Ironbutterfly
JF-Expert Member
- Feb 5, 2023
- 3,042
- 8,227
Aggrrr umeniudhi tu kutumia jina la my mother kwenye story yako 🙏lol
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Weuweeeeeeee bestieee, tamuuuuuuEPISODE 3
Kabla sijawaeleza namna nilivyoya terorise maisha ya mzee Kipipa hadi kufikia kupoteza fahamu kwa presha na jinsi nilivyomuwashia moto kwa kutumia pesa na connections zake hadi akafikia wakati fulani kufanya jaribio la kuikimbia nchi ili awe mbali na mkono wangu ningependa kwanza kumtambulisha kwenu mama yangu mzazi.
Mama yangu mzazi, Sophia ni binti wa kisambaa aliyezaliwa katika familia ya watoto 18.
Babu yangu mzaa mama alikua ni mzee tajiri wa kiislam aliyeishika dini ya kiislamu hasa hasa hasa.
Babu yangu aliyekua na wake wanne alikua anaheshimika sana na kuna msikiti mpaka leo una jina lake ambao yeye babu yangu aliujenga.Mbali ya kujenga misikiti babu yangu anakumbukwa kwa kutoa misaada kwa wasiojiweza.
Wake na watoto wote wa babu yangu waliishi kwa kufuata maadili na misingi ya dini ya kiislamu isipokua mtoto wake mmoja tu,Sophia.
Sophia alikua tofauti na alivyotamani baba yake kwani pamoja na kuzaliwa kijijiji tena katika familia bora ya kiislamu yeye alitokea tu kuwa na tabia za ki slay queen.Mambo ya kuvaa majuba na ushungi yalimshinda Sophia.
Sophia alijijua ana umbo na sura nzuri na alipenda dunia ilione umbo lake hivyo vimin na visuruali vya kubana ndo zilikua pigo za Sophia.
Mbali ya uslay queen wa kuzaliwa nao Sophia pia alizaliwa na roho ya kijasiri.Ukimzingua ndugu yake yeyote Sophia alikua anakufata na kukuzingua na wewe.Pamoja na ufupi wake ila Sophia alikua haogopi kupigana na wanaume na alikua ana kauli yake anasema "mimi napigana na wanaume wanawake wenzangu sipigani nao bali nawapiga" .
Baada ya babu na wazee wengine wa kiislamu kumuonya Sophia bila mafanikio babu akamfukuza Sophia nyumbani kwake.
Sophia akaenda kuishi nyumban kwa kina rafiki yake aitwae Hosana.Huyu Hosana alishaondokaga na kwenda kuishi Dar ambako alikua anafanya kazi za ndani lkn wakati Sophia alipoenda kuomba hifadhi pale alikua amekuja mara moja kusalimia wazazi wake na kuwaeleza kuwa ni mjamzito na kwamba kwa sasa kuna mwanaume wanaishi nae huko Dar na wana mpango wa kuoana.
Hosana akamaliza siku zake pale kijijini na kuondoka kwa ahadi ya kumtafutia kazi Sophia.
Sophia aliendelea kuishi na mama wa Hosana na baaada ya muda Hosana akampatia kazi ya u housegirl huko Dar na nauli ilipotumwa Sophia akaingia Dar na kwenda kuish kama housegirl.
Hata hivyo Sophia hakuwa anadumu kwenye kazi sbb ya kushindwa kuvumilia manyanyaso na kubaguliwa.Kuna siku alimchamba mama mwenye nyumba ambae alikua mchoyo na mwenye roho mbaya ya kutaka Sophia ale viporo hata vilivyo chacha.Sophia alivumilia kidogo ustaarabu ukamshinda siku ya siku akamwambia yule mama"Baba yangu ana uwezo wa kukulisha wewe,mumeo,watoto wako na koo zenu zote mpaka siku mnakufa!Usinione hapa kwako ukadhani nimekimbia njaa kwetu!".
Kwa hiyo Sophia alikua ana kazi ya leo ni housegirl nyumba hii kesho nyumba ile lkn wakati wote huo Hosana ndie shoga ake mkuu hapo mjini Dar.Kitendo cha Sophia kwenda kumtembelea Hosana mara kwa mara kikafanya Sophia atambulike kwa shem wake mume mtarajiwa wa Hosana.
Umbo namba 6 la Sophia na weupe wake wa kisambaa ukamchanganya mume mtarajiwa wa Hosana.Akamtongoza na kumuahidi kumpangishia chumba na kumpa mtaji wa biashara aachane na kazi za u housegirl.Sophia akapiga mahesabu akachekecha akaona hata yeye anatamani kuishi kwa bata kama shogake Hosana, akakubali.
Baada ya kupangishiwa chumba na kuanza kuhudumiwa Sophia akatamani ampindue kabisa shogake abaki yeye lakini kila alivyojitahidi kumtoa Hosana alishindwa.Badae akagundua Hosana ana thaminiwa na yule mwanaume wao sbb amemzalia mtoto hivyo miaka miwili na kitu hivi baadae na yeye akashika ujauzito na hatimae akazaa katoto kake kazuri ka kike akakaita Clepatina.
Mpaka Clepatina anazaliwa ndio Hosana ambae ndie mama yake na Prince Chibonge alipopata majibu ya kwanini mipango ya kuolewa na baba Prince Chibonge ilivurugika ghafla na ndipo alipojua kumbe Sophia ndiye sababu ya baba Prince Chibonge kupunguza mapenz yake kwake na ndio alipojua ya kwamba kumbe na Sophia amezaa na baba Prince Chibonge.
Urafiki wao ukazikwa rasmina uadui wa kuapizana na kutamkiana kutoana roho ukazaliwa kati yao na kila mmoja wao akawa anatumia kila mbinu aolewe yeye.Mama Prince Chibonge yeye kila siku alikua anaenda kwao kuloga na mama Clepatina yeye kazi yake ilikua kumuonyesha mwanaume wao madanga ya Hosana ili tu aonekane sio wife material.
Amani ikatoweka kwenye nyumba za wanawake zake wote.Akienda kwa mama Prince Chibonge anatuhumiwa hivi,akirudi kwa mama Clepatina anatuhumiwa hivi.Alivyoona makelele yamezidi akawabwaga wote.
Baada ya kuwaacha hawa wanawake haikuchukua muda mrefu faza akasimamishwa kazi.Akawa choka mbaya anashinda Bar na vijiwe vya madalali.
Hawa wanawake nao kila mmoja akawa anahangaika kivyake kupata hela ya kulisha mwanae.Mama Prince Chibonge yeye akajikita kwenye biashara ndogo ndogo na mama Clepatina yeye akaangukia kuwa muhudumu wa Bar.
Hata hivyo mama Clepatina hakuwa muhudumu wa Bar wa kawaida na hakwenda kuomba kaz ya kuuza Bar bali kuna mwenye Bar alimuona alivyo akajua huyu binti akikaa kwenye Bar yangu wanaume watakua wanapanga foleni hivyo akamshawishi akafanye hiyo kazi kwa dau kubwa.
Kwa Kweli Sophia alikua Bar maid mwenye viwango.Alikua slay queen kweli kweli na msambaa yule ni ana maringo mpaka leo hii.Mama yangu ilifikia level akawa ana drive kwenda kazin kwake Bar kuhudumu na alikua anaishi kwenye bonge ya jumba ila la kupangisha na alikua na housegirl wa kumlelea Clepatina wake.
