Hoja yako hiyo (maandishi mekundu) ina mashiko, ila ni ndoto kudhani kuwa vyombo vyetu vya usalama vinaweza kufuatilia!! Tanzanite inapatikana tu Tz lakini wauzaji kwenye soko la dunia siyo Tz. Ukuta umejengwa lakini utoroshaji umerudi kwa mwendokasi....
Nne,Miradi yote tajwa inajengwa kwenye ukanda wa madini ya thamani kubwa (Vito na Rare Earth Metals). Wachina wanajua nini Tuko nacho chini ya ardhi kupitia espionage satellite zao hivyo haya makampuni mengi makubwa ni State Owned or affiliated (SOE) hivyo yana mission zaidi ya ujenzi wa barabara (Ktk Hili nashauri vyombo vyetu vya usalama kufuatilia hili na kuwezeshwa ili kuziba mianya mikubwa ya utoroshaji na uvunaji wa rasilimali Za nchi....
Huu sio mwisho wa Ujenzi,zinakuja zingine kibao tuu pengine na huko zitakuwwpo..SIJAONA BARABARA ZA KANDA YA ZIWA, YAANI HATA MOJA TU, BASI KAMA SIO MOJA HATA KILOMETA MOJA YA LAMI, DUH HATARI SANA.... HII NCHI NGUMU SANA HII.
Barabara za kulipia Huwa ndio Zina element ya BOP na kiukweli ni chache sana Africa Kwa sababu inaleta ukakasi wa Kisiasa Kwa hapa Africa na Tanzania in particularNapongeza hii initiative ya Serikali
Japo yatupasa kuwa makini na gharama Za wakandarasi kutokuwa kubwa kuliko bei ya soko.
Pili lazima reinforcements ya quality monitoring iwe na uwezo pia mamlaka ya kuhakikisha barabara zetu zinakuwa na ubora stahili (Value for Money).
Tatu,Nchi yetu tayari Ina undertake turnkey mega infrastructure projects (SGR,Stigler,BRT,Etc)..Kimsingi uchumi wetu umeelemewa sana..Hatukupaswa kuharakisha kusign mikataba ya kandarasi zote Kwa wakati mmoja..EPC+F ni mkopo (Mkandarasi anajenga mradi Kwa kukopa Kwa niaba ya serikali in which sense tukilipa tunalipa na riba zote involved na zaidi sana tukichelewa kulipa kuna penalties..
Nchi yetu bado ni Changa,Hatupaswi kuwa na haraka sana ktk ujenzi wa miradi ambayo ROI si ya muda mfupi..Modalities Za EPC+F makampuni yanakopa kwenye commercial banks (Local or International)..Kuna riba..
Nadhani tuendako kwenye infrastructure projects tuangalie uwezekano wa ku implement EPC+F yenye BOT Modalities (Build,Operate and Transfer) hivyo contractor anakuwa na perspective ya kibiashara pia hivyo Hawezi ku overcharge au kujenga mradi chini ya kiwango.
Nne,Miradi yote tajwa inajengwa kwenye ukanda wa madini ya thamani kubwa (Vito na Rare Earth Metals)..Wachina wanajua nini Tuko nacho chini ya ardhi kupitia espionage satellite zao hivyo haya makampuni mengi makubwa ni State Owned or affiliated (SOE) hivyo yana mission zaidi ya ujenzi wa barabara (Ktk Hili nashauri vyombo vyetu vya usalama kufuatilia hili na kuwezeshwa ili kuziba mianya mikubwa ya utoroshaji na uvunaji wa rasilimali Za nchi..
Mwisho,Utekelezaji wa mipango ya maendeleo iende sambamba na ujenzi wa mifumo ya uzalishaji mkubwa (Kilimo,Ufugaji,Viwanda) ili kunenepesha uchumi na kuwezesha serikali kulipa madeni makubwa yatokanayo na mikopo toka Bank Ya Dunia,Benki ya maendeleo ya Afrika n.k.
