wengi wenu humu mmetokea kumpenda na kumuheshimu ila JE CLEPATINA ANAMPENDA BABA CLEPATINA?
Hivi nilikua naongelea mvua na radi eeh?Basi bwana jirani na nyumba ya faza tulikokua tukiishi kule bush kulikua na nyumba moja ya mzee mmoja tajiri lililokua likiishi Dar ila alikua akijenga shule kubwa ya boarding kijijini kwetu.Nyumba hiyo alikua akiitumia anapokuja kijijini kusimamia ujenzi wa shule yake.
Familia yetu ndio iliyokua ikiitunza nyumba hiyo anapokua hayupo na anapokua yupo alikua akimpa mama yangu wa kambo pesa kwa ajili ya huduma za kupikiwa na kufuliwa.Step maza alikua anapika kisha anakiweka vizuri kwenye kapu na kunipa nimpelekee uncle mzee Kipipa.
Mchana nilikua nampelekea kule site kunakojengwa shule na jion nilikua nampelekea nyumbani kwake.
Siku moja jion kwenye saa moja kasoro hivi kukiwa bado kuna mwanga kama kawaida mama yangu wa kambo alinipa kapu la chakula nimpelekee mzee Kipipa.
Nikiwa njiani mvua kubwa ikanyesha na kunilowesha chapachapa na kufanya kigauni changu king'ang'anie mwili na kulichora umbo langu kisawasawa.
Nilipofika nyumban kwa mzee Kipipa niligonga hodi akatoka nikanyoosha mkono huku nikipiga magoti kwa heshima ili nimkabidhi kapu la chakula kisha nikimbie kurud nyumban lkn badala ya kupokea chakula aliganda pale mlangoni akiniangalia huku akijilambalamba ulimi na baada ya muda macho yake yakageuka kuwa mekundu na taratibu nikaona suruali yake sehemu ya zipu ikifutuka mpaka ikawa kama mtu ameficha bastola pale.
Hali ya suruali yake ikanikumbusha mjomba wangu wakati naishi na shangazi.Nilikumbuka kuwa suruali au boxer ya mjomba ilikua inakuwaga vile siku alizokuwa akinibaka kule kwa shangazi.
Kengele ya hatari ikalia na sikutaka kupata tena maumivu kama niliyokuwa nayapata wakati mjomba alivyokua akinilalia kunibaka lkn sikuwa na uhakika kama hali ile ya suruali kutuna ni kwa watu wabaya kama mjomba tu au hata wababa wema hupatwa na hali hiyo.
Wakati nawaza hayo huku nikitetemeka kwa baridi na woga wa nilichokiona kwenye ile suruali nikamuona mzee Kipipa akiangalia huku na huko kisha akanishika mkono na kuniingiza ndani kwake.
Sikutaka kuingia ndani kwake ila niliogopa nikikataa atanisemea kwa mama kuwa sina heshima.
Tulivyofika ndani akanipa ishara nikae kwenye kiti,nikakaa huku nikizidi kutetemeka.Muda wote huo ananiangalia huku akijilamba midogo na kutoa tabasamu pana.
Akachukua kapu lenye chakula akaweka mahot pot mezani,akapakua ubwabwa wa mchuzi wa nyama uliopikwa kwa nazi na ufundi wa mama yangu wa kambo.Harufu nzuri nzuri ya kile chakula ikajaa mle ndani.Akanisogezea sahani ile ya ubwabwa iliyojaa minofu ya kuku na kunipa ishara nile.
Kwa njaa niliyokua nayo nilitamani sio kula tu bali kumeza ile sahani nzima nzima ila nilivyokumbuka nilivyochapwa kama mbwa koko siku watoto wa step maza walivyonidaka nakula kwa jirani na jinsi step maza alivyoniambia eti nakula kwa watu ili wamuone mbaya hanipi chakula uroho wote ukaniisha nikakataa kwa kutikisa kichwa.
Nilivyokataa mzee Kipipa huku akitumia tone na na tabasamu la kirafik akaniuliza asubuhi umekula nini?Nikamwambia uji na ndiz za kuchemsha.Akatikisa kichwa kwa masikitiko kisha akaniuliza tena mchana umekula nini?Sikumjibu kuwa sijala kitu bali niliinamisha kichwa changu chini.Akaniuliza mama na ndugu zako wamekula nin mchana?Nikamjibu sijui maana nilitumwa sokoni nikauze ndizi.Akatikisa tena kichwa mithili ya mtu anayenihurumia kisha akaniuliza tena "jion hii umekula nin au utakula nin?' sikutaka kumjibu kuwa sijala bado na sina uhakika kama nitakula au la mana siku mdomo uliponiponza nikamhadithia mtu kuwa mama ananinyimaga chakula nilichofanywa achen tu so nikainamisha zangu kichwa chin mambo yasiwe mengi.
Yule mzee akaniuliza tena mama na ndugu zako wamekula nin jion hii?Nikamwambia mama alivyokupakulia wewe kilichobakia wakala wao chote.