Hichi ndo kipindi Siphia alikua Sophia kweli.Mweupeee,softiii,sura sasa na ukija kwenye hilo umbo la namba 6 halafu ujumlishe na midhahabu aloijaza mwilini plus mavazi ya gharama na uchanganye na zile nyodo zake weeuwee!
Mama Clepatina akapata dili ya kwenda Afrika kusini ila haikuwa safari ya kuweza kwenda na mtoto.Ikabidi tusafiri kwenda mpaka usambaani kwa lengo la kwenda kuniacha kwa babu na bibi ili yeye akatafute maisha South.Mpaka wakati huo babu alishafulia na maisha yake yalikua yakutegemea watoto na katika watoto wake wote mama yangu Sophia ndo alikua na pesa kuliko wote.
Basi tulifika pale nyumbani kwa babu na pick up ikiwa imejaa mazagazaga kama yote ya zawadi.Viroba vya michele,vya sukari,ndoo za mafuta,mabox ya sabuni na kila takataka.Watu wa kijijini pale wakawa wanamshangaa mama yangu jinsi alivyokua kajiweka weka minywele na visuruali vyake vya kubana nakwambia alikua anajiona kama mzungu mapozi kama.yote.
Kwa mshangao mkubwa babu alivyotoka pale uwani mama alininyanyua kwa lengo la kumpa babu anibebe lakini babu alikataa kunipokea kisha akamwambia anaingia ndani kuswali ila akitoka tena nje asimkute yeye Sophia wala chochote alichokuja nacho kikiwa kimebaki pale nje kwake.
Mama alilia sana,kina bibi wakaongea na babu lkn haikusaidia na mwishowe ile pick up ikaenda kupaki kwenye nyumba ya mzee fulani ambae alikua rafiki kipenzi wa babu na mama akaomba aombewe msamaha.Tukiwa pale babu akapita akielwkea sehemu na swahiba wake akamsihi sana amsikikize Sophia hata kwa dakika moja.Baada ya kuombwa sana babu akakaa kusikiliza.
Katika kusikiliza maelezo ya mama babu akamwambia mama kwa sababu lengo lako la kuja halikua kuomba msamaha bali umekuja kutubwagia mwanao ili ukahangaike na anasa zako kwa uhuru ondoka na mwanao na siku ukiona haja ya kuomba msamaha funga safari nyingine uje uombe msamaha.Na siku utakayokuja unijie kama binti wa kiislamu.
Babu akaniita,nikaenda akanibeba akaniuliza unaitwa nani?Nikamwambia naitwa Clepatina.Akaniambia la hasha!wewe unaitwa Yusra!Nimesema unaitwa nani?Ninaitwa Yusra.Akasema naam!Yusra! Yusra ukue na uwe mashuhuri na mwenye mafanikio uendane na jina lako.Akanibusu kwenye paji la uso kisha akanisomea dua na mwisho akanipa na hela yakununulia biskuti.
Alipomalizana na mimi babu yangu akamuaga jamaa yake akasimama bila kumwambia mama chochote na polepole akaanza kuondoka kuendelea na safari yake.
Maza akabaki pale huku machozi yakimlengalenga lkn mwisho wa siku tulirudi Dar huku maza akiwa hajui akaniache wapi maana ndugu zake wote waliogopa laana ya babu iwapo wangenipokea wakati yeye alikataa.
Tulirudi Dar maza akiwa na ma stress kama yote.Alinipenda sana na hakutaka kuniacha kwa mtu asiye na uhakika.Siku ya siku nikaona maza kafungasha nguo zangu na vikolokolo vyangu vyote kisha akaniambia "Utaenda kukaa na baba halafu nitarudi kukuchukua".
Basi tukaingia kwenye gari yake akawa anapita kwenye vijiwe vyote ambavyo dingi anakaaga lakin hatukumkuta lkn baada ya kuzunguka zunguka tukafika kwenye ki statinery fulani ambayo ni moja ya vijiwe vya dingi.Ile kufika tukamuona faza anatokea ndani ya ile stationary akielekea ilipo paki gari fulani ya rafik yake na dingi,alikua kapata lift ya kumsogeza mpaka sehemu fulani.Ile dingi kuingia tu na kukaa kabla hata hajafunga mlango maza akaninyanyua fasta na kwenda kunibwaga mapajani kwa dingi.Kabla faza hajaelewa nini kinaendelea maza akawa anakuja na vimfuko anavirushia mle ndan ya ile gari,wanadaka anakuja na vingine anamtupia faza usoni,mwishowe akachukua kibegi changu akamtwishwa faza kichwani huku anamkandamizia lile begi kama anataka kumvunja shingo,dingi hasira zikampanda akawa anataka kutoka akampige maza lkn maza fasta akarudi kwenye gari yake akatutimulia vumbi akapotea.Yule mshikaj wa ding alotoa lift alikua anajjzuia kucheka wakat anadaka viatu na vimfuko anavyokua akirusha maza.
Maza alivyoondika Faza na yule rafik yake wakaangaliana kwa muda kisha yule rafik akampa pole kisha akamuuliza nikakuache wapi.
Baada ya hapo dingi akatafuta mpaka akaipata nyumba tuliyokua tukiishi na maza lkn kufika akaambiwa Sophia haishi tena hapa.Dingi akanitangisha tangisha wee mara leo aniache kwa mama Ntilie mara leo aniache kwa binamu yake mara leo aniombee kwa nani sijui na mwishowe akapata wazo la kurudiana na mama Prince Chibonge.
Wakarudiana na mama Prince Chibonge akawa step maza wangu rasmi.
Step maza alirudiana na dingi wakati dingi akiwa kafulia choka mbaya kwa hiyo step maza ndo alikua anatulisha sote kuanzia mim,dingi na prince Chibonge wake.
Muda mfupi baada ya faza na step maza kurudiana faza akalipwa hela walizokua wakidai huko kazin kwao walikosimamishwa na alipopata hizo pesa akaamua kurudi bush kwenye nyumba ya urithi ya baba yake kwa lengo la kuwekeza kwenye kilimo.Step maza akaacha mishe zake alizokua akifanya Dar na kuambatana na faza na sisi watoto wao.Huko kijijini ndo kule tulikoishi jiran na nyumba ya mzee Kipipa.
Siku za mwanzon tulivyohamia bush na wakati huo dingi alikua pia yuko, step maza hakuwa akionyesha kunichukia.Alitulea sawa kwa upendo.
Shida ilianza dingi alipoanza kuzingua, maana tuliingia bush dingi akiwa na mshiko.Basi dingi akawa na michepuko kibao na muda si muda akafulia na malengo ya kuwekeza kwenye kilimo yakafifia.Hapo ndo step maza akaanza gubu.Hasira za dingi ananitolea mim,kosa kidogo tu utasikia "we si mbwa tu kama baba yako"!Mara usikie ",mtoto wa nyoka ni nyoka tu,nahangaika na wewe hapa ila kuna siku utakuja kuning'ata tu kama mama yako wewe!"
