mimiamadiwenani
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 5,718
- 7,784
Nina mambo kadha wa kadha nataka niongee leo. Kwanza samahani mno kwa ndugu zangu walokole wenzangu kwa maneno na maswali makali ninayokwenda kuuliza humu!
Hivi kwa dunia ya sasa mtoto wako kufaulu darasa la saba ni jambo la kumshukuru Mungu mpaka kwenda kanisani KUTOA USHUHUDA?
Ndugu zangu kuna vitu naona kama havi make sense hivi.
Anyway twende kwenye ZAKA.
ZAKA ni sheria ya agano la kale, ambalo YESU alilitimiliza na kutuweka katika neema na si chini ya sheria tena.
Sasa kwa nini Wachungaji wa kileo wanalazimisha watu watoe zaka na kufikia mpak hatua ya kuwapigia simu kuwakumbusha?
Mtume Paulo anasema, "kama umeacha agano la kale liache lote(acha sheria zake zote), na kama unalifuata basi fuata na sheria zake zote".
Sasa kwa nini ndugu zangu WALOKOLE mnachagua chagua? Mpo agano jipya la imani ila kwa nini mnazing'ang'ania baadhi ya sheria ili ziwanufaishe?
Ni bora muweke wazi tu kuwa ZAKA ni hiyari na siyo lazima, kuliko kuwalazimisha watu mpaka kupigiana simu kukumbushana.
Mwisho, naamini Mungu anatoa utajiri na haangalii unamcha au humchi, akiamua yeye anakupa tu. Ila hii haimaanishi tusimche yeye.
Kuna watu wana miaka na miaka wanamuomba Mungu utajiri ila Mungu anasema NO.
Wakipata sana basi ni laki laki za kula tu ili wasife.
Mungu anaangalia zaidi moyo wako, anajua utakuwaje akikupa utajiri.
Zaidi hongereni ndugu zangu mliopata bahati ya kuteuliwa na Mungu mwenyewe muwe matajiri(wa halali lakini siongelei wale wenye ndumba) ili muwatunze wengine.
Asubuhi njema!
Ila msisahau maswali yangu nasubiri majibu hapa.
Hivi kwa dunia ya sasa mtoto wako kufaulu darasa la saba ni jambo la kumshukuru Mungu mpaka kwenda kanisani KUTOA USHUHUDA?
Ndugu zangu kuna vitu naona kama havi make sense hivi.
Anyway twende kwenye ZAKA.
ZAKA ni sheria ya agano la kale, ambalo YESU alilitimiliza na kutuweka katika neema na si chini ya sheria tena.
Sasa kwa nini Wachungaji wa kileo wanalazimisha watu watoe zaka na kufikia mpak hatua ya kuwapigia simu kuwakumbusha?
Mtume Paulo anasema, "kama umeacha agano la kale liache lote(acha sheria zake zote), na kama unalifuata basi fuata na sheria zake zote".
Sasa kwa nini ndugu zangu WALOKOLE mnachagua chagua? Mpo agano jipya la imani ila kwa nini mnazing'ang'ania baadhi ya sheria ili ziwanufaishe?
Ni bora muweke wazi tu kuwa ZAKA ni hiyari na siyo lazima, kuliko kuwalazimisha watu mpaka kupigiana simu kukumbushana.
Mwisho, naamini Mungu anatoa utajiri na haangalii unamcha au humchi, akiamua yeye anakupa tu. Ila hii haimaanishi tusimche yeye.
Kuna watu wana miaka na miaka wanamuomba Mungu utajiri ila Mungu anasema NO.
Wakipata sana basi ni laki laki za kula tu ili wasife.
Mungu anaangalia zaidi moyo wako, anajua utakuwaje akikupa utajiri.
Zaidi hongereni ndugu zangu mliopata bahati ya kuteuliwa na Mungu mwenyewe muwe matajiri(wa halali lakini siongelei wale wenye ndumba) ili muwatunze wengine.
Asubuhi njema!
Ila msisahau maswali yangu nasubiri majibu hapa.