Mzee akatikisa kichwa kwa masikitiko tena kisha akaniambia"Najua mama yako wa kambo sio mtu mzuri na ninajua anavyokutesa hivyo kula usiogope kamwe siwez kumwambia".
Nikayaamin maneno ya mzee Kipipa nikavuta sahani karibu nikaanza kupiga msosi bila hofu.Mzee Kipipa akatoa soda mbil za makopo,moja coca na moja fanta orange akanipa huku akitabasamu.Nikaipokea na kupiga fundo moja refu na nilipoweka kile kikopo chin kilikua tupu,mzee akatabasamu ,nikaendelea na wali kuku na huku akiendelea kunikodolea macho akaniambia"Unafanana sana na mjukuu wangu anayeishi ulaya"
.Niliposikia nafanana na mtoto anayekaa ulaya nilitoa tabasamu moja kubwa la furaha na hapo hapo mzee Kipipa akasema"sijawahi kukuona ukitabasamu ,kumbe ukitabasamu ndo unakua mrembo hivi kama malkia ?
Kusikia nafanana na malkia nikatoa kicheko cha furaha sbb hadithi zote alizonihadithia mama yangu mzazi enzi naishi nae zilimuongelea malkia kuwa ni mwanamke mrembo asiye na mfano.Na moja ya udhaifu wangu ni kusifiwa,napenda kusifiwa.Napenda kusikia watu wakimtukuza Mungu kwa ufundi alioufanya kwangu.
Basi nikaendelea kula na mpaka hapo nilimuona mzee Kipipa ni rafik nikawa nakula huku tukipiga story.Ananiuliza maswali najibu,namuuliza maswali ya kijinga ananipa majibu mazuri yaliyonifurahisha na kisha ikafika wakati akaniuliza "huwa unasali usiku?"
Nikamjibu ndio.Akatabasamu kwa furaha kisha akasema"Vizuri,Huwa ukisali unamuombaga Mungu akufanyie nini?"
Nikamwambia kila siku huwa namwambia Mungu "nataka kwenda kuishi na mama yangu mzazi.".Nikatabasamu kwanza kisha nikaendelea kumwambia,unajua ni siku nyingi sijamuona mama lakini siwez kusahau jinsi alivyo mrembo halafu unajua mama yangu alikua ananipenda sana?.Nakumbuka kuku walikua wakitaga ananikaangiaga mayai...(kufikia hapa machozi yakaanza kunilengalenga.Nikakumbuka nilivyokua kama mboni ya jicho la mama yangu,alivyohakikisha hali kwanza mpaka anibembeleze nile nishibe,alivyokua akinisuka vizuri na kuniogesha na kunivalisha vizuri kila siku.Nikalinganisha na jins mama yangu wa kambo anavyoishi na mim kama anaish na kijbwa koko,nanyimwa chakula,hakuna anayejal nimeoga au sijaoga,nakula peke yangu makombo,na vikiwa vitamu hata makombo sipewi.Nikiumwa wkt mwingine mpaka majiran waingilie kat ndo nipelekwe hospital na nguo navaa chafu zimechoka na mengi mengine).
Kumbukumbu za mama yangu kipenzi zilifanya nilie kwa kwikwi na mzee Kipipa alivyoona hivyo akanisogelea,akanifuta machozi na kunikumbatia nami nikamkumbatia huku nikizidi kulia. .Kumbato la mzee Kipipa lilinipa faraja ya kumbato la baba hasa ukizingatia sikumbuki kama baba yangu keshawahi kunikumbatia au japo kuwahi tu kuongea na mimi kwa upendo kama vile.
Huku akiwa anaendelea kunipa maneno ya faraja,mzee Kipipa alinibeba nikiwa nimemkumbatia na kwenda kunilaza kitandani kwake kisha na yeye kupanda.Nilikuja kujua mzee Kipipa ni mtu mbaya pale alipoanza kuingiza ulimi wake mdomoni mwangu kwani hicho ni moja ya vitendo alivyokuwa akinifanyia mjomba.wangu alipokua akinibaka.
Nikajua wali kuku umeniponza.Nikaparangana nijinasue nikimbie lakini sikuweza,nikataka kupiga yowe akaniziba mdomo,nikamuomba anisamehe aniache asiniumize ila hata hakua anasikia ninachosema sbb mdomo aliuziba.
Basi mzee Kipipa akamaliza jambo lake akawa ananiangalia kwa furaha kisha akaniambia kwa tone na uso wa kikatili"mama yako mzazi najua anapokaa!Ukimwambia mtu yeyote naenda kumuua!Sasa niahidi!!Utasema au hautasema".Akaniachia mdomo huku nikitetemeka nikatikisa kichwa kuwa sitasema.Akasema kwa ukali"toa sauti!!" nikajibu "sitasema".