Huku na huku faza akaona pale kijijin haiwezekan tena,ktk kuongea ongea na jamaa zake akapata kaz ya mkataba wa mwaka mmoja Dar.Mwanzoni akawa anatutumia matunzo na akawa anakuja mara moja moja kutuona ila badae ikawa hatumi pesa wala salamu.
Mara ya mwisho dingi kurudi,ukiachana na ile alivyorudi wakat step maza anaumwa(ep. 2).
ilikua ni wakati ambako step maza alisema ana ujauzito.Na dingi anadai habari za hiyo mimba ndo zilifanya amuache step maza kwani mtoto sio wake na kwa maana hiyo ilimaanisha step maza alikua akimsaliti dingi.Step maza analazimisha watu kuwa Tide anafanana na dingi ila ukweli Tide hafanani na dingi wala mama yake.Prince Chibonge na mim ndo tunafanana na faza etu kuanzia sura mpaka u giant.Mim na Prince chibonge tumeenda hewan kama dingi etu.
Basi ndo hivyo step maza akatelekezwa pale na wanae na mwana wa kambo na maisha yakawa yakuunga unga mara ajaribu kulima mara ajaribu vibarua mradi shida tupu.
Mama yangu Sophia nae kwa upande wake.Ile safari yake ya south haikufanikiwa bali alikwenda Kenya ambako huko mambo hayakua kama ilivyotarajiwa.Ikabidi arudi bongo lkn alivyorudi hakuwa yule Sophia aliyetikisa jiji bali alirud amechoka hana gari wala uwezo wa kupangisha mansion kama mwanzo.Akawa Bar maid kama Bar maid wengine tu.
Jeuri ya kunichukua akawa hana na dingi nae kwa upande wake alinasa kwa mwanamke aliyemwambia hataki kulea watoto wa kambo hivyo nika stack na step maza.
Mama yangu mzazi Sophia ni kama alisahau kama ana mtoto na kuna wakati nilifikiri amekufa wananificha.
Baada ya juhudi za kumtafuta mama yangu kugonga mwamba nilikuja kukutana nae nikiwa na miaka 17 huku nikionekana kama dada wa miaka 25 sbb ya urefu.Hapo tayari nina nyumba yangu ya kwanza.
Siku nakutana na mama yangu Sophia ilikua nimeenda kuoneshwa Bar yenye guest house ambayo mmiliki wake alikua anaiuza.Pamoja na kuwa ilikua inauzwa lkn bado ilikua ikifanya kaz japo biashara ilikua inapumulia mashine.
Mtu aliyenishaur niinunue aliniambia niinunue niikarabati then niigeuze hostel coz haikua mbali sana na chuo fulan kikubwa.
Tulipofika eneo hilo tukiwa tunatafuta sehemu ya kupaki gari ghafla akatokea mwanamke na mwanaume wanapigana.Mwanaume alionekana anataka kuondoka lakin mwanamke akawa anamdhibiti asiondoke.
Mwanamke alikua ni kadada keupe kafupii kamevaa kaptura.Kanarusha vichwa balaa na kuna saa kalirusha kichwa cha pua hadi mwanaume damu za pua zikaanza kumtoka.Mwanaume alivyoona damu akawa kama tembo aliyejeruhiwa. Akajiweka sawa kisha akatuma ngumi moja ambayo haikua na lengo la kuumiza bali kuua lkn yule dada akainama ikapita.Ile ngumi ilivyopita mwanaume akawa anamsogelea mdada kwa jazba amkamate lkn dada akacheza na timing ya hatua za yule kaka akamtegea mguu na kaka akayumba na
kudondoka.
Yule mwanaume alivyodondoka ndo wanawake wenzake wakaja kumsaidia kumtaitisha yule mwanaume wakamsachi na kumpora hela zote kisha wakaondoka huku wanasema "mshenzi kweli huyu kwa hiyo alijua tutamjacha aondoke bila kulipa".
Tukapaki gari na kwenda mapokezi ambako tulimkuta yule dada aliyekua akipigana akijisugua na barafu usoni mana alipata ngeu.
Mimi na yule dada aliyekua akipigana macho yetu yalivyokutana tukabaki tunaangaliana kama masanamu kisha tukarukiana na kukumbatiana huku tukilia kisha tukaanza kucheka kisha tukalia tena.
Alikua ni Sophia mama yangu mzazi.Pamoja na miaka mingi kuisha hakuna aliyemsahau mwenzie.
Pale mahali nilipanunua na mama Sophia ndie msimamizi wa hiyo investment.Yupo vizuri kazini na huwa namtaniaga kuwa akileta uzembe kazini kaz hana.Siku hiz ana drive tena,nyodo kama kawa na anapenda bata na ukimuina utadhan yuko 30s kumbe ni mid 40s.
Step maza na mama yangu kwa sasa wote nawapenda.Nimewasamehe wote ila shida iko upande wao.
Mpaka leo eti bado wanamgombea dingi[emoji23].
Yaani nina kazi ya kuwapatanisha kila siku na watajifanya wamepatana bla bla sasa hv sisi ni watu wazima lakin ikitokea tu siku wamekutana kwangu halafu ukawaacha peke yao hata nusu saa tu lazima walianzishe waanze kutukanana kisambaa.
My cute sisy Joannah darling broda Half american my guy Equation x bestie cocastic dokta Dr. Mariposa Gily Analyse Watu8 Glenn Depal Shunie InvisibleTarget Chizi Maarifa bitimkongwe len Lovie Lady Unique Flower
meaganita NALIA NGWENA wao ni wao Nkundwe Sr makwega7 Grahams @notfeyk Urban Edmund To yeye Lexus SUV Darlin Dr. restart dadapesa Zabron Hamis Doctor G Mwanagenzi Mgibeon
atlas copco Jogoo wa Shamba II TUMBOO Wagumu Tunadumu Omulasil Palina Rashid jololo Mubby777 Aaliyyah @makwenga aker2011 Mnyamb o HOPECOMFORT Sir Carter Ironbutterfly Angel Nylon Winnone Walas Ba
Story tamuu dear [emoji8][emoji8][emoji8]tayar dear
Aiseh!!EPISODE 2
Baada ya Prince Chibonge kunikurupua nilienda kwa step maza kuitikia wito.Nilimkuta yuko jikoni akipika chapati za maji na chai ya maziwa ikichemka kwenye jiko la pembeni huku mwanae wa mwisho ambae ni rika langu aitwae Tide akiwa kakaa kwenye kigoda pembeni ya mama yake akila chapati.Nyuma yangu alikua Prince chibonge.Alipoingia tu pale jikoni na kuona Tide anakula chapati na yeye akaomba akapewa moja akaikunja kisha yote akaitia mdomoni halafu akanyoosha mkono kuomba nyingine lkn mama yake akamwambia"Hebu toka hapa wewe nikikuendekeza utakula zote na bado hutashiba" lkn Prince chibonge akaendelea kunyoosha mkono huku akimuangalia mama yake kwa macho ya huzuni na mama yake kwa vile hapendi kuona wanae wakihuzunika akachukua chapati nyingine akampa na kumwambia nyingine asubirie mezani.
Na mimi nikamuangalia step maza kwa macho ya huruma nikiamin muujiza utatokea na mim nionjoshwe japo kipande lkn I was wrong kwani baada ya kumalizana na Prince Chibonge step maza akanigeukia na kuniambia"Nenda kule bafuni kuna nguo nimeziloweka ukafue",Nikaondoka kinyonge huku harufu nzuri ya chapati za step maza ikinisindikiza.Na mnyonge mnyongeni ila step maza wangu anajua kupika bana,sema tu sijui alikua ananikomoaga maana alikua akipika atahakikisha amechafua vyombo vyote.