Nchi haiweki dhamana badala yake Contractor ndio anatakiwa kuweka dhamana ya pesa ndefu in form of bank guarantee Ili sisi tumbane Financier wake..Hoja yako hiyo (maandishi mekundu) ina mashiko, ila ni ndoto kudhani kuwa vyombo vyetu vya usalama vinaweza kufuatilia!! Tanzanite inapatikana tu Tz lakini wauzaji kwenye soko la dunia siyo Tz. Ukuta umejengwa lakini utoroshaji umerudi kwa mwendokasi.
Najiuliza Tanzania imeweka dhamana gani kwa Mkondarasi akubali kukopa pesa Benki kutujengea barabara? Je, kwa nini Serikali haikukopa fedha Benki za kumwezesha huyo Mkondarasi (kwa kuwa inaamini ana uwezo wa kujenga hizo barabara [emoji848]) kwa masharti yetu?
Ni Kiongozi mwenye agenda binafsi anaweza kukubali aina hiyo ya mkataba. AIBU
ANAUPIGA MWINGI - kazi iendelee
Ukiacha ya Igawa Tunduma zingine zote hazikuwa na lami,hata hiyo ya Igawa Tunduma ilikuwa single lane Sasa itakuwa Dual Carriage road ndio kusema inajengwa Barabara Mpya.Hizo barabara zilikuwa hazina lami au wanaondoa ya mkoloni wanaweka ya mchina? Kama zilikuwa hazina tangia mkoloni basi tuna safari ndefu sana.
Nchi haiweki dhamana badala yake Contractor ndio anatakiwa kuweka dhamana ya pesa ndefu in form of bank guarantee Ili sisi tumbane Financier wake..
Kumbuka hii model mkandarasi ndio anabear takribani risks zote ambazo yeye ameziweka kwenye bei(offer price).
Mwisho uzuri contractors wengi ni Wachina na Taifa lao Lina uwezo Sasa Til.4 ni pesa ndogo sana kwao ndio maana umeona contractor wa 4 tuu kwenye miradi 7.
Akikiuka makubaliano unadhani itakuaje? Ni pesa yake lakini Serikali inamlipa hatua Kwa hatua so dhamana lazimaKwenye mikataba ya ujenzi, ambapo mwenye mradi anamlipa "Contractor" fedha ya kutekeleza, anapaswa kuweka dhamana. Lakini aina hii ya mkataba ambapo "Contractor" anatumia fedha yake aweke dhamana ya nini?
Nimependa plan ya hizo barabara , itafanya vaadi ya sehemu ziwe na njia fupi .Kwa mara ya Kwanza baada ya Uhuru Tanzania imepata Rais Samia apewe maua yake.
Serikali ya Rais Samia imeandika Historia nyingine ya ubunifu kwa kusaini kuanza ujenzi wa barabara za kuu za lami kwenye mikoa 13 kwa pamoja zenye jumla ya urefu wa KM 2035 kwa mtindo wa EPC+ F (Engineering, Procurement, Construction and Finance) kwa gharama ya Tsh.Tilioni 3.8 ambapo miradi inatarajiwa Kukamilika ndani ya miaka 4 (2023-2027).
Akizungumza wakati wa kushuhudia kutiwa saini kwa mikataba hiyo Jijini Dodoma, Waziri wa Ujenzi Prof. Mbarawa amesema kwamba, barabara hizo hazitokuwa za kulipia tozo kama wapotoshaji wanavyosema. Ikumbukwe hii haijawahi tokea toka Uhuru, walinda legacy mnafundishwa kazi.
My Take
Samia anawaonesha kwamba Private Sector inalipa kuliko Ujamaa mbuzi ambao baadhi ya watu wasiojielewa wanakumbatia.
Ndio maana hata kwenye Bandari anataka awafundishe namna ya kutumia rasilimali kwa manufaa ya watu badala ya kuhubiri propaganda za Uzalendo mbuzi na umaskini over years.
Hongera sana Mh. Rais, na Waziri wa Mbarawa Kwa Ubunifu,Historia itaandika jina lako kwa wino Mwekundu.