Akaniangalia kwa muda huku akitabasamu then akasema "Hakika wewe ni malkia,hakuna binti niliyebahatika kumjua aliyeniburudisha kama wewe" kisha akachukua shati lake akanifuta sehemu za siri kisha akaniamuru ninyanyuke anisindikize nyumbani.
Tulipofika nyumbani tukamkuta step maza akitoka jikoni (liko nje) kuelekea ndani.Alipotuona akasimama na bila kuchelewa mzee Kipipa akasema "naona huyu mmemtuma muda mbovu leo hivyo nikaona ni vyema nimsindikize mana na giza na mvua hiz asije akakutan na watu wabaya njian".
Step maza kusikia hivyo akang'aka kwa hasira.'Yaani kaka huyu mtoto ni ana tabia chafu hujapata kuona.Huwez kuamin ameondoka hapa jua bado linawaka halafu saa hiz kwel ndio anafikisha chakuka?!Natama watu wangejua jins huyu mtoto alivyo na tabia za ajabu labda wangepunguza kusema namnyanyasa!"
Mzee Kipipa akasema" Ni mambo ya watoto tu hayo dada,michezo mingi njiani"
Step maza akanikwapua kwa hasira anipige lakini mzee Kipipa akamzuia asinipige kisha akatoa kibunda cha hela nyingi na kumpatia step maza.
Baada ya kuona zile hela step maza mimacho ilimtoka kwa mshangao kisha akauliza'Hela zote hizi za nin kaka?"
Mzee Kipipa huku akijikuna kuna kitambi akajibu"Unajua dada kwa namna familia hii imenipokea na kunihudumia bila kuchoka nataman kutoa hata zaid ya hiyo kuonyesha jins ninavyowashukuru".
Step maza kusikia hivyo akawa anashukuru mfululizo huku akicheka cheka kama chiz aloona jalala jipya na mzee Kipipa akaaga huku akisisitiza nisichapwe.
Mzee Kipipa alivyopotelea mbali step maza akanitia kwenzi moja safi kisha akanisukumiza nikalale huku akiniambia"Kalale huko mbwa wewe usiyeweza kufika ulikotumwa mpaka upitie kwa wachawi wenzio ukadowee chakula.Na ndio mana hata sijisumbuagi kukupa chakula mana najua unakulaga huko unakoendaga kunisema!Ila waambie hata sijali"
Nikaingia chumbani kwangu kulala.Chumba changu kwa sasa nikiambiwa niingie sitaweza kwa jinsi kilivyokua kinanuka mikojo.Nilikuaga kikojozi.Nikilala lazima niharibu godoro,hasa siku za mvua ndo usiseme.Nilikua nikikojoa hamna wakuniambia nitoe godoro nje wala nini.Nilichokua nafanya ni nikikojoa upande huu kesho nalala upande huu na kesho narud upande ule unakua umenyauka kidogo.
Kile chumba kilikua kinasafishwa siku wakija wageni. tu.Watoto wa step maza walikua wanalala chumba kingine.Siku dingi akiwa kasafiri kama siku hii wanalala chhmban kwa baba na mama.
Ilipofika usiku wa manane mvua iliyokua imetulia ikaanza tena kunyesha ikiambatana na radi na vimulimuli.
Nikaamka na kujikunyata kwa woga maana siku chache radi ilipiga ikaua bibi na mjukuu nyumba ya sita kutoka kwetu.
Nikataman na mim niende kule chumban kwa baba na mama na mim nikalale nao lkn ningeenda na nilivyo mchafu na harufu yangu ya mikojo ningefukuzwa kama mbwa na kipigo juu.
Nikakumbuka enzi naishi na mama yangu,usiku wa radi kama ule nikishtuka na kuogopa alinikumbatia kisha kuniambia nisiogope maana hivyo vimulimuli ni macho ya Mungu yanatupa ishara kuwa tusiogope anatuona atatulinda.
Wakati nawaza haya ghafla nikaisikia sauti ya step maza akiongea kwa ukali akisema huku anahema kwa tabu kwa harufu ya mle chumbani kwangu"Hivi ulijaza maji kwenye mapipa?"
Nikamwambia wakati nataka kujaza uliniambia niende kwanza mashineni nikanunue pumba.Akaniambia" kwa hiyo mapipa hayana maji".
Nikamwambia ndio.Ana mwanae mkubwa wa kiume miaka 11 ila hata kufua nguo zake hawez mim mdogo wake ndo namfulia.Huyo alikua ni prince Chibonge,hawez chochote zaid ya kula na kunisemelea na yeye ndo expert wa zinakopatikana fimbo nzur za kunichapia.Mdogo mtu rika langu alikua akinipenda na mie nilimpenda ila step maza hakutaka kabisa anipende wala tuwe karibu.Na akitukuta tunacheza nae nilikula fimbo nakuambiwa naendekeza michezo wkt kuna kaz kibao za kufanya.)