Basi bana siku yangu ikaanza rasmi,baada ya udobi kuna kufagia uwanja,kuosha vyombo,kusafisha ndani,kuwekea bata maji na pumba,bado kuna kutumwa na katika yote hayo hakuna hata moja nililofanya akaridhika nalo,so shukran ilikua kama sio kwezi basi sitakosa japo tusi.
Nadhan mnakumbuka kuwa jana yake mzee Kipipa alimpa step maza mshiko wa maana eeh?Basi bwana lunch alopikiwa mzee Kipipa siku hiyo lilikua sio ya mchezo.Mama wa kisambaa alitulia jikon akapika vikapikika na vilivyoiva kama kawa nikaambiwa nimpelekee mjomba Kipipa chakula lkn kusikia tu hivyo nikaanza kutetemeka ghafla na nikakimbilia chumbani kulala nikajifunika gubigubi kwani nafsi yangu haikua radhi kumuona tena yule mzee lkn haikuchukua round step maza akaja kunifunua na kusema"Haya ndo mauzauza gan tena unayoniletea?Nikamwambia mama mim naumwa sitaweza kwenda lkn alinichomoa pale kitandani na kunivuta mpaka nje liliko kapu lenye msosi wa mzee Kipipa na kunishikisha kwa nguvu kisha bila kusema kitu akaweka sura ya subutu kukataa kwenda uone.Kinyonge sana nikaanza kutembea kupeleka chakula huku machozi yakinitoka na nilipokutana na watu njian nalijifuta machozi na kuficha uso mpaka nikafika site.Mzee Kipipa Alivyoniona tu kwa tabasamu la furaha akasema "Hujambo malkia wangu Clepatina" nikataka kujibu sijambo shikamoo mjomba lkn nikashindwa.Machozi yakaanza kunilenga lenga lakin nilipomuangalia niliona ananiangalia kwa macho ya kunitisha,nikawa najizuia kulia lkn nikaona mpaka nitoe mahot pot na sahani na vijiko ili nirud na kapu kama ninavyofanyaga machoz yatanizid nguvu mambo yawe mengi hivyo nikaacha kapu na kila kitu ndan yake kisha bila kuaga nikageuka na kukimbia nyumbani.
Wakati nakimbia niliwasikia baadhi ya mafundi pale site wakiulizana "kamepatwa na nin haka leo?"
Nilipokua njian nilipita sehemu kuna kichaka.Nikaingia humo nikajificha halafu nikaliaaa mpaka machoz yakawa hayatoki tena kisha nikasimama kwa lengo la kuondoka lkn nikasita baada ya kuona mti wenye vitunda fulani ambavyo nilisikiaga eti ukivila halafu ukilala unakufa huamki tena.Nikatabasamu kisha nikavichuma vingi vikajaa mikono yote miwili kisha nikakimbia kuelekea home.
Nilipofika karibu ya home nikaingia kwa kunyata ili mtu asinione.Maza nikamuona yuko nyuma ya nyumba na mashost zake wanasukana na kupiga umbea,Prince Chibonge na Tide sikujua wako wapi.Nikaingia kwa kujificha mpaka chumbani kwangu,nikafunga mlango kwa ndani na kutafuna vile vitunda vyote nikajifunika gubi gubi nikiamini usingizi ukinichukua tu ndo imetoka hiyo siamki tena na hakuna atakayeweza tena kunituma kwa mzee Kipipa.
Hata hivyo nilikuja kuamka saa mbili ya usiku ule.Kilichotokea ni kwamba mama alijua tokea nitumwe ule mchana kupeleka chakula kwa mzee Kipipa sikurudi tena kwa vile hakuna aliyeniona nikirudi.Masaa yakapita,prince Chibonge akatumwa akanitafute hakuniona na kwa majirani sikuwepo. Maza akamtuma Chibonge akatafute fimbo nzuri kubwa zinisubir nitakaporud lkn mpaka muda wa kupeleka chakula kwa mzee Kipipa ukafika hawakuwa na wazo la kutazama chumbani kwangu.Ikabidi Prince Chibonge ndio apeleke chakula siku hiyo.
Kufika kule mzee Kipipa akauliza kwanini leo umeleta wewe na sio Clepatina?Prince Chibonge akajibu"Shida yako ni chakula au Clepatina?"Mzee Kipipa akataka kumdaka Chibonge amchape ila Prince Chibonge akafanikiwa kukimbia.Prince Chibonge alitokea kumchukia mzee Kipipa tokea siku ya kwanza anafika nyumbani kwetu na shikamoo yake kwa mzee Kipipa ilikua inatoka kwa kulazimishwa.
Kufika saa moja na nusu hivi usiku, mmoja wa majirani aliyefika pale nyumban kusaidiana mawazo juu ya nini kifanyike kwa kupotea kwangu akiwa anelekea chooni kwetu ambako njia iko karibu na dirisha langu alisikia sauti ya kicheko kutoka chumbani kwangu.Akachungulia na kumulika na tochi zile za betri na hamadi ananiona nimelala fofofo nacheka usingizini.
Jirani yule akaahirisha safari ya kwenda chooni na kisha kwenda kumuuliza mama yangu wa kambo"Uliangalia chumban kwake?".
Hilo swali ndo likamkumbusha step maza kuwa wametafuta kijiji chote kasoro chumban kwangu.Basi yule jirani akawaambia alichokiona na kweli kufika pale dirishani wakanikuta nimelala fofofo sina habari nacheka zangu ndotoni.
Zoezi la kuniamsha likaanza lakini halikua rahisi maana waliita, walirusha magunzi,maji,vimawe lakini wapi.Kama sio kule kucheka ndotoni wangehisi nimekufa.Ilibidi mlango uvunjwe nitikiswe kwa nguvu ndio nikaamka.Kilichofanya nilale vile ni mlundikano wa usingizi wa siku nyingi na uchovu.Mara nyingi nilikua nachelewa kulala nawahi kuamka.Nikaulizwa kama niko sawa nikajibu niko sawa step maza akajifanya eti amefurahi hadi akalia kwa furaha eti maana alidhani eti mwanae kipenzi nimepotea au nimepatwa na kitu kibaya ila majirani walivyoondoka usitake kujua nini kilinipata.
Siku hiyo ikawa imepita hivyo na siku nyingine zikaja na kazi zangu ni zile zile ikiwa ni pamoja na kumpelekea mzee Kipipa chakula site na nyumbani kwake jion.
Mzee Kipipa nae akaendeleza ufiraun wake, mara ya pili ya tatu na mwishowe ikawa ni utamaduni na kilichomsaidia ni kwamba kila alipomakiza ushetani wake ilikua lazima anipe hela huku akiniambia "hizi kampe mama yako mwambie mjomba anasema asante".
