Zaka au sadaka ni hiari, kuwapigia simu waumini kuwakumbusha ni kuwalazimisha

Zaka au sadaka ni hiari, kuwapigia simu waumini kuwakumbusha ni kuwalazimisha

Wewe ndo masikini wa kwanza, kwa mtazamo wako huo hutokuja kufanikiwa (kiuchumi)
Siri ya utajiri ni kuheshimu kila senti unayoshika. Ukiona mtu anatoa sadaka au msaada mkubwa basi ujue katoa sehemu kidogo ya mali ambayo haiwezi kuathiri uchumi wake na huwa anajua ataifidia vipi. Chunguza makanisa mengi ya kilokole wamejaa masikini na fukara wa kutupwa!
Mkuu usiwe mbishi, siri ya utajiri ni kutoa sadaka kuanzia kina Mo na wengine, chunguza utajua ukweli.
 
Kwa shetani ukitoa unapata zaidi ila huko kanisani (siyo kwa Mungu) ukitoa ndo basi tena dhahama imekukuta! Tuna mifano mingi sana ya watu waliofirisika kwa kujifanya watoaji wakubwa makanisani.
Shetani mdiye mmiliki wa fedha, yeye anajua ni vipi atakupa hizo fedha maana ni miliki yake. Mungu ni mmiliki wa vyote duniani (uhai, afya, na uzima wa milele) isipokuwa pesa.

Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app

Rejea comment hapo juu kutoa sio kupata MUNGU anazo sababu zingine nje ya kutoa Ili akubariki.
Baraka sio pesa pekee.
Shetani ni Mkuu wa ulimwengu huu kwasababu dunia ni makazi ya muda kwa shetani na mwanadamu.
Makazi ya umilele ni paradiso na jehanamu. Mungu ni mmiliki wa vyote yaani kuzimu, duniani, mbinguni, paradiso na jehanamu.
 
Mimi huwa naelewa wapinga zaka na sadaka,huwa ni wajumbe wa shetani.Ili kuwapumbaza Wakristo wajinga Ili waweze kuwaangusha, sadaka na zaka ni hirizi tosha mchawi akugusi wala kuchezea mali yako.
Wao kwa shetani wanatoa hadi asilimia 80 Ili wapate nguvu. Uleta mafundisho ya kuwakatikisha tamaa Wakristo Ili wasiwe na ulinzi waweze kuwaloga kirahisi.
HUU NI UKWELI ASILIMIA 100.
 
Nchi zikizoendelea zina connection na Mungu kama hujui

Nakupa mfano Marekani ndio nchi pekee duniani ambayo haiamini kuwa pesa pekee ndio msingi wamafanikio

Na wameandika kabisa kwenye pesa yao ya noti ya dola kuwa In God we trust sio in our brain and our plans we trust!!

Narudia .utajiri una siri nyingi mojawapo ni kutoa ndio mabilionea wote wenye na wasio dini kwenye kutoa wanapenda mno.
Ndio maana huhamasisha hadi watu wao kutoa hata wawe dini hawana wanaambiwa basi toeni hata mitumba ziwe nguo.,magari nk vipelekwe kwa maskini Afrika huko

Ndio maana hata wewe waweza kuea mfaidika wa utoaji wao kwa kuvaa mitumba ya bei nafuu au kuendesha kagari mtumba toka ulaya au japani kalikotolewa na mtoaji wa kule kwa kabei kadogo ili kaletwe Africa na wewe maskini wa Afrika walau na wewe uwe na kagari kwa kuwa uwezo wa kununua kapya ulaya au japani huna

Sasa ukishakata kagari kako mtumba jeuri ndio inaanza sadaka au zaka kitu gani ujinga mtupu kisa una kagari used sasa wewe ndie bilionea tajiri kati ya maskini!!!
Unaenda nje ya mada, hapa tunajadili utoaji wa zaka na sadaka kwa lazima huko makanisani. Unataka kuniambia hao wazungu wanaoleta misaada ya nguo na magari wanafanya hivyo kwa neema ya kutoa zaka na sadaka kwa nguvu!!?? Kwanza huko Ulaya na Marekani hayo mambo ya dini hayana nguvu kihivyo unavyodhani, wao wanaamini Mungu yupo ila aliwapa akili na ufahamu wa kuijenga leo na kesho yao bila kutegemea miujiza. Nyie mliofungwa ufahamu ndo mnaamini hamtafanikiwa bila kumkabidhi pesa zenu sheikh au mchungaji!
 