Baada ya kusema ndio mapipa hayana maji mama akasogea pale nilipo.Akavuta shingo ya gaun langu kisha akaninyanyua kutoka kitandan na kuniburuza mpaka mlango mkubwa wa kutokea nje ya nyumba kisha akaufungua mlango.Alipofungua tu mlango ikapiga radi kubwa na kwa woga wote tukakimbilia ndani na kufika ndani tu mim nikadondoka chini kwa kutetemeka.Ile radi ikawaamsha wanae huko chumban wakaja wakilia na kumkumbatia kwa woga.Akawatuliza kisha akaniambia ninyanyuke pale chini.Nikanyanyuka kisha akaniambia nitoke nje nikajaze maji kwenye mapipa.Nikamwambia"nitajaza kesho mama".
Hakusema kitu bali alinifata niliposimama akanivuta na kunitoa nje kwa lengo la kunisukumizia huko then afunge mlango arud chumban na wanawe wakalale.
Ila kwa woga wa kufa kama yule mbibi nikamng'ang'ania utadhan nimeng'ang"ania pindo la Yesu.Kila akijaribu kunisukumia nje anakuta nimemganga.Mwishowe kwa hasira aliniwasha kibao nikamuachia ila kila akitaka kufunga mlango arud ndan mim huyu hapa na mim nataka kurud ndani.Radi zinapiga na zinavyopiga ndo nazid kuogopa kuachwa pale nje peke yangu.
Alivyoona namsumbua akaniambia"Wewe si jeuri.Sasa utachagua kujaza maji kwenye mapipa au uondoke hapa uende ukaishi kwa shangazi yako!"Tone na sura ya step maza viliniambia anamaanisha.Kuishi kwa shangaz nilishasema ni bora kufa kuliko kurudi kule ambako mjomba alikua ananibaka halafu nikimsemea kwa shangazi ananichapa.
Unabakwa leo unaumizwa,kesho bado kidonda kibichi unabakwa tena huku mwili umejaa makovu ya fimbo za shangazi.
Nikachagua kujaza mapipa maji nife kwa kupigwa na radi kuliko kwenda kuishi kwa shangazi.Taratibu nikaenda jikon kunakokaa ndoo na mapipa nikatoa ndoo nje,nikazipanga yanakodondoka maji ya bati na kwa vile mvua ilikua kubwa ndoo zikajaa haraka.Nikanyanyua moja nikajitwisha lkn wkt natembea kuelekea jikoni nikayamimine kwenye pipa nikateleza,ndoo ikadondokea kule,maji yakamwagika nikabaki pale chin naugulia maumivu
ya kudondoka.
Step maza ambae muda wote huo bado alikua kasimama pale mlangoni akinitizama kwa chuki akasema"Endelea kujikalisha hapo mvua iishe kabla mapipa hayajajaa ndo utanitambua" kisha akafunga mlango akaingia chumbani kulala na wanae.
Nikiwa bado nimekaa pale chini radi zilizokua zimetulia zikaanza kupiga tena.Safari hii hazikua zinapiga na kulia kama zinavyoliaga kama baruti bali zikawa zinanguruma kama simba mkubwa mwenye hasira halafu zikawa kama zinaenda na kurudi ktk anga ambalo mim niko chin yake halafu kuna saa nikawa nasikia kama ule muungurumo unashuka chini huku vimulimuli vinapiga na kutoa mwanga kama jua la saa saba mchana.Kwa woga kikojozi mie nikajikojolea ila safari hii sio kwenye godoro.
Vimulimuli vilivyozid kupiga nikakumbuka mama yangu aliniambia"Huo mwanga ni macho ya Mungu yanatupa ishara kuwa anatuona tusiogope anatulinda".
Nikapata ujasiri nikasimama huku nikilia nikanyanyua uso wangu mawinguni
nikasema"ASANTE MUNGU..NAJUA UNANIANGALIA .USIACHE KUNILINDA".
Nikanyanyua ndoo yangu ilomwagika maji nikaipeleka ikajae kisha nikachukua iliyojaa,nikajitwisha na kazi ya kujaza mapipa ya maji ikaendelea.
Kila radi zilivyopiga niliogopa lkn vimulimuli vilipowaka nikapata faraja kuwa Mungu ananiangalia na ananilinda.Mapipa yalijaa maji nami nikaingia ndani nikaenda kulala lkn kabla hata usingizi haujanishika vizuri nikaisikia sauti ya prince chibonge ikisema "Mama anasema unalala mpaka saa hiz unaumwa!?Kisha akavuta shuka langu akalitupa chini halafu akasema unapenda kulala lala ndo mana kikojozi iloooh!.Unaitwa huko!"
+++++++++++++++++++++
Jamani eeh mimi sio muandishi,leo ndo mara ya kwanza naandika story,sijioni muandishi ila natamani siku moja kuwa muandishi kama kina Analyse UMUGHAKA DeepPond na wengine wengi humu.
Im just doin this for fun.
Nategemea kukosolewa.
Na kama kuna atakayeburudika itakua poa.