Ghafla step maza aligeuka bosslay wa kijiji kwa pesa za mzee Kipipa.Hakuna kanga/tenge mpya ilitoka akashindwa kununua,alokula vizur mtaan alikua yeye,kuvaa vizur ni yeye, inshort pesa ndogondogo hazikua issue kwake.Nadhani kuna mahala ilifikia step maza akajua kinachoendelea kule kwa mzee Kipipa ila kwa vile sikua mwanae na kwa vile hela ya mzee Kipipa ilishamnogea ikafika wakati kabla ya kunituma nipeleke kapu jioni alikua ananiambia nikaoge kwanza na nilishangaa siku step maza aliponipa mafuta yake nijipake na kuniambia nisirudie gaun chafu bali nikavae gauni langu la kanisani.Mwayego nilipendeza kisha akanipa kikapu nipeleke chakula kwa mjomba mzee Kipipa.Mzee Kipipa alivyoniona akasema vile ndo napaswa kuwa kila niendapo kwake.Akafanya afabyayo na kama kawaida alipomaliza akinipa hela nimpelekee step maza tofaut ni kwamba siku hiyo hela zilikua nyingi.
Maisha yakaendelea hivyo,nikawa mnyonge siku hadi siku, sina raha na mara nyingi nilitamani kujiua.
Ujenz wa shule ya mzee Kipipa uliendelea na siku moja akaaga kuwa anarudi Dar mara moja kwenda kupumzika na kuwaona familia yake.Step maza aliipokea habar hiyo kwa huzun mithili ya mtu aliyesikia habari ya msiba lkn kwa upande wangu ilikua ni habari ya faraja tena nilitaman yule mzee agongwe na gari afe kabisa na asirud tena kijijin kwetu.Kwa upande wangu mzee Kipipa aliniaga tokea jana yake alipomaliza kunifanyia ushetani wake.Aliniambia kuwa kesho ataondoka kijijin ila akirud akasikia nimemwambia mtu yeyote kuhusu 'uchumba' wetu basi atamuua mama yangu mzazi.
Basi mzee Kipipa akasafiri huku akiaga kuwa atarud baada ya mwez mmoja lkn miez na miaka ikakatika ila hakurudi tena.
Kwa upande wangu kuondoka kwa mzee Kipipa kulipunguza mzigo mzito wa mateso lakini baada ya kipindi fulani nikaanza kutokwa na vitu vichafu sehemu za siri,homa kali na nilikua natoa harufu mbaya.
Baada ya majirani kuanza kunong'ona step maza akanipeleka hospitali.Nikatibiwa na kuambiwa niseme anayeniingilia.Nilibembelezwa,nilitishiwa lkn kila nilipoulizwa nilisema sijui na mwishowe yakaisha hayo.
Nilikua mtoto mwenye kupenda shule lakin mahudhurio yangu yalikua mabaya kutokana na majukumu ya nyumbani.Hata hivyo pamoja na kuwa Tide alikua hakosi shule lakini mim mwenye mahudhurio mabovu nilifaulu vizuri sana kwenye mitihani yetu ya mwisho ya darasa la nne na yeye kufeli kias cha kuhitajika kurudia darasa.Mim na Prince Chibonge ndio tuliokua tunaongoza kwa akili shule.
Wiki ya kwanza ya mim kuripoti shule kama mwanafunz wa darasa la tano step maza ambae alikua amelazwa hospitali kwa kupooza akaruhusiwa aendelee na matibabu nyumbani.Mpaka anarudishwa nyumnan ndugu zake wengi waliokuja kumuuguza wakawa wameondoka na hivyo ikawa amebakia mama yake ambae nae alikua ni mgonjwa.
Basi ikawa kila siku nikitaka kwenda shule naambiwa nibaki nimsaidie bibi yule kaz za nyumbani.Kina Tide na Prince Chibonge wao wanaenda shule.Wiki mwezi,miez mwaka na ndo ikawa bye bye sikurudi tena shule.
Baada ya kipindi kirefu sana baba akarud nyumban siku moja,ilikua ni furaha kubwa kwangu nikitumai ya kwamba ujio wa baba utabadili maisha yangu.
Nikatafuta wasaa,nikamueleza yote ninayopitia pale na kwamba kama inawezekana anipeleke nikaishi na mama yangu.Baba akasema amekuja mara moja kumuona mama na kwamba atakaa siku tatu tu na kuondoka ila atakuja kunichukua nikakae nae huko kazin anapokaa na nitaendelea na masomo huko lakin baada ya kuondoka dingi hakugeuka nyuma.
Kumbe zile chuki zote za step maza kwangu zilichangiwa pia na kutelekezwa na dingi.Dingi wangu alikua na bado ni mzee wa totozi nyingi.Wakat step maza anaumwa dingi alikua keshaanzisha maisha na mwanamke mwingine wanaishi kama mke na mume.Hata alivyokuja alikuja tu kibinadamu lkn hakuwa amekuja kama kwa mkewe.
Yule bibi,mama yake na step maza alikaa na sisi kama miez minne hivi kisha na yeye akaondoka ikawa wanakuja wale ndugu wakuja kumuona mgonjwa leo na kuondoka kesho lakin pia step maza alishapata nguvu wakutembea mwenyewe lakin alipata changamoto ya kudondoka kama mtu mwenye kifafa.Anaweza akawa kashinda vizuri tu ghalfla akadondoka.
Ugonjwa wa step maza ulinifanya nikomae akili kabla ya umri kwani alivyoondoka yule bibi ikawa kama vile mim ndo mama wa ile familia.
Imagine mtoto wa umri wa kuwa darasa la tano nilikua bila kuelekezwa najua nikiamka nifanye nini,nipange tutakula nin kulingana na pesa niliyopewa na siku hakuna pesa nilijua nikachume nini shamban au ndan kuna nin nipike tule.
Pamoja na kuwa prince Chibonge alikua mkubwa kwangu na Tide tulilingana ila mim ndo nilikua kama dada yao mkubwa.Nilikua naweza kwenda dukan bila kuambiwa na mtu na kukopa sabuni ili ndugu zangu wafue nguo za shule au nifue nguo za step maza.
Hichi ndo kipindi atep maza alikua akinionesha upendo.Nilipokua nikimpelekea msosi alikua akiuliza kama na mim nimekumbuka kula au nahudumia wengine tu.Ndo kipindi alitoa kanga zake sandukuni akanigea,ndo kipindi alinambia mim ni baraka kwake na aliniahid ni lazima nirud shule akishapona.
Kwa vile manyanyaso yaliisha na nilikua nakula nakushiba nilinenepa na kwa vile mim ni supa tall kama baba yangu na shepu kama la mama yangu nilionekana kama msichana mkubwa kumbe toto la la tano.Mrefuu,juu mwembamba chin nimwagie kama namba 6.
Vijana wazee na waume za watu wote walikua wanafukuzana kuonja makombo ya mzee kipipa lkn wote niliwaona kama mbweha tu na kama sikuwaona kama mzee Kipipa basi ni kama mjomba na kama si kama mjomba basi ni kama baba tu.Mpaka hapo nilishajijengea picha kuwa wanaume wote hawana huruma.
Siku moja mwezi wa December ya ule nwaka niliotakiwa niwe la tano nilikua nimeenda kuhemea na wakati narudi nyumbani nikamkuta step maza akiwa amekaa nje na mgeni aliyeonekana kutoka mbali.Kufika karibu wala haikuchukua muda kumkumbuka sura chafu ya mzee Kipipa japo alikonda hadi kitamb kikamuisha.Step maza kuniona tu akasema kwa furaha"Mwanao uliokua ukimuulizia kila saa huyo hapo"
Baada ya kuambiwa vile mzee Kipipa alionekana kunishangaa sana kisha akasema"Ina maana Clepatina ndio amekua..amekua...mmm...mmmkubwa hivi?"
