Zaka au sadaka ni hiari, kuwapigia simu waumini kuwakumbusha ni kuwalazimisha

Zaka au sadaka ni hiari, kuwapigia simu waumini kuwakumbusha ni kuwalazimisha

mimiamadiwenani

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
5,718
Reaction score
7,784
Nina mambo kadha wa kadha nataka niongee leo. Kwanza samahani mno kwa ndugu zangu walokole wenzangu kwa maneno na maswali makali ninayokwenda kuuliza humu!

Hivi kwa dunia ya sasa mtoto wako kufaulu darasa la saba ni jambo la kumshukuru Mungu mpaka kwenda kanisani KUTOA USHUHUDA?

Ndugu zangu kuna vitu naona kama havi make sense hivi.

Anyway twende kwenye ZAKA.
ZAKA ni sheria ya agano la kale, ambalo YESU alilitimiliza na kutuweka katika neema na si chini ya sheria tena.

Sasa kwa nini Wachungaji wa kileo wanalazimisha watu watoe zaka na kufikia mpak hatua ya kuwapigia simu kuwakumbusha?

Mtume Paulo anasema, "kama umeacha agano la kale liache lote(acha sheria zake zote), na kama unalifuata basi fuata na sheria zake zote".

Sasa kwa nini ndugu zangu WALOKOLE mnachagua chagua? Mpo agano jipya la imani ila kwa nini mnazing'ang'ania baadhi ya sheria ili ziwanufaishe?

Ni bora muweke wazi tu kuwa ZAKA ni hiyari na siyo lazima, kuliko kuwalazimisha watu mpaka kupigiana simu kukumbushana.

Mwisho, naamini Mungu anatoa utajiri na haangalii unamcha au humchi, akiamua yeye anakupa tu. Ila hii haimaanishi tusimche yeye.

Kuna watu wana miaka na miaka wanamuomba Mungu utajiri ila Mungu anasema NO.

Wakipata sana basi ni laki laki za kula tu ili wasife.

Mungu anaangalia zaidi moyo wako, anajua utakuwaje akikupa utajiri.

Zaidi hongereni ndugu zangu mliopata bahati ya kuteuliwa na Mungu mwenyewe muwe matajiri(wa halali lakini siongelei wale wenye ndumba) ili muwatunze wengine.

Asubuhi njema!
Ila msisahau maswali yangu nasubiri majibu hapa.
 
ni kama wakatolik walivyo rogwa hadi wanabatiza watoto na kutubu/kuungama kwa viongozi wao
Hii taasisi ingekuwa ni kama ticket ya kwenda mbinguni unapoitaja kuashiria ni wabaya hata kama utafanya dhambi zote nadhani hakuna ambaye angebaki!ninyi wote pepo mngeiona.

Mbona mnasumbuka sana!Catholics wamewafanya nini ikiwa hawaji majumbani mwenu wala kwenye majumba yenu ya ibada kuwalazimisha kuamini wanavyoamini wao kama mnavyowalazimisha wao kuamini kama mnavyoamini nyie?
 
Huyu mkuu wa wilaya kirombero alikuwa akilitumikia kanisa la kirokole la ulogo
 
Huendi mbinguni kwakua unatoa sadaka, na wala hutozuiwa kuingia mbinguni kwakua hutoi sadaka. Katika zile amri kumi toa ama usitoe sadaka haipo katika hizo..

Makanisa hasa ya kilokole 70% ya muda wa ibada ni kuhubiri baraka utakazopata ukitoa sadaka. Na makanisa haya huwa wana sadaka sijui zaka zaidi ya ngapi kwny ibada moja.

Na siyo hayo makanisa tu, hata katoliki nao wanaelekea hukohuko. Kwny jumuia mnaletewa sijui padre hana godoro sijui hana kile, mumchangie.
 
Yesu hakuja kutengua bali kutimiliza.
Amri kumi za MUNGU ni agano la kale. Vipi amri kumi leo tuziache...
Namna ya utoaji zaka ndo tatizo linapoanzia. Binafsi naona namna sahihi ni kupeleka kwa watoto yatima na watu wasiojiweza maana ndo lengo kuu la zaka. Angalau kanisa katoliki linamiliki vituo kadhaa vya kulea yatima, hao naweza kuwaelewa wakisisitiza utoaji zaka.
 
Utoaji ni kwa ajili ya watu wajuao utajiri ni nini na siri zake nini za kuupata sio kwa ajili.ya malofa wasiotarajia kuwa matajiri kwenye maisha yao

Utajiri una siri nyingi ndio maana watu wengi maskini
Ukiona mtu anatoa iwe sadaka,zaka au kuwapa maskini ,Au kusaidia jamii awe kaokoka au la bila mbwembwe wala kelele jua huyo mtu ana roho ya utajiri.