Kwani kuna miungu wangapi huko makanisani!? Nnavyojua mimi Mungu ni mmoja so tutayapima mafanikio ya kila mlokole kwa kuamini yanatoka kwa Mungu yuleyule anyewabariki wengine.
Kuna makanisa ya Mungu Jehovah na kuna makanisa ya shetani pia.
Kubarikiwa sio mali pekee ni zaidi ya hio
 
Mkuu usiwe mbishi, siri ya utajiri ni kutoa sadaka kuanzia kina Mo na wengine, chunguza utajua ukweli.
Sadaka unaitoa kwa nani? Sadaka kama ile ya Mengi ndo sadaka sahihi ila hapa tunapinga sadaka za kulazimishana, kupigiana simu kwa nguvu eti tupeleke kwa mchungaji! Sadaka zangu ninatoa na nitaendelea kutoa kwa wahitaji (yatima, wajane na wazee wasiojiweza) na ninaamini huko ndiko baraka zangu zilipo.
 
Hao hata wasingetoa zaka bado wangefanikiwa maana mafanikio huanzia kichwani kwa mtu.
Vipi kuhusu matajiri wa Kimarekani wasio wayahudi nao wanatoa zaka kwa nani!!!??? Nipe mifano ya matajiri wa hapa Tanzania pia then turudi kwa walokole wako wa hapahapa nchini.

Ninekuambia watoaji wakubwa wote wako beyond hizo terminologies wanatoa kuliko hizo asilimia kumi za vitabuni walishavuka huko


Ibrahim utajiri wake haukuanzia kichwani kwake,Mungu ndie alianzisha,Yakobo utajiri wake haukuanzia kichwani kwake ulianzishwa na Mungu aliyempa siri ya kondoo kuzaliana bila kujamiiiana,Taifa la Israeli walikuwa maskini wa kutupwa watumwa kwa waarabu misri Mungu akawapa nchi na utajiri

Wewe wewe ni muamini sana akili zako
Biblia inatamka wazi

Mit 3:5-6​

Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako


Pia inatamka Mungu ndie atoaye utajiri huamini basi baki hivyo


Kum 8:18​

Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.

Pia kuna utajiri wa aina mbili tofauti yake kubwa ni kudumu vizazi hadi vizazi Utajiri wa kupewa na shetani au wa kutegemea akili za kibinadamu tu huwa haudumu vizazi vingi Wa kupewa na Mungu hudumu vizazi vingi

Mit 8:18​

Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia.
 
Kunaa watu wana miaka na miaka wanamuomba Mungu wawe matajiri ila Mungu anasema NO.

Wakipata sana basi ni laki laki za kula tu ili wasife.

🥱😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Hakuna anayepinga zaka wala sadaka. Tunachopinga ni kupigiana sim kulazimishana kutoa. Wengine zaka na sadaka zetu huzipeleka kwa wahitaji moja kwa moja na si kanisani.

Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
Kanisa halina jeshi wala jela hakuna linalolazimisha Halina uwezo wa kukulazimisha kuwa muumini wala kukulazimisha kutoa
Kila jamii ina taratibu zake ukiona hukubaliani jiondokee tu nenda kaanzishe dini yako ambayo haikusanyi sadaka wala zaka

Tatizo kuna waleta fujo makanisani Kanisa lina utaratibu wake unasema sitaki mimi nitakuwa nafanya hivi si uende uanzishe kanisa lako liminal hayo unayoyaamini usiyokubaliana na hapo ulipo.? Au tafuta kanisa lenye misimamo kama yako badala ya kuleta vi imani vyako vya ajabu ajabu ambavyo hacienda na utaratibu uliopo hapo ulipo.