My sis Joannah darling bro Half
american my friend
Equation
x
Msiende piemuMikwara mbusi
Hatuendi pm mamii🤣Msiende piemu
Asante sanaStory nzuri sana hongera.
Nangoja muendelezo
Njooni huku Gily Antonnia Dejane Shunie Kalpana Bantu Lady Aaliyyah Mzee wa kupambania Uchira 1 Watu8 Nuzulati Depal Lenie Chakorii Leejay49 Johnnie Walker mshamba_hachekwi
Shukrani GilyHutaki shemeji? [emoji3]
Analyse
leadermoe
wao ni wao
Dr Restart
baby zu
Demi
Antonnia
Kalpana
Lovelovie
Glenn
Mamaya
Binadamu Mtakatifu
Darlin
Lloyd Munroe
mshamba_hachekwi
moneytalk
Dahan
Johnnie Walker
Leejay49
Amehlo
Palina
am 4 real
Shunie
Bantu Lady
charlote
Kalpana
Luv
masai dada
Tayukwa
Kelsea
Antennah
Cee
Litro
Missy Gf
Tumwambie kuna Chizi Maarifa na dr namugari hawapendi wakiona tunalia lia kuhus arosto [emoji23]Daah! Clepatina kuna jambo unalitafuta, umejibu comments zote umeshindwa kuweka ep 2,
Ngoja wananzengo wakushukie kama Eagle [emoji23]
[emoji23][emoji23] uzuri ameshaonywa kazi kwake sasa,Tumwambie kuna Chizi Maarifa na dr namugari hawapendi wakiona tunalia lia kuhus arosto [emoji23]
Huyo binti anatunga story ambayo imeshaanza mshinda. Ni ya kutafutia mabwana humu JF. Yaani anaingia kwa style ya kwamba ni single mazer ila ana uwezo kiuchumi. Sasa kuna maeneo kakosea. Ngoja namwelekeza mwendelezo atakuja wacheck. Alidhani kutunga hadithi ni kama kujisaidia tu haja ndogo. Then nitampa masaa kadhaa akishindwa namwondoa JF. Sipendi watu waongo waongo.Tumwambie kuna Chizi Maarifa na dr namugari hawapendi wakiona tunalia lia kuhus arosto [emoji23]
NIpo live sijui kilimkuta nn mzee kipipa mpaka akakondeana?EPISODE 2
Baada ya Prince Chibonge kunikurupua nilienda kwa step maza kuitikia wito.Nilimkuta yuko jikoni akipika chapati za maji na chai ya maziwa ikichemka kwenye jiko la pembeni huku mwanae wa mwisho ambae ni rika langu aitwae Tide akiwa kakaa kwenye kigoda pembeni ya mama yake akila chapati.Nyuma yangu alikua Prince chibonge.Alipoingia tu pale jikoni na kuona Tide anakula chapati na yeye akaomba akapewa moja akaikunja kisha yote akaitia mdomoni halafu akanyoosha mkono kuomba nyingine lkn mama yake akamwambia"Hebu toka hapa wewe nikikuendekeza utakula zote na bado hutashiba" lkn Prince chibonge akaendelea kunyoosha mkono huku akimuangalia mama yake kwa macho ya huzuni na mama yake kwa vile hapendi kuona wanae wakihuzunika akachukua chapati nyingine akampa na kumwambia nyingine asubirie mezani.
Na mimi nikamuangalia step maza kwa macho ya huruma nikiamin muujiza utatokea na mim nionjoshwe japo kipande lkn I was wrong kwani baada ya kumalizana na Prince Chibonge step maza akanigeukia na kuniambia"Nenda kule bafuni kuna nguo nimeziloweka ukafue",Nikaondoka kinyonge huku harufu nzuri ya chapati za step maza ikinisindikiza.Na mnyonge mnyongeni ila step maza wangu anajua kupika bana,sema tu sijui alikua ananikomoaga maana alikua akipika atahakikisha amechafua vyombo vyote.
Basi bana siku yangu ikaanza rasmi,baada ya udobi kuna kufagia uwanja,kuosha vyombo,kusafisha ndani,kuwekea bata maji na pumba,bado kuna kutumwa na katika yote hayo hakuna hata moja nililofanya akaridhika nalo,so shukran ilikua kama sio kwezi basi sitakosa japo tusi.