=====
MIRADI YA BARABARA ILIYOSAINIWA KWA UTARATIBU WA EPC + F
i) Barabara ya Kidatu β Ifakara β Lupiro β Malinyi β Kilosa Kwa Mpepo β Londo β Lumecha/Songea (km 435.8) inapita katika mikoa ya Morogoro na Ruvuma na inapita pia katika Majimbo ya Kilombelo, Ulanga, Malinyi na Namtumbo;
ii) Barabara ya Arusha β Kibaya β Kongwa (km 453.42) inapita katika Mikoa ya Arusha, Manyara na Dodoma na inapita katika Majimbo ya Arusha Mjini, Arumeru Magharibi, Simanjiro, Kiteto na Kongwa;
iii) Barabara ya Handeni β Kiberashi β Kijungu β Kibaya β Njoro β Olboroti β Mrijo Chini β Dalai β Bicha β Chambolo β Chemba β Kwa Mtoro β Singida (km 384.33) inapita katika Mikoa ya Tanga, Manyara, Dodoma na Singida na inapita katika Majimbo ya Kilindi, Chemba, Kiteto, Singida Mashariki na Iramba Mashariki;
iv) Barabara ya Igawa β Songwe β Tunduma (njia nne) (km 237.9) inapita katika Mikoa ya Mbeya na Songwe na inapita katika Majimbo ya Mbarali, Mbeya Vijijini, Mbeya Mjini, Mbozi, Vwawa na Tunduma;
v) Barabara ya Masasi β Nachingwea β Liwale (km 175) inapita katika Mikoa ya Lindi na Mtwara na inapita katika Majimbo ya Masasi, Nachingwea na Liwale;
vi) Barabara ya Karatu β Mbulu β Haydom β Sibiti River β Lalago β Maswa (km 339) inapita katika Mikoa ya Manyara, Simiyu, Singida na Arusha na inapita katika Majimbo ya Mbulu Mjini, Mbulu Vijijini, Karatu, Iramba Mashariki, Meatu, Maswa Mashariki na Kisesa; na
vii) Barabara ya Mafinga β Mtwango β Mgololo (km 81) inapita katika Mkoa wa Iringa na inapita katika Majimbo ya Mufindi Kusini na Mafinga.
Nakupa mfano Mwingine unaoonesha kwamba gharama Huwa sio uniform kama unavyotaka kulazimisha..Yule aliyewafanya wahandisi wote wa Tanroads kuhamia kwenye siasa za chama cha kijani
Mkataba wa "Engineering, Procurement, Construction and Financing (EPC+F)" ni tofauti na mikataba migeni ya ushirikiano kati ya mwenye mradi na mwekezaji km "Public Private Partnership (PPP)" au "Build Operate and Transfer (BOT)" ambayo yote hiyo "Mwekezaji" anabeba "risks" zote na mwenye mradi anachohitajika ni kuwa na uhakika "Contractor" anao uwezo kifedha, utaalamu na anaaminika. Pia mwenye mradi anapaswa kuingia na mwekezaji mkataba utakaolinda uwekezaji.Akikiuka makubaliano unadhani itakuaje? Ni pesa yake lakini Serikali inamlipa hatua Kwa hatua so dhamana lazima
Pengine ni naming ya jina tuu au kutakuwa na Changamoto Kwa Barabara ya Sasa kiasi kwamba inatakiwa kufanyiwa rehabilitation (sijapita hii so hapa am just guessing) maana hata Igawa-Tunduama Kuna Barabara ya lami pia..Nimependa plan ya hizo barabara , itafanya vaadi ya sehemu ziwe na njia fupi .
Byw kidatu ifakara tayari kunamalizika lami kwa nini mkataba wa barabara hii mpya uanzie tena kidatu?