Step maza akacheka halafu akasema "watoto wa siku hizi kaka wanakua kama uyoga sijui wanakimbilia wapi" kisha step maza akanigeukia na kuniuliza "Klee unamkumbuka mjomba wako au umeshamsahau?"
Baada ya swali hilo
Nikamgeukia mzee Kipipa aliyekua akijichekesha chekesha pale nikamtizama kama sekunde ishirini hivi kwa sura ya kumchimba biti nililomaanisha kisha kwa sauti iliyochanganyika hasira,uchungu,kisasi na kwa kujiamini nikamkazia macho nikamwambia
"NAWEZA KUISAHAU SURA YA BABA YANGU NA NIKAWA NA AMANI LAKINI SIWEZI KUISAHAU SURA YAKO NA NIKAISHI KWA AMANI!!".
Baada ya kumtamkia maneno hayo niliendelea kumkazia macho kwa muda mrefu kisha nikageuka polepole na kutembea kuelekea jikoni na kimya kikuu kikatawala nyuma yangu.
My sis Joannah darling bro Half american bestie Equation x
Watu8 Analyse To yeye Shunie Antonia Gautama cocastic babukijana Depal Glenn Unique Flower dronedrake
Dr. Mariposa
Okay,wengi tunatamani kujua chanzo cha hela yakoEPISODE 3
Kabla sijawaeleza namna nilivyoya terorise maisha ya mzee Kipipa hadi kufikia kupoteza fahamu kwa presha na jinsi nilivyomuwashia moto kwa kutumia pesa na connections zake hadi akafikia wakati fulani kufanya jaribio la kuikimbia nchi ili awe mbali na mkono wangu ningependa kwanza kumtambulisha kwenu mama yangu mzazi.
Mama yangu mzazi, Sophia ni binti wa kisambaa aliyezaliwa katika familia ya watoto 18.
Babu yangu mzaa mama alikua ni mzee tajiri wa kiislam aliyeishika dini ya kiislamu hasa hasa hasa.
Babu yangu aliyekua na wake wanne alikua anaheshimika sana na kuna msikiti mpaka leo una jina lake ambao yeye babu yangu aliujenga.Mbali ya kujenga misikiti babu yangu anakumbukwa kwa kutoa misaada kwa wasiojiweza.
Wake na watoto wote wa babu yangu waliishi kwa kufuata maadili na misingi ya dini ya kiislamu isipokua mtoto wake mmoja tu,Sophia.
Sophia alikua tofauti na alivyotamani baba yake kwani pamoja na kuzaliwa kijijiji tena katika familia bora ya kiislamu yeye alitokea tu kuwa na tabia za ki slay queen.Mambo ya kuvaa majuba na ushungi yalimshinda Sophia.
Sophia alijijua ana umbo na sura nzuri na alipenda dunia ilione umbo lake hivyo vimin na visuruali vya kubana ndo zilikua pigo za Sophia.
Mbali ya uslay queen wa kuzaliwa nao Sophia pia alizaliwa na roho ya kijasiri.Ukimzingua ndugu yake yeyote Sophia alikua anakufata na kukuzingua na wewe.Pamoja na ufupi wake ila Sophia alikua haogopi kupigana na wanaume na alikua ana kauli yake anasema "mimi napigana na wanaume wanawake wenzangu sipigani nao bali nawapiga" .
Baada ya babu na wazee wengine wa kiislamu kumuonya Sophia bila mafanikio babu akamfukuza Sophia nyumbani kwake.
Sophia akaenda kuishi nyumban kwa kina rafiki yake aitwae Hosana.Huyu Hosana alishaondokaga na kwenda kuishi Dar ambako alikua anafanya kazi za ndani lkn wakati Sophia alipoenda kuomba hifadhi pale alikua amekuja mara moja kusalimia wazazi wake na kuwaeleza kuwa ni mjamzito na kwamba kwa sasa kuna mwanaume wanaishi nae huko Dar na wana mpango wa kuoana.
Hosana akamaliza siku zake pale kijijini na kuondoka kwa ahadi ya kumtafutia kazi Sophia.
Sophia aliendelea kuishi na mama wa Hosana na baaada ya muda Hosana akampatia kazi ya u housegirl huko Dar na nauli ilipotumwa Sophia akaingia Dar na kwenda kuish kama housegirl.
Hata hivyo Sophia hakuwa anadumu kwenye kazi sbb ya kushindwa kuvumilia manyanyaso na kubaguliwa.Kuna siku alimchamba mama mwenye nyumba ambae alikua mchoyo na mwenye roho mbaya ya kutaka Sophia ale viporo hata vilivyo chacha.Sophia alivumilia kidogo ustaarabu ukamshinda siku ya siku akamwambia yule mama"Baba yangu ana uwezo wa kukulisha wewe,mumeo,watoto wako na koo zenu zote mpaka siku mnakufa!Usinione hapa kwako ukadhani nimekimbia njaa kwetu!".
Kwa hiyo Sophia alikua ana kazi ya leo ni housegirl nyumba hii kesho nyumba ile lkn wakati wote huo Hosana ndie shoga ake mkuu hapo mjini Dar.Kitendo cha Sophia kwenda kumtembelea Hosana mara kwa mara kikafanya Sophia atambulike kwa shem wake mume mtarajiwa wa Hosana.
Umbo namba 6 la Sophia na weupe wake wa kisambaa ukamchanganya mume mtarajiwa wa Hosana.Akamtongoza na kumuahidi kumpangishia chumba na kumpa mtaji wa biashara aachane na kazi za u housegirl.Sophia akapiga mahesabu akachekecha akaona hata yeye anatamani kuishi kwa bata kama shogake Hosana, akakubali.
Baada ya kupangishiwa chumba na kuanza kuhudumiwa Sophia akatamani ampindue kabisa shogake abaki yeye lakini kila alivyojitahidi kumtoa Hosana alishindwa.Badae akagundua Hosana ana thaminiwa na yule mwanaume wao sbb amemzalia mtoto hivyo miaka miwili na kitu hivi baadae na yeye akashika ujauzito na hatimae akazaa katoto kake kazuri ka kike akakaita Clepatina.
Mpaka Clepatina anazaliwa ndio Hosana ambae ndie mama yake na Prince Chibonge alipopata majibu ya kwanini mipango ya kuolewa na baba Prince Chibonge ilivurugika ghafla na ndipo alipojua kumbe Sophia ndiye sababu ya baba Prince Chibonge kupunguza mapenz yake kwake na ndio alipojua ya kwamba kumbe na Sophia amezaa na baba Prince Chibonge.
Urafiki wao ukazikwa rasmina uadui wa kuapizana na kutamkiana kutoana roho ukazaliwa kati yao na kila mmoja wao akawa anatumia kila mbinu aolewe yeye.Mama Prince Chibonge yeye kila siku alikua anaenda kwao kuloga na mama Clepatina yeye kazi yake ilikua kumuonyesha mwanaume wao madanga ya Hosana ili tu aonekane sio wife material.