Nadhan mnakumbuka kuwa jana yake mzee Kipipa alimpa step maza mshiko wa maana eeh?Basi bwana lunch alopikiwa mzee Kipipa siku hiyo lilikua sio ya mchezo.Mama wa kisambaa alitulia jikon akapika vikapikika na vilivyoiva kama kawa nikaambiwa nimpelekee mjomba Kipipa chakula lkn kusikia tu hivyo nikaanza kutetemeka ghafla na nikakimbilia chumbani kulala nikajifunika gubigubi kwani nafsi yangu haikua radhi kumuona tena yule mzee lkn haikuchukua round step maza akaja kunifunua na kusema"Haya ndo mauzauza gan tena unayoniletea?Nikamwambia mama mim naumwa sitaweza kwenda lkn alinichomoa pale kitandani na kunivuta mpaka nje liliko kapu lenye msosi wa mzee Kipipa na kunishikisha kwa nguvu kisha bila kusema kitu akaweka sura ya subutu kukataa kwenda uone.Kinyonge sana nikaanza kutembea kupeleka chakula huku machozi yakinitoka na nilipokutana na watu njian nalijifuta machozi na kuficha uso mpaka nikafika site.Mzee Kipipa Alivyoniona tu kwa tabasamu la furaha akasema "Hujambo malkia wangu Clepatina" nikataka kujibu sijambo shikamoo mjomba lkn nikashindwa.Machozi yakaanza kunilenga lenga lakin nilipomuangalia niliona ananiangalia kwa macho ya kunitisha,nikawa najizuia kulia lkn nikaona mpaka nitoe mahot pot na sahani na vijiko ili nirud na kapu kama ninavyofanyaga machoz yatanizid nguvu mambo yawe mengi hivyo nikaacha kapu na kila kitu ndan yake kisha bila kuaga nikageuka na kukimbia nyumbani.
Wakati nakimbia niliwasikia baadhi ya mafundi pale site wakiulizana "kamepatwa na nin haka leo?"
Nilipokua njian nilipita sehemu kuna kichaka.Nikaingia humo nikajificha halafu nikaliaaa mpaka machoz yakawa hayatoki tena kisha nikasimama kwa lengo la kuondoka lkn nikasita baada ya kuona mti wenye vitunda fulani ambavyo nilisikiaga eti ukivila halafu ukilala unakufa huamki tena.Nikatabasamu kisha nikavichuma vingi vikajaa mikono yote miwili kisha nikakimbia kuelekea home.
Nilipofika karibu ya home nikaingia kwa kunyata ili mtu asinione.Maza nikamuona yuko nyuma ya nyumba na mashost zake wanasukana na kupiga umbea,Prince Chibonge na Tide sikujua wako wapi.Nikaingia kwa kujificha mpaka chumbani kwangu,nikafunga mlango kwa ndani na kutafuna vile vitunda vyote nikajifunika gubi gubi nikiamini usingizi ukinichukua tu ndo imetoka hiyo siamki tena na hakuna atakayeweza tena kunituma kwa mzee Kipipa.
Hata hivyo nilikuja kuamka saa mbili ya usiku ule.Kilichotokea ni kwamba mama alijua tokea nitumwe ule mchana kupeleka chakula kwa mzee Kipipa sikurudi tena kwa vile hakuna aliyeniona nikirudi.Masaa yakapita,prince Chibonge akatumwa akanitafute hakuniona na kwa majirani sikuwepo. Maza akamtuma Chibonge akatafute fimbo nzuri kubwa zinisubir nitakaporud lkn mpaka muda wa kupeleka chakula kwa mzee Kipipa ukafika hawakuwa na wazo la kutazama chumbani kwangu.Ikabidi Prince Chibonge ndio apeleke chakula siku hiyo.
Kufika kule mzee Kipipa akauliza kwanini leo umeleta wewe na sio Clepatina?Prince Chibonge akajibu"Shida yako ni chakula au Clepatina?"Mzee Kipipa akataka kumdaka Chibonge amchape ila Prince Chibonge akafanikiwa kukimbia.Prince Chibonge alitokea kumchukia mzee Kipipa tokea siku ya kwanza anafika nyumbani kwetu na shikamoo yake kwa mzee Kipipa ilikua inatoka kwa kulazimishwa.
Kufika saa moja na nusu hivi usiku, mmoja wa majirani aliyefika pale nyumban kusaidiana mawazo juu ya nini kifanyike kwa kupotea kwangu akiwa anelekea chooni kwetu ambako njia iko karibu na dirisha langu alisikia sauti ya kicheko kutoka chumbani kwangu.Akachungulia na kumulika na tochi zile za betri na hamadi ananiona nimelala fofofo nacheka usingizini.
Jirani yule akaahirisha safari ya kwenda chooni na kisha kwenda kumuuliza mama yangu wa kambo"Uliangalia chumban kwake?".
Hilo swali ndo likamkumbusha step maza kuwa wametafuta kijiji chote kasoro chumban kwangu.Basi yule jirani akawaambia alichokiona na kweli kufika pale dirishani wakanikuta nimelala fofofo sina habari nacheka zangu ndotoni.
Zoezi la kuniamsha likaanza lakini halikua rahisi maana waliita, walirusha magunzi,maji,vimawe lakini wapi.Kama sio kule kucheka ndotoni wangehisi nimekufa.Ilibidi mlango uvunjwe nitikiswe kwa nguvu ndio nikaamka.Kilichofanya nilale vile ni mlundikano wa usingizi wa siku nyingi na uchovu.Mara nyingi nilikua nachelewa kulala nawahi kuamka.Nikaulizwa kama niko sawa nikajibu niko sawa step maza akajifanya eti amefurahi hadi akalia kwa furaha eti maana alidhani eti mwanae kipenzi nimepotea au nimepatwa na kitu kibaya ila majirani walivyoondoka usitake kujua nini kilinipata.