Mleta mada ni mfano mzuri wa watu wenye roho ya umaskini na pepo la umaskini ukija kutajirika wewe niite mbwa sio rahisi kwa hiyo roho uko.nayo

Mwenye roho ya utajiri hana shida hata ya kusubiri kitabu cha dini kiseme atajenga kanisa au msikiti nk na hata kutoa mamilioni yanayozidi hata hizo zaka na mafungu ya kumi .Yuko juu ya sheria kama Paulo alivyosema siko chini ya sheria tena nimevuka huko

Mtu kuhamasishwa kuwa atoe fungu la kumi kanisani ni ushahidi mmojawapo kuwa kwenye hilo kanisa kuna wengi wenye pepo na roho ya umaskini

Watu wanatoa asilimia tisini ya mapato yao na hawafiliski ni matajiri wakubwa duniani lofa ana struggle kutoa kafungu tu ka kumi na bado hiyo hata asipotoa umadkini unamfuata hadi kwenye nyayo

Tanzania wako watu kibao hutoa nusu za mapato yao na zaidi kusaidia dini na jamii walokole na wasio walokole na hawafiliski

Mleta mada wala hahitajiki malaika atueleze hali ya maisha yako ikoje ila ukweli ni kuwa una changamoto kubwa za kifedha na pepo la umaskini limeweka makao makuu kwenye maisha yako
 
Nina mambo kadha wa kadha nataka niongee leo. Kwanza samahani mno kwa ndugu zangu walokole wenzangu kwa maneno na maswali makali ninayokwenda kuuliza humu!

Hivi kwa dunia ya sasa mtoto wako kufaulu darasa la saba ni jambo la kumshukuru Mungu mpaka kwenda kanisani KUTOA USHUHUDA?

Ndugu zangu kuna vitu naona kama havi make sense hivi.

Anyway twende kwenye ZAKA.
ZAKA ni sheria ya agano la kale, ambalo YESU alilitimiliza na kutuweka katika neema na si chini ya sheria tena.

Sasa kwa nini Wachungaji wa kileo wanalazimisha watu watoe zaka na kufikia mpak hatua ya kuwapigia simu kuwakumbusha?

Mtume Paulo anasema, "kama umeacha agano la kale liache lote(acha sheria zake zote), na kama unalifuata basi fuata na sheria zake zote".

Sasa kwa nini ndugu zangu WALOKOLE mnachagua chagua? Mpo agano jipya la imani ila kwa nini mnazing'ang'ania baadhi ya sheria ili ziwanufaishe?

Ni bora muweke wazi tu kuwa ZAKA ni hiyari na siyo lazima, kuliko kuwalazimisha watu mpaka kupigiana simu kukumbushana.

Mwisho, naamini Mungu anatoa utajiri na haangalii unamcha au humchi, akiamua yeye anakupa tu. Ila hii haimaanishi tusimche yeye.

Kuna watu wana miaka na miaka wanamuomba Mungu utajiri ila Mungu anasema NO.

Wakipata sana basi ni laki laki za kula tu ili wasife.

Mungu anaangalia zaidi moyo wako, anajua utakuwaje akikupa utajiri.

Zaidi hongereni ndugu zangu mliopata bahati ya kuteuliwa na Mungu mwenyewe muwe matajiri(wa halali lakini siongelei wale wenye ndumba) ili muwatunze wengine.

Asubuhi njema!
Ila msisahau maswali yangu nasubiri majibu hapa.
Kwa Kifupi naona wewe ndiye una shida...

Kama mimi nimeamua kutoa Sehemu ya Kumi ya mali zangu na kupeleka kanisani na hiyo hela ikatumika kunua vyakula na kulipa mishahara watumishi na kujenga miundo mbinu mizuri ya kiibada wewe kinachokuuma ni nini?

Hata kama ni agano la kale wewe unasumbuka na nini?

Mbona kuna watu wengi wanakesha bar kila siku na kununua pombe za gharama na Nyama na kununua Makahaba na ulafi uliopindukia wanatumia fedha nyingi tena mara nyingine hata mshahara wote?? Hao hauwaoni kuwa wa na shida? Ila unaumia roho kwa Mimi kutoa 10% ya mapato yangu kupeleka kanisani? Unasisitiza kwamba ni Agano la kale..

Kuna vitu vingi sana vya aibu na kutapanya fedha vinafanywa na watu lakini hamuoni, ila mnasumbuka na Sadaka...

Pilipili usiyoila yakuwashia nini??
 
Back
Top Bottom