Amani ikatoweka kwenye nyumba za wanawake zake wote.Akienda kwa mama Prince Chibonge anatuhumiwa hivi,akirudi kwa mama Clepatina anatuhumiwa hivi.Alivyoona makelele yamezidi akawabwaga wote.
Baada ya kuwaacha hawa wanawake haikuchukua muda mrefu faza akasimamishwa kazi.Akawa choka mbaya anashinda Bar na vijiwe vya madalali.
Hawa wanawake nao kila mmoja akawa anahangaika kivyake kupata hela ya kulisha mwanae.Mama Prince Chibonge yeye akajikita kwenye biashara ndogo ndogo na mama Clepatina yeye akaangukia kuwa muhudumu wa Bar.
Hata hivyo mama Clepatina hakuwa muhudumu wa Bar wa kawaida na hakwenda kuomba kaz ya kuuza Bar bali kuna mwenye Bar alimuona alivyo akajua huyu binti akikaa kwenye Bar yangu wanaume watakua wanapanga foleni hivyo akamshawishi akafanye hiyo kazi kwa dau kubwa.
Kwa Kweli Sophia alikua Bar maid mwenye viwango.Alikua slay queen kweli kweli na msambaa yule ni ana maringo mpaka leo hii.Mama yangu ilifikia level akawa ana drive kwenda kazin kwake Bar kuhudumu na alikua anaishi kwenye bonge ya jumba ila la kupangisha na alikua na housegirl wa kumlelea Clepatina wake.
Hichi ndo kipindi Siphia alikua Sophia kweli.Mweupeee,softiii,sura sasa na ukija kwenye hilo umbo la namba 6 halafu ujumlishe na midhahabu aloijaza mwilini plus mavazi ya gharama na uchanganye na zile nyodo zake weeuwee!
Mama Clepatina akapata dili ya kwenda Afrika kusini ila haikuwa safari ya kuweza kwenda na mtoto.Ikabidi tusafiri kwenda mpaka usambaani kwa lengo la kwenda kuniacha kwa babu na bibi ili yeye akatafute maisha South.Mpaka wakati huo babu alishafulia na maisha yake yalikua yakutegemea watoto na katika watoto wake wote mama yangu Sophia ndo alikua na pesa kuliko wote.
Basi tulifika pale nyumbani kwa babu na pick up ikiwa imejaa mazagazaga kama yote ya zawadi.Viroba vya michele,vya sukari,ndoo za mafuta,mabox ya sabuni na kila takataka.Watu wa kijijini pale wakawa wanamshangaa mama yangu jinsi alivyokua kajiweka weka minywele na visuruali vyake vya kubana nakwambia alikua anajiona kama mzungu mapozi kama.yote.
Kwa mshangao mkubwa babu alivyotoka pale uwani mama alininyanyua kwa lengo la kumpa babu anibebe lakini babu alikataa kunipokea kisha akamwambia anaingia ndani kuswali ila akitoka tena nje asimkute yeye Sophia wala chochote alichokuja nacho kikiwa kimebaki pale nje kwake.
Mama alilia sana,kina bibi wakaongea na babu lkn haikusaidia na mwishowe ile pick up ikaenda kupaki kwenye nyumba ya mzee fulani ambae alikua rafiki kipenzi wa babu na mama akaomba aombewe msamaha.Tukiwa pale babu akapita akielwkea sehemu na swahiba wake akamsihi sana amsikikize Sophia hata kwa dakika moja.Baada ya kuombwa sana babu akakaa kusikiliza.
Katika kusikiliza maelezo ya mama babu akamwambia mama kwa sababu lengo lako la kuja halikua kuomba msamaha bali umekuja kutubwagia mwanao ili ukahangaike na anasa zako kwa uhuru ondoka na mwanao na siku ukiona haja ya kuomba msamaha funga safari nyingine uje uombe msamaha.Na siku utakayokuja unijie kama binti wa kiislamu.
Babu akaniita,nikaenda akanibeba akaniuliza unaitwa nani?Nikamwambia naitwa Clepatina.Akaniambia la hasha!wewe unaitwa Yusra!Nimesema unaitwa nani?Ninaitwa Yusra.Akasema naam!Yusra! Yusra ukue na uwe mashuhuri na mwenye mafanikio uendane na jina lako.Akanibusu kwenye paji la uso kisha akanisomea dua na mwisho akanipa na hela yakununulia biskuti.
Alipomalizana na mimi babu yangu akamuaga jamaa yake akasimama bila kumwambia mama chochote na polepole akaanza kuondoka kuendelea na safari yake.
Maza akabaki pale huku machozi yakimlengalenga lkn mwisho wa siku tulirudi Dar huku maza akiwa hajui akaniache wapi maana ndugu zake wote waliogopa laana ya babu iwapo wangenipokea wakati yeye alikataa.
Tulirudi Dar maza akiwa na ma stress kama yote.Alinipenda sana na hakutaka kuniacha kwa mtu asiye na uhakika.Siku ya siku nikaona maza kafungasha nguo zangu na vikolokolo vyangu vyote kisha akaniambia "Utaenda kukaa na baba halafu nitarudi kukuchukua".
Basi tukaingia kwenye gari yake akawa anapita kwenye vijiwe vyote ambavyo dingi anakaaga lakin hatukumkuta lkn baada ya kuzunguka zunguka tukafika kwenye ki statinery fulani ambayo ni moja ya vijiwe vya dingi.Ile kufika tukamuona faza anatokea ndani ya ile stationary akielekea ilipo paki gari fulani ya rafik yake na dingi,alikua kapata lift ya kumsogeza mpaka sehemu fulani.Ile dingi kuingia tu na kukaa kabla hata hajafunga mlango maza akaninyanyua fasta na kwenda kunibwaga mapajani kwa dingi.Kabla faza hajaelewa nini kinaendelea maza akawa anakuja na vimfuko anavirushia mle ndan ya ile gari,wanadaka anakuja na vingine anamtupia faza usoni,mwishowe akachukua kibegi changu akamtwishwa faza kichwani huku anamkandamizia lile begi kama anataka kumvunja shingo,dingi hasira zikampanda akawa anataka kutoka akampige maza lkn maza fasta akarudi kwenye gari yake akatutimulia vumbi akapotea.Yule mshikaj wa ding alotoa lift alikua anajjzuia kucheka wakat anadaka viatu na vimfuko anavyokua akirusha maza.
Maza alivyoondika Faza na yule rafik yake wakaangaliana kwa muda kisha yule rafik akampa pole kisha akamuuliza nikakuache wapi.
Baada ya hapo dingi akatafuta mpaka akaipata nyumba tuliyokua tukiishi na maza lkn kufika akaambiwa Sophia haishi tena hapa.Dingi akanitangisha tangisha wee mara leo aniache kwa mama Ntilie mara leo aniache kwa binamu yake mara leo aniombee kwa nani sijui na mwishowe akapata wazo la kurudiana na mama Prince Chibonge.
Wakarudiana na mama Prince Chibonge akawa step maza wangu rasmi.
Step maza alirudiana na dingi wakati dingi akiwa kafulia choka mbaya kwa hiyo step maza ndo alikua anatulisha sote kuanzia mim,dingi na prince Chibonge wake.