Siku hiyo ikawa imepita hivyo na siku nyingine zikaja na kazi zangu ni zile zile ikiwa ni pamoja na kumpelekea mzee Kipipa chakula site na nyumbani kwake jion.
Mzee Kipipa nae akaendeleza ufiraun wake, mara ya pili ya tatu na mwishowe ikawa ni utamaduni na kilichomsaidia ni kwamba kila alipomakiza ushetani wake ilikua lazima anipe hela huku akiniambia "hizi kampe mama yako mwambie mjomba anasema asante".
Ghafla step maza aligeuka bosslay wa kijiji kwa pesa za mzee Kipipa.Hakuna kanga/tenge mpya ilitoka akashindwa kununua,alokula vizur mtaan alikua yeye,kuvaa vizur ni yeye, inshort pesa ndogondogo hazikua issue kwake.Nadhani kuna mahala ilifikia step maza akajua kinachoendelea kule kwa mzee Kipipa ila kwa vile sikua mwanae na kwa vile hela ya mzee Kipipa ilishamnogea ikafika wakati kabla ya kunituma nipeleke kapu jioni alikua ananiambia nikaoge kwanza na nilishangaa siku step maza aliponipa mafuta yake nijipake na kuniambia nisirudie gaun chafu bali nikavae gauni langu la kanisani.Mwayego nilipendeza kisha akanipa kikapu nipeleke chakula kwa mjomba mzee Kipipa.Mzee Kipipa alivyoniona akasema vile ndo napaswa kuwa kila niendapo kwake.Akafanya afabyayo na kama kawaida alipomaliza akinipa hela nimpelekee step maza tofaut ni kwamba siku hiyo hela zilikua nyingi.
Maisha yakaendelea hivyo,nikawa mnyonge siku hadi siku, sina raha na mara nyingi nilitamani kujiua.
Ujenz wa shule ya mzee Kipipa uliendelea na siku moja akaaga kuwa anarudi Dar mara moja kwenda kupumzika na kuwaona familia yake.Step maza aliipokea habar hiyo kwa huzun mithili ya mtu aliyesikia habari ya msiba lkn kwa upande wangu ilikua ni habari ya faraja tena nilitaman yule mzee agongwe na gari afe kabisa na asirud tena kijijin kwetu.Kwa upande wangu mzee Kipipa aliniaga tokea jana yake alipomaliza kunifanyia ushetani wake.Aliniambia kuwa kesho ataondoka kijijin ila akirud akasikia nimemwambia mtu yeyote kuhusu 'uchumba' wetu basi atamuua mama yangu mzazi.
Basi mzee Kipipa akasafiri huku akiaga kuwa atarud baada ya mwez mmoja lkn miez na miaka ikakatika ila hakurudi tena.
Kwa upande wangu kuondoka kwa mzee Kipipa kulipunguza mzigo mzito wa mateso lakini baada ya kipindi fulani nikaanza kutokwa na vitu vichafu sehemu za siri,homa kali na nilikua natoa harufu mbaya.
Baada ya majirani kuanza kunong'ona step maza akanipeleka hospitali.Nikatibiwa na kuambiwa niseme anayeniingilia.Nilibembelezwa,nilitishiwa lkn kila nilipoulizwa nilisema sijui na mwishowe yakaisha hayo.
Nilikua mtoto mwenye kupenda shule lakin mahudhurio yangu yalikua mabaya kutokana na majukumu ya nyumbani.Hata hivyo pamoja na kuwa Tide alikua hakosi shule lakini mim mwenye mahudhurio mabovu nilifaulu vizuri sana kwenye mitihani yetu ya mwisho ya darasa la nne na yeye kufeli kias cha kuhitajika kurudia darasa.Mim na Prince Chibonge ndio tuliokua tunaongoza kwa akili shule.
Wiki ya kwanza ya mim kuripoti shule kama mwanafunz wa darasa la tano step maza ambae alikua amelazwa hospitali kwa kupooza akaruhusiwa aendelee na matibabu nyumbani.Mpaka anarudishwa nyumnan ndugu zake wengi waliokuja kumuuguza wakawa wameondoka na hivyo ikawa amebakia mama yake ambae nae alikua ni mgonjwa.
Basi ikawa kila siku nikitaka kwenda shule naambiwa nibaki nimsaidie bibi yule kaz za nyumbani.Kina Tide na Prince Chibonge wao wanaenda shule.Wiki mwezi,miez mwaka na ndo ikawa bye bye sikurudi tena shule.
Baada ya kipindi kirefu sana baba akarud nyumban siku moja,ilikua ni furaha kubwa kwangu nikitumai ya kwamba ujio wa baba utabadili maisha yangu.