Ukiona una kiiimani chako kinatofautiana na jamii ulipo au kanisa ulipo.unaanza tukelele twa hiki sikubaliani ni wakati wako muafaka uhame au ukaanzishe kidini chako
 
Nina mambo kadha wa kadha nataka niongee leo. Kwanza samahani mno kwa ndugu zangu walokole wenzangu kwa maneno na maswali makali ninayokwenda kuuliza humu!

Hivi kwa dunia ya sasa mtoto wako kufaulu darasa la saba ni jambo la kumshukuru Mungu mpaka kwenda kanisani KUTOA USHUHUDA?

Ndugu zangu kuna vitu naona kama havi make sense hivi.

Anyway twende kwenye ZAKA.
ZAKA ni sheria ya agano la kale, ambalo YESU alilitimiliza na kutuweka katika neema na si chini ya sheria tena.

Sasa kwa nini Wachungaji wa kileo wanalazimisha watu watoe zaka na kufikia mpak hatua ya kuwapigia simu kuwakumbusha?

Mtume Paulo anasema, "kama umeacha agano la kale liache lote(acha sheria zake zote), na kama unalifuata basi fuata na sheria zake zote".

Sasa kwa nini ndugu zangu WALOKOLE mnachagua chagua? Mpo agano jipya la imani ila kwa nini mnazing'ang'ania baadhi ya sheria ili ziwanufaishe?

Ni bora muweke wazi tu kuwa ZAKA ni hiyari na siyo lazima, kuliko kuwalazimisha watu mpaka kupigiana simu kukumbushana.

Mwisho, naamini Mungu anatoa utajiri na haangalii unamcha au humchi, akiamua yeye anakupa tu. Ila hii haimaanishi tusimche yeye.

Kuna watu wana miaka na miaka wanamuomba Mungu utajiri ila Mungu anasema NO.

Wakipata sana basi ni laki laki za kula tu ili wasife.

Mungu anaangalia zaidi moyo wako, anajua utakuwaje akikupa utajiri.

Zaidi hongereni ndugu zangu mliopata bahati ya kuteuliwa na Mungu mwenyewe muwe matajiri(wa halali lakini siongelei wale wenye ndumba) ili muwatunze wengine.

Asubuhi njema!
Ila msisahau maswali yangu nasubiri majibu hapa.
Wewe siyo Mkristo ni Mnafiki ndiyo maana taratibu za kanisa lako Unaleta Jamiiforums.
Ukiwa mwanakanisa hai unajua kuwa kanisa linahitaji Nini kwa Sasa na inawezekana ulihaidi Mwenyewe Sasa Kama huna hela hiyo Mwambie huna.Acha kukashifu
 
Wewe siyo Mkristo ni Mnafiki ndiyo maana taratibu za kanisa lako Unaleta Jamiiforums.
Ukiwa mwanakanisa hai unajua kuwa kanisa linahitaji Nini kwa Sasa na inawezekana ulihaidi Mwenyewe Sasa Kama huna hela hiyo Mwambie huna.Acha kukashifu

Ni kweli unachoongea
Badala ya yeye kushinda humu anapinga kinachofanywa na kanisa lake ahame aende kwingine kwenye hiyo imani yake isiyoendana na kanisa alipo au kama haliko popote akaanzishe lake lisilokusanya sadaka au zaka au fungu la kumi full stop.

Viongozi wa dini ni wakati waanze kuwa wakali mtu anasema hiki sikubaliani aambiwe tu ondoka nenda huko.mnaoendana kiimani au kaanzishe dini yako
Watu wa aina hii wanaleta vurugu makanisani zisizo za lazima

Kanisa libaki tu na wale wakubaliana na kuendana taratibu za kanisa husika
 
Nina mambo kadha wa kadha nataka niongee leo. Kwanza samahani mno kwa ndugu zangu walokole wenzangu kwa maneno na maswali makali ninayokwenda kuuliza humu!

Hivi kwa dunia ya sasa mtoto wako kufaulu darasa la saba ni jambo la kumshukuru Mungu mpaka kwenda kanisani KUTOA USHUHUDA?

Ndugu zangu kuna vitu naona kama havi make sense hivi.