Muda mfupi baada ya faza na step maza kurudiana faza akalipwa hela walizokua wakidai huko kazin kwao walikosimamishwa na alipopata hizo pesa akaamua kurudi bush kwenye nyumba ya urithi ya baba yake kwa lengo la kuwekeza kwenye kilimo.Step maza akaacha mishe zake alizokua akifanya Dar na kuambatana na faza na sisi watoto wao.Huko kijijini ndo kule tulikoishi jiran na nyumba ya mzee Kipipa.
Siku za mwanzon tulivyohamia bush na wakati huo dingi alikua pia yuko, step maza hakuwa akionyesha kunichukia.Alitulea sawa kwa upendo.
Shida ilianza dingi alipoanza kuzingua, maana tuliingia bush dingi akiwa na mshiko.Basi dingi akawa na michepuko kibao na muda si muda akafulia na malengo ya kuwekeza kwenye kilimo yakafifia.Hapo ndo step maza akaanza gubu.Hasira za dingi ananitolea mim,kosa kidogo tu utasikia "we si mbwa tu kama baba yako"!Mara usikie ",mtoto wa nyoka ni nyoka tu,nahangaika na wewe hapa ila kuna siku utakuja kuning'ata tu kama mama yako wewe!"
Huku na huku faza akaona pale kijijin haiwezekan tena,ktk kuongea ongea na jamaa zake akapata kaz ya mkataba wa mwaka mmoja Dar.Mwanzoni akawa anatutumia matunzo na akawa anakuja mara moja moja kutuona ila badae ikawa hatumi pesa wala salamu.
Mara ya mwisho dingi kurudi,ukiachana na ile alivyorudi wakat step maza anaumwa(ep. 2).
ilikua ni wakati ambako step maza alisema ana ujauzito.Na dingi anadai habari za hiyo mimba ndo zilifanya amuache step maza kwani mtoto sio wake na kwa maana hiyo ilimaanisha step maza alikua akimsaliti dingi.Step maza analazimisha watu kuwa Tide anafanana na dingi ila ukweli Tide hafanani na dingi wala mama yake.Prince Chibonge na mim ndo tunafanana na faza etu kuanzia sura mpaka u giant.Mim na Prince chibonge tumeenda hewan kama dingi etu.
Basi ndo hivyo step maza akatelekezwa pale na wanae na mwana wa kambo na maisha yakawa yakuunga unga mara ajaribu kulima mara ajaribu vibarua mradi shida tupu.
Mama yangu Sophia nae kwa upande wake.Ile safari yake ya south haikufanikiwa bali alikwenda Kenya ambako huko mambo hayakua kama ilivyotarajiwa.Ikabidi arudi bongo lkn alivyorudi hakuwa yule Sophia aliyetikisa jiji bali alirud amechoka hana gari wala uwezo wa kupangisha mansion kama mwanzo.Akawa Bar maid kama Bar maid wengine tu.
Jeuri ya kunichukua akawa hana na dingi nae kwa upande wake alinasa kwa mwanamke aliyemwambia hataki kulea watoto wa kambo hivyo nika stack na step maza.
Mama yangu mzazi Sophia ni kama alisahau kama ana mtoto na kuna wakati nilifikiri amekufa wananificha.
Baada ya juhudi za kumtafuta mama yangu kugonga mwamba nilikuja kukutana nae nikiwa na miaka 17 huku nikionekana kama dada wa miaka 25 sbb ya urefu.Hapo tayari nina nyumba yangu ya kwanza.
Siku nakutana na mama yangu Sophia ilikua nimeenda kuoneshwa Bar yenye guest house ambayo mmiliki wake alikua anaiuza.Pamoja na kuwa ilikua inauzwa lkn bado ilikua ikifanya kaz japo biashara ilikua inapumulia mashine.
Mtu aliyenishaur niinunue aliniambia niinunue niikarabati then niigeuze hostel coz haikua mbali sana na chuo fulan kikubwa.
Tulipofika eneo hilo tukiwa tunatafuta sehemu ya kupaki gari ghafla akatokea mwanamke na mwanaume wanapigana.Mwanaume alionekana anataka kuondoka lakin mwanamke akawa anamdhibiti asiondoke.
Mwanamke alikua ni kadada keupe kafupii kamevaa kaptura.Kanarusha vichwa balaa na kuna saa kalirusha kichwa cha pua hadi mwanaume damu za pua zikaanza kumtoka.Mwanaume alivyoona damu akawa kama tembo aliyejeruhiwa. Akajiweka sawa kisha akatuma ngumi moja ambayo haikua na lengo la kuumiza bali kuua lkn yule dada akainama ikapita.Ile ngumi ilivyopita mwanaume akawa anamsogelea mdada kwa jazba amkamate lkn dada akacheza na timing ya hatua za yule kaka akamtegea mguu na kaka akayumba na
kudondoka.
Yule mwanaume alivyodondoka ndo wanawake wenzake wakaja kumsaidia kumtaitisha yule mwanaume wakamsachi na kumpora hela zote kisha wakaondoka huku wanasema "mshenzi kweli huyu kwa hiyo alijua tutamjacha aondoke bila kulipa".
Tukapaki gari na kwenda mapokezi ambako tulimkuta yule dada aliyekua akipigana akijisugua na barafu usoni mana alipata ngeu.
Mimi na yule dada aliyekua akipigana macho yetu yalivyokutana tukabaki tunaangaliana kama masanamu kisha tukarukiana na kukumbatiana huku tukilia kisha tukaanza kucheka kisha tukalia tena.
Alikua ni Sophia mama yangu mzazi.Pamoja na miaka mingi kuisha hakuna aliyemsahau mwenzie.
Pale mahali nilipanunua na mama Sophia ndie msimamizi wa hiyo investment.Yupo vizuri kazini na huwa namtaniaga kuwa akileta uzembe kazini kaz hana.Siku hiz ana drive tena,nyodo kama kawa na anapenda bata na ukimuina utadhan yuko 30s kumbe ni mid 40s.
Step maza na mama yangu kwa sasa wote nawapenda.Nimewasamehe wote ila shida iko upande wao.
Mpaka leo eti bado wanamgombea dingi[emoji23].
Yaani nina kazi ya kuwapatanisha kila siku na watajifanya wamepatana bla bla sasa hv sisi ni watu wazima lakin ikitokea tu siku wamekutana kwangu halafu ukawaacha peke yao hata nusu saa tu lazima walianzishe waanze kutukanana kisambaa.
My cute sisy Joannah darling broda Half american my guy Equation x bestie cocastic dokta Dr. Mariposa Gily Analyse Watu8 Glenn Depal Shunie InvisibleTarget Chizi Maarifa bitimkongwe len Lovie Lady Unique Flower
meaganita NALIA NGWENA wao ni wao Nkundwe Sr makwega7 Grahams @notfeyk Urban Edmund To yeye Lexus SUV Darlin Dr. restart dadapesa Zabron Hamis Doctor G Mwanagenzi Mgibeon
atlas copco Jogoo wa Shamba II TUMBOO Wagumu Tunadumu Omulasil Palina Rashid jololo Mubby777 Aaliyyah @makwenga aker2011 Mnyamb o HOPECOMFORT Sir Carter Ironbutterfly Angel Nylon Winnone Walas Ba
At the age of 26 [emoji1787][emoji1787]