Sawa ila sidhani kama Serikali inaweza kiuka makubaliano ya kimkataba maana hata Kwa mikataba ya Sasa kwani contractor Huwa analindwaje? Mbona sijawahi ona sehemu ambayo contractor analindwa per say? Sana sana ni kwamba Kuna riba ya kuchelewesha mkataba na Serikali ndio inalindwa dhidi ya Mkandarasi kuingia mitini.Mkataba wa "Engineering, Procurement, Construction and Financing (EPC+F)" ni tofauti na mikataba migeni ya ushirikiano kati ya mwenye mradi na mwekezaji km "Public Private Partnership (PPP)" au "Build Operate and Transfer (BOT)" ambayo yote hiyo "Mwekezaji" anabeba "risks" zote na mwenye mradi anachohitajika ni kuwa na uhakika "Contractor" anao uwezo kifedha, utaalamu na anaaminika. Pia mwenye mradi anapaswa kuingia na mwekezaji mkataba utakaolinda uwekezaji.
Je, kwenye hii mikataba ya EPC+F, ya ujenzi wa barabara, mwekezaji/"Contractor" analindwa vipi? Itapendeza kuona moja ya mikataba hiyo.
Bandari ya Tanga inakwamishwa na kina . Meli za Roro hazitii nanga pale.Pengine ni naming ya jina tuu au kutakuwa na Changamoto Kwa Barabara ya Sasa kiasi kwamba inatakiwa kufanyiwa rehabilitation (sijapita hii so hapa am just guessing) maana hata Igawa-Tunduama Kuna Barabara ya lami pia..
Mwisho itafupisha umbali na kufungua uchumi Mpya mathalani kutoka Songea Hadi Dar Magari Yote Sasa yatapitia Ifakara na Moro umbali utakuwa sawa na Dar -Mbeya km 800 plus kutoka zaidi ya km 1000 za Sasa..
Aidha umbali wa Tanga Hadi Mwanza au Mikoa yote ya Lake Zone au Nchi za Magharibi itakuwa mfupi chini ya km 800,hakuna route ya Bus ,Tanga-Mwanza Sasa itakuwepo.
Ila Kizuri zaidi Sasa Bandari ya Tanga itaanza kuwa Busy maana kutoka Tanga kwenda huko Kanda ya Ziwa ni pafupi kuliko kutoka Dar,just imagine Km 1300 vs km 800
Hili ni jukwaa la kuelimishana na kwa kuwa wewe ndiye uliyeleta uzi na unatetea aina hiyo ya mkataba wa ujenzi, tujuze zaidi. Ukifanya hivyo utakuwa unaondoa maswali kuhusu uhalali wake, kama ilivyo kwa mkataba wa BandariSawa ila sidhani kama Serikali inaweza kiuka makubaliano ya kimkataba maana hata Kwa mikataba ya Sasa kwani contractor Huwa analindwaje? Mbona sijawahi ona sehemu ambayo contractor analindwa per say? Sana sana ni kwamba Kuna riba ya kuchelewesha mkataba na Serikali ndio inalindwa dhidi ya Mkandarasi kuingia mitini.
Mwisho sio lazima kuona mkataba ingia tovuti ya idara ya Manunuzi au ingia shule mwenyewe Kwa ku google Kila kitu utaona kinavyofanyika..
Hata zingekuwa zinatia Nanga ,Barabara gani ingetumika kufika Mwanza? Ya kupitia Arusha Hadi Singida? Nani afanye huo mzunguko?Bandari ya Tanga inakwamishwa na kina . Meli za Roro hazitii nanga pale.
Achana nae mkuu, amezoea zile kiki za kijimaAhadi hewa watu wamesaini mikataba ππ we Jamaa Bure kabisa..
Kwanza tangu lini Samia amewahi kukupa ahadi hewa? Kwanza sio Barabara tuu Bali Hadi kwenye Afya amefanya mapinduzi, kwenye Elimu ndio kabisa Watoto wooote wanapata mkopo na Sasa kawaongeza wa diploma,Ajira ndio usiseme..
Samia ni kichwa kingine,anataka awasaidie huko kwenye bandari Wajamaa mbakaza Kwa kung'ang'ania umaskini na ujinga πππ
Ukiacha ya Igawa Tunduma zingine zote hazikuwa na lami,hata hiyo ya Igawa Tunduma ilikuwa single lane Sasa itakuwa Dual Carriage road ndio kusema inajengwa Barabara Mpya.