Nikatafuta wasaa,nikamueleza yote ninayopitia pale na kwamba kama inawezekana anipeleke nikaishi na mama yangu.Baba akasema amekuja mara moja kumuona mama na kwamba atakaa siku tatu tu na kuondoka ila atakuja kunichukua nikakae nae huko kazin anapokaa na nitaendelea na masomo huko lakin baada ya kuondoka dingi hakugeuka nyuma.
Kumbe zile chuki zote za step maza kwangu zilichangiwa pia na kutelekezwa na dingi.Dingi wangu alikua na bado ni mzee wa totozi nyingi.Wakat step maza anaumwa dingi alikua keshaanzisha maisha na mwanamke mwingine wanaishi kama mke na mume.Hata alivyokuja alikuja tu kibinadamu lkn hakuwa amekuja kama kwa mkewe.
Yule bibi,mama yake na step maza alikaa na sisi kama miez minne hivi kisha na yeye akaondoka ikawa wanakuja wale ndugu wakuja kumuona mgonjwa leo na kuondoka kesho lakin pia step maza alishapata nguvu wakutembea mwenyewe lakin alipata changamoto ya kudondoka kama mtu mwenye kifafa.Anaweza akawa kashinda vizuri tu ghalfla akadondoka.
Ugonjwa wa step maza ulinifanya nikomae akili kabla ya umri kwani alivyoondoka yule bibi ikawa kama vile mim ndo mama wa ile familia.
Imagine mtoto wa umri wa kuwa darasa la tano nilikua bila kuelekezwa najua nikiamka nifanye nini,nipange tutakula nin kulingana na pesa niliyopewa na siku hakuna pesa nilijua nikachume nini shamban au ndan kuna nin nipike tule.
Pamoja na kuwa prince Chibonge alikua mkubwa kwangu na Tide tulilingana ila mim ndo nilikua kama dada yao mkubwa.Nilikua naweza kwenda dukan bila kuambiwa na mtu na kukopa sabuni ili ndugu zangu wafue nguo za shule au nifue nguo za step maza.
Hichi ndo kipindi atep maza alikua akinionesha upendo.Nilipokua nikimpelekea msosi alikua akiuliza kama na mim nimekumbuka kula au nahudumia wengine tu.Ndo kipindi alitoa kanga zake sandukuni akanigea,ndo kipindi alinambia mim ni baraka kwake na aliniahid ni lazima nirud shule akishapona.
Kwa vile manyanyaso yaliisha na nilikua nakula nakushiba nilinenepa na kwa vile mim ni supa tall kama baba yangu na shepu kama la mama yangu nilionekana kama msichana mkubwa kumbe toto la la tano.Mrefuu,juu mwembamba chin nimwagie kama namba 6.
Vijana wazee na waume za watu wote walikua wanafukuzana kuonja makombo ya mzee kipipa lkn wote niliwaona kama mbweha tu na kama sikuwaona kama mzee Kipipa basi ni kama mjomba na kama si kama mjomba basi ni kama baba tu.Mpaka hapo nilishajijengea picha kuwa wanaume wote hawana huruma.
Siku moja mwezi wa December ya ule nwaka niliotakiwa niwe la tano nilikua nimeenda kuhemea na wakati narudi nyumbani nikamkuta step maza akiwa amekaa nje na mgeni aliyeonekana kutoka mbali.Kufika karibu wala haikuchukua muda kumkumbuka sura chafu ya mzee Kipipa japo alikonda hadi kitamb kikamuisha.Step maza kuniona tu akasema kwa furaha"Mwanao uliokua ukimuulizia kila saa huyo hapo"
Baada ya kuambiwa vile mzee Kipipa alionekana kunishangaa sana kisha akasema"Ina maana Clepatina ndio amekua..amekua...mmm...mmmkubwa hivi?"
Step maza akacheka halafu akasema "watoto wa siku hizi kaka wanakua kama uyoga sijui wanakimbilia wapi" kisha step maza akanigeukia na kuniuliza "Klee unamkumbuka mjomba wako au umeshamsahau?"
Baada ya swali hilo
Nikamgeukia mzee Kipipa aliyekua akijichekesha chekesha pale nikamtizama kama sekunde ishirini hivi kwa sura ya kumchimba biti nililomaanisha kisha kwa sauti iliyochanganyika hasira,uchungu,kisasi na kwa kujiamini nikamkazia macho nikamwambia
"NAWEZA KUISAHAU SURA YA BABA YANGU NA NIKAWA NA AMANI LAKINI SIWEZI KUISAHAU SURA YAKO NA NIKAISHI KWA AMANI!!".
Baada ya kumtamkia maneno hayo niliendelea kumkazia macho kwa muda mrefu kisha nikageuka polepole na kutembea kuelekea jikoni na kimya kikuu kikatawala nyuma yangu.
My sis Joannah darling bro Half american bestie Equation x
Watu8 Analyse To yeye Shunie Antonia Gautama cocastic babukijana Depal Glenn Unique Flower dronedrake
Dr. Mariposa