Anyway twende kwenye ZAKA.
ZAKA ni sheria ya agano la kale, ambalo YESU alilitimiliza na kutuweka katika neema na si chini ya sheria tena.

Sasa kwa nini Wachungaji wa kileo wanalazimisha watu watoe zaka na kufikia mpak hatua ya kuwapigia simu kuwakumbusha?

Mtume Paulo anasema, "kama umeacha agano la kale liache lote(acha sheria zake zote), na kama unalifuata basi fuata na sheria zake zote".

Sasa kwa nini ndugu zangu WALOKOLE mnachagua chagua? Mpo agano jipya la imani ila kwa nini mnazing'ang'ania baadhi ya sheria ili ziwanufaishe?

Ni bora muweke wazi tu kuwa ZAKA ni hiyari na siyo lazima, kuliko kuwalazimisha watu mpaka kupigiana simu kukumbushana.

Mwisho, naamini Mungu anatoa utajiri na haangalii unamcha au humchi, akiamua yeye anakupa tu. Ila hii haimaanishi tusimche yeye.

Kuna watu wana miaka na miaka wanamuomba Mungu utajiri ila Mungu anasema NO.

Wakipata sana basi ni laki laki za kula tu ili wasife.

Mungu anaangalia zaidi moyo wako, anajua utakuwaje akikupa utajiri.

Zaidi hongereni ndugu zangu mliopata bahati ya kuteuliwa na Mungu mwenyewe muwe matajiri(wa halali lakini siongelei wale wenye ndumba) ili muwatunze wengine.

Asubuhi njema!
Ila msisahau maswali yangu nasubiri majibu hapa.i
Kwa Kifupi naona wewe ndiye una shida...

Kama mimi nimeamua kutoa Sehemu ya Kumi ya mali zangu na kupeleka kanisani na hiyo hela ikatumika kunua vyakula na kulipa mishahara watumishi na kujenga miundo mbinu mizuri ya kiibada wewe kinachokuuma ni nini?

Hata kama ni agano la kale wewe unasumbuka na nini?

Mbona kuna watu wengi wanakesha bar kila siku na kununua pombe za gharama na Nyama na kununua Makahaba na ulafi uliopindukia wanatumia fedha nyingi tena mara nyingine hata mshahara wote?? Hao hauwaoni kuwa wa na shida? Ila unaumia roho kwa Mimi kutoa 10% ya mapato yangu kupeleka kanisani? Unasisitiza kwamba ni Agano la kale..

Kuna vitu vingi sana vya aibu na kutapanya fedha vinafanywa na watu lakini hamuoni, ila mnasumbuka na Sadaka...

Pilipili usiyoila yakuwashia nini??
Lipa zaka acha kujitetea, asiyelipa zaka anamwibia Mungu kwa hiyo siyo hiari ni lazima kulipa zaka "Malaki 3:7-10"
 
Huyo mungu waliyemuandika kwenye noti zao unamfahamu!? Vipi matendo yao yanasadifu kuamini katika Mungu?
Wao ndo watetezi wa mashoga na ushoga, je ndiyo maagizo ya Mungu waliyemuandika katika noti? Mungu wa kweli haandikwi kwenye noti ambayo ni mali ya shetani.
Shida kubwa umekalili kuwa ucha Mungu ni kujitoa muhanga, kuuwa na kuwachukia watenda dhambi. Mungu alishatoka huko aliua sana na uovu haukuisha akaamua kujivika Rehema na Neema. Bwana Yesu alikuwa rafiki wa watenda dhambi na watoza ushuru.
 
Kondoo wa Bwana watalala njaa wewe ,😁
 
Luka 11:42
Lakini ole wenu Mafarisayo, kwa sababu mnatoa sehemu ya kumi ya mnanaa na mchicha na kila aina ya mboga, lakini mnapuuza haki na kumpenda Mungu! Mlipaswa kufanya mambo hayo, bila kupuuza yale mengine. 43 Ole wenu Mafarisayo,

Hilo hapo andiko la fungu la kumi katika agano jipya. Yesu anawaambia wasipuuze hayo mengine. Yaani sehemu za kumi.
 
Back
Top Bottom